Pongezi Rais Samia, Serikali, Kukubali Kubadili Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi!. Tuanze na Katiba Kwanza Ndipo Sheria Au?.

Pongezi Rais Samia, Serikali, Kukubali Kubadili Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi!. Tuanze na Katiba Kwanza Ndipo Sheria Au?.

Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.

Nilipata fursa kuhudhuria kongamano la siku 3 la vyama vya siasa nchini, lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kujadili ripoti ya Kikosi Kazi cha Rais Samia, na mapendekezo yake kuelekea chaguzi za serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, uliofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.

Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.

Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.

Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...

Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.

Pendekezo la pili, ni tufanye uchaguzi wote kwa siku moja, na kusimamiwa na Tume moja huru ya uchaguzi. Kama Zanzibar wanaweza kufanya chaguzi 5 kwa siku moja, Tanzania hatuwezi kushindwa kufanya chaguzi 4 kwa siku moja!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!

Hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 halafu uchaguzi Mkuu 2025, kwa sasa tufanye mabadiliko ya katiba na sheria, halafu 2025 tufanye chaguzi zote 4 kwa siku moja, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa.

Kongamano hilo lilifunguliwa na Rais Samia ambaye ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa nchini kutumia mikutano ya hadhara kutoa hoja na fikra zenye tija zinazolenga kuimarisha utendaji serikalini.

Aidha, Rais Samia amevitaka vyama vya siasa kutumia mikutano ya hadhara kujitangaza ili kukua kisiasa na kuutumia uhuru wa kujieleza kutoa mawazo mbadala yatakayoendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Rais Samia pia amesema uhuru wa kutoa maoni kusisababishe kudhalilisha watu
wengine, kuibua hisia za kidini, ukabila au kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Vile vile, Rais Samia amesisitiza kutumia uhuru huo vizuri bila kuingilia haki na
uhuru wa watu wengine pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu.

“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.

Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali imeyapitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vilivyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria na Bunge likalo, itapeleka marekebisho ya sheria kadhaa ikiwemo sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa ratiba ya utekelezaji itaanza na mabadiliko ya sheria kadha ambazo zitapelekwa Bungeni kwenye Bunge lijalo la October/November ili zifanyiwe mabadiliko.

Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.

Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.

Paskali
Huyu ndo Pascal Mayalla niliyekuwa namfahamu siyo huyu wa siku hizi.
Hongera Pascal Mayalla wa zamani kwa kutoa maoni mazuri!

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Tusikenue kwenye badiliko la tume ya uchaguzi

Vipi ,kuhusu mamlaka ya rais na kupingwa mahakamani matokeo ya urais

Pascal mayala

Hili hakugusia kabisa! Kama ndio hakuna haja ya tume huru ,najibu swali lako

Ni kwamba ,tupate kwanza katiba mpya na uchaguzi serikali za mitaa uhairishwe
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.

Nilipata fursa kuhudhuria kongamano la siku 3 la vyama vya siasa nchini, lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kujadili ripoti ya Kikosi Kazi cha Rais Samia, na mapendekezo yake kuelekea chaguzi za serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, uliofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.

Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.

Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.

Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...

Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.

Pendekezo la pili, ni tufanye uchaguzi wote kwa siku moja, na kusimamiwa na Tume moja huru ya uchaguzi. Kama Zanzibar wanaweza kufanya chaguzi 5 kwa siku moja, Tanzania hatuwezi kushindwa kufanya chaguzi 4 kwa siku moja!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!

Hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 halafu uchaguzi Mkuu 2025, kwa sasa tufanye mabadiliko ya katiba na sheria, halafu 2025 tufanye chaguzi zote 4 kwa siku moja, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa.

Kongamano hilo lilifunguliwa na Rais Samia ambaye ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa nchini kutumia mikutano ya hadhara kutoa hoja na fikra zenye tija zinazolenga kuimarisha utendaji serikalini.

Aidha, Rais Samia amevitaka vyama vya siasa kutumia mikutano ya hadhara kujitangaza ili kukua kisiasa na kuutumia uhuru wa kujieleza kutoa mawazo mbadala yatakayoendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Rais Samia pia amesema uhuru wa kutoa maoni kusisababishe kudhalilisha watu
wengine, kuibua hisia za kidini, ukabila au kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Vile vile, Rais Samia amesisitiza kutumia uhuru huo vizuri bila kuingilia haki na
uhuru wa watu wengine pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu.

