Pongezi kwenu Single Mothers
Kwa mtu mwenye malezi mazuri hawezi kukurupuka kupenda kwa sababu ya sifa za nje. Wako wanawake wengo warembo lakini si kila mwanamke ni wife material, wengine wameumbwa kuipamba dunia tu.
Ama ulikuwa umelewa, ama hujui mke w ndoa anapatikanaje.
Hujui kuwa thamani ya mwanamke ni bikira yake? Sasa huyo aliyezalishwa akaachwa unadhani anajiona mwenye thamani tena? Mbona hata wahuni husema mwanamke akijidai mjanja mzalishe tu, ndio mwisho wa kuringa?
Halafu unaomba namba tu hapo ulevini anakupa!! Wife materiak hawi cheap namna hiyo mkuu, hapo wewe ndio dhaifu wala si yeye. Kacheza na saikolojia yako tu, kakumaliza. Ushahidi ni hapo unaposema ulipojilinganisha naye ulijiona sio wa hadhi yako, tena uliishiwa hata pumzi ya kutongoza, hivyo hukusimama kwenye nafasi yako kama mwanamume.
Huyo alishakubali, ila alihitaji kukufanyia hivyo baada ya kukuona ni mgeni wa mapenzi. Hakuna jipya hapo. Hiyo kutaja taja mistari ya kidini ilikufanya uamini ni mcha Mungu, lakini kuna tatizo kubwa. Mcha Mungu asingekubali kukutana nawe baa!! Afu huyo Mungu alimjua kabla ama baada ya kupata mimba? Huyo alikuwa desperate wa kupata ndoa, alikuwa akitafuta mwanamume yeyote amuoe.
Ni hatari kubwa kuoa mke mwenye uzoefu wa maisha. Aliupata wapi huo uzoefu? Halafu kukulipia bia ndio sifa ya mke wa ndoa?
Yaani baada ya kuonana wiki moja tu, unapangandoa!! Nadhani tatizo lakk ni kubwa zaidi. Wewe ni dhaifu wa mapenzi. Wife material haswaa kwa mahusiano ya wiki moja, hujajua hata habari zake mwenyewe, alipataje huyo mtoto, kwa nini baba wa mtoto alimtosa, wazazi wake ni kin nani, anafanya shughuli gani haoo mjini n.k. Wife material unamwita saa nane usiku anakuja, hii ni zaidi ya hatari!! Halafu hiyo shape ya Wema ndio uchafu gani? Ni heri basi ungemsaka wema tu awe mkeo, yaani wewe umedata kwa Wema kuliko huyo mkeo, jitafakari utagundua hilo. Unampima mkeo kwa kupitia Wema, yaani huyo ndio SI unit yako!!
Miaka mitatu single mama alikuwa anasubiri mwanamume wa aina yako, hongera mkuu. Hakika umepata mke, nikutakie maisha marefu kwenye ndoa yako.
Huko ni kukurupuka kwenye mapenzi kwa kiwango cha SG, bado unahitaji mwongozo zaidi kujua mapenzi ni nini. Ama umri wako ni mdogo bado, ama hukuwa na maelekezo mazuri kuhusu maisha.
Asiyejua maana haambiwi maana, hongera kwa kutoka kwenye upumbavu na kuingia kwenye daraja la werevu. Hongera pia kwa mtoto wa nyongeza, uzazi mgumu siku hizi.
Jifunze kuyatawala mapenzi, usiwe mtumwa wa papuchi. Hapo hakuna cha mapenzi wala nini, ni tamaa tu ama lust. Unahitaji msaada kabla hujapotea kabisa.
Na hizo mbinu ndio zimekunasa, umepoteza hadhi yako kama mwanamume sasa wewe ndio unaolewa hapa.
Story yako wala haisadifu hoja, ingawa unajitahidi kujenga mazingira ya kuoa single mother. Jaribu utunzi wenye ubunifuzaidi ya hiki kituko ulichoandika. Hakuna anayekashifu single mother ila ukweli utasemwa. Nakushauri usome thread inayosema wanaume walioharibika akili, itakupa mwanga kidogo.

Kwahiyo ndugu unahisi nimepotea. Nikuulize swali: Ushawahi kupenda achana na kutamani kutokana na sifa za nje kupenda ishawahi kukutokea ?
 
