Pongezi kwa Raia Mwema (Mtoa Taarifa) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora

Pongezi kwa Raia Mwema (Mtoa Taarifa) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora

Ni sawa na mimi uniletee changamoto hapa ya kijamii nikuambie kuwa, kwa nini huko uliko hujashirikisha mtendaji wako wa serikali za mtaa wako wakati hilo jambo ni la dharura na mimi nipo hapo kwenye access yako. Mfano mtoa taarifa ningemwambia wewe mtafute waziri wa mambo ya Ndani mwenye trafiki kisha mtafute wa Tamisemi mwenye wakuu wa mikoa halafu mtafute na wa uchukuzi? Hapo ndiyo tunaokoa mtoto na dharura zake?

Nimesema, nilipopokea hilo jambo, nilimtafuta kwanza mkuu wa mkoa, ningemkosa ningeshuka chini kwa mkuu wa wilaya. Bahati nzuri mkuu wa mkoa alikuwa ziara nzega, na si ajabu walikuwa wote na mkuu wake wa wilaya, ndiyo wakaenda hapo.

Ni sawa na kuuliza mfano ningemtafuta mkuu wa wilaya Bahatu nzuri nikampata, si ungejiuliza mbona hakuanza na mkuu wa mkoa?

Unaweza kuteremsha mguu ngazi ya nne chini kabla ya walau kukanyaga ya tatu? Uongozi ni itifaki na pia kuna mazingira ya dharura ambapo itifaki hukaa pembeni kwanza kutegemeana na scene. Sawa au kuna swali bado ndugu yangu🇹🇿
Dkt.gwajima Asante kwa ufafanuzi wako. Umefanya kazi nzurii unastahili pongezi kwa kweli.

Hongeraaaa sanaa kwa kuwepo humu jukwaani bila kificho na umekua msaada kwa wengi 🇹🇿
 
Nimeguswa na utendaji wako Shem Mhe. Dr. Doro. Hongera sana kwa jinsi unavyojitoa kuwahudumia Watanzania. Ni Mungu tuu atakulipia. Ubarikiwe sana. Salaam kwa Kaka.
P
Salaam kiongozi. Ahsante Sana. Ubarikiwe, salaam zimefika, mume wangu naye Adv. Gwajima anakusalimia🙏🏽
 
Pongezi ziwafikie raia mwema (jina kapuni) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Timu yake ya Usalama kwa ushirikiano wao jana 5 Oktoba, 2024 ambapo, Saa 9.56 jioni nilipokea ujumbe wa simu kutoka kwa raia mwema mzalendo (jina kapuni) kuwa kwenye gari la abiria (bus) linalojulikana kama Kisbo lenye namba za usajili T408EFH lililokuwa linatokea Kahama kuelekea Dar es Salaam kulikuwa na abiria binti mdogo aliyekuwa akilia na kuhangaika kwamba ateremshwe maana hajui anakoenda na amepakiwa tu kwenye gari na mtu ambaye hakusafiri naye.

Mara baada ya kupokea taarifa hizi, niliwasiliana na Mheshimiwa Paul Chacha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili afahamu na kuchukua hatua zake ambapo, mara moja alichukua hatua za kuwaelekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua na kufikia majira ya saa 10.30 jioni bus hilo likiwa ndiyo linaingia stendi ya Nzega lilisimamishwa na kukaguliwa na Askari wakiwa na Mhe Mkuu wa Mkoa na binti huyo kubainiwa na mahojiano stahiki kufanyika. Pia rejea video fupi ya Mhe Mkuu wa Mkoa wa Tabora hapa chini.

Binti huyo sasa yuko mikono salama chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora huku hatua zaidi za kubaini kisa mkasa zikiendelea.

PONGEZI; narudia tena kutoa Pongezi kwa raia mwema aliyejali na kuthubutu kutoa taarifa kwa kunitumia ujumbe huo. Hakika mlinzi wa kwanza wa jamii ni jamii yenyewe. Pongezi ziende kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa wepesi wake kwenye kuitikia taarifa niliyompa na kuchukua hatua mara moja. Pongezi kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora kwa kutekeleza jukumu lao kikamilifu na kumuokoa binti huyu mdogo na kwa hatua wanazoendelea nazo.