“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.

Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali imeyapitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vilivyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria na Bunge likalo, itapeleka marekebisho ya sheria kadhaa ikiwemo sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa ratiba ya utekelezaji itaanza na mabadiliko ya sheria kadha ambazo zitapelekwa Bungeni kwenye Bunge lijalo la October/November ili zifanyiwe mabadiliko.

Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.

Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.

Paskali
Kama Muswada wa Bima ya Afya kwa wote umekwama na kuwekwa kapuni mpaka leo,suala ambalo ni nyeti linahusu maisha na Uhai wa Mtanzania.
Leo waruhusu Tume huru ya Uchaguzi ambayo itapelekea The Green kupoteza madaraka,sahau!
Katiba mpya ilipigwa mweleka Dodoma mwaka 2014.
Hivi Mkuu unaamini kabisa Mwenyekiti wa CCM ataruhusu hayo masuala,kweli!!
"Ogopa sana watu wanaopenda kuimba na kusikiliza muziki wa taarabu"!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Pascal Mayala wewe ni miongoni mwa Watanzania wachache sana wenye akili lkn,kwa bahati mbaya sana umekuwa ukitumia akili yako vibaya sana kuitetea na kuilinda ccm mitandaoni kwa kuandika upuuzi uliopitiliza.

Suala la Katiba likipelekwa Bungeni wabunge wetu ni watu wenye njaa,ujinga,ushamba na upumbavu kwa 100% maamuzi yao yatatazama usalama wa nafasi zao za ubunge kwa uchaguzi ujao.Kuna kipindi the late Babylon from Chattle alipeleka mswaada wake Bungeni na akawaambia Wabunge "msipoupitisha nalivunja Bunge"

So,hayo yote ni sehemu ya sarakasi za kijinga za ccm!
Afu tangu huyu jamaa kutuonyesha kuwa,taaluma yake haimripi baasi yote yakawa hovyo.
Kiufupi sipendi mtu ndumilamuwili.
Na hao anaodai ni wachache wanaomwelewa,kwa Great thinker Kama huyu,hoja yake ni dhaifu.

Kiufupi siasa za Nchi hii CCM haiziwezi,maana imejaa viongozi WAJINGA wengi.
 
Pascal Mayala wewe ni miongoni mwa Watanzania wachache sana wenye akili
Mkuu monde arabe , kwanza asante kuniona nina akili miongoni mwa Watanzania wachache, the reality, mimi ni mtu wa kawaida sana, pili Watanzania wenye akili ni wengi kuliko unavyo wafikiria!.
lkn,kwa bahati mbaya sana umekuwa ukitumia akili yako vibaya sana kuitetea na kuilinda ccm mitandaoni
Kutumia akili kufanya jambo lolote la kheri, ni matumizi mazuri ya akili!.
kwa kuandika upuuzi uliopitiliza.
Hii hoja kuwa mimi naandika upuuzi uliopitiliza, naomba tuu niheshimu mawazo yako.
Suala la Katiba likipelekwa Bungeni wabunge wetu ni watu wenye njaa,ujinga,ushamba na upumbavu kwa 100% maamuzi yao yatatazama usalama wa nafasi zao za ubunge kwa uchaguzi ujao.
Naomba niheshimu mawazo yako ila pia kuhusu baadhi ya wabunge wetu, tuliisha waelezea humu Baadhi ya Wabunge ni Stupid!, Tanzania haina Demokrasia!, Bunge ni Rubber Stamp!- TBC, Watch Now!
Kuna kipindi the late Babylon from Chattle alipeleka mswaada wake Bungeni na akawaambia Wabunge "msipoupitisha nalivunja Bunge"
It's very unfortunately hoja hii sikubahatika kusikia, ukinipatia links yoyote ya hii, nitakushukuru
So,hayo yote ni sehemu ya sarakasi za kijinga za ccm!
Hapa kwenye sarakasi za kijinga za CCM, naomba niheshimu maoni yako, ila ukiona watu wanafanyiwa sarakasi za kijinga mwaka hadi mwaka, then wajinga sio wafanya sarakasi bali wafanyiwa sarakasi!.
P
 
Katiba ndiyo sheria Mama,
Haya wengine ni watoto tu. Tukianza na chochote kile bila kuanzia na Katiba nina uhakika tutakuwa tumepanda mti juu ya jiwe.
Huo ndio ukweli vinginevyo tunadanganyana.
 

