Poverty Elimination in Tanzania is a 'Result Oriented Business'

Poverty Elimination in Tanzania is a 'Result Oriented Business'

Sungura tupo kuongea kitu kimoja mkuu…. Sema tu kua tatizo ni mitazamo ambayo inagongana huku ikiwiaana sehemu na sehemu. Tokana na maelezo yako naona upo pamoja na Zakumi, kua lawama zote abebe Kiongozi for s/he is the one wholly responsible….

Tukitolwa mfano wa gari uliotoa.. Kumbuka kua hata magari nayo sio madereva wote waweza endesha, kwa kuzingatia hilo hilo gari dogo unakuta kua kuna dereva; tena ni derevaq mzuri…. ambae anaendesha automatic tu! Ukimletea manual, unakua umem Knock out! Hivo basi mtu anapokua kiongozi peke yake haitoshi…. Dereva kama dereva anakua tu analiongoza lile gari…. What matters katika uendeshaji salama na ulio reliable katika gari ni injin, matairi na mafuta….. Kwa muktadha huo Viongozi na watu wake wote wanatakiwa kuwajibika ipasavo. Kikubwa huyo kiongozi ahakikishe ni dereva mtunzaji (sio rough!); na pia kuahakikisha entities zote za muhimu katika hilo gari zaenda sawa kabisa… ahakikishe mafuta ya kutosha, ahakikishe oil kwenye injini ni safi na ahakikishe kua tairi zipo katika hali nzuri na tire bolts zimekazwa vilivo…

Nikija nchi ya Ruanda, hio ni moja ya nchi I am so proud of katika a group ya hizi za developing nations…. Sa ingine genuinely hata hua najiuliza kua viongozi wetu (hasa JK) kama kamtembelea Kagame na kumuuliza how has he done it? After a short while of such development katika sector nyeti za maendeleo ya nchi….. Hata hivo tujiangalie wa Tanzania…. Nidhamu zetu zipo vipi makazini? Wenzetu Warundi, Wakenya wakija makazini wapo vipi attitude yao towards work? Tukipata jibu hapo tunapata jibu tatizo sio viongozi peke yao… Tatizo ni pana zaidi ya Viongozi kua Responsible and good Leaders….

AshaDii,

Kwenye thread "Kwanini watanzania ni maskini?" Niliambiwa kuwa ninailinda "The Status Quo" pale niliposema kuwa wananchi nao wanatakiwa kuchukua wajibu wao katika utekelezaji wa mambo. Je inakuwaje kwenye thread hii nimepabadilika na kuanza kukosoa uongozi?

Threads hizi mbili zinafanana. Lakini kuna tofauti za kimsingi. Kwenye "kwanini Watanzania ni masikini" kuna sababu nyingi za kueleza. Tupo masikini kwa sababu ya hali ya hewa, rushwa, ukoloni, sera mbovu, uongozi mbovu na mambo mengine. Au kuna sehemu nyani wanakula mahindi na kufanya watu wawe masikini.


Katika thread hii tunaangalia process ya kujitoa kwenye umasikini. Baada ya kuzijua sababu, tunatakiwa tuchukue hatua. Je ni hatua gani? Tanzania hatua hizi zinachaguliwa na viongozi, hivyo wao ndio wenye kubeba lawama pale wanaposhindwa.

Mfano wako wa Rwanda ni ushahidi mkubwa kuwa process ya maendeleo inahitaji viongozi wawe makini. Kwani wao ndio wata-instill the right attitudes kwa watu wao.
 
AshaDii,

Unalosema lina ukweli mkubwa sana. Lakini miaka ya 70 watanzania walifanya vitu vingi bila kutegemea sana serikali. Walijenga mashule ya msingi kwa nguvu za wananchi. Kwa sisi tulio kaa Mwanza, kiwanja cha Kirumba na sekondari za wakulima ni ushahidi wa kutosha.

Tatizo linalokuja ni kuwa, viongozi wa Tanzania hawajuhi ku-manage expectations za kazi za kujitolea. Na hii imekatisha tamaa sana. Unapowajengesha watu shule, wanategemea watoto wao wafanye vizuri. Waendelee na masomo au kupata ujuzi wa kuwasaidia.