WITO KWA JAMII; tuendelee kushirikiana kwenye kubaini na kutoa taarifa za matukio ambayo hayaeleweki na yanaleta maswali kwenye maisha ya jamii kila siku kwani, ni kwa jamii kuwa macho na kutoa ushirikiano ndiyo tunaweza kuwadhibiti wafanya uovu kwa watoto wetu kabla ya kutimiza nia zao ovu.

WITO KWA WAHUDUMU WA USAFIRI; kuwa makini na abiria hususan watoto wadogo wanaopakizwa kwa maelekezo kuwa huko waendako watapokelewa na mtu fulani kwani, tunaishi kwenye nyakati ambazo watoto ni wahanga wakubwa wa ukatili mbalimbali ikiwemo kutoroshwa na kwenda kutumikishwa kinyume na umri wao. Jumapili njema kwenu wote🇹🇿
Pongezi pia zirudi kwako Mh Dkt. Gwajima D kwa kuchukua hatua za haraka na kwa jinsi ambavyo umekuwa ukitetea haki za wanyonge katika nchi hii.

Naomba kama hautajali nipate namba yako ili nikipata tukio lisiloeleweka nikuletee ujumbe. Ni viongozi wachache sana wenye moyo kama wako na walio tayari kutetea maslahi ya wanyonge. Mungu akubariki sana.
 
Tulikutumia ukapiga kimya, umeibukia Nzega😭
Ndiyo maana kuna mbadala pale ninapokuwa sijawahi kujibu. Tumetengeneza kabisa na simu 5 za kituo cha wizara na tumetangaza. Na pia kumbuka, wizara zote Zina mawasilino yao moja kwa moja. Na Mimi sijaja na namba zangu kutengua utaratibu rasmi bali kuongezea tu nguvu. Pai ukumbuke, admin wa simu zangu ni Mimi mwenyewe nami ni binadamu nina dharura zangu za kibinadamu kama wengine..

Hivyo, kabla ya kulaumu nikuulize, je ulichukua hatua zipi baada ya kuona kwangu kimya? Shukrani
 
Pongezi ziwafikie raia mwema (jina kapuni) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Timu yake ya Usalama kwa ushirikiano wao jana 5 Oktoba, 2024 ambapo, Saa 9.56 jioni nilipokea ujumbe wa simu kutoka kwa raia mwema mzalendo (jina kapuni) kuwa kwenye gari la abiria (bus) linalojulikana kama Kisbo lenye namba za usajili T408EFH lililokuwa linatokea Kahama kuelekea Dar es Salaam kulikuwa na abiria binti mdogo aliyekuwa akilia na kuhangaika kwamba ateremshwe maana hajui anakoenda na amepakiwa tu kwenye gari na mtu ambaye hakusafiri naye.

Mara baada ya kupokea taarifa hizi, niliwasiliana na Mheshimiwa Paul Chacha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili afahamu na kuchukua hatua zake ambapo, mara moja alichukua hatua za kuwaelekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua na kufikia majira ya saa 10.30 jioni bus hilo likiwa ndiyo linaingia stendi ya Nzega lilisimamishwa na kukaguliwa na Askari wakiwa na Mhe Mkuu wa Mkoa na binti huyo kubainiwa na mahojiano stahiki kufanyika. Pia rejea video fupi ya Mhe Mkuu wa Mkoa wa Tabora hapa chini.

Binti huyo sasa yuko mikono salama chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora huku hatua zaidi za kubaini kisa mkasa zikiendelea.

PONGEZI; narudia tena kutoa Pongezi kwa raia mwema aliyejali na kuthubutu kutoa taarifa kwa kunitumia ujumbe huo. Hakika mlinzi wa kwanza wa jamii ni jamii yenyewe. Pongezi ziende kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa wepesi wake kwenye kuitikia taarifa niliyompa na kuchukua hatua mara moja. Pongezi kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora kwa kutekeleza jukumu lao kikamilifu na kumuokoa binti huyu mdogo na kwa hatua wanazoendelea nazo.

WITO KWA JAMII; tuendelee kushirikiana kwenye kubaini na kutoa taarifa za matukio ambayo hayaeleweki na yanaleta maswali kwenye maisha ya jamii kila siku kwani, ni kwa jamii kuwa macho na kutoa ushirikiano ndiyo tunaweza kuwadhibiti wafanya uovu kwa watoto wetu kabla ya kutimiza nia zao ovu.