Attachments

  • 20231002_104257.jpg
    20231002_104257.jpg
    42.3 KB · Views: 1
Asante mkuu P.

Pamoja na mambo mengine yote, lakini kwa habari ya demokrasia huyu mama yapasa ashukuriwe. Ingawa kwa issue ya katiba ni kama kuna genge la wahafidhina ndani ya chama halitaki kuskia kabisa na kujaribu kumgeuza au kuchelewesha nia ya mh raisi.
Lakini naamini huyu raisi anayo nia njema kukomesha uhuni na watanzania wanaokufa kila nyakati za uchaguzi hasa pale haki inapoporwa kama 2020.

Raisi wangu Mungu akutie nguvu. Hakika unaweza kufanya na ukakumbukwa milele.
Kwanini ashukuriwe? Sheria zetu sizinaruhusu? kwanini mnadhani ni hisani
 
Ashinde Uchaguzi kihalali sio abebwe na vyombo vya Dola
Mkuu imhotep , hili la kushinda kihalali, nalo neno!, kama nilivyoshauri kwenye bandiko hili, katiba ndio msingi Mkuu wa haki, tatizo lulilopo ni kwa CCM, sio tuu ni chama cha siasa, bali ni chama dola!. CCM sio tu ni chama tawala, bali pia ni chama Dola! hivyo vyombo vya dola kuibeba CCM, kavyo ni kutimiza wajibu wake!. Hivyo dawa ni katiba, iivue CCM udola wake, uwanja wa siasa uwe levelled ndipo kipute kipigwe!.
P
 
HAKI haiombwi!
Mkuu Rabbon , ni kweli haki haiombwi, wala haki sio hisani, bali ni stahiki na stahili inayopaswa kutolewa na isipotolewa, haiombwi bali inadaiwa!. Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki
na Haki Huinua Taifa! Rais Samia kwa Kauli na Matendo ameonesha ni mtu wa Haki. Akitekeleza hili kama alivyosema, atabarikiwa, Tanzania itabarikiwa
Tume huru ya Uchaguzi ni Hadi vifungu muhimu vya Katiba vibadilishwe.
Ni kweli, naunga mkono hoja.
Matokeo ya Urais yahojiwe mahakamani.
Hili ni la kwenye katiba mpya.
Na Rais aondolewe Kinga ya kutoshtakiwa, wote tuwe sawa mbele ya SHERIA.
Hili hapana!.
P.
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.

Nilipata fursa kuhudhuria kongamano la siku 3 la vyama vya siasa nchini, lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kujadili ripoti ya Kikosi Kazi cha Rais Samia, na mapendekezo yake kuelekea chaguzi za serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, uliofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.

Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.

Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.

Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...

Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.

Pendekezo la pili, ni tufanye uchaguzi wote kwa siku moja, na kusimamiwa na Tume moja huru ya uchaguzi. Kama Zanzibar wanaweza kufanya chaguzi 5 kwa siku moja, Tanzania hatuwezi kushindwa kufanya chaguzi 4 kwa siku moja!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!

Hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 halafu uchaguzi Mkuu 2025, kwa sasa tufanye mabadiliko ya katiba na sheria, halafu 2025 tufanye chaguzi zote 4 kwa siku moja, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa.

Kongamano hilo lilifunguliwa na Rais Samia ambaye ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa nchini kutumia mikutano ya hadhara kutoa hoja na fikra zenye tija zinazolenga kuimarisha utendaji serikalini.