Kuna nchi zimeanza kutoa MBA za jinsi ya kuendesha mashirika ya kujitolea (NGO) Nadhani umefika kwa viongozi wa Tanzania nao kuanza kujifunza kuwa hili watu waendelee kujitolea na kutoitegemea sana serikali kuna vitu muhimu vya kuangalia.
Kuna mtu kaandika haya (hana access na jukwaa hili):
Dr mayunga said:

Kwanza heri ya pasaka...

Nashukuru kwa mawazo mazuri yenye lengo la kuendeleza nchi yetu.

Mimi napenda kueleza pande zote tatu na jins gan kila pande imeshindwa kutekeleza jukumu lake il kuleta maendeleo kwa watanzania wenyewe na nchi nzima kwa ujumla. Pande ninazokwenda kuongelea ni VIONGOZI WA NCHI NA WATANZANIA WENYEWE, PAMOJA MITAALA YA ELIMU YETU.

Kwanza nianze na upande wa VIONGOZI:
Viongozi wa Tz hawana uzalendo si kwa nchi tu bal kwa wananchi kwa ujumla. Tuongelee umuhim wa kuwepo kwa financial institution in Tz.... tuache mabenk twende kwenye non banking financial institutions(NAFKR MMENPATA) sipend kuztaja majina... Hizi taasisi zinatoa mikopo mpaka asilimia 300% believe me or not. Hv tunakwenda wap? Tunawatakia nini watanzania? Haya achana na hiyo tuna TUNA SECURITY FUNDS, znafanya nn? Kaz yake ni kutumia pesa zetu kujiendeleza zenyewe...lakin unafk r tatzo ni nn? VIONGOZ WETU, HAKUNA SHERIA ZINAZOZBANA HZ TAASIS ZIWEZE KUWAFEVA WANACHAMA WAKE, wanakaa na pesa zetu zaid ya miaka 30 mwisho wa siku anakurudishia pesa ileile bila kuangalia thaman ya pesa kwa wakat huo,Tatzo n nn? UONGOZI...

NARUD KWA WATANZANIA WENYEWE, watanzania tuna tatzo la uvivu, hatuko tayar kufanya kaz kwa bidii, tunataka vtu kwa miujiza. Hatuko tayar kujitoa.

NAOMBA NIONGELEE MITAALA YA SHULE ZETU, SHULE za msing mpaka VYUO...
TUNAFUNDISHWA KUAJIRIWA, HATUFUNDSHWI KUJIAJIRI...

Napenda kumnukuu mmoja wa wshadhili wa chuo kimoja ni rafk yangu. Huyu bwana ana ADA,CPA NA MASTERS, ingawa sijui ana masters ya kitu gan... Nilmpigia simu na kumuuliza, how is life? Aliniambia NILITEGEMEA NIKISOMA SANA NDO NITAKUWA NA MAISHA BORA, LAKINI SIONI NILCHOKITARAJIA. Y? Elimu tuipatayo shuleni/haitupi elimu ya kujiajiri bali kuajiliwa.


Mapendekezo:
1. Tuchague viongozi waadilifu na wenye uzalendo kwa nchi yetu.
2. Iundwe SECURITY FUND REGURATHORY AUTHORITY na FINANCIAL REGU ambayo ita regulate hz security funds.
3. Katba, katba,katba!! Jaman katba tuwe nayo karibu, tuifuatilie , tutoe michango yetu il tuweze kupata katba ambayo iyaweza kuwabana viongozi ambao si waadilifu.
4. Jaman mitaala yetu irekebishwe ili iweze kutoa elimu ya kujiajiri si kuajiriwa.
5. Nasi wananchi tubadlke tufanye kazi kwa bidii, tuachane na mambo ya miujiza, hata biblia inasema "ASIYEFANYA KAZI NA ASILE" hakuna kitu kizuri unachoweza kupata kirahisi, unapaswa kufanya kazi.

