Polisi, Wakurugenzi, Wakuu wa wilaya/Mikoa na Usalama wa Taifa kuingilia uchaguzi kwa amri toka juu ndio kinaharibu, sio Katiba

Polisi, Wakurugenzi, Wakuu wa wilaya/Mikoa na Usalama wa Taifa kuingilia uchaguzi kwa amri toka juu ndio kinaharibu, sio Katiba

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Sina tatizo na suala la kuwa na Katiba mpya, lakini tatizo langu ni kuona watu wakidhani Katiba mpya ndio suluhisho la matatizo ya kisiasa nchini. Huko ni kupotoka. Nchi kama Marekani wana katiba ya kidemokrasia sana, lakini leo wanalia Trump na kundi lake kufanya mambo kihuni tu na kwa mabavu. Na hata wanatumia katiba hiyohiyo ya USA kuvuruga demokrasia ya Marekani.

Kwa hiyo tusidhani kwamba tatizo la kukosekana haki na usawa kwa vyama vya upinzani nchini liko kwenye katiba, hapana. Tatizo ni matumizi mabaya ya madaraka na ubabe tu wa wale wanaokuwa katika uongozi. Tatizo ni kiburi na ulevi tu wa madaraka.

Suala la kujiuliza ni kama uwepo wa Katiba mpya utazuia ubabe na ulevi huo wa madaraka. Labda. Lakini tusisahau kwamba viongozi wetu wametumia ubabe hata katika kukiuka mambo ambayo yako wazi kwenye katiba. Mtu ambaye ni mbabe wa kukiuka katiba iliyopo kwa kuwatumia Polisi, Wakurugenzi, Wakuu wa wilaya/Mikoa na Usalama wa Taifa katika kuingilia uchaguzi na kuufanya usiwe huru na haki, hawezi kuacha kufanya hivyo kwa sababu kuna Katiba mpya. Na hawaingilii uchaguzi kwa kuwa Katiba iliyopo inawapa mamlaka ya kuingilia uchaguzi.

Kwa hiyo watu wasijikite kwenye suala la katiba mpya peke yake kama wanataka mabadiliko hapa nchini. Kuna njia nyingi za kumchuna mbuzi ili aliwe kitoweo.
 
Pole umejikunja kuandika ukidhani umeandika pointi kumbe ni ugoro, unajicontradict hebu jipanga tuandike vitu objectively
Mkuu, unapingana na kilichoandikwa hapa?
Hata Diallo alikiongelea hicho! Hata katiba iwe nzuri kiasi gani, mtawala anaweza kuikanyaga tu!
Kule Zenji kulikuwa na Tume huru, lakini CCM kwa kumtumia Jecha, akafanya yake. Alifanywa nini? Nakubalina na mleta uzi huu, kwa 100%.
 
Katiba iliyopo inawezesha kuunda watawala miunguwatu,ambao
-Wanaenesha nchi kwa matamko
-Hawahojiwi, hawakosolewi wala hawataki kushauriwa na yeyote kwa lolote hata wanapokanyaga haki za binadamu.
-Wanaojiwekea kinga za kuwalinda wasiguswe hata wanapoboronga.
 
Katiba inahusika kwa sababu katika hiyo chain ya mamlaka kuna mnufaika mmoja anaweza kushiriki matendo hayo ili kuumiza upande shindani kisha hakuna consequence zozote za kisheria juu yake maana ana kinga ya kutoshtakiwa.

Ni mpaka katiba itakapoweza kumhold kila mtu accountable kwa kuvunja sheria ndipo hoja yako itakuwa na maana
 
Mkuu, unapingana na kilichoandikwa hapa?
Hata Diallo alikiongelea hicho! Hata katiba iwe nzuri kiasi gani, mtawala anaweza kuikanyaga tu!
Kule Zenji kulikuwa na Tume huru, lakini CCM kwa kumtumia Jecha, akafanya yake. Alifanywa nini? Nakubalina na mleta uzi huu, kwa 100%.
Zenji ni nchi au kawilaya tu
 
Katiba inahusika kwa sababu katika hiyo chain ya mamlaka kuna mnufaika mmoja anaweza kushiriki matendo hayo ili kuumiza upande shindani kisha hakuna consequence zozote za kisheria juu yake maana ana kinga ya kutoshtakiwa.

Ni mpaka katiba itakapoweza kumhold kila mtu accountable kwa kuvunja sheria ndipo hoja yako itakuwa na maana
Kuna mambo Katiba inahusika. Lakini fikiria zuio la mikutano, hakuna sehemu katiba imezuia mikutano ya kisiasa, lakini mbona inazuiwa japo Katiba inaruhusu?

