Pongezi kwa Raia Mwema (Mtoa Taarifa) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora

Pongezi kwa Raia Mwema (Mtoa Taarifa) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora

Ameniitikia haraka na kufanyia kazi. Angeanza itifaki sijui Hadi nipitie wapi na wapi Ili aambiwe na mamlaka fulani kwa mujibu wa muundo, huyo mtoto angeshushwa porini na bus likaondoka. Amejiongeza maana wako watu huku duniani huanza na fuata itifaki hii, mwambie fulani ndiyo atuambie. Kufanya kazi kwingi kuona mengi pia. Amekuwa mwepesi kusoma sms na kupokea simu, angeweza kuwa kaiweka mbali tu, kakaa kidigitali, labda niishie hapa kwanza.
Sawa gyule, nami nakupongeza kwa kumpongeza Chacha
 
Mama yangu!

Hautakaa kamwe umtoshe kila mtu!

Ukweli wengine tumekubali kazi hii njema yako,trafiki na RC bila kumsahau raia aliyetoa taarifa.

Sasa wengine watatafuta mapungufu kwenye hili,hata usijibu hao,wewe sehemu yako umefanya na mtoto yuko salama!

Mama nakutakia jumapili njema yenye amani.
Aaamina, uko sahihi kabisa. Nadhani imetosha kama elimu nimetoa, wa kuelewa haya wa kutoelewa, Mungu ni mwema ataelewa wakati ukifika. Ngoja sasa nikapike kaugali na kisamvu changu natwanga mwenyewe😘🇹🇿
 
Ungesoma
Sheria na. 23 ya Mwaka 2002 ya Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala ambayo, imeunda Baraza la usajili wa dawa za tiba asili na kurugenzi ya tiba asili na taasisi za utafiti ungejua kuwa wote hawa wana bajeti zao zinapitishwa bungeni kutoka pato la taifa na ni washauri eneo hili, nadhani hukumu yako ingekuwa ya haki Sana.

Shida yetu wengi wetu hatujui mambo ya sheria zetu wenyewe tunapiganaga mishale tu utekelezaji ukianza tunaanza kudhani ni vitu vya mtu binafsi kumbe vya sheria zetu wenyewe na Kodi zetu wenyewe zinatenga bajeti. Nisiposema mwenyewe, nani atasema maana wanaojua ukweli huwa hawasemi alisema marehemu Ruge Mutahaba na wasiojua ukweli ndiyo wanasema. Upside down duniani humu, Majanga.

Nakutakia jumapili njema.

Nianze kwa kukushukuru mheshimiwa kwa kuchukua wakati wako kuijibu post yangu ambayo niliandika kwa nia njema.

Hii si post yangu ya kwanza kuhusiana na niyaonayo kupelekeshwa kisiasa huku maisha ya watu yakipotea bure.

Kwamba kuna sheria nzuri au mbovu zinazopelekea kupoteza maisha ya watu ambayo yangeweza kuepukika?

Kulikuwa na huu uzi humu:

Serikali ina wajibu wa kuzuia matangazo ya kibiashara ya kidini/imani kwenye vyombo vya habari kulinda raia wake

Na hii hapa ilikuwa post yangu kwenye uzi huo:

IMG_20241006_101046.jpg


Sheria nzuri au mbaya isiyotusaidia ni ya nini?

Tunakupongeza sana tu kwenye mengi mazuri unayofanya kwenye wizara hii. Laiti kungekuwa na wizara mahsusi kwa ajili ya haki, hakika ungetufaa mno huko.

Ila hii ya kuachia miti shamba, maombezi, nk kwa sababu yoyote huku watu wakiangamia; kwenye karne hii, uhalali wake uko wapi?

Misahafu inasema: "watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa."

Hii ndiyo ilikuwa hoja yangu pekee ya dhati hapa.
 
Pongezi ziwafikie raia mwema (jina kapuni) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Timu yake ya Usalama kwa ushirikiano wao jana 5 Oktoba, 2024 ambapo, Saa 9.56 jioni nilipokea ujumbe wa simu kutoka kwa raia mwema mzalendo (jina kapuni) kuwa kwenye gari la abiria (bus) linalojulikana kama Kisbo lenye namba za usajili T408EFH lililokuwa linatokea Kahama kuelekea Dar es Salaam kulikuwa na abiria binti mdogo aliyekuwa akilia na kuhangaika kwamba ateremshwe maana hajui anakoenda na amepakiwa tu kwenye gari na mtu ambaye hakusafiri naye.