Watanzania tubadlike, viongozi peke yao hawawezi kuleta mabadliko kama sisi wenyewe hatuko tayari kufanya kazi, let's play our part and the government wl play its parts.
........let's take action.......
.....asanten watanzania....
 
Azimio Jipya, Sio kwamba mtu anapokuwa Result Oriented basi ethic and moral anakuwa hana. Ethics na moral code ni lazima viwepo. Kiongozi wanapowachangisha watu kwa sababu ya miradi ya maendeleo, ni lazima awe na uhakika kuwa michango ya watu haitatumiwa kwa matumizi binafsi na vilevile watu watapata kile walichoambiwa au kuchangishwa.

Nia ya mada hii ni kutoka kwenye maamuzi ya kisiasa ambayo ni utamaduni wa nchi yetu na kuangalia mbinu mbalimbali za uongozi na utekelezaji ambazo zinatumika na wenzetu. Au zimetumika katika fani nyingine kama vile za biashara, elimu, uhandisi na kijeshi kuleta maendeleo.

Kwa mfano ukichukua ujenzi wa daraja, kwa sisi watumiaji tunaona kama vile limeshuka kutoka mbinguni. Lakini kwa wajenzi kuna mambo mengi. Kuna architect anayechora daraja. Kuna soil mechanics wanaongalia aina ya udongo. Kuna concrete engineers, kuna muhasibu anayefanya malipo, kuna mtu wa utumishi ambaye anafanya ajira, kuna mtu wa procurement, na wengine wengi.

Ukichukua mfano wa ujenzi wa daraja na kuutumia katika kuinua kiwango cha elimu ya sekondari kwa watoto wa mkoa wa Lindi katika kipindi cha miaka mitano utaona kuna mambo yanayofanana ki-uongozi na kwenye usimamizi wa utekelezaji.

Tukirudi kwenye hoja yako ya ufafanuzi au definition. Utaona kuwa wajenzi wa daraja wana clear definition kabla ya kuanza kazi. Na hawaanzi kazi kabla detail ya kile kinachotakiwa (matokeo au results) kuwepo.

Kuhusiana na miradi ya kisiasa nchini Tanzania, definition, details na uchambuzi wake ni vitu vinavyokuwa havieleweki. Serikali inajenga mashuleni na baadaye inaonekana kuna upungufu wa waalimu na vifaa vya kufundishia. Hili ni tatizo kubwa ambalo limeshajenga utamaduni.

Hivyo definition za kiutendaji ambazo zinakubalika na watendaji na wafaidika wa matokeo ni lazima ziwe za kueleweka na sio kila mtu atumie vile anavyoelewa yeye.

Kwa mfano, utekelezaji wa elimu ya UPE ulikuwa na matatizo yake. Matatizo haya yameandikwa na kufanyiwa kazi na watanzania waliopo kwenye sekta ya elimu. Hivyo utekelezaji wa mipango ya elimu ya kata ulitakiwa usirudie makosa ya UPE. Cha kushangaza umerudi.

Nafikiri naafiki kuwa mtindo tulio nao wa kujikitika kwenye mwelekeo wa kisiasa peke yake ili kujenga Ustawi wa jamii na Taifa la Tanzania haujatuletea mafanikio ya kiwango chenye kuleta matumaini.

Niseme pia kuwa nimevutiwa na mtizamo au mfumo wa "RESULT ORIENTED". Ambacho nina hakika nacho kuhusu mfumo huo kufanya kazi kikamilifu ni kuwa uko so demanding kwa watumiaji wake wawe highly ethical and fully awakened in moral superiority as the primary driving force running all human activities in their society! Kwa hiyo kama ninachoongea na kuona kama ni kweli huo mfumo una mahitaji MAZITO sana ambayo sidhani Watanzania wengi wanaweza kufikia hatua ya kuutumia kwa ufanisi wa kuleta sio Development ila Civilization. Huwa napenda kutenganisha hizo dhana mbili kwani Development (Maendeleo) yanawez akufikiwa bila driving forces za Ethics na Moral Codes wakati Civilaizastion(Ustawi wa maendeleo ya Ki/Ustaarabu) ni maendeleo yaliyozingatia Ethics, moral codes and all human factors.

