Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
tunaongozwa na kile kitabu cha purple na sio vile blacks。wewe UNAZEEKA VIBAYA! kwa taatifa yako vitabu vyeusi haviruhusu mtu kama yeye! jifunze kukaa kimya
Dini ya mtu sii miongoni mwa vigezo vya jambo letu!Ni ngumu sababu Tulia si mkatoliki.
Mkuu。PiiWii, PeeWee , mimi sio nimeandika kama mtu wa kijiweni, mimi ni mtu wa kijiweni kabisa!Paskali umeandika hii makala kama mtu wa kijiweni kabisa brother. So sorry kwa kusema hivi lakini nimelia sana.
duu 。。。!Kuwakolemea wazungu ndo iwe sababu kweli ya kupewa hiyo position!!! Kama ameshindwa kukolomea wa humu ndani kwake, utawaweza watoto wajirani?
Yaani pale tulia alifanya nini cha maana , pasco akiandika hizi sifa zake zamani tukiita upambe na Leo ndio uchawa wenyewe , kwani kule IPU kabadili kipi au kawa na impact gani kubwaUtani mwingine utakugharimu.
huyo hata deepstate hawatamuweka! we bakia na ubashiri tu kuchumia tumbo! sahau! umekua pungu siku hizitunaongozwa na kile kitabu cha purple na sio vile blacks。
p
Wengi humu ni average,hivyo they miss the point kwenye mabandiko yangu, sijawahi kuwa chawa wala kujipendekeza kwa yeyote, kosa langu ni moja tuu kuwa mkweli daima,being open,truthful and very transparentUlijipendekeza sana kwa mama mwanzoni, sasa baada ya kuona ulikuwa unaota ndoto za mchana kwenye uteuzi, umeamua kama mbwa iwe mbwai
it was not about shouting, its about being firm and standing up against bullying and intimidation。By the way, huyo mnyakyusa hakuna cha maana alichofanya zaidi ya kupiga makelele kikao kizima
Aliwekwa kwenye kitimoto badala ya kujitetea kwa stara, akaona panick na kuanza kupiga makelele,
na kwanini aombe kuheshimiwa, ina maana hajielewi kwenye nafasi yake, ulishaona Katibu wa UN anaomba kuheshimiwa?
Ni kigezo japo huwa haisemwi hadharaniDini ya mtu sii miongoni mwa vigezo vya jambo letu!
p
Duu。。。!, unamaanisha mimi ni mpambe wa Dr Tulia?。Yaani pale tulia alifanya nini cha maana , pasco akiandika hizi sifa zake zamani tukiita upambe na Leo ndio uchawa wenyewe , kwani kule IPU kabadili kipi au kawa na impact gani kubwa
Kama unajijua hutafuti uteuzi, una express your opinion freely and objectively with points,mtu aki miss the points na kukuona chawa, mtu huyu utamuitaje?Kutuhumu wengine ni average, tayari unaonyesha wewe hujapevuka unatumia ad homen attack fallacy
Halafu, leta hapa ushahidi wa maswali aliyoulizwa yalionyesha ya bullying na intimidation ?
... most people mistake playful behavior as IMMATURITY, though it's highly recommended for innovative minds!Wengi humu ni average,hivyo they miss the point kwenye mabandiko yangu, sijawahi kuwa chawa wala kujipendekeza kwa yeyote, kosa langu ni moja tuu kuwa mkweli daima,being open,truthful and very transparent
it was not about shouting, its about being firm and standing up against bullying and intimidation。
P
Shauri yako.Wanabodi,
Makala yangu Nipashe ya Leo, 20/10/24
Hizi ni pongezi za dhati kwa Spika wetu, Dr, Tulia Akson Mwansasu, alivyowajibu kwa kuwakemea waandishi wanchi za mabeberu, walioanza kumsakama kukutana na Rais Putin wa Urusi, kabla ya Zalenski wa Ukraine.
Uwezo.
Uwezo ni ability, kuna kazi zinazotaka kutumia nguvu, mtu kuonyesha uwezo, ni kuwa na muscles powers na kulifanya hilo jambo. Kuna kazi zinazohitaji professionalism, kuonyesha uwezo ni kuwa na profession husika, na uwezo wa kutekeleza.
Kuna kazi zinazohitaji kutumia brain power, kuwa na uwezo ni lazi mtu uwe na high IQ ya brain power ya kulitekekeza kama quantum physics, au hesabu calculs, algebra etc.