Mara baada ya kupokea taarifa hizi, niliwasiliana na Mheshimiwa Paul Chacha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili afahamu na kuchukua hatua zake ambapo, mara moja alichukua hatua za kuwaelekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua na kufikia majira ya saa 10.30 jioni bus hilo likiwa ndiyo linaingia stendi ya Nzega lilisimamishwa na kukaguliwa na Askari wakiwa na Mhe Mkuu wa Mkoa na binti huyo kubainiwa na mahojiano stahiki kufanyika. Pia rejea video fupi ya Mhe Mkuu wa Mkoa wa Tabora hapa chini.

Binti huyo sasa yuko mikono salama chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora huku hatua zaidi za kubaini kisa mkasa zikiendelea.

PONGEZI; narudia tena kutoa Pongezi kwa raia mwema aliyejali na kuthubutu kutoa taarifa kwa kunitumia ujumbe huo. Hakika mlinzi wa kwanza wa jamii ni jamii yenyewe. Pongezi ziende kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa wepesi wake kwenye kuitikia taarifa niliyompa na kuchukua hatua mara moja. Pongezi kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora kwa kutekeleza jukumu lao kikamilifu na kumuokoa binti huyu mdogo na kwa hatua wanazoendelea nazo.

WITO KWA JAMII; tuendelee kushirikiana kwenye kubaini na kutoa taarifa za matukio ambayo hayaeleweki na yanaleta maswali kwenye maisha ya jamii kila siku kwani, ni kwa jamii kuwa macho na kutoa ushirikiano ndiyo tunaweza kuwadhibiti wafanya uovu kwa watoto wetu kabla ya kutimiza nia zao ovu.

WITO KWA WAHUDUMU WA USAFIRI; kuwa makini na abiria hususan watoto wadogo wanaopakizwa kwa maelekezo kuwa huko waendako watapokelewa na mtu fulani kwani, tunaishi kwenye nyakati ambazo watoto ni wahanga wakubwa wa ukatili mbalimbali ikiwemo kutoroshwa na kwenda kutumikishwa kinyume na umri wao. Jumapili njema kwenu wote🇹🇿
Hongera sana mheshimiwa waziri kwa hili jambo la kumuokoa huyo binti!

Nafikiri kuna haja kubwa sana ya kutoa elimu endelevu kwa jamii kuhusu haya mambo ya haki na ulinzi wa watoto hasa kupitia vyombo vya habari (radio, television) ili ujumbe na elimu iwafikie walioko vijijini.
 
Niweke wazi bandiko langu kuhusu ukak

Nianze kwa kukushukuru mheshimiwa kwa kuchukua wakati wako kuijibu post yangu ambayo niliandika kwa nia njema.

Hii si post yangu ya kwanza kuhusiana na niyaonayo kupelekeshwa kisiasa huku maisha ya watu yakipotea bure.

Kwamba kuna sheria nzuri au mbovu zinazopelekea kupoteza maisha ya watu ambayo yangeweza kuepukika?

Kulikuwa na huu uzi humu:

Serikali ina wajibu wa kuzuia matangazo ya kibiashara ya kidini/imani kwenye vyombo vya habari kulinda raia wake

Na hii hapa ilikuwa post yangu kwenye uzi huo:

View attachment 3116612

Sheria nzuri au mbaya isiyotusaidia ni ya nini?

Tunakupongeza sana tu kwenye mengi mazuri unayofanya kwenye wizara hii. Laiti kungekuwa na wizara mahsusi kwa ajili ya haki, hakika ungetufaa mno huko.

Ila hii ya kuachia miti shamba, maombezi, nk kwa sababu yoyote huku watu wakiangamia; hata wewe mheshimiwa, kwenye karne hii, uhalali wake uko wapi?

Misahafu inasema: "watu wangu wanaangamia kwa kukosa maalifa."

Hii ndiyo ilikuwa hoja yangu pekee ya dhati hapa.
Kwanza ahsante Sana kwa kupokea chanya, haya ndiyo majadiliano yenye afya kwa ajili ya kujenga na siyo kubomoa. Uzuri mimi huwa pia Niko positive tu na napenda watu critical lakini critical chanya ya hoja. Kwanza ilikuwa vema tu ijulikane kuwa, tiba asili hiyo ya kujifukiza haikuwa ajenda yangu binafsi kwamba niliichukua bidhaa hizo private Bali ijulikane ni Mali ya baraza letu la tiba asili na ndiyo maana siku ile kulikuwa na mkurugenzi mwenyewe mtaalamu wa tiba asili pale ambaye naye ni Daktari pia na maafisa wengine. Wanatakiwa siku moja nao watoe elimu kuhusu utekelezaji huu wa kisheria.

