Pongezi Rais Samia, Serikali, Kukubali Kubadili Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi!. Tuanze na Katiba Kwanza Ndipo Sheria Au?.

Pongezi Rais Samia, Serikali, Kukubali Kubadili Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi!. Tuanze na Katiba Kwanza Ndipo Sheria Au?.

Mimi nina mashaka inaundwa tume huru ya aina gani. Ninamashaka sana kama muundo wa tume hiyo huru inapojadiliwa kwenye bunge hili la chama kimoja.
Lazima watatengeneza tume huru yenye muundo wa kuegemea upande mmoja. Hii itakua ni kuwazubaisha watanzania.
Isipokua kwa muundo wa aina yoyote ila inaleta picha ya kule tunakoelekea hata kwa miaka kadhaa mbele tunaweza kupata kile watanzania wanachokilia..ila kwa sasa naamini hata ikiundwa tume huru bado itakua ya ccm.
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.

Nilipata fursa kuhudhuria kongamano la siku 3 la vyama vya siasa nchini, lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kujadili ripoti ya Kikosi Kazi cha Rais Samia, na mapendekezo yake kuelekea chaguzi za serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, uliofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.

Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.

Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.

Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...

Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.

Pendekezo la pili, ni tufanye uchaguzi wote kwa siku moja, na kusimamiwa na Tume moja huru ya uchaguzi. Kama Zanzibar wanaweza kufanya chaguzi 5 kwa siku moja, Tanzania hatuwezi kushindwa kufanya chaguzi 4 kwa siku moja!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!

Hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 halafu uchaguzi Mkuu 2025, kwa sasa tufanye mabadiliko ya katiba na sheria, halafu 2025 tufanye chaguzi zote 4 kwa siku moja, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa.

Kongamano hilo lilifunguliwa na Rais Samia ambaye ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa nchini kutumia mikutano ya hadhara kutoa hoja na fikra zenye tija zinazolenga kuimarisha utendaji serikalini.

Aidha, Rais Samia amevitaka vyama vya siasa kutumia mikutano ya hadhara kujitangaza ili kukua kisiasa na kuutumia uhuru wa kujieleza kutoa mawazo mbadala yatakayoendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Rais Samia pia amesema uhuru wa kutoa maoni kusisababishe kudhalilisha watu
wengine, kuibua hisia za kidini, ukabila au kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Vile vile, Rais Samia amesisitiza kutumia uhuru huo vizuri bila kuingilia haki na
uhuru wa watu wengine pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu.

“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.

Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali imeyapitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vilivyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria na Bunge likalo, itapeleka marekebisho ya sheria kadhaa ikiwemo sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa ratiba ya utekelezaji itaanza na mabadiliko ya sheria kadha ambazo zitapelekwa Bungeni kwenye Bunge lijalo la October/November ili zifanyiwe mabadiliko.

Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.

Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.

Paskali
Msemaji mkuu wa Serikali.
 
Kwanini ashukuriwe? Sheria zetu sizinaruhusu? kwanini mnadhani ni hisani
1. Amefufua mambo ya upatikanaji wa katiba mpya, mambo ambayo mtangulizi wake alisema siyo kipaumbele chake na hatukumfanya chochote, hata alipozuia mikutano ya kisiasa na UKUTA mkwara mmoja tu wa "mtapigwa hadi mchakae" ulitosha kuzima ukuta. 2. Hata leo samia akiamua kufuata nyayo za magu hakuna mtanganyika wa kuandamana kupinga, sana sana watamwachia Mungu. 3. Marekebisho ya muundo wa sheria za uchaguzi haya yote raisi ameyaridhia na alikuwa na uwezo wa kuwaminya wapinzani kama magu alivyofanya 2020 na wanakondoo wa tanganyika tusingemfanya chochote na ccm chama dola kingeshinda au kushindishwa kwa kishindo.
 
Mkuu Hismastersvoice , nimesema kwanza tuwe watu wa shukrani, kushukuru kwa kidogo ili tujaaliwe kikubwa!. Uananchi wake uko gredi ya juu sana!?