Aidha, Rais Samia amevitaka vyama vya siasa kutumia mikutano ya hadhara kujitangaza ili kukua kisiasa na kuutumia uhuru wa kujieleza kutoa mawazo mbadala yatakayoendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Rais Samia pia amesema uhuru wa kutoa maoni kusisababishe kudhalilisha watu
wengine, kuibua hisia za kidini, ukabila au kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Vile vile, Rais Samia amesisitiza kutumia uhuru huo vizuri bila kuingilia haki na
uhuru wa watu wengine pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu.

“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.

Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali imeyapitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vilivyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria na Bunge likalo, itapeleka marekebisho ya sheria kadhaa ikiwemo sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa ratiba ya utekelezaji itaanza na mabadiliko ya sheria kadha ambazo zitapelekwa Bungeni kwenye Bunge lijalo la October/November ili zifanyiwe mabadiliko.

Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.

Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.

Paskali
Mkuu natumai umesoma sheria na una uwezo mkubwa wa kuchanganua mambo

Hili jambo umeliweka hapa ni kana kwamba tunaishi kwa kudra na nchi yetu inamilikiwa na aliye juu kiuongozi na siyo umiliki wa wananchi.

Tume Huru ya Uchaguzi siyo hisani
Katiba Mpya siyo hisani mkuu.
Haki yetu inadai uwajibikaji wa wenye dhamana. Hivyo ondoa ktk mawazo kwamba Mama anatutendea hisani na tunapaswa kumshukuru.

Tutambue wajibu wetu wa kujitambua
 
Pamoja sana ndugu yangu Pascal Mayalla, maoni yangu yanatekelezwa hivi sasa.
Asante.
sinaga shaka na makala zako ambazo huwa zinastaili ya zile nyaraka katoliki.
Duh...!
unanisakazia niseme jambo ila itoshe tu kusema sina maoni
No sikukazii kusema jambo, miongoni mwa haki, pia kuna haki ya kunyamaza, the right to remain silent.
Tena mimi ni mwalimu wa somo la kujifunza kunyamaza Swali la Morality: Je, ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele maslahi ya Taifa?
P
 
Mkuu natumai umesoma sheria na una uwezo mkubwa wa kuchanganua mambo
Mkuu Msanii , kwanza asante kwa utambuzi huu, ni kweli nina uwezo sio mkubwa wa kuchanganua mambo, uwezo wangu ni wa wastani tuu, na wala sio kwa sababu ya kusoma sheria, ni exposure tuu ya miaka 30 newsroom!. Wako wanasheria manguli wabobezi na wabobevu ila ndio waliotufanyia Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?
Hili jambo umeliweka hapa ni kana kwamba tunaishi kwa kudra na nchi yetu inamilikiwa na aliye juu kiuongozi na siyo umiliki wa wananchi.
Hapana, nimesema tuwe watu wa shukrani kwa madogo ili tupatiwe makubwa!. Japo haki ni stahiki kuna vitu Rais Samia anavifanya kwa hisani tuu. Samia ameingia madarakani akakuta hakuna issue yoyote ya katiba mpya kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, hivyo ameunda kikosi kazi kwa hisani tuu, lazima tuseme asante Asante Mungu kwa Rais Samia: Ni Msema Kweli na Mtenda Kweli, Ni Msema Haki na Mtenda Haki. Je, Ataruhusu Ubatili Huu Kuendelea Ndani ya Katiba Yetu?
Tume Huru ya Uchaguzi siyo hisani
Tume ya uchaguzi iliyopo ni tume huru ila sio Shirikishi, Pascal Mayalla: NEC ni Tume huru ya uchaguzi kama lilivyo bunge na mahakama kwa sababu vyote hivi msingi wake ni Rais
Katiba Mpya siyo hisani mkuu.
Kwa vile haipo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, kitendo cha Samia kuanzisha mchakato ni kwa hisani tuu!
Haki yetu inadai uwajibikaji wa wenye dhamana. Hivyo ondoa ktk mawazo kwamba Mama anatutendea hisani na tunapaswa kumshukuru.
Natambua haki sio hisani Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki
Tutambue wajibu wetu wa kujitambua
Naunga mkono hoja, Watanzania wanatakiwa wasaidiwe kuelimishwa ili wajitambue na kutambua haki zao. Hii kazi mimi nimeianza kwa kujitolea Rais Samia ana nia njema Watanzania wapate haki, ila Watanzania hawajui Haki! Je, Tumsaidie kuelimisha umma Katiba, Sheria na Haki au?