Kuhusu Hawa waombeaji matapeli, mbona hata mimi nimeshiriki kwenye hatua za kufikia wengi tu leseni zao kufutwa ? Ila tu labda mambo mengi siweki online au watanzania ni wasahaulifu. La yule anajiita mungu kule Kanda ya ziwa nimeshiriki, la huyu kiboko ya washirikina, nimeshiriki, mambo ni mengi, vigumu kuanzisha. Sasa ukipata muda uka share moja tu watu baadhi wanadhani ni hilo hilo tu 🥲

Hawa wabeba nyoka nao mbona nimepambana nao tu.

Anyway, Raha ya uongozi ni ufanye kwa dhati halafu ulaumiwe ilimradi tu, moyo wako ushuhudie vinginevyo na kuungoja wakati useme.
 
Hili tukio limetengenezwa!
Mkuu wa wilaya ya Nzega alikuwa wapi wakati bus linapita nzega?
RC Tabora ofisi yake iko tabora mjini au ipo nzega?
Je Kuna umbali Gani tangu tabora mjini hadi Nzega?
 
Hili tukio limetengenezwa!
Mkuu wa wilaya ya Nzega alikuwa wapi wakati bus linapita nzega?
RC Tabora ofisi yake iko tabora mjini au ipo nzega?
Je Kuna umbali Gani tangu tabora mjini hadi Nzega?
Swali zuri. Mkuu wa Mkoa alikuwa ziara nzega, Mimi nilikuwa Dar, mtoa taarifa alikuwa kwenye gari. Bahati nzuri simu nilikuwa nayo mkononi najibu sms za watanzania. Kwa ngazi yangu mimi ilikuwa nianze na mkuu wa mkoa kwanza na ningemkosa ningeshuka wilayani Hadi kwa OCD ningefika. Ningekosa hata mtendaji wa Kijiji ningefika.

Kuna swali lingine?

Ila je na la morogoro juzi kuhusu msichana kusafirishwa kwenye happy nation bus akiwa amefungwa kamba ambalo alitoa taarifa Maria Sarungi huko x nikalipokea nikapiga mkoa wa Dodoma na Morogoro wapige stop gari hilo na Binti akabainiwa na kupelekwa hospitali, hili nalo alitengeneza nani?
 
Swali zuri. Mkuu wa Mkoa alikuwa ziara nzega, Mimi nilikuwa Dar, mtoa taarifa alikuwa kwenye gari. Bahati nzuri simu nilikuwa nayo mkononi najibu sms za watanzania. Kwa ngazi yangu mimi ilikuwa nianze na mkuu wa mkoa kwanza na ningemkosa ningeshuka wilayani Hadi kwa OCD ningefika. Ningekosa hata mtendaji wa Kijiji ningefika.

Kuna swali lingine?

Ila je na la morogoro juzi kuhusu msichana kusafirishwa kwenye happy nation bus akiwa amefungwa kamba ambalo alitoa taarifa Maria Sarungi huko x nikalipokea nikapiga mkoa wa Dodoma na Morogoro wapige stop gari hilo na Binti akabainiwa na kupelekwa hospitali, hili nalo alitengeneza nani?
Kwanini hakushirikisha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Nzega?

Je likitokea tukio kama hilo lotasubiri mkuu wa mkoa wakati mkuu wa wilaya Yuko eneo la tukio?

Kwahiyo unataka kuniambia RC alifanya kazi hiyo na OCD wa Nzega au na RPC wa nzega?

Nikikuambia kuwa DC Nzega ni Ke ,na RC hamtaki kwa sababu Fulani utakataa?
 
Pongezi ziwafikie raia mwema (jina kapuni) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Timu yake ya Usalama kwa ushirikiano wao jana 5 Oktoba, 2024 ambapo, Saa 9.56 jioni nilipokea ujumbe wa simu kutoka kwa raia mwema mzalendo (jina kapuni) kuwa kwenye gari la abiria (bus) linalojulikana kama Kisbo lenye namba za usajili T408EFH lililokuwa linatokea Kahama kuelekea Dar es Salaam kulikuwa na abiria binti mdogo aliyekuwa akilia na kuhangaika kwamba ateremshwe maana hajui anakoenda na amepakiwa tu kwenye gari na mtu ambaye hakusafiri naye.