Hicho ndicho anachofanya, huyu ni mtu wa haki bin haki Rais Samia ana nia njema Watanzania wapate haki, ila Watanzania hawajui Haki! Je, Tumsaidie kuelimisha umma Katiba, Sheria na Haki au? ni Muwaza haki, msema haki na mtenda haki! Asante Mungu kwa Rais Samia: Ni Msema Kweli na Mtenda Kweli, Ni Msema Haki na Mtenda Haki. Je, Ataruhusu Ubatili Huu Kuendelea Ndani ya Katiba Yetu?

Hiyo ilikuwa ni enzi ya nyapara, imepita!, sasa tuko kwenye enzi ya majadiliano na kufikia muafaka kisha kwenda pamoja!.

Hakuna Tume huru popote isiyo na uteuzi, tofauti ya tume iliyopo na ijayo ni ijayo ni Shirikishi.
P
Sasa haki yetu tushukuru kitu gani mkuu
 
Vikosi kazi vya nini? Tunayo katiba pendekezwa iliyo tokana na bunge la katiba, kwanini tusianzia hapo, tuendelee. Nafahamu mapungufu yake ni pale Ukawa walipojitoa CCM ika hodhi mchakato mzima na kuja na katiba pendekezwa, hilo ndio lilikuwa kosa. lakini tungeanzia kuchakata maoni ya Tume ya warioba na Bunge la katiba likae tena tupate katiba.
CCM wakiachiwa wanaharibu makusudi, na hao ndio kikosi kazi.
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.

Nilipata fursa kuhudhuria kongamano la siku 3 la vyama vya siasa nchini, lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kujadili ripoti ya Kikosi Kazi cha Rais Samia, na mapendekezo yake kuelekea chaguzi za serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, uliofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.

Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.

Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.

Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...

Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.

Pendekezo la pili, ni tufanye uchaguzi wote kwa siku moja, na kusimamiwa na Tume moja huru ya uchaguzi. Kama Zanzibar wanaweza kufanya chaguzi 5 kwa siku moja, Tanzania hatuwezi kushindwa kufanya chaguzi 4 kwa siku moja!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!

Hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 halafu uchaguzi Mkuu 2025, kwa sasa tufanye mabadiliko ya katiba na sheria, halafu 2025 tufanye chaguzi zote 4 kwa siku moja, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa.

Kongamano hilo lilifunguliwa na Rais Samia ambaye ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa nchini kutumia mikutano ya hadhara kutoa hoja na fikra zenye tija zinazolenga kuimarisha utendaji serikalini.

Aidha, Rais Samia amevitaka vyama vya siasa kutumia mikutano ya hadhara kujitangaza ili kukua kisiasa na kuutumia uhuru wa kujieleza kutoa mawazo mbadala yatakayoendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Rais Samia pia amesema uhuru wa kutoa maoni kusisababishe kudhalilisha watu
wengine, kuibua hisia za kidini, ukabila au kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Vile vile, Rais Samia amesisitiza kutumia uhuru huo vizuri bila kuingilia haki na
uhuru wa watu wengine pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu.

“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.

Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali imeyapitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vilivyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria na Bunge likalo, itapeleka marekebisho ya sheria kadhaa ikiwemo sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa ratiba ya utekelezaji itaanza na mabadiliko ya sheria kadha ambazo zitapelekwa Bungeni kwenye Bunge lijalo la October/November ili zifanyiwe mabadiliko.

Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.

Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.

Paskali
Shida ya wewe wakili msomi (Adv),Freelance Journalist, Columnist n.k Pascal Mayalla unapenda sana siasa zakujipendekeza ili uteuliwe ndiyo mana kabla ya uhai wa marehemu Jiwe alikuchana laivu ..eti wewe ni mganga njaa unawazia tumbo lako tuu.
 
Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.
Katiba ni 'sheria mama' kwamba zingine zote zinatengenezwa kwa kuiakisi.

Haiwezekani kupata Tume huru ya uchaguzi bila kugusa Katiba kwasababu Tume ya uchaguzi ipo kikatiba.
Kuanza na Sheria ni kuweka viraka . Watu wenye akili na weledi huanza na msingi na hapa ni Katiba! period
Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.
Hakukuwepo sababu ya kuunda kikosi kazi.

Tume ya Nyalali na mapendekezo yake yapo. Tume ya Jaji Kisanga, Tume ya Balozi Amina Salum, Tume ya Mzee Warioba.

