Pongezi Spika Dkt. Tulia umeonesha uwezo na unaweza! Je, tumshauri Dada Mkubwa, ikimpendeza, ampishe Dada Mdogo kwenye lile jambo letu?

Pongezi Spika Dkt. Tulia umeonesha uwezo na unaweza! Je, tumshauri Dada Mkubwa, ikimpendeza, ampishe Dada Mdogo kwenye lile jambo letu?

Hapo nadhani umeteleza kidogo. Hao aliowakemea hawakuwa waandishi bali walikuwa ni ma speakers wa mabunge ya nchi 12 zinazojulikana kwa jina la 12+. Hizi ndizo nchi tunazoziita za mabeberu. Tulishawahi kuwa makoloni wao na bado zinaamini badk tuko makoloni yao in our minds. Hizi ndizo nchi ambazo chadema wanaziita na wanaamini kwamba ndiyo dunia. Kwa kweli. Kwa kweli kazichapa za uzo nchi hizo na kushangiliwa na ma speakers wengine wote kwenye mkutano huo wa mabunge yote ya dunia aka IPU.
Mkuu @dr akili,kwanza asante kwa kunielimisha hili la 12+, nikijua Tulia anawakoromea waandishi wa habari wa nchi za mabeberu, kumbe ni maspika wa nchi za mabeberu!, yelewii!, Tulia hatunaye tena IPU!。
Hawezi kufanya hivyo. Yeye si mjinga kiasi hicho. She's very smart. Yaani wewe unataka aikemee na kuikoromea serikali ya dada mkubwa kama alivyozikemea hizo serikali za nchi 12+? Unataka ayapate yale yaliyompata Job Ndugaye? Kumbuka hizo nafasi alizonazo, spika wa bunge la Tanzania na ile ya uraisi wa bunge la dunia, akapewa na dada mkubwa. Huyu dada mkubwa anaweza kumtoa kwenye hizo nafasi anytime kama ambavyo Ruto wa Kenya alivyomtoa Gachagua.

Huyu dada mdogo anapaswa kufuata kile ambacho dada mkubwa anachotaka. Hata hicho kitendo cha kuwakemea hao 12+ aliyeanza ni dada mkubwa alipokuwa huko Moshi kwenye kilele cha sherehe ya jeshi letu la polisi kutimiza miaka 60. Hivyo Tulia alichofanya huko kwenye mkutano wa IPU ilikuwa ni kuendeleza kushindilia msumari wa dada mkubwa kwenye hizo nchi. Hivyo the credit goes to dada mkubwa and not to dada mdogo.
Thanks for this too, hili sikulijua ila Dada mdogo ni akili kubwa wakati dada mkubwa ni wa kawaida, kitendo cha akili ndogo kuongoza akili kubwa ni submission, huku ni mhimili wa Bunge kuji submit kwa the executive, ndio maana wanaletewa miswada batili, wanapitisha!,wanaletewa an illegal IGA, wanapitisha!mtu anayeweza kuwakoromea kubwa la mabeberu, anashindwaje kuisimamia serikali inayowategemea hao mabeberu!。 Hivyo inawezekana hapa mimi nampongeza Dr Tulia na kumuona ni shujaa kumbe kwa umasikini wetu as beggars as we are, na hao mabeberu ndio tunaowategemea kwa kuwatembezea bakuli letu, then koromeo lile litasababisha a diplomatic fiasco na Tulia aka risk kung'olewa!。
Hilo unaloliita jambo letu ni jambo kubwa sana. Si jambo la mchezo mchezo. Hicho kigezo alichokionesha Tulia huko IPU hakitoshi kwa mbali kwenye vigezo vyetu vya hilo jambo letu. Wapo vijana na hata wazee wengi tu wenye vigezo vyingi kumpita yeye kwenye hilo jambo letu.
Naunga mkono hoja ila kwa Dada mkubwa anakwenda 70 na dada mdogo ni under 50, yupi ni afadhali?。
Watu kama akina Mpina wameshaonesha mapungufu yake hadi kumshitaki kwenye ule mhimili wetu wa tatu. Bado ni kijana. Apewe muda wa kuendelea kujifunza na kupata uwezo na vigezo zaidi kwenye hilo jambo letu.
thanks
Mwaka 2030 tutampima kama atakuwa ame aquire vigezo vyetu vyote vya hilo jambo letu.
hapa kwenye hili la 2030, imepita mule mule, mwake mwake kwenye bandiko langu kuhusu HII kitu ya hili jambo letu, humo nilisema
Wanabodi

Na kipindi hicho cha 2025- 2030 ndipo sasa sasa tufanye grooming ya Mwanamke competant candidate atakaye kuja kugombea urais wa JMT kwa 2030, na kwa maoni yangu, Mwanamke huyu sii mwingine yeyote zaidi ya Dr. Tulia Akson Mwansasu, Spika wa sasa wa Bunge la JMT.

Japo Tanzania, tulipania 2025 twende na mgombea mwanamke, na mimi niliunga mkono hoja hii Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!
kama hii sauti ni yake YEYE kweli, then inamaanisha kwa uchaguzi wa 2025, Tanzania tuna mgombea mmoja tuu Mwanamke, yaani the one and only ambaye ama anatakiwa na YEYE apumzike ampishe mgombea mwanaume, ama ...

Natumaini nimeeleweka.
P.
Last but not least, we save the best for last, wewe, Dr Akili ni miongoni mwa baraka za jikwaa hili。
Ubarikiwe sana。
P
 
Paskali akitabiri kitu namba muwe makini sana kufuatilia.

He is accurate 98%
Mkuu Saint Ivuga , kwanza asante, kunipigia promo watu wanizingatie, ila huu sio utabiri, huu ni ushauri tuu wa logical kwa Dada Mkubwa kumu consider Dada Mdogo, kwa vile kwenye lile jambo letu, tumeamua twende na mwanamke, and she will be 70, then its logical kumshauri afanye tuu consideration ya kumuangalia dada mdogo au mwanamke mwingine yoyote under 60 ambaye ni capable na energetic!. Utabiri wangu huhusu jambo letu la 2025 uko kwenye HII kitu!..
P
 
Mkuu Saint Ivuga , huu sio utabiri, huu ni ushauri tuu logical kwa Dada Mkubwa kumu consider Dada Mdogo, kwa vile kwenye lile jambo letu, tumeamua twende na mwanamke, and she will be 70, then its logical kumshauri afanye tuu consideration ya kumuangalia dada mdogo. Utabiri wangu wa 2025 uko kwenye HII mada.
P
Ujio wa Magufuli, ulitanguliwa na ushindi wa Trump,

Akishinda Harris November US, na huku 2025 atakuwa mwanamke,

Sasa Kwa kuwa Ajaye US ni Trump, tegemea huku mtu Mwanaume wa kuimalizia KAZI aliyoiacha Magu.

Tusubiri.
 
Nadhani Kuna watu wanakutuma kupima upepo..!! watch out mzee
Wanaotumwa ni walioajiriwa,wanatumwa na ma bosi wao, mimi ni freelance, sijaariwa na yeyote, situmwi na mtu wala siwajibiki kwa yeyote, I am my own boss!na bandiko hili sio la kupima upepo wowote, ni bandiko la an honest opinion advise kwa Dada Mkubwa na dada mdogo。
P
 
Back
Top Bottom