Na kuna kazi zinazotoka uwe muongeaji mzuri, kuonyesha uwezo, ni ule uwezo wa kuongea vizuri, kwa ufasaha na kuwa in full control. Lile jambo letu la 2005, the top 3 walikuwa 1. Top Brain, Prof. Mwando, 2. Top Diplomat. Dr. Salumu, 3. Mkwere. Sifa kuu iliyomfanya Mkwere kuwapita Top Brain na Top Diplomati, ni kuongeo tuu, "cheko na bashasha zake".
Hivyo Kitendo cha Spika Tulia, kuwajibu tuu vile alivyo wajibu, huku ni kuonyesha uwezo tosha wa lile jambo letu!. Uwezo huu ameonyeshea akiwa nje ya nchi, swali ni kama ameweza kuonyesha uwezo huo, akiwa nje ya nchi, nini kinamfanya asionyeshe uwezo huo kwenye kuisimimia serikali yetu kupitia Bunge lake ndani ya nchi?. Take it from me, soon mtauona uwezo huo ndani ya Bunge letu!
Hapa ninauzungumzia huo uwezo mkubwa wa Dr. Tulia alionao na aliouonyesha hapo juzi kati, akiwa nje ya nchi, na kujiuliza ni kwanini Dr. Tulia auonyeshee uwezo wake huo kule badala ya hapa nyumbani wakati ni jukumu la mhimili wake kuisimamia serikali yetu!, Je tumshinikize kuonyesha uwezo huo hapa nyumbani tena kwa kuanza na Bunge letu kuitekeleza ile hukumu ya Mahakama ya Rufaa, kuhusu ubatili wa katiba yetu na ubatili wa sheria zetu?.
Spika Tulia ni Mwanasheria, kwanini Bunge letu liendelee kututungia sheria batili zinazokwenda kinyume na katiba?. Kitendo cha kumpa Rais wetu kuzisaini sheria batili kinyume cha katiba, kutakuja kutokea wabunge makini ambao watahitaji Ibara ya 46A ya katiba yetu itekelezwe, kwanini huu mhimili wetu wa Bunge utufanyie hivi wakati mhimili huu uko chini ya Mwanasheria nguli, mbobezi na mbobevu?.
Dada Wawili.
Japo Rais Samia anaitwa zaidi Mama, lakini kwa umri wangu mimi ni Dada (mimi ni mtu wa 60s) na Dr. Tulia, ni mdogo kwangu, hivyo mimi nawaita ni madada wawili, mtu na dada mtu, au mtu na dada yake, mmoja ni Dada Mkubwa , mwingine ni Dada Mdogo.
Mhimili Mkuu kabisa ni Serikali unaongozwa na Dada Mkubwa, mhimili wa pili kwa ukubwa ni Bunge, unaongozwa na Dada mdogo, tena almanusa na ule mhimili wa tatu, kama tusingepindisha kidogo katiba, CJ aendelee kuwa CJ licha ya kutimiza umri wa kisheria wa kustaafu kwa mujibu wa katiba, kwenye hierarchy ya mhimili ile, the most senior ilikuwa aingie Mwanamke!, hivyo tungekuwa chini ya madada watatu, "Three Sisters", ili kuliepuka hili, imebidi katiba ipindishwe kidogo, CJ aendelee kidogo kinyume cha katiba, ili kuipusha mihimili yote mitatu kuwa chini ya madada watatu!.
Naomba kuanza na declaration of Interest, Dada Mdogo ni mwalimu wangu wa sheria, mwaka wa kwanza UDSM, somo letu la kwanza, hivyo naomba usijekuonekana hapa ni mwanafunzi anampigia promo mwalimu wake ili ndio awe yeye kwenye lile jambo letu!. No!, hapa ni meritis, facts na hoja pekee.
Mwaka 2019, niliandika makala ya Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini... nilikuwa naandika kitu fulani, mara ghafla nikasikia sauti from within, ikiniambia kuwa "Spika ajaye ni Mhe. Dr. Tulia Akson.
