Pongezi kwa CDF Jenerali Venance Salvatory Mabeyo

Pongezi kwa CDF Jenerali Venance Salvatory Mabeyo

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
Salaam

Kwanza nikiri wazi kwamba mimi sio mwanajeshi kuweza kuufahamu utendaji wa ndani kabisa wa CDF wetu wa JMT lakini kwa jicho la nje ningependa kutoa pongezi nyingi kwake kwa utendaji na uzalendo uliotukuka.

Mbali na utendaji wake ndani ya jeshi, Kiongozi huyu ameonekana sehemu mbali mbali akitoa mchango wake katika jamii katika kuhakikisha ustawi wa kifikra, kiuchumi,na maendeleo ya jamii kiujumla.

Kwa namna hii ya viongozi kujishusha na kuwa karibu zaidi na wananchi na kuweza kusaidia pale ambapo anahisi kwa kadri ya uwezo wake na nafasi aliyonayo anaweza kutoa msaada ni jambo la mfano na kuigwa na kiongozi yeyote. Na huu ni mfano Bora katika jamii.

Mbali na nafasi kubwa aliyonayo, Jenerali Mabeyo pia amekuwa akishiriki katika harambee mbalimbali kama ujenzi wa vituo vya watoto yatima, shule,mahospitali n.k

Pia Jenerali Mabeyo ameandika vitabu vingi ambavyo kwa namna moja ama nyingine vimekuwa na mchango mkubwa katika kuielimisha na kuibadilisha jamii katika kuhakikisha kuwa tunakuwa na jamii bora zenye misingi imara kifikra,kimaadili na kiuchumi kwa maslahi mapana ya taifa letu kiujumla.

Binafsi kinachonifurahisha zaidi ni kwamba amekuwa akifanya na kushiriki haya yote nje ya camera! Wala hakufanya kama wafanyavyo wanasiasa wengine kwa lengo la kujipatia umaarufu.Hakika unyenyekevu huu ni wa kipekee sana.

Kwa kiongozi wa aina hii, Sina shaka kabisa kwamba hata ndani ya jeshi la ulinzi hakika kutakuwa na mabadiliko mengi chanya na yenye tija kwa taifa.

Nimalizie kwa kumsihi na kumtia moyo Jenerali huyu, kwamba watanzania tunaona na kufurahishwa na kazi zako na tunazidi kukuombea Afya njema na maisha marefu ili uzidi kutoa mchango kwa taifa hili.

20220203_103057.jpg
20220203_115855.jpg
 
Bila Jenerali Mabeyo kusimama kidete, 'mama' asingeapishwa…. alikuwa ashaanza kusetiwa atangaze kuwa viatu havimtoshi.

Na sasa muda wa Mabeyo kustaafu ushafika lakini mama hataki kumruhusu, sijui atamwongezea muda hadi lini.!

Nafurahi ila NAOGOPA.
 
Anachanganya kazi na dini inaweza kumletea matatizo.

U Jenerali ni cheo chake kikazi, habari za Kristo ni dini yake binafsi, kwa nini anaweka U Jenerali kwenye kitabu cha Kristo, habari za imani yake binafsi?

Kwani na yeye ni Jenerali wa jina kama Jenerali Ulimwengu?
 
Anachanganya kazi na dini inaweza kumletea matatizo.

U Jenerali ni cheo chake kikazi, habari za Kristo ni dini yake binafsi, kwa nini anaweka U Jenerali kwenye kitabu cha Kristo, habari za imani yake binafsi?

Kwani na yeye ni Jenerali wa jina kama Jenerali Ulimwengu?
Acha upumbavu huo Kwan si ni cdf kweli ulitaka asiandikee
 
Anachanganya kazi na dini inaweza kumletea matatizo.

U Jenerali ni cheo chake kikazi, habari za Kristo ni dini yake binafsi, kwa nini anaweka U Jenerali kwenye kitabu cha Kristo, habari za imani yake binafsi?

Kwani na yeye ni Jenerali wa jina kama Jenerali Ulimwengu?
Mbona kawaida tu. Colombia, mexico na nchi nyngne za south america hio kitu ni kawaida kabisa. Af hata ukifuatilia utaona watu type ya Mobeyo wenye achievement kubwa jeshini au kwenye biashara wengi wana msimamo thabiti kwenye mambo yao ya kiroho( iwe dini ama issue nyngne za kiroho), na huwa wnafanikiwa zaidi na zaidi kila kukicha
 
Acha upumbavu huo Kwan si ni cdf kweli ulitaka asiandikee
Unaelewa kanuni ya kutenganisha dini na uongozi wa nchi ni nini, ina umuhimu gani, na madhara ya kutoifuata ni yapi?

Waislamu wakisema jeshi linaongozwa kwa Mfumokristo na Mkuu wa Majeshi anajinadi kidini utasema waongo?
 
Mbona kawaida tu. Colombia, mexico na nchi nyngne za south america hio kitu ni kawaida kabisa. Af hata ukifuatilia utaona watu type ya Mobeyo wenye achievement kubwa jeshini au kwenye biashara wengi wana msimamo thabiti kwenye mambo yao ya kiroho( iwe dini ama issue nyngne za kiroho), na huwa wnafanikiwa zaidi na zaidi kila kukicha
Colombia na Mexico ni nchi zenye Waislamu na Wakristo kama Tanzania?

Mkuu wa Majeshi gani wa Colombia au Mexico kaandika kitabu cha kidini na kujinadi u Jenerali wake kwenye cover la kitabu?
 
Ukiingia jeshini unapewa materials mapya ata kama una masters ubongo wako unafinyangwa upya
Ndio nimekuelewa ila elimu ya ziada ina muhimu sana,je alienda University? Maana katika biography yake naona ameishia elimu ya juu mzumbe
 
Unaelewa kanuni ya kutenganisha dini na uongozi wa nchi ni nini, ina umuhimu gani, na madhara ya kutoifuata ni yapi?

Waislamu wakisema jeshi linaongozwa kwa Mfumokristo na Mkuu wa Majeshi anajinadi kidini utasema waongo?
Acha ujuaji kwani Kuna siku alishaingia kanisani na kombati? Au alisha lishirikisha jeshi kwenye mambo ya kanisa? Yeye ni mkatoliki kama Samia alivyo Muislamu
 
Anachanganya kazi na dini inaweza kumletea matatizo.

U Jenerali ni cheo chake kikazi, habari za Kristo ni dini yake binafsi, kwa nini anaweka U Jenerali kwenye kitabu cha Kristo, habari za imani yake binafsi?

Kwani na yeye ni Jenerali wa jina kama Jenerali Ulimwengu?
Kachanganyaje dini na kazi hapo?

Kalazimisha subordinates wake wakinunue hicho kitabu chake?
 
Ndio nimekuelewa ila elimu ya ziada ina muhimu sana,je alienda University? Maana katika biography yake naona ameishia elimu ya juu mzumbe
Huko jeshini kufikia ngazi ya kuwa general huyo kashasoma kozi nyingi sana za uongozi na utawala, mahusiano na diplomasia na mambo chungu nzima ata kama una bachelor yako ya mzumbe humkuti Kwa kupambanua mambo ya kisiasa na kijamii huyo ni full cooked cake
 
Back
Top Bottom