Polisi wadaiwa kupokea amri ya kumpeleka mahakamani Msanii Optter

Polisi wadaiwa kupokea amri ya kumpeleka mahakamani Msanii Optter

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Jeshi la polisi limeendelea na danadana zake kukwepa kumpeleka msanii Optter Mahakamani huku likiendelea kuzuia dhamana yake.

Wakili kutoka kituo cha THRDC amepeleka hati ya kimahakama kuwataka Polisi kumpeleka mchora katuni Mahakamani.

Kwa mujibu wa sakata hili, RCO wa Kinondoni ameendelea kushikilia suala la mchora katuni huyu huku akielezea kuwa anatekeleza maagizo.

Jana afisa upelelezi wa shauri hili anadaiwa kuchukua maelezo ya mtuhumiwa na jana hiyo hiyo polisi wameenda kupekua kwenye makazi ya Optter. Inadaiwa mazingira yanaonesha kuwa Polisi wamekuwa wakimlazimisha mtuhumiwa akiri makosa wanayomtuhumu nayo au la ataozea jela

Polisi kituo cha Oysterbay wanadaiwa kuendelea kutengeneza mazingira ya kuhakikisha wanaendelea kumshikilia hapo kituoni.

Baadhi ya Askari wanadai, kuna shinikizo kutoka kwa wavaa viatu wakitaka kujua msanii ametumwa na nani kuchora picha inayowasumbua wakubwa.

Tutaendelea kuwajuza kinachojiri
 
Naamini hata huyo aliedhaniwa kwamba mhanga wa huo mchoro, kama anajua kuna mtu amewekwa ndani Polisi kwa kosa la kudhaniwa.

Polisi wanakera sana aisee.. Ndio maana Raia tunawashangilia akina Hamza, na kuwaona kama mashujaa waliosimama na kufanya kitu, katika kupambana na udhalimu wa Jeshi la Polisi..
 
Naamini hata huyo aliedhaniwa kwamba mhanga wa huo mchoro, kama anajua kuna mtu amewekwa ndani Polisi kwa kosa la kudhaniwa.. Polisi wanakera sana aisee.. Ndio maana Raia tunawashangilia akina Hamza, na kuwaona kama mashujaa waliosimama na kufanya kitu, katika kupambana na udhalimu wa Jeshi la Polisi..
RCO wa Kinondoni ndiye ameishikilia kesi hii.

Ametaka kumuachia kwa dhamana ya polisi, lakini anabanwa na amri ya mahakama kumpeleka mahakamani.

Wasanii wametaka suala lipelekwe mahakamani kwani kuna dalili ya kutaka kumtengenezea kosa lingine endapo watatoa dhamana yao bila kumpeleka mahakamani
 
Back
Top Bottom