Polisi wadai kumhoji 'mtesaji' wa Ulimboka

Polisi wadai kumhoji 'mtesaji' wa Ulimboka

Wahuni tu hao polisi magamba wanataka kutuzuga kwamba wanafanya kazi zao kumbe siye tumeshawastukia. Dr Ulimboka aliteswa ili kuuwawa tangu June 2012 miezi 9 hiyo yote polisi magamba walikuwa wapi kumhoji mtuhumiwa Mkuu!? Na ni nani anayeweza kuhakikisha huyo aliyehojiwa ndiye huyo Mtuhumiwa mkuu na siyo Mkenya mwingine wanayejaribu kumbambikia kesi!?

Mtuhumiwa lazima gwaride la utambulisho lifanyike, mbona walihoji bila kumshirikisha mhanga?
 
Heri wangekaa kimya tu!kudanganya umma wa watanzania kwanza ni kinyume ma katiba ya nchi,pili ni aibu sana kwa kiongozi mkuu wa jeshi kama Mnguklu kudanganya akijua kuwa maandishi yake hayatafutika milele....hapo hawana ujanja wakitaka ukweli waite tune huru au FBI waone hata kama week 2 zitafika kama Rama hajakamatwa na kuaibishwa!
 
'Mh habari za kazi'
'nzuri tu, kuna nin?
'aaaaa... Eeeeee... Karibu chai kwanza mheshimiwa'
'sina mda wa kunywa chai hapa, nambie ulichoniitia'
'Akchuale..aaa ..unajua bwana vyombo vya habari vinaandika upuuzi sana... aaaa hasa hawa mwanahalisi aaaa kuhusu hii ishu ya huyu mjinga Ulimboka.., sasaaa, sijui tunafanyaje..'
'hakuna shida, mwanahalisi nimeshaagiza lifungiwe... hao wengine waache tu waongee, si wanatumiwa na cdm?... Aaa haina shida kuna mpango tunakamilisha kuhakikisha hili suala linawageukia cdm... Watakomaje?.... Hahhahahaaa... Kuna jingine?'

'hakuna mheshimiwa sisi tunawaahidi tu kutoa ushirikiano wa hali ha juu kwa lolote mtakapotutaka tufanye kukamisha hiyo mipango yenu.... hahahhahhaaaa..asante mheshiwa, pole kwa usumbufu... si unajua tena fomalite?
'hakuna cha fomalite wewe, hizo fomalite zinafanya kazi huko kwa akina mramba na yona, sio ikulu... Kwaheri'

Hahahaaahaaà!!!!!
 
Mtuhumiwa lazima gwaride la utambulisho lifanyike, mbona walihoji bila kumshirikisha mhanga?
Ni kwa sababu hao polisi wana watuhumiwa wao kulingana na script ya movie waliyoiandaa... Ndio maana wanawakataa watuhumiwa wanaotajwa na mwathirika


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
"Sisi tunapeleka mtuhumiwa mahakamani tunaporidhika kuwa ushahidi tulioupata una nguvu, na siyo kweli kwamba kila mtu anayehojiwa na polisi lazima afikishwe mahakamani," alifafanua Mngulu.

Aidha Mngulu alisema kuwa mbali ya kumhoji Ighondu, pia walimhoji wakili wa kujitegemea, Nyaronyo Kicheere, kuhusiana na suala hilohilo.

Hata hivyo, Kicheere alikanusha kuhojiwa na polisi kuhusiana na suala la Dk. Ulimboka, bali aliitwa polisi kuwasilisha tamko la kisheria (hati ya kiapo) la Dk. Ulimboka ambamo anathibitisha kuwa Ramadhan Ighondu ndiye aliyepanga na kuratibu njama zote za kutekwa na kuteswa kwake.

"Siyo kweli kwamba nimewahi kuhojiwa na polisi kuhusu suala la Dk. Ulimboka, hawajanihoji, ila niliitwa makao makuu ya polisi na nilipofika pale hawakunihoji chochote bali waliomba niwape ile hati ya kiapo ya Dk. Ulimboka ambayo niliisoma mbele ya waandishi wa habari, na pia niliwapatia cheti cha kisheria cha kuniidhinisha kuisoma hati hiyo kwa waandishi wa habari," alibainisha Kicheere na kuongeza:

"Ila nimepata taarifa kwamba polisi wamepanga kuniita tena ili nikaandikishe maelezo, kwa hiyo nawasubiri waniite rasmi, lakini nasisitiza kuwa kwa sasa polisi hawajanihoji chochote kuhusu suala hilo," alisisitiza.