Hapa nitahitaji kusahihiswa na kusaidiwa sana! Kwani ninaamini kuwa kufikia ngazi ya Maendeleo yenye Ustaarabu kamili lazima hiyo jamii iwe imepitia SHOCK OF PAINFULLY TRUTH inayolingana na Vita ya dunia. Sidhani kama kuna lecture au kongamano, Azimio, Sera au Mustakabali wa kitaifa ua kijamii unaweza kuzaa Ustawi wa ngazi ya Civilization Bila jamii hiyo kujikuta kwenye vita kuu ya kidunia moja kwa moja au Maumivu Makali ya kuiamsha jamii hiyo yenye uzito kama wa vita ya dunia. Mfano ni kama Ruanda. Imepitia MSHINDO wa MAUMIVU makali sana kwa mauaji ya wenyewe kwa wenyewe yenye uzito wa kutosha na hilo limewaamsha kwenye Thamani za UTAMBUZI wa thamani za UBINADAMU na kuwafanya wawe tayari kustawi katika misingi ya kutokuusaliti thamani za ubinadamu katika ustawi na maendeleo ya Mwanadamu.

MSHINDO WA MAUMIVU ni muhimu sana kumreform mwanadamu na kumfanya aweze kutumia mfumo mzuri kama wa Result Oriented. Jambo ambalo sidhani kama kuna mtu yuko tayari kuyasababisha hayo maumivu mwenyewe na kuyakabili ili kufikia lengo la mjadala huu. Lakini Kama kuna mbinu zaidi ya VITA na Machafuko niko tayari kuisikia.

Mimi nafikiri Azimio la Arusha lilikuwa na Maumivi makali yanayozidi vita kuu ya kwanza na ya pili weka pamoja!! Sio kwamba naliunga mkono lakini naonyesha kuwa kilikuwa ni CHOMBO kisichokwepeka kwani kwangu ni sawa na Maumivu VITA au Maumivu ya Machafuko ambayo wenzetu wamepitia na Kuwaamsha KIUFAHAMU na sasa wana AKILI na FIKRA Timamu katika maswala ya uzalishaji, ustawishaji na maendeleo kwenye jamii zao.
 
Sidhani kama kuna universal definition ya development na kujaribu ku-define is like fighting a loosing battle. Wengine wamejaribu kuja na indicators of development lakini ukweli ni kwamba maendeleo yanatofautiana kati ya jamii na jamii na hata mtu na mtu. Kuna mtu kuwa na hosipitali anaona ni maendeleo zaidi kuliko kuwa na barabara ya lami, n.k.

Lakini nadhani kuwa katika suala zima la kuondoa umaskini kuna umuhimu mkubwa sana wa kuwahusisha walengwa moja kwa moja. Kwa sana una kukuta policies nyingi za maendeleo zinawekwa na kufanyiwa kazi bila kuwahusisha hao masikini. Matokeo yake tunaishia kujenga daraja sehemu fulani tukidhani ndio tunawaletea maendeleo jamii husika kumbe wao wanahitaji kitu kingine tofauti kabisa.

Kama nilivyosema kwenye post yangu ya mwanzo kuwa katika kuondoa umaskini kuna umuhimu mkubwa wa kutumia indigenous knowledge kutoka kwa hao maskini wenyewe. Kukaa tuu kwenye ghorofa Dar Es Salaam au New York na ku-design alleviation policies kwa watu wanaoishi Tandahimu bila hata kuwahusisha, sidhani kama kutasaidia kuindoa tatizo la umaskini hata kama ni result oriented.

EMT

Nilipokuwa collage nikadhihirisha kabisa kuwa yule professor alinipa jibu kama la kwako kuhusu what really define what is development ... sikurudi tena kwneye lile darasa la DS(?) kwani angenisahihishia huo mtihani basing on what?! Kwani niliona the whole thing is so subjective na hakuna objectivity yeyote hivyo kila mtu anaweza kusema chochote na hasa kama ana MAMLAKA makubwa kama, World Bank, UN, Donors, Presidents, Lecturers nk Lakini sidhai kama hiyo ni fair kabisa!