WITO KWA WAHUDUMU WA USAFIRI; kuwa makini na abiria hususan watoto wadogo wanaopakizwa kwa maelekezo kuwa huko waendako watapokelewa na mtu fulani kwani, tunaishi kwenye nyakati ambazo watoto ni wahanga wakubwa wa ukatili mbalimbali ikiwemo kutoroshwa na kwenda kutumikishwa kinyume na umri wao. Jumapili njema kwenu wote🇹🇿
Pongezi zaidi zikufikie wewe kwa kukubali kuwa karibu na jamii. Mwanzo nilikuwa sikuelewi lakini hv sasa kwenye list ya mawaziri 10 wanaofanya kazi zao bila makelele ya media, wewe ni wa kwanza hadi watano. Anayekufuatia yuko namba 6
 
Pongezi pia zirudi kwako Mh Dkt. Gwajima D kwa kuchukua hatua za haraka na kwa jinsi ambavyo umekuwa ukitetea haki za wanyonge katika nchi hii.

Naomba kama hautajali nipate namba yako ili nikipata tukio lisiloeleweka nikuletee ujumbe. Ni viongozi wachache sana wenye moyo kama wako na walio tayari kutetea maslahi ya wanyonge. Mungu akubariki sana.
Shukrani kwa ushirikiano wako. Namba zangu ziko wazi kwa kupokea ujumbe wa kuandika tu kama kupiga napiga mwenyewe. Nazo ni 0765345777 na copy 0734124191. Namshukuru Mungu huduma hii ninayo tangu mwaka 2003 bahati mbaya sikuwa na Majukwaa ya online. Nakushukuru kwa ushirikiano wako 🙏🏽 wape na wengine ila waambie waandike ujumbe pia watumie mifumo rasmi maana huwa napenda kwangu iwe rufaa Ili nijue pia nani hatimizi wajibu wake vema chini yangu au anatimiza vema🙏🏽

EDIT NAMBA hapo revised kulikuwa na error tpaul
 
Pongezi zaidi zikufikie wewe kwa kukubali kuwa karibu na jamii. Mwanzo nilikuwa sikuelewi lakini hv sasa kwenye list ya mawaziri 10 wanaofanya kazi zao bila makelele ya media, wewe ni wa kwanza hadi watano. Anayekufuatia yuko namba 6
Ubarikiwe tuendelee kushirikiana. Mambo Duniani humu ni mengi na mengi huwa hayaeleweki hadi wakati ufanye kazi yake. Tuendelee kushirikiana. Shukrani
 
Kwenye utekaji wa watoto wizara inajitahidi!
Watu wazima wakitekwa, ni wizara ipi tuwajulishe!
 
Pongezi ziwafikie raia mwema (jina kapuni) na Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Timu yake ya Usalama kwa ushirikiano wao jana 5 Oktoba, 2024 ambapo, Saa 9.56 jioni nilipokea ujumbe wa simu kutoka kwa raia mwema mzalendo (jina kapuni) kuwa kwenye gari la abiria (bus) linalojulikana kama Kisbo lenye namba za usajili T408EFH lililokuwa linatokea Kahama kuelekea Dar es Salaam kulikuwa na abiria binti mdogo aliyekuwa akilia na kuhangaika kwamba ateremshwe maana hajui anakoenda na amepakiwa tu kwenye gari na mtu ambaye hakusafiri naye.

Mara baada ya kupokea taarifa hizi, niliwasiliana na Mheshimiwa Paul Chacha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili afahamu na kuchukua hatua zake ambapo, mara moja alichukua hatua za kuwaelekeza Jeshi la Polisi kuchukua hatua na kufikia majira ya saa 10.30 jioni bus hilo likiwa ndiyo linaingia stendi ya Nzega lilisimamishwa na kukaguliwa na Askari wakiwa na Mhe Mkuu wa Mkoa na binti huyo kubainiwa na mahojiano stahiki kufanyika. Pia rejea video fupi ya Mhe Mkuu wa Mkoa wa Tabora hapa chini.

Binti huyo sasa yuko mikono salama chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora huku hatua zaidi za kubaini kisa mkasa zikiendelea.

