Polisi yakiri kumshikilia Kada wa CHADEMA Kombo aliyedaiwa kutoweka kwa siku 29!

Polisi yakiri kumshikilia Kada wa CHADEMA Kombo aliyedaiwa kutoweka kwa siku 29!

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
1720962506555.png

Zikiwa zimepita siku 29 tangu kada wa Chadema, wilayani Handeni mkoani Tanga, Kombo Mbwana (29) adaiwe kupotea, hatimaye leo Julai 14, 2024 Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Zacharia Bernard amesema wanamshikilia kwa tuhuma za makosa ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi Julai 14, 2024 Kaimu kamanda Benard amesema mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia vifaa vya kielektroniki pamoja na laini za simu za mitandao mbalimbali zisizo na usajili wake katika kutekeleza uhalifu huo kinyume cha sheria za nchi.

Pia soma:
Mke wa Kombo alivyosimulia jinsi Kombo alivyotekwa na watu wasiyojulikana na juhudi zilizofanyika kumtafuta Julai 2, 2024

Amesema upelelezi wa matukio hayo umefikia hatua nzuri na wakati wowote mtuhumiwa atafikishwa mahakamani. Anadaiwa kutenda makosa hayo kwenye mikoa tofauti na kuongeza Jeshi hilo linatoa wito kwa wananchi kuacha kujihusisha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ambayo ni kosa kisheria.

1720963945517.png

Kombo Mbwana

Hata hivyo, Julai 2, 2024 Mwananchi lilimtafuta Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Albert Msando kuhusu madai hayo ya kupotea kwa Kombo ambapo alisema tukio hilo lipo kwenye uchunguzi chini ya Jeshi la Polisi na amewaomba wanafamilia na wananchi kuwa watulivu wakati Serikali ikilishughulikia.

“Serikali haijawahi kushindwa jambo, nawaomba tuwe watulivu,” alisema Msando.
 

Zikiwa zimepita siku 29 tangu kada wa Chadema, wilayani Handeni mkoani Tanga, Kombo Mbwana (29) adaiwe kupotea, hatimaye leo Julai 14, 2024 Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Zacharia Bernard amesema wanamshikilia kwa tuhuma za makosa ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi Julai 14, 2024 Kaimu kamanda Benard amesema mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia vifaa vya kielektroniki pamoja na laini za simu za mitandao mbalimbali zisizo na usajili wake katika kutekeleza uhalifu huo kinyume cha sheria za nchi.

Hata hivyo, Julai 2, 2024 Mwananchi lilimtafuta Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Albert Msando kuhusu madai hayo ya kupotea kwa Kombo ambapo alisema tukio hilo lipo kwenye uchunguzi chini ya Jeshi la Polisi na amewaomba wanafamilia na wananchi kuwa watulivu wakati Serikali ikilishughulikia.

“Serikali haijawahi kushindwa jambo, nawaomba tuwe watulivu,” alisema Msando.
nadhani ni baada ya mtoa maelekezo kutumbuliwa na kupangiwa kazi nyingine. polisi hawawezi kuteka watu bila DG wa teeth. samia kastuka mapema sana kaona upunguani wa jiwe umerudishwa ameamua kuadjust watu wake manake wanamuaibisha. nina uhakika issue ya sativa maza hakuifurahia, either kuona amepona kifo au kuona ametekwa na kuaibika ndio maana aliamua kumchangia hadi pesa.
 
Zikiwa zimepita siku 29 tangu kada wa Chadema, wilayani Handeni mkoani Tanga, Kombo Mbwana (29) adaiwe kupotea, hatimaye leo Julai 14, 2024 Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Zacharia Bernard amesema wanamshikilia kwa tuhuma za makosa ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

GScuJnsXwAA9Lkn.jpg

Sijaelewa!! Watu wametoa taarifa police juu ya kutekwa kwa mtu! Then police walikanusha!! Kibaya zaidi ukamataji wake haukufuata Sheria. Alaf siku zote mtu hapelekwi mahakamani ! Mbona mnatufanya tukose imani na jeshi la police ? Huu ndio utaratibu Sasa wa kukamata watu?
 

Zikiwa zimepita siku 29 tangu kada wa Chadema, wilayani Handeni mkoani Tanga, Kombo Mbwana (29) adaiwe kupotea, hatimaye leo Julai 14, 2024 Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Zacharia Bernard amesema wanamshikilia kwa tuhuma za makosa ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi Julai 14, 2024 Kaimu kamanda Benard amesema mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia vifaa vya kielektroniki pamoja na laini za simu za mitandao mbalimbali zisizo na usajili wake katika kutekeleza uhalifu huo kinyume cha sheria za nchi.

Hata hivyo, Julai 2, 2024 Mwananchi lilimtafuta Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Albert Msando kuhusu madai hayo ya kupotea kwa Kombo ambapo alisema tukio hilo lipo kwenye uchunguzi chini ya Jeshi la Polisi na amewaomba wanafamilia na wananchi kuwa watulivu wakati Serikali ikilishughulikia.

“Serikali haijawahi kushindwa jambo, nawaomba tuwe watulivu,” alisema Msando.
Hii habari imethibitishwa ni ukweli?
 
Back
Top Bottom