Tuje kwenye mada! Nafikiri kama hutajali, labada ungenifafanulia kuhusu Indigenous knowledge ni zipi na zinavyoweza kutumika kikamilifu kwenye ujenzi na ustawi wa maendeleo ya jamii unaozingatia kutosalitiwa kwa human values za jamii husika.
 
Kwa sana una kukuta policies nyingi za maendeleo zinawekwa na kufanyiwa kazi bila kuwahusisha hao masikini. Matokeo yake tunaishia kujenga daraja sehemu fulani tukidhani ndio tunawaletea maendeleo jamii husika kumbe wao wanahitaji kitu kingine tofauti kabisa.

Kama nilivyosema kwenye post yangu ya mwanzo kuwa katika kuondoa umaskini kuna umuhimu mkubwa wa kutumia indigenous knowledge kutoka kwa hao maskini wenyewe. Kukaa tuu kwenye ghorofa Dar Es Salaam au New York na ku-design alleviation policies kwa watu wanaoishi Tandahimu bila hata kuwahusisha, sidhani kama kutasaidia kuindoa tatizo la umaskini hata kama ni result oriented.

Niiliwa Kuandika huko nyuma sisi watu wa mjini ( Ilala,kindndni,Mwanza mjiniarushamjin au NYC) sometime tuna kasumba Priority zetu za kmijini mjini ndio tunadahni zinatakuwa uwa za sehemu zote
Utaona watu wanapiga picha shule fulani kibondo.au kasulu au manyoni wakiwa wanafudishwa chini ya mwembe au wamekaa chini au shule ya kijijini ikiwa hina choo cha kmijini mjini ......Ofcorse ni tatizo shule kutokuwan a choo au madawati lakini je ni sahihi priority za shule ya msingi kibondo ziwe sawana bunge primary . Je Kuna faida kubwa kupeleka dawati kwa shule ambazo hata majumbani kwao hawana utamaduni wa viti ?

So Kwangu mara nyingi huwa nafikiria badala ya dawati kuwa 1st Priority Bora ile Pesa itumike kununua vitabu kwa kila mwanafuzi.Then Priority ya madawati na mengine yaje baadae

zakumi said:
EMT,

Miaka ya zamani kulikuwa na sera ya adult education. Ilikuwa ni noble idea. Wazee wakalazimishwa kwenda kujifunza kusoma na kuandika. Lakini moja ya matatizo ya sera hii haikutilia mkazo indigenous knowledge au uboreshaji wa skills ambazo indigenous wanazitumia katika maisha yao ya kila siku. Sera hii ilipokufa nguvu, matokeo yake yalikuwa yaleyale kabla ya sera haijaanzishwa.

Hivyo nakubaliana na hoja kuwa matokeo tunayotarajiwa ni lazima yahusishe the concerns of stakeholders: their culture, expectations, and environmental factors.

Zakumi bora hiyo elimu ya lazima kwa watu wazima ilisaidia kuondoa ujinga wa kusoma na kuandika . Hiyo ilikuwa hatua moja. Iikuwa na mapugufu lakini milestone ya kupunguza watu wasijuo kusoma na kuandika kwa TZ ilifanikiwa kidunia. Kotoka kwenye base hiyo ilitakiwa sasa itolewe elimu ya kumsaidia mwananchi katika Real life ya mazingira yake

Ila kwa sasa nachoshangaa kwa nn serikali haioni umuhimu wa kutoa elimu fulani kulingana na mazingira.

Enzi nasoma nakumbuka jiografia darasa la tatu tuliijifunza Mkoa , la nne Tanzania ,LaTano afrika........