PONGEZI; narudia tena kutoa Pongezi kwa raia mwema aliyejali na kuthubutu kutoa taarifa kwa kunitumia ujumbe huo. Hakika mlinzi wa kwanza wa jamii ni jamii yenyewe. Pongezi ziende kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa wepesi wake kwenye kuitikia taarifa niliyompa na kuchukua hatua mara moja. Pongezi kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora kwa kutekeleza jukumu lao kikamilifu na kumuokoa binti huyu mdogo na kwa hatua wanazoendelea nazo.

WITO KWA JAMII; tuendelee kushirikiana kwenye kubaini na kutoa taarifa za matukio ambayo hayaeleweki na yanaleta maswali kwenye maisha ya jamii kila siku kwani, ni kwa jamii kuwa macho na kutoa ushirikiano ndiyo tunaweza kuwadhibiti wafanya uovu kwa watoto wetu kabla ya kutimiza nia zao ovu.

WITO KWA WAHUDUMU WA USAFIRI; kuwa makini na abiria hususan watoto wadogo wanaopakizwa kwa maelekezo kuwa huko waendako watapokelewa na mtu fulani kwani, tunaishi kwenye nyakati ambazo watoto ni wahanga wakubwa wa ukatili mbalimbali ikiwemo kutoroshwa na kwenda kutumikishwa kinyume na umri wao.

Jumapili njema kwenu wote🇹🇿

View attachment 3116555
Da Dorice, ya the best
 
Hili nalo ulipiga kimya! Kisa huyu ni CDM!
Siyo kweli. Jiunge x uwe unafuatilia Dunia pande zote. Mbona nilichati na watu kibao kuhusu hili jambo Hadi wakani quote wengine tofauti na nilichomaanisha nikaanza tena kuelimisha siku nzima.

Ulimwengu wa kidigitali ni mpana Sana, unayedhani hayuko huku anaweza kuwa kule ambako na wewe haupo pia.
 
Nimelizambaza Jf, na hata Saa100 amepiga kimya kama mama na mlezi
Siyo Kila taarifa nitaiona, hakuna binadamu anafanya kwa efficiency ya asilimia mia moja ndugu zangu. Na ndiyo maana kuna mifumo rasmi na kuna additional. Labda tuanzie tu ulipoishia tuone tunaendaje. Aidha, poleni sana kwa tukio hilo ambalo sikuliona bahati mbaya . Shukrani
 
Kwanza ahsante Sana kwa kupokea chanya, haya ndiyo majadiliano yenye afya kwa ajili ya kujenga na siyo kubomoa. Uzuri mimi huwa pia Niko positive tu na napenda watu critical lakini critical chanya ya hoja. Kwanza ilikuwa vema tu ijulikane kuwa, tiba asili hiyo ya kujifukiza haikuwa ajenda yangu binafsi kwamba niliichukua bidhaa hizo private Bali ijulikane ni Mali ya baraza letu la tiba asili na ndiyo maana siku ile kulikuwa na mkurugenzi mwenyewe mtaalamu wa tiba asili pale ambaye naye ni Daktari pia na maafisa wengine. Wanatakiwa siku moja nao watoe elimu kuhusu utekelezaji huu wa kisheria.

Kuhusu Hawa waombeaji matapeli, mbona hata mimi nimeshiriki kwenye hatua za kufikia wengi tu leseni zao kufutwa ? Ila tu labda mambo mengi siweki online au watanzania ni wasahaulifu. La yule anajiita mungu kule Kanda ya ziwa nimeshiriki, la huyu kiboko ya washirikina, nimeshiriki, mambo ni mengi, vigumu kuanzisha. Sasa ukipata muda uka share moja tu watu baadhi wanadhani ni hilo hilo tu 🥲

Hawa wabeba nyoka nao mbona nimepambana nao tu.

Anyway, Raha ya uongozi ni ufanye kwa dhati halafu ulaumiwe ilimradi tu, moyo wako ushuhudie vinginevyo na kuungoja wakati useme.

Kwa mara nyingine nikushukuru tena na zaidi sana kwa kutambua yote haya ni kwa nia njema.

Hata hivyo nikuombe kuzitambua pia frustrations zetu tunapowaona kwenye endorsements ambazo bila shaka nanyi zinawakwaza.