- Ijue Katiba ya JMT-1: Katiba ni nini, ya nani, ya kazi gani? Msemo "Katiba ndio kila kitu" Una maana gani? Katiba ina umuhimu gani?

P
 
Mkuu Msanii , kwanza asante kwa utambuzi huu, ni kweli nina uwezo sio mkubwa wa kuchanganua mambo, uwezo wangu ni wa wastani tuu, na wala sio kwa sababu ya kusoma sheria, ni exposure tuu ya miaka 30 newsroom!. Wako wanasheria manguli wabobezi na wabobevu ila ndio waliotufanyia Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?

Hapana, nimesema tuwe watu wa shukrani kwa madogo ili tupatiwe makubwa!. Japo haki ni stahiki kuna vitu Rais Samia anavifanya kwa hisani tuu. Samia ameingia madarakani akakuta hakuna issue yoyote ya katiba mpya kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, hivyo ameunda kikosi kazi kwa hisani tuu, lazima tuseme asante Asante Mungu kwa Rais Samia: Ni Msema Kweli na Mtenda Kweli, Ni Msema Haki na Mtenda Haki. Je, Ataruhusu Ubatili Huu Kuendelea Ndani ya Katiba Yetu?

Tume ya uchaguzi iliyopo ni tume huru ila sio Shirikishi, Pascal Mayalla: NEC ni Tume huru ya uchaguzi kama lilivyo bunge na mahakama kwa sababu vyote hivi msingi wake ni Rais

Kwa vile haipo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, kitendo cha Samia kuanzisha mchakato ni kwa hisani tuu!

Natambua haki sio hisani Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki

Naunga mkono hoja, Watanzania wanatakiwa wasaidiwe kuelimishwa ili wajitambue na kutambua haki zao. Hii kazi mimi nimeianza kwa kujitolea Rais Samia ana nia njema Watanzania wapate haki, ila Watanzania hawajui Haki! Je, Tumsaidie kuelimisha umma Katiba, Sheria na Haki au?

- Ijue Katiba ya JMT-1: Katiba ni nini, ya nani, ya kazi gani? Msemo "Katiba ndio kila kitu" Una maana gani? Katiba ina umuhimu gani?

P
Nilianza kusoma majibu yako nikiwa nimetuna sana lakini hadi mwisho wa passage nimeelimika kiasi fulani.

Kuna baadhi ya hoja zangu umezidadavua ktk majibu yako kwangu. Bado nahisi tunahitaji sasa kuondokana na hili suala la HEWALA x 2 kwani ndilo linalojenga jamii ya kuishi kwa hisani kila jambo ambalo ni haki na wajibu.

Nashukuru yes
 
Mkuu imhotep , hili la kushinda kihalali, nalo neno!, kama nilivyoshauri kwenye bandiko hili, katiba ndio msingi Mkuu wa haki, tatizo lulilopo ni kwa CCM, sio tuu ni chama cha siasa, bali ni chama dola!. CCM sio tu ni chama tawala, bali pia ni chama Dola! hivyo vyombo vya dola kuibeba CCM, kavyo ni kutimiza wajibu wake!. Hivyo dawa ni katiba, iivue CCM udola wake, uwanja wa siasa uwe levelled ndipo kipute kipigwe!.
P
Sidhani kama jamaa watakubali levelling.....
 
Nilianza kusoma majibu yako nikiwa nimetuna sana lakini hadi mwisho wa passage nimeelimika kiasi fulani.

Kuna baadhi ya hoja zangu umezidadavua ktk majibu yako kwangu. Bado nahisi tunahitaji sasa kuondokana na hili suala la HEWALA x 2 kwani ndilo linalojenga jamii ya kuishi kwa hisani kila jambo ambalo ni haki na wajibu.

Nashukuru yes
Asante, niliwahi kuuliza Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga. Kuzuiwa bila kifungu, kuruhusu bila Kifungu. Ni hisani ya Rais Samia. Haki kuhisaniwa hadi lini?
P
 
Back
Top Bottom