Katiba ndio ilimruhusu Magufuli kumtuma Sabaya kwenye mission zao zile? Sawa utasema kama Ktiba ingeruhusu Raisi kufunguliwa mashitaka asingefanya vile. Lakini usisahau alifanya kwa siri. Katiba haikuruhusu kuunda kikosi cha Wasiojulikana
 
Mtu kama wewe ni wa kuhurumiwa tu
Mkuu uwezo wako wa kuelewa mambo ni mdogo unauliza maswali ya kitoto
Hebu uliza uambiwe nini maana checks and balances ambayo itakuwa msingi mkuu wa kuandika katiba
Umeona kilichofanyika Zambia au kilichofanyika uchaguzi wa marekani , katiba inaweka misingi ya taasisi huru kutoingiliwa na wanasiasiaa
 
Mkuu, unapingana na kilichoandikwa hapa?
Hata Diallo alikiongelea hicho! Hata katiba iwe nzuri kiasi gani, mtawala anaweza kuikanyaga tu!
Kule Zenji kulikuwa na Tume huru, lakini CCM kwa kumtumia Jecha, akafanya yake. Alifanywa nini? Nakubalina na mleta uzi huu, kwa 100%.
Achana nae huyu. Hawa ndio wanaotaka kuwapotosha kina Mbowe kwamba jibu la matatizo yao liko kwenye Katiba mpya. Zambia wapinzani walinyanyasawa sana na serikali ya Lungu, lakini wameshinda bila Katiba mpya. Nadhani kina Mbowe hawapaswi kusahau kwamba wasielekeze nguvu zote kwenye Katiba
 
Mkuu uwezo wako wa kuelewa mambo ni mdogo unauliza maswali ya kitoto
Hebu uliza uambiwe nini maana checks and balances ambayo itakuwa msingi mkuu wa kuandika katiba
Umeona kilichofanyika Zambia au kilichofanyika uchaguzi wa marekani , katiba inaweka misingi ya taasisi huru kutoingiliwa na wanasiasiaa
Kwa hiyo unafikiri Katiba za nchi kama Israel, Uganda, Saudi Arabia, Venezuela nk ndio mbaya kuliko zote duniani?
 
Kuna mambo Katiba inahusika. Lakini fikiria zuio la mikutano, hakuna sehemu katiba imezuia mikutano ya kisiasa, lakini mbona inazuiwa japo Katiba inaruhusu?

Katiba ndio ilimruhusu Magufuli kumtuma Sabaya kwenye mission zao zile? Sawa utasema kama Ktiba ingeruhusu Raisi kufunguliwa mashitaka asingefanya vile. Lakini usisahau alifanya kwa siri. Katiba haikuruhusu kuunda kikosi cha Wasiojulikana
Childish argument
 
Sina tatizo na suala la kuwa na Katiba mpya, lakini tatizo langu ni kuona watu wakidhani Katiba mpya ndio suluhisho la matatizo ya kisiasa nchini. Huko ni kupotoka. Nchi kama Marekani wana katiba ya kidemokrasia sana, lakini leo wanalia Trump na kundi lake kufanya mambo kihuni tu na kwa mabavu. Na hata wanatumia katiba hiyohiyo ya USA kuvuruga demokrasia ya Marekani.

Kwa hiyo tusidhani kwamba tatizo la kukosekana haki na usawa kwa vyama vya upinzani nchini liko kwenye katiba, hapana. Tatizo ni matumizi mabaya ya madaraka na ubabe tu wa wale wanaokuwa katika uongozi. Tatizo ni kiburi na ulevi tu wa madaraka.

Suala la kujiuliza ni kama uwepo wa Katiba mpya utazuia ubabe na ulevi huo wa madaraka. Labda. Lakini tusisahau kwamba viongozi wetu wametumia ubabe hata katika kukiuka mambo ambayo yako wazi kwenye katiba. Mtu ambaye ni mbabe wa kukiuka katiba iliyopo kwa kuwatumia Polisi, Wakurugenzi, Wakuu wa wilaya/Mikoa na Usalama wa Taifa katika kuingilia uchaguzi na kuufanya usiwe huru na haki, hawezi kuacha kufanya hivyo kwa sababu kuna Katiba mpya.

Kwa hiyo watu wasijikite kwenye suala la katiba mpya peke yake kama wanataka mabadiliko hapa nchini. Kuna njia nyingi za kumchuna mbuzi ili aliwe kitoweo.


Ulipaswa kutumia muda kidgo kufatilia haya.

Pia mwisho rejea kauli ya Nyerere "kwa Katiba hii tukioata rais wa ajabu hatuta pona"
 
Mkuu, unapingana na kilichoandikwa hapa?
Hata Diallo alikiongelea hicho! Hata katiba iwe nzuri kiasi gani, mtawala anaweza kuikanyaga tu!
Kule Zenji kulikuwa na Tume huru, lakini CCM kwa kumtumia Jecha, akafanya yake. Alifanywa nini? Nakubalina na mleta uzi huu, kwa 100%.
Ukiona hivo ujue sio katiba hio. Katiba inaruhusu watu kuhoji au kushtaki mienendo mibaya ya serikali. Na mahakama zote ni huru. Taasisi kama ya uchaguzi ni huru n.k.
 