Nitambue kuwa wewe nyungu haikuwa yako, hukuwa msemaji wake na wala hukuwa na mamlaka juu yake.

Kuwahusu matapeli wa tiba na wenzao, natambua Roma haikujengwa siku moja. Kwa hili nikupongeze sana na mapambano yaendelee. Ni matumaini yetu siku moja wote wa aina yao hawatakuwapo mahali popote nchini kuwapotosha wengine kuhusu tiba.

Kufikia hapa lawama zangu na nyungu na wa namna hiyo si kwako tena, ila wahusika wake.

Ninaondoa hofu niliyokuwa nayo nawe, huko afya. Labda Kumbe inaweza kuwa nafasi nyingine kuturekebishia mengine kama haya huko au hata kumfikishia waziri Mhagama:

1. Gharama kubwa za matibabu hospitali. Uzi huu unahusika:

Gharama kufuru za matibabu hospitali za umma ni kwa uhalali upi?

2. Sokomoko la wahudumu mahospitalini kupigania maslahi yao binafsi ambapo:

a) Wenye nazo hugombewa (kama na wapiga debe stendi) kwa sababu hutegemea malipo kama % ya malipo ya mgonjwa mmoja mmoja. Kwenye hili wagonjwa ni wahanga zaidi ..

b) upendeleo kwenye upangiwaji majukumu kiutendaji ambapo wasiopangiwa kwenye wagonjwa wa pesa hulia njaa daima ..

c) Hospitali za umma kutumika kutibu wagonjwa kinyemela kama hospitali binafsi ..

Yapo mengi ila kwa hakika kwenye afya na kote kwenye haki, ikimpendeza mkuu wa nchi, mbona asingejilaumu?

Pongezi kwako mheshimiwa!
 
Biashara ya utumwa ipo Tanzania, tena imeshamiri sana.
 
Kwa mara nyingine nikushukuru tena na zaidi sana kwa kutambua yote haya ni kwa nia njema.

Hata hivyo nikuombe kuzitambua pia frustrations zetu tunapowaona kwenye endorsements ambazo bila shaka nanyi zinawakwaza.

Nitambue kuwa wewe nyungu haikuwa yako, hukuwa msemaji wake na wala hukuwa na mamlaka juu yake.

Kuwahusu matapeli wa tiba na wenzao, natambua Roma haikujengwa siku moja. Kwa hili nikupongeze sana na mapambano yaendelee. Ni matumaini yetu siku moja wote wa aina yao hawatakuwapo mahali popote nchini kuwapotosha wengine kuhusu tiba.

Kufikia hapa lawama zangu na nyungu na wa namna hiyo si kwako tena, ila wahusika wake.

Ninaondoa hofu niliyokuwa nayo nawe, huko afya. Labda Kumbe inaweza kuwa nafasi nyingine kuturekebishia mengine kama haya huko au hata kumfikishia waziri Mhagama:

1. Gharama kubwa za matibabu hospitali. Uzi huu unahusika:

Gharama kufuru za matibabu hospitali za umma ni kwa uhalali upi?

2. Sokomoko la wahudumu mahospitalini kupigania maslahi yao binafsi ambapo:

a) Wenye nazo hugombewa (kama na wapiga debe stendi) kwa sababu hutegemea malipo kama % mgonjwa mmoja mmoja. Hili wagonjwa ni wahanga zaidi ..

b) upendeleo kwenye upangiwaji majukumu kiutendaji ambapo wasiopangiwa kwenye wagonjwa wa pesa huli njaa daima ..

c) Hospitali za umma kutumika kinyemela kutibu wagonjwa kinyemela kama hospitali binafsi ..

Yapo mengi ila kwa hakika kwenye afya na kote kwenye haki, ikimpendeza mkuu wa nchi, mbona asingejilaumu?

Pongezi kwako mheshimiwa!
Ubarikiwe, ahsante kwa mjadala mwema chanya na ushirikiano, nimepokea maoni yako, nitayafikisha. Shukrani
 
Mwaka 2025 mola akipenda tutafanya uchaguzi Mkuu, Mimi ninakuomba nikuchukulie fomu ya kugombea, kama itakupendeza.

Umekuwa ukifuatilia,kusikiliza kero za watanganyika bila kuchagua dini,kabila Wala umri.

Ninaomba ukubali ombi langu.
 
Back
Top Bottom