Posho mbili, Spika Sitta, Takukuru na Maadili yake!

Kwa taarifa za chini ya Kapeti, atakuwa anatangaza kuachia ngazi PCCB.
 
Tarehe halisi ya hii press inachaganya kidogo! thread ilitumwa saa 5.45 usiku (robo saa tu kabla ya tarehe ya leo). Hii inatuwia vigumu kuwa na hakika bayana kuwa press ni leo tarehe 2/11 au ni kesho tar 3/11. Hebu tufafanulieni hili
 
Hiki kiini macho cha kulileta/kuitaimu hoja ya Richmond bungeni kwa kuingiza hii issue ya posho za wabunge naamini imeletwa na Mkulu mwenyewe.Na hii inatia shaka juu ya dhamira ya kweli ya Mheshimiwa Rais katika kushughulikia grand corruption na ufisadi kwa ujumla.

Naamini kwamba ni kosa kwa wabunge kupokea posho mara mbili kwa kikao kimoja na hili lazima liwe punishable in law lakini kwanini iletwe au ianzishwe wakati huu na kwanini ianzie ikulu?? kwanini imeletwa wakati Richmond inatakiwa ijadiliwe bungeni?? Hamuoni kama nia ni ku-distract hoja ya richmond na kuwanyima wabunge kujipanga vyema kwenye suala la Richmond??

Kwanini order hii iletwe na Ikulu sasa??? Naamini mheshimiwa Rais au kurugenzi ya mawasiliano ya ikulu itatoa ufafanuzi wa hii timing ya issue ya uchunguzi wa posho za wabunge ku-coincide na taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya bunge kuhusiana na suala la Richmond.

Hivi watu wakianza kusema sema pembeni tena kwamba kuna mkono mzito wa ikulu katika suala la Richmond pamoja na clarification iliyotolewa na ofisi kubwa na Rais mwenyewe ikulu italalamika tena?
Kwani huko Ikulu hamkuliona hili kama litaleta controversy ambayo ni unnecessary??
 
Nahisi kama atatangaza kuachia ngazi-maana kauli zake na vitendo tofouti?
tusubiri na tuone anakuja na nini?
mdau Lusungo Ipinda Kyela.
 
hana lolote

Sasa hiyo ndio update ya mkutano na waandishi au ameshidwa kuongea? Tupeni basi updates wakuu!! Tuna kiu na kujua mkurugenzi wa taasisi muhimu sana hapa tanzania atasema nini
 
vipi atalipa "posho" kwa waandishi wa habari?
 
Kama hayo ndiyo kayatamka basi tusubiri tuone maana waliowengi walitaraji mzamivu hosea kuja ktk sura ya kinafiki kumbe kaja na nondo zao wenyewe na mjengo wao. Maneno ya kumsakama ya nini kama wao na ofisi yao ndio walioomba upembuzi huo yakinifu, wamuulize six na kashilila full stop.

Nina mashaka kama six hataongea na media kujibu haya ya hosea leo leo na kavu kavu. Maana wakuu wanazichapa za mchangani nowadays!!! Bo gloves wala ulingo....
 
Am sick and tired of the games these big shorts play.Na wale wanaofanya hizi strategy sijui nao wanafikiria nini.Maana hatuangalii tena maendeleo.Tunaangalia namna ya kudhibiti personalities kwenye the so called ufisadi. Ndo maana TBL na Serengetiu wanazidi kuongezea viwanda vya pombe ili wote tuwe walevi kupindukia
 
Tunasubiri aseme jambo lenye manufaa kwa nchi yetu katika kufifisha rushwa na ufisadi na sio kuendeleza libeneke la malumbano yasiyokuwa na tija. Tumechoka na maneno mengi yasiyokuwa na mnofu
 
Ndo maana TBL na Serengetiu wanazidi kuongezea viwanda vya pombe ili wote tuwe walevi kupindukia
ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha
Tulewe na kusahau yale magumu na kutafuat mbinu za kujisafisha
Nashanga eti TBL na Serengeti inajadiliwa Bungeni!!!
Nchi yetu jamani tulipewa kila kitu tukanyimwa akili timamu tu!
 
labda anatangaza kujiuzulu


kabla ya jumatano hajasulubiwa
 
ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha
Tulewe na kusahau yale magumu na kutafuat mbinu za kujisafisha
Nashanga eti TBL na Serengeti inajadiliwa Bungeni!!!
Nchi yetu jamani tulipewa kila kitu tukanyimwa akili timamu tu!

Wapi twaweza zipata hizo au nani kazichukua maana awali zilikuwepo
 
Kutoka kwa mdau.

-Nimetoka kwenye mkutano wa Dr Edward Hoseah ambao umemalizika muda mchache uliopita katika ofisi za makao makuu ya TAKUKURU Upanga jijini Dar es Salaam.

Katika Mkutano huo, kwanza Dr Hoseah kaanza kwa kusema "Sijiuzulu ng'o, maana toka asubuhi ninapokea simu za watu wakiuliza kama nimejiuzulu tayari" hayo yalikuwa maneno yake wakati anaingia ukumbi wa mikutano kabla hata ya kusamiliana na wanahabari.

Dr Hoseah anasema "kuna nini mpaka wabunge waogope kuchunguzwa na TAKUKURU? kinachomshangaza ni kuwa hata sheria inayotekelezwa na TAKUKURU imepitishwa na bunge lenyewe tena na wabunge hao hao, iweje leo waanze kulalamika kuwa hawatendewi haki? haki wanayoitaka waheshimiwa wabunge ni ipi?" anahoji Hoseah.

Aidha anasema , barua ya bunge ya tarehe 26/02/2009 iliyokuwa imeelekezwa kwake, ilikitaka chombo chake kufanya uchunguzi ili kujiridhisha maana kulikuwa na minong'ono ya wabunge kulipwa posho mbili, huku wanalipwa na bunge pamoja na taasisi wanayokwenda kuitembelea!

Amewataka wabumge ambao wamekuwa na sifa kubwa ya kupinga vitendo vya kifisadi watoe ushirikiano ili chombo hicho kiweze kuwafanyia 'natural justice' maana katika detection tayari makachero wa TAKUKURU walishapata kila kitu kuhusu posho hizo mbili za wabunge.

Aidha amewataka wabunge ambao wanaona anafanya makosa kuwachinguza, wapige kura ya kutokuwa na imani naye, na yupo tayari kwa lolote litakalotokea, huku akijiganba kuwa TAKUKURU sio mwisho wa maisha yake hata kidogo, "there is life after PCCB" anasema Dr Hoseah-
 
ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha
Tulewe na kusahau yale magumu na kutafuat mbinu za kujisafisha
Nashanga eti TBL na Serengeti inajadiliwa Bungeni!!!
Nchi yetu jamani tulipewa kila kitu tukanyimwa akili timamu tu!

mzee umeua ha ha ha ha ha.
 
Kwani Bunge lina uwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na imani dhidi ya kiongozi aliyeteuliwa na Rais?
 
Shalom,
Unaona sasa. Kumbe BUNGE lenyewe liliandika BARUA kuomba lichunguzwe. Jamaa kaingia kazini na watu wanalalamika. Mambo hayo sasa. Mwakyembe lazima amsulubu Hosea mapema na asipofanya hivyo, basi NGOSHA atamsulubu yeye.

Wanasema SIFA ya mpigani mkubwa duniani ni mbili:
1. Uwe na uwezo wakuhimili KIPIGO.
2. Uwe fast na flexible.

Mwenye hizo mbili kati ya Hosea na Mwakyembe, basi kashinda GAME.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…