Mara baada ya kupokea taarifa hizi, niliwasiliana na Mheshimiwa Paul Chacha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili afahamu na kuchukua hatua zake ambapo, mara moja alichukua hatua za kuwaelekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua na kufikia majira ya saa 10.30 jioni bus hilo likiwa ndiyo linaingia stendi ya Nzega lilisimamishwa na kukaguliwa na Askari wakiwa na Mhe Mkuu wa Mkoa na binti huyo kubainiwa na mahojiano stahiki kufanyika. Pia rejea video fupi ya Mhe Mkuu wa Mkoa wa Tabora hapa chini.

Binti huyo sasa yuko mikono salama chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora huku hatua zaidi za kubaini kisa mkasa zikiendelea.

PONGEZI; narudia tena kutoa Pongezi kwa raia mwema aliyejali na kuthubutu kutoa taarifa kwa kunitumia ujumbe huo. Hakika mlinzi wa kwanza wa jamii ni jamii yenyewe. Pongezi ziende kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa wepesi wake kwenye kuitikia taarifa niliyompa na kuchukua hatua mara moja. Pongezi kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora kwa kutekeleza jukumu lao kikamilifu na kumuokoa binti huyu mdogo na kwa hatua wanazoendelea nazo.

WITO KWA JAMII; tuendelee kushirikiana kwenye kubaini na kutoa taarifa za matukio ambayo hayaeleweki na yanaleta maswali kwenye maisha ya jamii kila siku kwani, ni kwa jamii kuwa macho na kutoa ushirikiano ndiyo tunaweza kuwadhibiti wafanya uovu kwa watoto wetu kabla ya kutimiza nia zao ovu.

WITO KWA WAHUDUMU WA USAFIRI; kuwa makini na abiria hususan watoto wadogo wanaopakizwa kwa maelekezo kuwa huko waendako watapokelewa na mtu fulani kwani, tunaishi kwenye nyakati ambazo watoto ni wahanga wakubwa wa ukatili mbalimbali ikiwemo kutoroshwa na kwenda kutumikishwa kinyume na umri wao. Jumapili njema kwenu wote🇹🇿
Shikamoo Mama yetu mpendwa sana. Mimi binafsi nakupongeza sana kwa kazi nzuri unazofanya. Ili tuweze kuendeleza kazi hii nzuri naomba namba yako.
 
Kwanini hakushirikisha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Nzega?

Je likitokea tukio kama hilo lotasubiri mkuu wa mkoa wakati mkuu wa wilaya Yuko eneo la tukio?

Kwahiyo unataka kuniambia RC alifanya kazi hiyo na OCD wa Nzega au na RPC wa nzega?

Nikikuambia kuwa DC Nzega ni Ke ,na RC hamtaki kwa sababu Fulani utakataa?
Ni sawa na mimi uniletee changamoto hapa ya kijamii nikuambie kuwa, kwa nini huko uliko hujashirikisha mtendaji wako wa serikali za mtaa wako wakati hilo jambo ni la dharura na mimi nipo hapo kwenye access yako. Mfano mtoa taarifa ningemwambia wewe mtafute waziri wa mambo ya Ndani mwenye trafiki kisha mtafute wa Tamisemi mwenye wakuu wa mikoa halafu mtafute na wa uchukuzi? Hapo ndiyo tunaokoa mtoto na dharura zake?

Nimesema, nilipopokea hilo jambo, nilimtafuta kwanza mkuu wa mkoa, ningemkosa ningeshuka chini kwa mkuu wa wilaya. Bahati nzuri mkuu wa mkoa alikuwa ziara nzega, na si ajabu walikuwa wote na mkuu wake wa wilaya, ndiyo wakaenda hapo.

Ni sawa na kuuliza mfano ningemtafuta mkuu wa wilaya Bahatu nzuri nikampata, si ungejiuliza mbona hakuanza na mkuu wa mkoa?

Unaweza kuteremsha mguu ngazi ya nne chini kabla ya walau kukanyaga ya tatu? Uongozi ni itifaki na pia kuna mazingira ya dharura ambapo itifaki hukaa pembeni kwanza kutegemeana na scene. Sawa au kuna swali bado ndugu yangu🇹🇿
 
Kwanini hakushirikisha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Nzega?

Je likitokea tukio kama hilo lotasubiri mkuu wa mkoa wakati mkuu wa wilaya Yuko eneo la tukio?