Kwa mtiririko huo huo yangewekwa masomo amabayo hata kama mtu akiishia Prmary au sekondary Moa fulani basi awe na maarifa fulani ya jamii kulinganana eneo. Masomo kama haya mwazoni wanaweza kuyafundisha tu kama invyofundishwa (DS) A level

Mfano
  • mi naona si nafunzi wa tabora au singida wa darala sabaau hata Fourm IV wanamaliza bila kujua kitu kuhusu ufugaji wa nyuki na kurina asali
  • Si sawa wanafunzi wa mikoa inayozunguka ziwa victoria/Tanganyika/Nyasa kutofundishwa intro japo ya uvuvi na au Kuogelea

Ukiangalia taaluma ya hayo mambo mawilii inarithishwa na na sometime bado ni ya kazamani. sijui nani alaumiwe.

Kuna wanariadha wa ethiopia na kenya wameondoa umasikini wa famiia na vijiji vyao na zaidi kutangaza publicity nautaii wa nchi zao. Sasa sisi tatizo 99% tume focus kweny elimu ya kalamu. na mtu kufika mlimani,IFM mzumbe basi inaonekana huyo ndiyo anajua........
 
EMT

Nilipokuwa collage nikadhihirisha kabisa kuwa yule professor alinipa jibu kama la kwako kuhusu what really define what is development ... sikurudi tena kwneye lile darasa la DS(?) kwani angenisahihishia humo mtihani basing on what?! Kwani niliona the whole thing is so subjective na hakuna objective yeyote hivyo kila mtu anaweza kusema chochote na hasa kama ana MAMLAKA makubwa kama, World Bank, UN, President, Lecturers nk Lakini sidhai kama hiyo ni fair kabisa!

Tuje kwenye mada! Nafikiri kama hutajali, labada ungenifafanulia kuhusu Indigenous knowledge ni zipi na zinavyoweza kutumika kikamilifu kwenye ujenzi na ustawi wa maendeleo ya jamii unaozingatia kutosalitiwa kwa human values za jamii husika.

Indigenous knowledge ni resource inayotumika at the local level na jamii husika kama basis ya kufanya maamuzi yanahusiana na mambo mbalimbali kama kilimo afya, elimu, natural resources management na shughuli nyingine muhimu za kijamii na kiuchumi. Indigenous knowledge ndiyo social capital ya watu maskini na pia ni asset kubwa ya ki-control maisha yao ya kila siku.

Kwa mfano, kwa Tanzania, indigenous knowledge kwenye kilimo iko kwenye form ya tacit knowledge (than explicit knowledge) gained through experience. Tacit knowledge inawasadia wakulima kufanya maamuzi bila kuhusisha principles. Kwa mfano, upandaji mazao, kukabidhiana wadudu wanaoharibu mazao, kutunza maji, vyakula, mgawanyo wa ardhi (soil and land classification, soil management, conservation and treatment of seeds).

Nakumbuka wakati nikiwa mdogo kijijini kwetu tulikuwa tunalima mahindi marefu. Ilikuwa inatuchukua zaidi ya miezi sita mpaka nane kuyavuna. Mara serikali ikaleta mbegu mpya za mahindi mafupi. Haya ulikuwa unavuna mapema sana. Lakini wazee kijijini walikuwa wananung'unika kimya kimya kuwa japokuwa waliweza kuyavuna mapema, hayo mahindi mapya yalikuwa yanamaliza rutuba ya ardhi kwa speed kali sana. Yalihitaji rutuba kubwa na maji.

Hali hii ililazimisha kutumia mbolea ya kukuzia ya chumvi chumvi badala ya mbolea za kawaida tulizokuwa tunatumia kwa sababu zilikuwa zinachukua muda mrefu kidogo kurutubisha ardhi. Zaidi, mbolea ya chumvi chumvi ilikuwa inaua kabisa ardhi in the long term. Matokeo yake walikuwa wanavuna mapema lakini kadri muda ilivyokuwa unaenda ardhi ilikuwa inakufa kwa kukosa rutuba.

Sasa hivi ukipanda tena mahindi pale hayastawi unless utumie mbolea ya chumvi chumvi. Lakini watu vijijini hawana uwezo wa kununua hiyo mbolea. Kama serikali ingetumia indigenous knowledge ya hawa wanavijiji wangejua kuwa kilimo cha yale mahindi yangeharibu ardhi in the long term.