Kuna facts ambazo zipo wazi;
1 . Uwepo wa huyo mtoto ni changamoto kwenye uhusiano mpya ( hili hutaliona sasa ) kuna legal and social implications
2. Wewe si Baba Mzazi wa huyo mtoto na kamwe hutakuwa Baba kwa huyo mtoto, haijalishi utatumia muda na pesa kiasi gani kwenye malezi ya huyo mtoto
3. Uhusiano wako na huyo mama automatically utakufanya mtoto akuzoee na kukuchukulia kama baba, hii itajenga bonding kati yako na mtoto ila kumbuka kinachowaunganisha ni mapenzi yako na huyo mama, siku ikitokea uhusiano wenu ukivunjika hutakuwa na namna ya kuwa tena karibu na huyo mtoto haijalishi utakuwa umemzoea na kumpenda kiasi gani , hii itamuathiri sana huyo mtoto kisaikolojia
4. Kama baba mzazi wa huyo mtoto yupo hai itazidisha ugumu kwenye mahusiano unayotaka kuanzisha, kumbuka kisheria huyo baba ana haki zote za kumuona na kumhudumia mtoto kama akiamua kufanya hivyo hutaweza kumzuia kisheria!
5. Utapata wakati mgumu sana kwenye kumlea huyo mtoto haswa kwenye kumuadhibu atakapokosea, ipo siku mama yake atakuambia MWACHE MTOTO WANGU, hutakuwa na la kufanya maana huyo SI MTOTO WAKO
6. Omba / sali sana huyo mtoto akikua na kuanza kujitambua aendelee kukuheshimu, huwa inatokea akishajua wewe si baba yake mzazi atakutamkia hivyo haswa akifika umri wa balehe hutakuwa na mamlaka ya kumuadhibu

Ndugu yangu nashkuru umenipa mambo ya kutafakari upya.

Nakwenda kutafakari.
 
Mwaya Mungu awalinde mfikie malengo. Wangekuwa wazungu hapa ungepewa hongera Ila kwa kuwa umeleta swala lako kwa wachawi wasiopenda furaha za watu a.k.a wabongo utakatishwa tamaa wee. Kwani single mother Hana K?? Hana ubongo?? Watu daily wanatoa mimba ili wasionekane wamezaa na tunawajua. Sasa hao Ndio bora? Mwaya km unaona umependa oaa

Kwa kweli nashukuru sana kwa kunielewa.
 
Kwani kila ndoa inapofeli chanzo lazima ni mwanamke??
Kwa kiasi kikumbwa Mkuu, ndoa inatawaliwa na mwanamke hata ikifaili utakua utashi wake....in only few isolated cases ni wanaumme kusababisha ndoa kufeili
 
Niwe mkwel silipend hili neno "Single Mother" nahis kama ni kuwapa ulemavu usiostahili.
Unafikiri jina gani sahihi litumike???

Single mother/ single parent lina ubaya upi, kuwa single si ulemavu
 
Write your reply...we jamaa ni fala Sana embu jaribu kutuskiliza sisi wanaume wenzako tunajua tuliyokutana nao tunajua uchungu wako usipotusikiliza sisi utamsikiliza Nani?

angalia kwa akili ya kawaida wengi wanakwambiaje? na siku zote wengi wape hao wanaume wanakushauri usitusikilize hawataki kuumia peke yao wengi wameumizwa wengi hawakutakii mema na wengi wanao kusapoti ni wanawake hii Mada inamuhusu mwenzao unataka wafanyaje?


mkuu lisemwalo lipo Kama halipo lajaa we hivi vitu hujawahi kuvishuhudia in real life ila sisi tumewahi hivi inamaana unataka uniambie pia ujawahi kuona hata nyuzi za mrejesho kuhusu hili swala?


we unadhani wazazi wako watajiskiaje sema tu ukwel wanaskia mwanao kaoa mwanamke mwenye mtoto unadhani watajiskiaje? kweli umeshindwa utafute binti kigori uanze nae familia unaenda oa demu alienda mzalisha mwenzako yaani mke wa mwanaume mwenzio?

embu jifikirie Mara mbilimbili akili yako haiko sawa au amekuroga nini
 
Kwa kiasi kikumbwa Mkuu, ndoa inatawaliwa na mwanamke hata ikifaili utakua utashi wake....in only few isolated cases ni wanaumme kusababisha ndoa kufeili
Ndoa inatawaliwa na mwanamke?? Kwani wanaume si ndiyo huwa mnasema kuwa ninyi ndiyo vichwa vya familia na ndiyo watawala kwenye ndoa au??
 