Kwahiyo unataka kuniambia RC alifanya kazi hiyo na OCD wa Nzega au na RPC wa nzega?

Nikikuambia kuwa DC Nzega ni Ke ,na RC hamtaki kwa sababu Fulani utakataa?
Ni sawa na mimi uniletee changamoto hapa ya kijamii nikuambie kuwa, kwa nini huko uliko hujashirikisha mtendaji wako wa serikali za mtaa wako wakati hilo jambo ni la dharura na mimi nipo hapo kwenye access yako.

Nimesema, nilipopokea hilo jambo, nilimtafuta kwanza mkuu wa mkoa, ningemkosa ningeshuka chini kwa mkuu wa wilaya. Bahati nzuri mkuu wa mkoa alikuwa ziara nzega, na si ajabu walikuwa wote na mkuu wake wa wilaya, ndiyo wakaenda hapo.

Kwa upande mwingine pia, ni sawa na kuuliza mfano ningemtafuta mkuu wa wilaya Bahati nzuri nikampata, si ungejiuliza mbona hakuanza na mkuu wa mkoa?

Hivi unaweza kuteremsha mguu ngazi ya nne chini kabla ya walau kukanyaga ya tatu? Uongozi ni itifaki na pia kuna mazingira ya dharura ambapo itifaki hukaa pembeni kwanza kitegemeana na scene. Husika.
 
Pongezi ziwafikie raia mwema (jina kapuni) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Timu yake ya Usalama kwa ushirikiano wao jana 5 Oktoba, 2024 ambapo, Saa 9.56 jioni nilipokea ujumbe wa simu kutoka kwa raia mwema mzalendo (jina kapuni) kuwa kwenye gari la abiria (bus) linalojulikana kama Kisbo lenye namba za usajili T408EFH lililokuwa linatokea Kahama kuelekea Dar es Salaam kulikuwa na abiria binti mdogo aliyekuwa akilia na kuhangaika kwamba ateremshwe maana hajui anakoenda na amepakiwa tu kwenye gari na mtu ambaye hakusafiri naye.

Mara baada ya kupokea taarifa hizi, niliwasiliana na Mheshimiwa Paul Chacha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili afahamu na kuchukua hatua zake ambapo, mara moja alichukua hatua za kuwaelekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua na kufikia majira ya saa 10.30 jioni bus hilo likiwa ndiyo linaingia stendi ya Nzega lilisimamishwa na kukaguliwa na Askari wakiwa na Mhe Mkuu wa Mkoa na binti huyo kubainiwa na mahojiano stahiki kufanyika. Pia rejea video fupi ya Mhe Mkuu wa Mkoa wa Tabora hapa chini.

Binti huyo sasa yuko mikono salama chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora huku hatua zaidi za kubaini kisa mkasa zikiendelea.

PONGEZI; narudia tena kutoa Pongezi kwa raia mwema aliyejali na kuthubutu kutoa taarifa kwa kunitumia ujumbe huo. Hakika mlinzi wa kwanza wa jamii ni jamii yenyewe. Pongezi ziende kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa wepesi wake kwenye kuitikia taarifa niliyompa na kuchukua hatua mara moja. Pongezi kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora kwa kutekeleza jukumu lao kikamilifu na kumuokoa binti huyu mdogo na kwa hatua wanazoendelea nazo.

WITO KWA JAMII; tuendelee kushirikiana kwenye kubaini na kutoa taarifa za matukio ambayo hayaeleweki na yanaleta maswali kwenye maisha ya jamii kila siku kwani, ni kwa jamii kuwa macho na kutoa ushirikiano ndiyo tunaweza kuwadhibiti wafanya uovu kwa watoto wetu kabla ya kutimiza nia zao ovu.

WITO KWA WAHUDUMU WA USAFIRI; kuwa makini na abiria hususan watoto wadogo wanaopakizwa kwa maelekezo kuwa huko waendako watapokelewa na mtu fulani kwani, tunaishi kwenye nyakati ambazo watoto ni wahanga wakubwa wa ukatili mbalimbali ikiwemo kutoroshwa na kwenda kutumikishwa kinyume na umri wao. Jumapili njema kwenu wote🇹🇿
Kwa wanao mfahamu Paul chacha ni mchapakazi ,msikivu,mnyenyekevu,muungwana Sana, anasaidia ame saidia watu wengi Sana anao wajua na asio wajua pia hongeraaaa sanaa kwako muheshimiwa wazir gwajima.
 
