Polisi wakimbizana na Wamachinga Dar

Polisi wakimbizana na Wamachinga Dar

Jamaa mchonganishi sana huyu, hapendi nchi itulie kabisa, amekaa sharishari tu, hawa hawa walikuwa wanamtukana Jiwe kuhusu Machinga, leo hii suala la Machinga linatafutiwa suluhishi watu walewale wanapinga na kuleta uchochezi, Stupid people
Nimeshangaa Sana unafiki wake aisee.
 
Jamaa mchonganishi sana huyu, hapendi nchi itulie kabisa, amekaa sharishari tu, hawa hawa walikuwa wanamtukana Jiwe kuhusu Machinga, leo hii suala la Machinga linatafutiwa suluhishi watu walewale wanapinga na kuleta uchochezi, Stupid people
Ni ujingaujinga tu. Hakuna miji isiyo na utaratibu duniani. Serikali ipo sahihi ktk hili, hizi cheap popularity sijui kujitafutia riziki haina nafasi.
 
Jamaa mchonganishi sana huyu, hapendi nchi itulie kabisa, amekaa sharishari tu, hawa hawa walikuwa wanamtukana Jiwe kuhusu Machinga, leo hii suala la Machinga linatafutiwa suluhishi watu walewale wanapinga na kuleta uchochezi, Stupid people
Acha ujinga wewe wa kubebesha lawama wasiohusika. Serikali yako ya CCM ndiyo inaifanya hii nchi isitulie
 
Wewe unadhani kwanini hawataki kwenda huko? Likipatikana jibu la hili, suluhisho haliko mbali.
Wanataka Serikali iwatafutie wateja huko wanakoelekezwa kwenda. Madai ya hovyo sana
 
Machinga waliwahi kuua kijana mbichi aliyekanyaga nyanya kwa bahati mbaya tokea hapo siwapendi kabisa yaani.
Hawa na bodaboda ni watu wa kuogopa wana ile kitu inaitwa “Mob psychology” ni muda wao kukubali kuwa na sehemu maalamu za kufanyia biashara zao na sio kila mahali ni pakuvamia na kuweka meza chafuchafu kwanza hawa ndio wamekuwa wakichafua mazingira wameweka vibanda hadi kwenye mitaro hivyo kusababisha kutuama kwa maji..

Kuna wale ambao wako pale mwenge naomba serikali isiwaache kabisa waondolewe wamekuwa kero kubwa kwa waenda kwa miguu..

Mwisho kabisa nimpongeze Mh. Samia Suluhu na mkuu wa mkoa kwa uthubutu huu, mimi ni Pro- Magufuli ila kwa hili niko na mama yetu samia suluhu, piga kazi mama tuko pamoja na wewe kwenye hili…
 
Hahahaaaa....... Usimwamini mwanasiasa yoyote by Zitto Kabwe
Binafsi nilishangaa wao kuongezewa siku 12 mbona barabara ya makumbusho hadi viktoria pale ni safi hii yote ni kwa sababu hakuna uchafu unaoitwa machinga na kwa sasa hakuna sehemu safi kwa dar kama hiki kipande tajwa hapo juu.

Hawa watu sio wakuwalea kabisa ni vyema wakahamishwa kabisa nje ya mji, huu upuuzi huwezi ukuta kwa madiba.
 
Back
Top Bottom