Sauti hiyo ikaniambia japo Mhe. Ndugai, atakuwa anatamani sana kuendelea kuwa Spika, lakini Ndugai hatakuwa kwa sababu fulani, (japo sauti hiyo imenieleza hizo sababu za kwa nini Mhe. Ndugai hataendelea kuwa Spika Bunge lijalo, lakini sio lazima kusema kila unachosikia, kwa sababu sometimes sio kila unachosikia from within ni sauti kutoka kwa Mungu au ni maono, sauti nyingine ni sauti za shetani tuu na sio sauti za Mungu, kama zilivyo ndoto nyingine, ni ndoto za shetani kama ile "ndoto ya Lema", ukisikia sauti ukahisi inaweza isiwe sauti ya Mungu, au ukiota ndoto ya jambo la ajabu ajabu ukahisi jambo hilo sio la kheri, sio lazima uliseme).
Tangu baada ya Spika Sitta, trends za uspika zimeonyesha kiti cha Spika ni just one term only na term hiyo ikiisha, Naibu Spika ndio huwa Spika. Wakati wa Spika Sitta, Naibu Spika alikuwa Anna Makinda, japo Sitta alitamani kuendelea, aliwekwa pembeni, Naibu wake Anna Makinda akachaguliwa kuwa Spika.
Wakati wa Spika Anna Makinda, Job Ndugai alikuwa Naibu Spika, baada ya Makinda kumaliza one term yake, Naibu wake Job Ndugai akawa Spika, hivyo trends zinaelekeza baada ya Spika Job Ndugai, automatically, Spika anayefuatia ni Naibu Spika Dr. Tulia Akson
Hivyo, ilipojitokeza fursa ya U Spika, nilisema Kujiuzulu kwa Ndugai ni mpango wa Mungu kwa Tanzania ili tupate Spika Bora. CCM itateua Spika Bora au Bora Spika kama kawa? na Dr. Tulia alipoukwaa Uspika, hatukumkopesha nilisema Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!
Na kweli Spika Tulia alipoingia akaanza moto wake Spika Dkt. Tulia yuko sahihi sana, CHADEMA wajifunze kufanya vitu kwa usahihi na wafanye kiusahihi
Pamoja na mazuri yake yote, Dr. Tulia pia ni binadamu, anaweza kukosoea, hivyo alipokosea kwenye madudu ya IGA ya DPW na bandari zetu, tulimpa "IGA ya DPW imetusaidia sana kujitambua. Tuna wanasheria wa Aina Gani!, Bunge na Serikali yetu, Ilipitishaje IGA Hii?
Mazuri yake, yameendelea na tumeendelea kumpongeza na kushauri Hongera Spika Dkt. Tulia Ackson. Kuna haja MaSpika wetu iwe lazima kuwa Wanasheria? na alipoukwaa urais wa IPU ndio funga kazi, juzi kati ndio kafunga kazi kwa kuwawakia mabeberu kutudharau Afrika kuwa hatuwezi.
Hitimisho.
Kwa vile Dada Mdogo ameonyesha uwezo kuwa anaweza na kweli anaweza, kwa vile kwenye lile jambo letu, tumeamua twende na mwanamke, mnaonaje kama Dada Mkubwa, kwa vile umri umesongea songea, na kwa kadri miaka inavyokwenda mikiki mikiki ya Gen.Z, itaongezeka, kwa mtu wa umri wa miaka 70, kusumbuliwa na hivi vijukuu vya Gen Z, ni mateso!, mnaonaje tukimshauri Dada Mkubwa, kwa vile Dada Mdogo pia anaweza, anaonaje akiamua kumpisha na kumuachia Dada Mdogo lile jambo letu lile, ili yeye apumzike at 65, akiwa na nguvu zake na taifa kuendelea kumtumia kama tunavyomtumia JK?.
Umri wa kustaafu utumishi wa umma, kwa hiyari ni 55, kwa lazima ni 60, na kwa viongozi wakubwa ni 65. Hakuna asiyejua kuwa kuna wengi wanafikisha umri wa miaka 60, wakiwa fiti na nguvu zao, ndio maana viongozi wakubwa ni miaka 65.
Lengo sio kustaafu kwa vile wamechoka, lakini ni kustaafu ukiwa bado unanguvu ili muda uliobakia uutumie kula pensheni yako vizuri ukiwa na nguvu zako, na sio unastaafu ukiwa umechoka kabisa hivyo unajikuta hauna hata nguvu za kuenjoy kwenda beach na wajukuu, wewe ni kiti, kitanda mpaka ile siku. Kumaliza utumishi wa mikiki mikiki at 70, is not a joke!.
