Polisi yazuia maandamano ya ACT Wazalendo

Polisi yazuia maandamano ya ACT Wazalendo

Nawapongeza ACT na Nondo Kwa kudiriki kuandamana ingawa Kuna watu wabupinzani wanaAMINI ni staged.

Ngoja tusubiri maandamano ya chama kikuu Cha upinzani kikiongozwa na Lissu kuwataka walioguswa na Ripoti ya cag wakae pembeni Ili uchunguzi wa kurudisha pesa zetu uendelee.
 
Hilo halibadilishi udikteta WA MAGUFULI. Mbona enzi ya jakaya maandamano mengi tu yalizuiwa. Mkuu MAGUFULI alikuwa DIKTETA Tena hatari kusini mwa jangwa la sahara
Udikteta wa Magufuli ni kuwatumbua vyeti feki, wakwepa kodi, wadhulumaji, mafisadi, wezi, walamba asali, majizi, wauza ngada
 
Safi sana watu wafate utaratibu ndio msingi w sheria.
Wamekosa kazi tutawapatia kazi
 
Nawapongeza ACT na Nondo Kwa kudiriki kuandamana ingawa Kuna watu wabupinzani wanaAMINI ni staged.

Ngoja tusubiri maandamano ya chama kikuu Cha upinzani kikiongozwa na Lissu kuwataka walioguswa na Ripoti ya cag wakae pembeni Ili uchunguzi wa kurudisha pesa zetu uendelee.
ACT si mnajionaga ni chama kikuu cha upinzani? Hivi kweli polisi wanakuwa wengi kuliko waandamanaji halafu useme una chama hapo? chadema itakuja mpango mkakati wa nn kifanyike na sio maandamano... Level ya maandamàno walishaivuka

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
 
Lakini kuwawajibisha wezi wa fedha za umma kunakosababisha maisha kuzidi kuwa magumu kwa "wanyonge" sio kipaumbele?
Wao kipaombele chao nikuwawajibisha wezi wakuku ili iwe fundisho kwa wengine. Kwao hawataki iwe fundisho
 
Act c mnajionaga ni chama kikuu cha upinzani??? Hv kweli polisi wanakuwa wengi kuliko waandamanaji alafu useme una chama hapo??? chadema itakuja mpango mkakati wa nn kifanyike na sio maandamano... Level ya maandamàno walishaivuka

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
Mkakati huo kabambe una baraka za wananchi?

Au una baraka ya the So called "Maridhiano"?
 
Nawapongeza ACT na Nondo Kwa kudiriki kuandamana ingawa Kuna watu wabupinzani wanaAMINI ni staged.

Ngoja tusubiri maandamano ya chama kikuu Cha upinzani kikiongozwa na Lissu kuwataka walioguswa na Ripoti ya cag wakae pembeni Ili uchunguzi wa kurudisha pesa zetu uendelee.
Bravo ACT Wazalendo!!
 
Yaani kabisa, walitegemea wanaandamana mpaka ikulu? Hata adabu hawana....who can allow such nonsense. Kila mtu akiruhusiwa kuandamana kwenda Ikulu heshima ya ikulu itakuwaje. Mambo ya kutazama kwenye movie wanadhani ni uhalisia
Heshima ipo hiyo unayoizungumzia ilhali wakwepa Kodi wakuu na wahuni wanakwenda kula futari huko??

Hapo palikuwa na heshima yake miaka ya 60-84 ila sio Sasa.
 
Mimi thread zangu ni check an balance kati ya awamu ya sita na ile ya tano,leo ngome ya vijana ya Act wazalendo ilipanga kufanya maandamano hadi ikulu kwa mama yao kipenzi rafiki wa demokrasia, diplomasia na maendeleo aliyekuja kuwapa uhuru walio ukosa kwa miaka sita ya Magufuli.

Wamekutana na na kukabiliana na polisi wakiwa bado eneo la ofisi zao , polisi walijihami kwa siraha , mabomu ,virungu na pingu wakawambia wasithubutu kuvuka eneo lao,yako wapi ya kusema Magufuli alikuwa dikiteta

USSR View attachment 2591863

===
Dar es Salaam, Tanzania - Maandamano ya amani yaliyokuwa yakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Ngome ya Vijana, Abdul Nondo, kuelekea Ikulu kwa Rais Samia Suluhu Hassan, yamekabiliwa na zuio la polisi katika ofisi za chama hicho zilizopo Magomeni Jijini Dar es Salaam leo.

Maandamano hayo yaliyoandaliwa na vijana wa ACT yalilenga kuonesha hisia zao dhidi ya wabadhirifu wa fedha za umma waliotajwa kwenye ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Abdul Nondo, aliongoza maandamano hayo akiwa na vijana wengine.

Hii ni mara ya kwanza kwa vijana wa ACT kufanya maandamano ya aina hii, na tukio hili limezua mjadala mkubwa katika jamii kuhusu suala la ufisadi na uwajibikaji wa watumishi wa umma. Rais Samia Suluhu Hassan hajatoa tamko lolote kuhusu maandamano hayo hadi sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app

CAG ni kama wakaguzi wengine.wanapotoa ripoti ya ukaguzi haimanishi kuwa kila kilichoandikwa mule ni ukweli mtupu.zile ni hoja ambazo zinatakiwa kujibiwa .so kusema eti hasara ya wizi ule ni zaidi ya trillion 30 siyo kweli.subirini wahusika wajibu hoja then ndipo tuandamane.sawaaa???/
 
maandamano ya Ngome ya Vijana wa ACT-Walendo yakishindwa kufanyika, Mwenyekiti wa Ngome hiyo Abdul Nondo amesema wanajipanga kufanya maandamano siku nyingine.

Nondo amesema maandamano hayo ya amani yalipangwa kuanzia Manzese hadi Ikulu kuonana na Rais Samia Suluhu Hasaan na kumfikishia ujumbe wa kutokukubaliana na ubadhilifu wa fedha za umma uliofanywa, kwa mujibu wa ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) ya kila mwaka.

Aprili 5 Mwaka huu, (CAG), Charles Kichele aliwasilisha ripoti yake mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan ikionyesha ubadhilifu wa mali za umma kiasi cha kuwaibua wananchi wanaotaka hatua stahiki zichukuliwe.
 
Huyu zitto kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo si kila siku wewe na majuha wenzio mnasema amelambishwa asali? Leo kawa mwema????
Unafiki jambo baya sana! Yaani kulwa jilala umepandisha uzi bila kumnanga zitto seriously?
 
Huyu zitto kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo si kila siku wewe na majuha wenzio mnasema amelambishwa asali? Leo kawa mwema????
Unafiki jambo baya sana! Yaani kulwa jilala umepandisha uzi bila kumnanga zitto seriously?
 
Back
Top Bottom