Tume hizi ziliundwa na kwenda kwa Wananchi kuchukua maoni.

Tume ya Mkandara imepewa hadidu za rejea na SSH halafu imeita watu wawili watatu ikamaliza na kusema ni maoni ya Watanzania.

Pasco, unafahamu ukweli huu na kwamba kilichofanyika ni ghiliba tu, Tume ya Prof Mkandara ni upuuzi wa kupoteza muda , pesa na kudanganya watu.

Kwa bahati mbaya Prof Mkandara ni wale wale akina Prof Bana n.k, ni machawa tu kama chawa wengine.
Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.
Tanzania ni mali ya Watanzani si mali ya mtu au kikundi cha watu.
Haki haiombwi inadaiwa. Hao wanaotoa hiyo haki si wafalme au malkia ni watumishi wanaolipwa na kodi zetu.

With all due respect haya mawazo ya kupewa hata haki yako ni very archaic and pathetic
Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.
Tunarudi pale pale, Rais anajipongeza kwa kufanya ghiliba. Tume ya Nyalali, Kisanga, Amina, Warioba zipo, kulikuwa na haja gani ya kuunda kikosi kazi ambacho kimehoji watu wasiozidi 2000 eti ndio Watanzania.

Anachokifanya SSH ni kukwepa suala la Muungano , kutumia katiba ya sasa kubaki madarakani.

Zama zimebadilika na tunaweza kuona nini kinatokea kwa generations za nchi nyingine.

Yanayotokea kwa Omar Bongo ni haya haya ya kudhani Wananchi ni wapumbavu na kila siku watabaki hiyo.
Bila katiba mpya SSH atakuwa na wakati mgumu sana. Hii ni generation tofauti.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.
Tazama chawa anavyofanya kazi. Mambo ya uchumi yanahusu vipi? Haya ya kuwaletea maendeleo yanatoka wapi? Prof anaongea ' kuleta maendeleo kama wagombea udiwani'

Rais aliomba kazi akifanya kazi yake hakuna hisiani ni wajibu. Tuna matatizo ya prof Tanzania, yaani akina Benson na Mkandara ni ''protoype '' ya elimu na kielelezo cha kushuka kwa elimu yetu

Sorry Pasco, I'll call a spade a spade !

JokaKuu
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.

Nilipata fursa kuhudhuria kongamano la siku 3 la vyama vya siasa nchini, lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kujadili ripoti ya Kikosi Kazi cha Rais Samia, na mapendekezo yake kuelekea chaguzi za serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, uliofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.

Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.

Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.

Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...

Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.

Pendekezo la pili, ni tufanye uchaguzi wote kwa siku moja, na kusimamiwa na Tume moja huru ya uchaguzi. Kama Zanzibar wanaweza kufanya chaguzi 5 kwa siku moja, Tanzania hatuwezi kushindwa kufanya chaguzi 4 kwa siku moja!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!

Hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 halafu uchaguzi Mkuu 2025, kwa sasa tufanye mabadiliko ya katiba na sheria, halafu 2025 tufanye chaguzi zote 4 kwa siku moja, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa.

Kongamano hilo lilifunguliwa na Rais Samia ambaye ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa nchini kutumia mikutano ya hadhara kutoa hoja na fikra zenye tija zinazolenga kuimarisha utendaji serikalini.

Aidha, Rais Samia amevitaka vyama vya siasa kutumia mikutano ya hadhara kujitangaza ili kukua kisiasa na kuutumia uhuru wa kujieleza kutoa mawazo mbadala yatakayoendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Rais Samia pia amesema uhuru wa kutoa maoni kusisababishe kudhalilisha watu
wengine, kuibua hisia za kidini, ukabila au kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Vile vile, Rais Samia amesisitiza kutumia uhuru huo vizuri bila kuingilia haki na
uhuru wa watu wengine pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu.

“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.

Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali imeyapitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vilivyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria na Bunge likalo, itapeleka marekebisho ya sheria kadhaa ikiwemo sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa ratiba ya utekelezaji itaanza na mabadiliko ya sheria kadha ambazo zitapelekwa Bungeni kwenye Bunge lijalo la October/November ili zifanyiwe mabadiliko.

Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.

Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.