Mkuu, unapingana na kilichoandikwa hapa?
Hata Diallo alikiongelea hicho! Hata katiba iwe nzuri kiasi gani, mtawala anaweza kuikanyaga tu!
Kule Zenji kulikuwa na Tume huru, lakini CCM kwa kumtumia Jecha, akafanya yake. Alifanywa nini? Nakubalina na mleta uzi huu, kwa 100%.
Zanzibar ni koloni ulishawahi kuona wapi koloni likajiamulia mambo yake ?
 
Katiba lazima itengeneze mifumo ya kujilinda ili asitokee mhuni kufanya uhuni wake.
 


Ulipaswa kutumia muda kidgo kufatilia haya.

Pia mwisho rejea kauli ya Nyerere "kwa Katiba hii tukioata rais wa ajabu hatuta pona"

Hapa Magufuli alijibu nje kabisa ya swali.

Ni sawa na kuwaambia majaji wasisafiri kwenda kwenye kesi za mikoani kwa ajili ya kubana matumizi, halafu useme sijaingilia uhuru wa Mahakama
 
Katiba inahusika sana Mkuu. Hawa wanavunja katiba hadharani lakini katiba husika iko kimya kuhusu adhabu za hawa wahuni ambao wanajua wanachokifanya ni kinyume na katiba lakini hawana woga kwa kujua mapungufu makubwa ya katiba husika ambayo ni lazima yaondolewe kwenye katiba mpya.
Sina tatizo na suala la kuwa na Katiba mpya, lakini tatizo langu ni kuona watu wakidhani Katiba mpya ndio suluhisho la matatizo ya kisiasa nchini. Huko ni kupotoka. Nchi kama Marekani wana katiba ya kidemokrasia sana, lakini leo wanalia Trump na kundi lake kufanya mambo kihuni tu na kwa mabavu. Na hata wanatumia katiba hiyohiyo ya USA kuvuruga demokrasia ya Marekani.

Kwa hiyo tusidhani kwamba tatizo la kukosekana haki na usawa kwa vyama vya upinzani nchini liko kwenye katiba, hapana. Tatizo ni matumizi mabaya ya madaraka na ubabe tu wa wale wanaokuwa katika uongozi. Tatizo ni kiburi na ulevi tu wa madaraka.

Suala la kujiuliza ni kama uwepo wa Katiba mpya utazuia ubabe na ulevi huo wa madaraka. Labda. Lakini tusisahau kwamba viongozi wetu wametumia ubabe hata katika kukiuka mambo ambayo yako wazi kwenye katiba. Mtu ambaye ni mbabe wa kukiuka katiba iliyopo kwa kuwatumia Polisi, Wakurugenzi, Wakuu wa wilaya/Mikoa na Usalama wa Taifa katika kuingilia uchaguzi na kuufanya usiwe huru na haki, hawezi kuacha kufanya hivyo kwa sababu kuna Katiba mpya. Na hawaingilii uchaguzi kwa kuwa Katiba iliyopo inawapa mamlaka ya kuingilia uchaguzi.

Kwa hiyo watu wasijikite kwenye suala la katiba mpya peke yake kama wanataka mabadiliko hapa nchini. Kuna njia nyingi za kumchuna mbuzi ili aliwe kitoweo.
 
Katiba inahusika sana Mkuu. Hawa wanavunja katiba hadharani lakini katiba husika iko kimya kuhusu adhabu za hawa wahuni ambao wanajua wanachokifanya ni kinyume na katiba lakini hawana woga kwa kujua mapungufu makubwa ya katiba husika ambayo ni lazima yaondolewe kwenye katiba mpya.
Sawa kabisa, nakuunga mkono. Lakini hoja yangu ni kwamba, Katiba mpya sio suluhisho la tatizo la kuvunja Katiba ya sasa au uongozi wa kimabavu na ulevi wa madaraka!

Hadi sasa kilichobadilika ni vyama vingi tu, na hatuwezi kusema tatizo kubwa la Katiba iliyopo ni jinsi inavyoshughulika na uwepo wa vyama vingi
 
Hapa Magufuli alijibu nje kabisa ya swali.

Ni sawa na kuwaambia majaji wasisafiri kwenda kwenye kesi za mikoani kwa ajili ya kubana matumizi, halafu useme sijaingilia uhuru wa Mahakama
Hapa ungepita kwanza hakuna ulichoeleza!!
 
Back
Top Bottom