Hivyo kwenye lile jambo letu, kwa vile tumeamua twende na mwanamke, na Dada Mdogo kaonyesha uwezo, Dada Mkubwa anaweza kuamua twende na Dada Mdogo, unless kama ile "twende na Mwanamke", lengo lake ni lazima twende na mwanamke fulani tuu specific, if this, being the case, then twende naye tuu kwa ule ule utaratibu wa fomu moja na mserereko, ila at 70, nitawakumbusha, nilishauri nini na lini!.
Hata yule Blaza wangu, niliwahi kumshauri kitu hapa. "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza nilisema
Ushauri huo, ulipuuzwa, lakini Blaza saa hizi amejilalia zake pale Chato, tausi wapo wanarandanda around, akiwa amewekewa jiwe kubwa la granite, badala ya yale majabali ya Chamwino. Hivyo hata ushauri huu ukipuuzwa, kwa mujibu wa umri wangu wa sasa, mtu wetu at 70, nitakuwepo if God is willng nitawakumbusha au tutakumbushana na ni kipindi hicho ndipo nitaikamilisha hii MTR Ili kuisaidia nchi na kumsaidia Rais Samia, je tumfanyie an honest MTR based on SMART Objectives za tulipotoka, tulipo to determine tunapokwenda?
Jumapili Njema.
Kaka Paskali
Hapo nadhani umeteleza kidogo. Hao aliowakemea hawakuwa waandishi bali walikuwa ni ma speakers wa mabunge ya nchi 12 zinazojulikana kwa jina la 12+. Hizi ndizo nchi tunazoziita za mabeberu. Tulishawahi kuwa makoloni wao na bado zinaamini badk tuko makoloni yao in our minds. Hizi ndizo nchi ambazo chadema wanaziita na wanaamini kwamba ndiyo dunia. Kwa kweli. Kwa kweli kazichapa za uzo nchi hizo na kushangiliwa na ma speakers wengine wote kwenye mkutano huo wa mabunge yote ya dunia aka IPU.Dr, Tulia Akson Mwansasu, alivyowajibu kwa kuwakemea waandishi wanchi za mabeberu, walioanza kumsakama kukutana na Rais Putin wa Urusi, kabla ya Zalenski wa Ukraine.
Hawezi kufanya hivyo. Yeye si mjinga kiasi hicho. She's very smart. Yaani wewe unataka aikemee na kuikoromea serikali ya dada mkubwa kama alivyozikemea hizo serikali za nchi 12+? Unataka ayapate yale yaliyompata Job Ndugaye? Kumbuka hizo nafasi alizonazo, spika wa bunge la Tanzania na ile ya uraisi wa bunge la dunia, akapewa na dada mkubwa. Huyu dada mkubwa anaweza kumtoa kwenye hizo nafasi anytime kama ambavyo Ruto wa Kenya alivyomtoa Gachagua.Uwezo huu ameonyeshea akiwa nje ya nchi, swali ni kama ameweza kuonyesha uwezo huo, akiwa nje ya nchi, nini kinamfanya asionyeshe uwezo huo kwenye kuisimimia serikali yetu kupitia Bunge lake ndani ya nchi?.
Hilo unaloliita jambo letu ni jambo kubwa sana. Si jambo la mchezo mchezo. Hicho kigezo alichokionesha Tulia huko IPU hakitoshi kwa mbali kwenye vigezo vyetu vya hilo jambo letu. Wapo vijana na hata wazee wengi tu wenye vigezo vyingi kumpita yeye kwenye hilo jambo letu.Hivyo Kitendo cha Spika Tulia, kuwajibu tuu vile alivyo wajibu, huku ni kuonyesha uwezo tosha wa lile jambo letu!.
Haya mambo ya utatu haya, kunaMagu alikwisha waambia tena Kwa msisitizo akirudia mara tatu kwamba :
1. " Nileteeeni Gwajima, "
2. "Nileteeni Gwajima",
3. "Nileteeni Gwajimaaaaa "
😀 Haya!
Proved Mkuu jiongeze. Ni mwaka huu tuliambiwa na cdf mstaafu kuwa alishindwa kutii amri ya Hayati Magufuli kumrudisha nyumbani, kutokana na taratibu za kitabibu. Unataka niongeze neno gani Tena?...alifarikia hospitalini London na siyo Moscow au shanghai, why... ???