Nikupe mfano mwingine huko Msumbiji. Baada ya miaka mingi ya civil wars, local community leaders waliweza ku-manage karibu 500,000 informal land transactions. Ndani ya miaka miwili tuu waliweza pia kusaidia wakimbizi zaidi ya milioni 5 ku-settle. Walifanikiwa haya yote bila kupata msaada toka nje (donors na serikali kuu).

Walifanikiwa kufanya hivyo kwa kujikita zaidi kwenye mila na desturi zao za kutatua migogoro iliyokuwa inajitokeza kati ya wakimbizi waliokuwa wanarudi na wale waliokuwa wanaishi kwenye hiyo ardhi wakati wa civil war. Matokeo yake, wamiliki wadogo wadogo wa ardhi waliweza ku-settle kwa haraka zaidi na kuanza tena kilimo kilichoweza kuchangia kukua kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo. Utakumbuka our traditional dispute settlement methods - win a little, loose a little. Lakini siku hizi, the winner takes all.

Mfano mwingine, huko Senegal, donors wakishirikiana na serikali kuu walikuwa walijitahidi kwa miaka mingi kupiga marufuku ukeketaji wa wanawake bila mafanikio. Eventually, indigenous knowledge ilisaidia kuleta mabadiliko kitaifa. Baada ya kuhudhuria an adult literacy course, makundi ya wanawake kutoka vijijini waliamua kulizungumzia tatizo hilo ndani ya jamii zao na kuweza ku-convince traditional spiritual leaders kuungana nao kupiga kampeni dhidi ya ukeketaji.

Ndani ya miaka miwili tuu, hao wanawake walifanikiwa kuwashauri jamii jirani 16 kupiga marufuku ukeketaji wa wanawake. Wanawake hao waliendelea kushawishi jamii nyingine kwa mafanikio makubwa na hatimaye serikali ikafanikiwa kupitisha sheria bila pingamizi yoyote to declare the practice illegal in Senegal. Kitu cha kushangaza ni kwamba kampeni ya hawa akina mama iliweza kusambaa pia kwa wanawake wa nchi jirani na kusaidia jamii zaidi ya 200 kupiga marufuku ukeketaji wa wanawake.

Uzuri wa indigenous knowledge haina gharama kubwa, inaongeza ufanisi kwenye programmes za maendeleo kwa sababu it is a locally owned and managed resource. Indigenous knowledge inasaidia kuongeza efforts za sustainable development kwa sababu process ya integration inatoa nafasi for mutual learning and adaptation, which in turn contributes to the empowerment of local communities, which is the core objective of most development efforts.

Kwa kuelewa za indigenous knowledge kuna mbongo mmoja ameandika article titled: "The relationship of indigenous knowledge and Technological innovation to poverty alleviation in Tanzania" (http://smartech.gatech.edu/xmlui/bi...efa_Mwantimwa_The_relationship.pdf?sequence=1) Huyu anaangalia zaidi jinsi uhusiani wa indigenous knowledge na teknologia katika kuondoa umaskini Tanzania.
 
Kuna wanariadha wa ethiopia na kenya wameondoa umasikini wa famiia na vijiji vyao na zaidi kutangaza publicitynautaii wa nchi zao. Sasa sisi tatizo 99% tume focus kweny elimu ya kalamu. na mtu kufika mlimani,IFM mzumbe basi inaonekana huyo ndiyo anajua.

Yep, hili nalo ni tatizo. Wapo watu wengi tuu wenye vipaji vya aina mbalimbali lakini hatuthamni hawa watu na kuendeleza vipaji vyao. Hakuna investment kwenye kuendeleza vipaji vya watu hasa watoto. Pia plans zetu hasa kwenye michezo ni mbovu na hazina realistic approach.

Kwa mfano mwaka 2010, baada ya nchi za Afrika Mashariki kukosa kuwa na mshiriki hata mmoja kwenye Kombe la Dunia, Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga alisema: "First we are aiming at the African Cup of Nations finals in two years from now. Thereafter we are going to work towards the 2014 World Cup. I am confident Kenya will be there in 2014."