Hili ni bandiko mwendelezo wa bandiko hili Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?
Paskali
umeisoma miswada ? wa tume ya uchaguzi ikoje? Kuna tume huru pale?
 
Wanabodi,

Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.

Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.

Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...

Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.

Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.

Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.

Hili ni bandiko mwendelezo wa bandiko hili Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?
Paskali
Mambo yameanza!, mabadiliko ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni haya...
.... loading

P
 
sasa ulisifia nini Pascal? CCM hawawezi kuachia nchi kwa uchaguzi..........nilijua na nimetoa harsh comment kwako maana kwa level yako unajua fika kuwa ccm haiwezi kuleta tume huru maana wanajua ikiwepo wanaondoka....
Tatizo la Tume yetu ya uchaguzi ni tume huru ila ilikuwa sio shirikishi!, kwenye muswada huu bado sijauona huo ushirikishi, hivyo huu ni mvinyo ule ule wa zamani ila kwenye chupa mpya!.

P
 
Tatizo la Tume yetu ya uchaguzi ni tume huru ila ilikuwa sio shirikishi!, kwenye muswada huu bado sijauona huo ushirikishi, hivyo huu ni mvinyo ule ule wa zamani ila kwenye chupa mpya!.

P
Nilitegemea rais asiwe na ushiriki wowote ktika kuteua commissioners wa tume na kama ulivyosema uwe shirikish
 
Wanabodi,

Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.

Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...

Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.

Hili ni bandiko mwendelezo wa bandiko hili Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?
Paskali
Hakuna mwana CCM hata mmoja anayethubutu kudai Tume Huru ya Uchaguzi.
Wewe Paskali huwezi kuthubutu kudai Tume Huru ya Uchaguzi, hususan kwenye 'forum' za CCM.
Duh...!, Mkuu fundimchundo , karibu bandiko hili, jee hapa ninadai nini?.
P
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.
Paskali
Hii ni zawadi yangu kwa Birthday ya Mama leo, nilipanga kumpa wiki ya mwisho ya October 2025,

Ili zawadi hii iwe na manufaa kwake, nikisubiri mpaka hiyo 2025, it might be a bit too little too late, kuna ubaya hiyo zawadi, kutolewa mapema mwaka huu ili iweze kutumika mwaka kesho?.

Zawadi yenyewe ni Salaam tuu za Birthday zenye ki parcel fulani!

HBD Mhe. Rais Samia kwa kutimiza miaka 64!, nakupongeza sana na kukuombea afya njema!.

Mwakani 2025 utakuwa unatimiza umri wa miaka 65 na 2030 utakuwa na umri wa miaka 70, hivyo zawadi yangu ya pekee kwako ni HII na kukusisitizia, sio lazima kuizingatia saana kivile, ila ni muhimu kuisikiliza na kujisikilizia kama na wewe pia uliambiwa kama nilivyoambiwa mimi, kwasababu yule YEYE, sometimes ana tabia na mtindo wa kuwaambia watu wake, kupitia kwa watu wengine!, hivyo just listen and try to make sense of this, a think about it, if makes any sense to you, ikitokea it doesn't make any sense to you, then dismiss it as just another set of crap!.

Ila ikitokea na wewe pia uliambiwa, but you are not very sure kama ni YEYE au ni yeye, then don't take a chance!, usipuuze!, maana hicho kitu chenyewe, is nothing compared!.

If this being the case, then tunakuomba sana sana sana, ututekelezee haya mambo tunayokulilia nayo tangu umeingia kwenye usukani, tekeleza tuu yale yaliyomo ndani ya uwezo wako, maana kusubiria post 2025, it might be too little too late!. Please Mama!.

Na ikitokea wewe hujaambiwa mpaka 2025 inaingia na hujawahi kuambiwa na mtu mwingine yeyote, then ipuuze HII itakuwa sio sauti yake YEYE bali itakuwa ni sauti ya yeye tuu ambaye sio YEYE!.

Hivyo endelea na ule mpango wako wa 2025!, na Watanzania wanaolitakia mema taifa letu hili, wote tutakuwa Tuko nyuma yako,
Tuko pamoja nawe,
Tuko nawe!.

Mungu Akubariki Sana!.
HBD Mamaa!.
Paskali
 
Back
Top Bottom