Write your reply...we jamaa ni fala Sana embu jaribu kutuskiliza sisi wanaume wenzako tunajua tuliyokutana nao tunajua uchungu wako usipotusikiliza sisi utamsikiliza Nani?

angalia kwa akili ya kawaida wengi wanakwambiaje? na siku zote wengi wape hao wanaume wanakushauri usitusikilize hawataki kuumia peke yao wengi wameumizwa wengi hawakutakii mema na wengi wanao kusapoti ni wanawake hii Mada inamuhusu mwenzao unataka wafanyaje?


mkuu lisemwalo lipo Kama halipo lajaa we hivi vitu hujawahi kuvishuhudia in real life ila sisi tumewahi hivi inamaana unataka uniambie pia ujawahi kuona hata nyuzi za mrejesho kuhusu hili swala?


we unadhani wazazi wako watajiskiaje sema tu ukwel wanaskia mwanao kaoa mwanamke mwenye mtoto unadhani watajiskiaje? kweli umeshindwa utafute binti kigori uanze nae familia unaenda oa demu alienda mzalisha mwenzako yaani mke wa mwanaume mwenzio?

embu jifikirie Mara mbilimbili akili yako haiko sawa au amekuroga nini
Kwahiyo mkuu unashauri pia hata mwanamke asiye na mtoto asiolewe na mwanaume mwenye mtoto?? Au unajaribu kusemaje labda??
 
Kuna facts ambazo zipo wazi;

1 . Uwepo wa huyo mtoto ni changamoto kwenye uhusiano mpya ( hili hutaliona sasa ) kuna legal and social implications
2. Wewe si Baba Mzazi wa huyo mtoto na kamwe hutakuwa Baba kwa huyo mtoto, haijalishi utatumia muda na pesa kiasi gani kwenye malezi ya huyo mtoto

3. Uhusiano wako na huyo mama automatically utakufanya mtoto akuzoee na kukuchukulia kama baba, hii itajenga bonding kati yako na mtoto ila kumbuka kinachowaunganisha ni mapenzi yako na huyo mama, siku ikitokea uhusiano wenu ukivunjika hutakuwa na namna ya kuwa tena karibu na huyo mtoto haijalishi utakuwa umemzoea na kumpenda kiasi gani , hii itamuathiri sana huyo mtoto kisaikolojia

4. Kama baba mzazi wa huyo mtoto yupo hai itazidisha ugumu kwenye mahusiano unayotaka kuanzisha, kumbuka kisheria huyo baba ana haki zote za kumuona na kumhudumia mtoto kama akiamua kufanya hivyo hutaweza kumzuia kisheria!

5. Utapata wakati mgumu sana kwenye kumlea huyo mtoto haswa kwenye kumuadhibu atakapokosea, ipo siku mama yake atakuambia MWACHE MTOTO WANGU, hutakuwa na la kufanya maana huyo SI MTOTO WAKO

6. Omba / sali sana huyo mtoto akikua na kuanza kujitambua aendelee kukuheshimu, huwa inatokea akishajua wewe si baba yake mzazi atakutamkia hivyo haswa akifika umri wa balehe hutakuwa na mamlaka ya kumuadhibu
Tatizo wanaume wengi tunakuwa na mawazo negative, na mawazo ya namna hiyo siku zote yanakuwa yanawafanya msifanikiwe.
Ni sawa na bondia anayepanda ulingoni huku kichwani mwake ameshakata tamaa kwamba anaenda kupigwa, hapo ulingoni ni lazima apigwe tena sana kipigo cha aibu.

Lazima tuwe na mtazamo chanya kwenye maisha ya kila siku , siyo wanawake wote ni wabaya au wana tabia mbaya hapana.
Na mara nyingine nyie wenyewe ndiyo mnasababisha hali hizo kwa mawazo hasi juu yao.
 
Wala usitetereke na comments za humu..

Nimeona watu wanaingia ndoa ya pili au ya tatu na watoto wao,tena watoto wanajua kabisa huyu ni step dad/mom na wana share malezi,hivyo sioni ugumu wa single mothers kuwa na uhusiano,for any relatiship kitu important ni Chemistry ama Compatibility..ukipata mtu ana great personality anakufanya uwe na furaha then kuwa nae, mtoto chukulia kama ndugu tu wa mkeo,kama unaheshimu na kuwajali ndugu wa mkeo then tatizo liko wapi ukimjali mtoto wa mkeo?
Yes , hii ni point.
Hakuna kisichowezekana, watu wanapenda kupotosha wenzao humu.
 