Hata hivyo, wakati polisi wakidai kumhoji Ighondu, hawajawahi kumuita wala kumhoji Dk. Ulimboka ambaye ndiye shahidi namba moja na mtu pekee anayewajua bila chembe ya shaka watekaji na watesi wake

Hapa kwa kuwa intamhusu mtu wa Ikulu ni jinai. Kwa Rwakatare ni ughaidi.

Ndugu zangu hapa ni mwendelezo wa kuonyesha namna polisi wanafanya kazi ya kulinda maslahi ya watawala na wala si usalama wa raia na mali zao.

Mara elfu elfu ni afadhali tungebaki mikononi mwa Mwingereza kuliko kudanganywa uhuru halafu tunakuwa chini ya ccm - jk - genge la kimafia.

HATA HIVYO TUSIKATE TAMAA. NJIA IPO.
 
Hatuhami kwenye hoja ng'oooooo, Lwakatare featuring Ludovick in Bukoba Boys ndio habari ya mujini kwa sasa. R.I.P propaganda za kipumbavu za tz daima.
 
Rama tena? Mwanahalisi ikafungiwa, eekhe! Yuko wapi yule kichaa wa Kova aliyekwenda Kanisani? Sirikali imekuwa Sirihewa
 
Cha ajabu wanasema hawakuona ushahidi uliojitosheleza kumpeleka mahakamani... Pambafffff zao ... Ulimboka kamtaja.... Sasa ushahidi gani tena wanaoutaka ? Tangu lini mtesi Wa mtu au mwizi akaulizwa kukubali kwamba ni yeye mwizi au mtesi ?

Kama waliona matamshi ya ighondu hayana ukweli , ni kwa nini wasimchukulie hatua hata walau onyo huyo ulimboka au ni kwa nini ighondu asifungue defamation case !

Hawa polisi wetu wanafaa kuwemo kwenye Guinness world book ! Sijui mchakato Wa Guinness ukoje ili niwaombee waingizwe?
 
Alaa kumbe! Kuna wengine wanahojiwa kwa siri!

Sent using wireless by wire
 
Huyo mtuhumiwa wa mada yuko ndani? Na yule aliyemua Mwangosi kuna update zozote kujua yuko wapi? Awa polisi wana play double standards.
 
Na bado watazidi kulikoroga. damu ya Dr Uli haikumwagika bure wanafikiri Watanzania wa Leo ni mambumbumbu hawajui kuchambua habari na kuzifuatilia.
Asilimia chache sana ya waTZ wanao jitambua, tena hasa mijini, huko vijijini bado saana, wapo watu ukiwasimulia habari ya DR ulimboka kwao watadhani ni hadithi ya alifu lela olea, kwahiyo serkali yetu ndio inajidaia watu dizine hiyo
 
Wanajaribu kufukua mizimu ili kufukia hili la Kina Lwakatare. Mtu wa kwanza kufika Eneo la tukio alipotekwa Dkt Uli alikuwa Kijokisimba maana alikuwa anaskilizia maana alifanikiwa kwenda na Jopo la waandishi ili wampige Picha Uli akiwa eneo la Tukio, baada ya hapo aka Organise maandamano yalokosa watu Pale salenda Bridge, baadae eti akaenda Amnest Internation 'kumlilia' Dkt Uli, Msiban mafia huwa wanalia mpaka kukosa nguvu sijui kwa nn?Ukweli uliahirishwa ila haukufutwa!

Mkuu unaongea uhalo wa mlevi
 
Hahaha..... Nimekumbuka hii hadithi "Nani amfunge paka kengele". Huu ni usanii wa mchana kati ya usalama wa taifa na polisi.
 
Hapa kwa kuwa intamhusu mtu wa Ikulu ni jinai. Kwa Rwakatare ni ughaidi.

Ndugu zangu hapa ni mwendelezo wa kuonyesha namna polisi wanafanya kazi ya kulinda maslahi ya watawala na wala si usalama wa raia na mali zao.

Mara elfu elfu ni afadhali tungebaki mikononi mwa Mwingereza kuliko kudanganywa uhuru halafu tunakuwa chini ya ccm - jk - genge la kimafia.

HATA HIVYO TUSIKATE TAMAA. NJIA IPO.
Njia gani tena hiyoo?
 
Why now? What happened? Wazungu wameibana serikali nini?
 
hivi kumuhoji afisa usallama wa ikulu bila kumvua vyeo vyake inaruhusiwa?
 
Back
Top Bottom