Shikamoo Mama yetu mpendwa sana. Mimi binafsi nakupongeza sana kwa kazi nzuri unazofanya. Ili tuweze kuendeleza kazi hii nzuri naomba namba yako.

Ahsante Sana kwa ushirikiano wako. Namba zangu huwa ziko hewani miaka yote nazo ni 0765345777 na copy 0734124191. Andika ujumbe usipige nitapiga mwenye ikibidi.

Za kituo cha wizara nazo zipo nitakutumia bango ukinitumia sms. Shukrani 🙏🏽
 
Pongezi ziwafikie raia mwema (jina kapuni) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Timu yake ya Usalama kwa ushirikiano wao jana 5 Oktoba, 2024 ambapo, Saa 9.56 jioni nilipokea ujumbe wa simu kutoka kwa raia mwema mzalendo (jina kapuni) kuwa kwenye gari la abiria (bus) linalojulikana kama Kisbo lenye namba za usajili T408EFH lililokuwa linatokea Kahama kuelekea Dar es Salaam kulikuwa na abiria binti mdogo aliyekuwa akilia na kuhangaika kwamba ateremshwe maana hajui anakoenda na amepakiwa tu kwenye gari na mtu ambaye hakusafiri naye.

Mara baada ya kupokea taarifa hizi, niliwasiliana na Mheshimiwa Paul Chacha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili afahamu na kuchukua hatua zake ambapo, mara moja alichukua hatua za kuwaelekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua na kufikia majira ya saa 10.30 jioni bus hilo likiwa ndiyo linaingia stendi ya Nzega lilisimamishwa na kukaguliwa na Askari wakiwa na Mhe Mkuu wa Mkoa na binti huyo kubainiwa na mahojiano stahiki kufanyika. Pia rejea video fupi ya Mhe Mkuu wa Mkoa wa Tabora hapa chini.

Binti huyo sasa yuko mikono salama chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora huku hatua zaidi za kubaini kisa mkasa zikiendelea.

PONGEZI; narudia tena kutoa Pongezi kwa raia mwema aliyejali na kuthubutu kutoa taarifa kwa kunitumia ujumbe huo. Hakika mlinzi wa kwanza wa jamii ni jamii yenyewe. Pongezi ziende kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa wepesi wake kwenye kuitikia taarifa niliyompa na kuchukua hatua mara moja. Pongezi kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora kwa kutekeleza jukumu lao kikamilifu na kumuokoa binti huyu mdogo na kwa hatua wanazoendelea nazo.

WITO KWA JAMII; tuendelee kushirikiana kwenye kubaini na kutoa taarifa za matukio ambayo hayaeleweki na yanaleta maswali kwenye maisha ya jamii kila siku kwani, ni kwa jamii kuwa macho na kutoa ushirikiano ndiyo tunaweza kuwadhibiti wafanya uovu kwa watoto wetu kabla ya kutimiza nia zao ovu.

WITO KWA WAHUDUMU WA USAFIRI; kuwa makini na abiria hususan watoto wadogo wanaopakizwa kwa maelekezo kuwa huko waendako watapokelewa na mtu fulani kwani, tunaishi kwenye nyakati ambazo watoto ni wahanga wakubwa wa ukatili mbalimbali ikiwemo kutoroshwa na kwenda kutumikishwa kinyume na umri wao. Jumapili njema kwenu wote🇹🇿
Nimeguswa na utendaji wako Shem Mhe. Dr. Doro. Hongera sana kwa jinsi unavyojitoa kuwahudumia Watanzania. Ni Mungu tuu atakulipia. Ubarikiwe sana. Salaam kwa Kaka.
P
 
Viongozi wengi WA CCM wanstengeneza matukio Ili bibi ayaone kwrnye mitandao ya kijamii.
Kwani namba za RC Tabora ziko Facebook?
Ili Kila MTU awe nazo na amtumia matukio?
Hiyo namba uliyompata nayo RC ni private number su in public number,?
Chacha tunamfahamu!
Maswali mengine siwezi kuyajibu ila nitajibu yangu haya kuwa namba zangu mimi kunitumia ujumbe ni 0734124191 na 0765345777. Halafu sifanyi kazi za maonesho kwa kuwa kutangaza namba zangu kwa umma nilianza tangu mwaka 2003 nikiwa intern bungando hospitali mwanza na nimeendelea hivyo hatua zote za utumishi wangu Hadi nitakapostaafu. Sema sikuwaga online humu.

Mwenyewe nabarikiwa kuMoyo😘

Una swali jipya?
 
Back
Top Bottom