Daniel Adrian,
Wewe endelea na maisha yako na mtarajiwa wako, usikatishwe tamaa na ushauri hasi unaotolewa humu jf.

Maisha ya ndoa kitu cha kwanza unamtanguliza YESU KRISTO, pili maisha ya ndoa ni nyinyi kuwa na lugha moja na kupatana katika kila jambo . Kuaminiana na uwazi hapo mtafanikiwa sana kwenye maisha yenu.
Nikwambie jambo mkuu, ndoa ni "paradiso hakika" , mkiweza kuwa na mawasiliano mazuri na ya karibu yenye uwazi.
Kuwa na mtoto wala hakuna tatizo , wewe mpende tena toka moyoni mwako mkubali kuwa ni mwanao, haijalishi baba yake yupo hai au amefariki.
Na mtoto anapokosea wewe ongea na vizuri tu kama baba yake na kumweleza kipi kizuri na kipi kibaya muda ule ule anapokuwa amekosea , kupiga kuchapa siyo siyo dawa ya kumrekebisha mtoto.
Penda kuwa na muda mwingi na familia na siyo marafiki.
Familia ndiyo kila kitu.

Angalizo: ndoa nyingi zinaharibika mmoja wapo anapoanza kuchepuka. Ambako kuna sababishwa na kununiana, kutokuwa na mawasiliano mazuri toka asubuhi mpaka jioni, kutokuheshimiana, mazoea ndiyo hasa yanaharibu sana ndoa.
Jitahidi kumfanya mkeo mpya kila siku.
Hata kama hamjui mapenzi muwe wazi mfundishane. Msioneane aibu.
Mzee wa Msoga alisema akili za kuambiwa changanya na zako mambo yanaenda.
Habari za saa hizi Wanajamvi.

Leo kuna jambo fulani nataka kushare nanyi, jambo ambalo huenda mnalifahamu au hamlifahamu lakini kwa vyovyote najua kwa mjadala huu mtafahamu zaidi.

Tunatofautiana mitazamo. Kuna mitazamo tofauti tofauti kuelekea swala la kuoa Singo maza (naomba nitohoe najua inapaswa kuwa 'Single mother' ila sipendi kuchanganya lugha).

Kuna watu tumejizatiti hatutaoa singo maza ila hii kitu ni rahisi zaidi kuzungumza kuliko kuweka katika matendo. Kwanini ?

Mara nyingi kumpenda mtu hutokea bila hiari. Bila kuamua na kupatanisha maamuzi yako na mtazamo wako hiyo ndiyo sababu baadhi yetu tumejikuta tukienda kinyume na mitazamo yetu linapokuja swala la kuoa singo maza.

Acha nieleze jinsi nilivyozama kwa Singo Maza na kujikuta napuuza mtazamo wangu.

Mwishoni mwa mwezi wa tisa nilipewa mwaliko wa kuhudhuria sherehe za harusi fulani ya swahiba wangu sana.
Ilikuwa siku ya Jumamos usiku wa hiyo sherehe, wakati sherehe inaendelea na sisi (mimi na kampani fulani ya rafiki yetu) tumekaa kwenye meza ile kwenye meza jirani palikuwa na msichana fulani. Mweupee, mzuri kweli kweli, shape kama la Wema Sepetu. Nilipomuona nikamstua nikampa hi kisha nikakausha maana niliamini sio hadhi yangu ile . Najijua life langu 'dongotee' kula kwa kuunga unga na mishe ziende vizuri ndo nivae. Watoto wazuri kama wale wanataka matunzo.





Basi nikiwa naendelea kushusha bia, nikapaliwa. Bia ikanimwagikia kwenye shati. Shati likachafuka, miongoni mwa watu waliniona hili likitokea ni yule mrembo, rafiki zangu walipoona hili walinicheka sana ila yule mrembo (acha nimwite Asha) aliinuka alipokuwa na kunifata akanipa pole akatoa kitambaa chake akanipa nijifute. Nikakataa akanibembeleza nikaona sooo nikachukua ila sikujifutia chake niliinuka nikaenda msalani. Ila mpaka hapo akawa amenigusa kwa kiasi fulani nikaanza kumuona wife material.

