Posho za Wizara ya Fedha mwezi Machi, Aprili na Mei

Baada ya Aids, Covid 19 nadhani kuna jipya litaibuka very soon
 
Reactions: BAK
huu ni ubadhirifu wa fedha za walipa kodi. kamwe usivumiliwe.
watu wana haki zao zimekaliwa hapo lkn wao wanajimegea wanavyo taka, hii ni aibu, watu hawana huruma wala hawana hofu ya Mungu ni hatari san.
 
Majitu ni majinga Sana na yanatafuta kiki yaani ukiangalia mgawanyo wa hizo posho kwa idadi ya watu unakuta ni posho za wastani wa mil.2 au 3..Sasa hizi si posho za kawaida tuu huku maofisini kwa mtu amefanya Kazi mwezi

Maofisa wengi wa ngazi za Juu Wana pesa ya knight au extra duty kubwa.

Kama hizo pesa ni nyingi hebu waangalie kipindi marehemu yuko madarakani.Kwa taarifa yenu kipindi cha mwendazake unaweza piga pesa na asiwepo wa kutoa taarifa kwa sababu ya hofu ya kutojuana.

Saizi kwa vile ile hofu uchwara haipo ndio uropokaji umekuwa mkubwa,mwezi wa 12 2020 kwa mfano niliwahi lipwa posho zinazofikia mil.2 kwa Kazi Halali kabisa sasa nashangaa watu mnavyotoa povu kwa posho,tena sikuhizi pesa inalipwa kutoka huko huko BOT.

Huo wizi unakujaje kwa staili hiyo? Labda ufute posho.Mtu anasema eti unalipwa posho kwa Kazi unazotakiwa kufanya sasa nini maana ya extra duty au per diem? Kwani hao wanasiasa hawalipwi hizo ?

Kiki zisizokuwa na maana
 
Hawa ndo walikuwa wanasema bila shaka nchi haina furaha na kwa namna hii furaha imerudi ,na inaonyesha walikuwa na kiu balaa yaani hawakusubir hata shughuli za msiba zipoe
Mkuu ndiyo namna ya kuruhusu mzunguko wa pesa mtaani, maza kaamua kuachia fedha zije mtaani sababu hawa watu watanunua cement, bia, nguo, magari, kulipa mafundi n.k
 
Alafu unakuta ni mkusanyiko wa posho za muda mrefu zimelipwa kwa pamoja baada ya fedha kupatikana hakuna cha ajabu
 
Mambo ni mengi sana kwenye hii nchi na hapo kuna Ukaguzi ulifanyika BOT na majibu yake hadi leo hayajapatikana inaelekea kuna madudu mengi mno, na hiyo Wizara ya fedha ndiko katokea makamu wa Rais mjue
 
Yamepigwa leta ushahidi zile ni hasara
Kama walikuwa walikuwa wanaendesha shughuli kwa hasara kwanini walikuwa wanapeleka gawio kwa serikali na kujisifu wanaingiza faida ,yule kichaa alikuwa fisadi balaq
 
sidhani uko sahihi sana lkn kinachoonekana hata baada ya JPM kufariki kasi ya majizi nayo imeanza kurudi kwa kasi kubwa.hao waliotuhumiwa kufanya malipo haya ingekuwa ni kipindi cha JPM sidhani wangesimamishwa bali wangefukuzwa na mali zao kutaifishwa.hizo ni pesa nyingi za walipa kodi haziwezi tu kuchezewa hivyo.watumishi wanaambiwa hawawezi kupandishwa vyeo sababu hakuna pesa lkn wajanja wachache wanafuja pesa ya walipa kodi kipuuzipuuzi tu.hapana hawa watu ingekuwa kama nchi za wenzetu kama china walipaswa kupigwa risasi hadharani.kwa kweli nchi hii baadhi ya watumishi wamekosa maadili kabisaa,ni wabinafsi ambao wanajali matumbo yao pamoja na familia zao.hatuwezi kukubali mambo haya yaache hivyo ni lazima serikali iwe makini na hatua kali za kisheria zichukuliwe.
 
bavicha watakwambia enzi za jpm walikuwa hawawezi kuwka majina wazi
 
hawa ndio walima wananchi hawama hela na JPM dictator
 
hivi hata kama ni wewe ungeiba kipindi cha JPM?
 
acha uhuni lete ushahidi. mnatafuta pakutokea sasa
 
tunashukuru sana angalau kwa kuyajua haya leo kuliko awamu ya jiwe ambapo ilikuwa vigumu kupata taarifa kama hizi.enzi hizo taarifa zote ukiwemo ufisadi zilidhibitiwa, ilikuwa ni kusifu na kuabudu tu.
uhuru huu wa habari ulikuwa matatani na yeyote yule ambaye angethubutu kuandika chcochote kuhusu ufisadi au kuuibua angeshughurikiwa kwa kesi za uchochezi,uhujumu uchumi,madawa ya kulevya au utakatishaji fedha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…