Niliporudi nikamuomba namba akanipa. Niliporudi home nilimpigia simu aiseee! tulizungumza mpaka asubuhi, akanambia anaomba alale nikamuacha ila nikamuomba tukutane siku hiyo hiyo (jumapili) akasema sawa tutakutana jioni. Kweli jioni hiyo tukaweza kukutana maeneo fulani hivi ya ubungo tukaenda Bar fulani hivi. Kwanza kujiamini kuliniisha maana toto zuri vile linakubali appointment na mie tena sehemu km ile ila nikajikaza mpaka nikafanikiwa kumtongoza.

Hakukataa wala hakunambia chochote ila akasema ntakujibu siku nyingine. Nikaona 'Sawa.' mazungumzo yakaendelea ila sasa katika mazungumzo yake alikuwa mwepesi sana kusema maneno fulani yakuonesha kuwa yeye ni mtu wa dini. Lakini pia alikuwa mwenye ushauri chanya sana na kuonesha uzoefu mkubwa wa maisha jambo ambalo lilinifanya nione huyu ni 'wife material.' Istoshe hakuaguza pombe wala soda ila maji tu na akanambia atalipia yeye, nikasema mke si ndo huyu sasa.
Baada ya kama wiki moja hivi toka tuanze kuwasiliana mahusiano yakawa yameanza rasmi na kwakuwa nilishazama na KUDATA kwake sana nikaona sasa ni wasaa rasmi wa kupanga maswala ya harusi maana ni wife material haswa: hana lawama, hana mizinga, ata ukimwambia njoo saa nane usiku anaweza akaja, mshauri mzuri na mzoefu sana wa maisha istoshe ni MZURI MNO wa muonekano mpaka shape yaani kama ya wema.

Waswahili wanasema usione vyaelea vimeundwa, tukiwa katika mazungumzo akanambia kuna kitu nataka nikwambie, nikamwambia niambie, basi nilijua anaomba hela(maana hivyo ndivyo nnavowajua wanawake kwa uzoefu wangu) kumbe na tofauti kabisa na hilo. "Mimi nna mtoto," unasemaje ? niliuliza "Nna mtoto ana miaka mitatu, Nimeona bora nikwambie mapema kabla hatujaingia kwenye ndoa".

Sasa ndo tunarudi kwenye mada hii, unaweza kuwa na mtazamo fulani kuhusu wanawake wenye watoto, kwamba labda hutooa mwanamke mwenye mtoto katika maisha yako lakini mi nakwambia mwanaume mwenzangu unasema hivyo kwa sababu hujawai PENDA mwanamke mwenye mtoto.
Mimi nilikuwa na mtazamo huo huo lakini mpaka kufikia hatua hii ambayo nimependa kiasi hiki, mtazamo wangu nauona wa Kipumbavu sana, najiuliza kwanini nilikuwa naona si vizuri kuoa mwanamke mwenye mtoto ? Hapa saa hizi nawaza namna maisha yatakavyokuwa nitakapokuwa na familia yangu mpya na mtoto wa nyongeza, nna mtazamo mzuri sana kuelekea singo maza wangu na nataka nimpende mwanae kama mwanangu wa kumzaa kwa sababu sasa nimebaini nguvu ya upendo.

Kama hupendi kuoa singo maza sawa huo ni mtazamo wako, ila Mtazamo wako waweza badilika siku moja ukikutana na mwanamke utakaempenda kweli kweli kama mimi ilivonitokea kwahiyo nikushauri usiseme wala kukashifu watu waliooa masingo maza kama hujui nguvu ya upendo, huenda nawe ukajikuta katika njia hii hii.

Singo maza wote jamani nyie watu mna mbinu sana maana leo nimejikuta nakana nilichokishikilia kwa mda mrefu.

Mnisamehe wote niliowakwaza kwa kushea swala hili lililonikuta kwa kweli acha tu nikiri kuwa nimedata, na nimebadili mtazamo wangu.

Ila ushauri kwa wanaume wenzangu, usikashifu wala usiweke itikadi ya SITAOA singo maza, maana utajikuta unakana mtazamo wa kukolea kwa singo maza fulani, hii imenitokea kama mipango itakwenda vizuri basi tutaalikana kwenye harusi.

Mnisamehe kwa kuandika maneno meengi. Karibuni kwa mchango wenu.
 
Back
Top Bottom