Je, walifanikiwa kushiriki African Cup of Nations baada ya miaka miwili (yaani mwaka huu)? Nope. Kuna uwezekano wa Kenya kushiriki kwenye Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014? Sidhani. Kwa upande wa Tanzania ni hivyo hivyo. Hatuna long term strategic plannings kwenye fani za michezo ambayo inaweza kuondoa umaskini kwa kiwango kikubwa tuu. Mpaka sasa hata sijui maandalizi ya ushiriki wetu kwenye Olympic ijayo yakoje.

Sasa linganisha na Ivory Coast. Aliyekuwa rais wao huko nyuma ali-set a strategic plan (result-oriented?) ya Ivory Coast kushiriki kwenye Finaili za Kombe la Dunia baada ya miaka 25. Kuanzia hapo walianza kuwaandaa watoto wadogo for that purpose. Ndio hao akina Drogba, n.k tunaowaona sasa. Waliandaliwa tokea utotoni. Kweli walifanikiwa kucheza Fainali za kombe la dunia kwa mara ya kwanza mwaka 2006.

Kuanzia hapo, Ivory Coast sio tuu imefanikuwa kimpira barani Afrika, bali pia imekuwa na wachezaji nyoja ambao wanasaidia sana kupunguza umasjini nchini kwao. Nasikia wachezaji 23 wa timu yao ya taifa wamejitolea kujenga hosipitali kubwa na ya kisasa na Drogba ame-pledge pounds milioni tatu.

 
Last edited by a moderator:
......Mpaka sasa hata sijui maandalizi ya ushiriki wetu kwenye Olympic ijayo yakoje.

Kuna ka- thread niliazisha january nikilienga kuleta mjadal wenyes wali kama lako. Lakini sote tunajua 100% tutashiriki inawezekana viongzi wa msafaar tayari wana visa lakinivievile wotetunajua 99% hatuna na hatujajiandaa watu wetu kushindana..

Angalia JWTZ ina vituo kadhaa vya kuuza pombe kwa raia kwa bei chee. lakini hajatokea Kiongzoi hata mmoja wa jeshi au serikali kuona hatari ya wale watoto pale magogoni wanaoogolea kwa kujirusha kutoka kwenye pantoni.Hivi kuna gharama gani Kikosi cha kigamboni kuazisha kituo cha kuonglea na wakakifungua japo kila weekend kwa watoto. Tena huu ni uwekezaji endelevu kwenye jamii na taifa kwa ujumla

Angalia yule kijana mwendesha baskeli wa kisukuma alipotembelea kikwete . Kwa kiongozi mwenye VISION ndogo anaweza kumpa zawadi ya Milioni then kwisha . Lakini kwa kiongozi mwenye strategicVISION alitakiwa aone kipaji na binsfi ningekuwa mimi basi angedhminiwa kwenye kushiriki kwenye tour mojawapo ya mashindano ya basikeli ya kimataifa. Ni iasi cha mafunzo kidogo tu sababu kipaji vijana wa usukumani kwa kuendesha baiskeli hata kina Armstroong hawaoni ndani. Hii nimeshuhudia mimi mwenyewe wakiwa wanaedesha hizo baiskeli zao( Wao wanziita dala-dala)

Mwaka jana nilishangaa kwenye michezo fulani ya kimataifa Kulikuwa na muogeleaji wa burundi. Sasa Tanzania tuna faida gani ya kuwa na ukanda wote wa bahari na maziwa matatu. Vitu vingineni kashfa ukisikia waogoleaji kutoka dodoma wamewashinda waogeleaji kutoka Zanzibar au Tanga

So kuna tatizo tumeconcetrate kwenye kazi za kalamu tu ( white collar jobs)

BTN
Someni uzi huu wa jwtz-jkt-je-hii-haiwezekani.html . Ila inashangaza kuna watu wanaamini kuna taaisis hatutakiwi kuzzizungumia katika sula zima la kushiria kundoa umasikini japo taasis hizo nyeti zinaweza kuwa na mchango na zina rasimali muhimuya kuwawezesha na kufanikisha mambo mengi watanzania
 
Mkandara,

Nafikiri si kukuelwa vizuri au sikukulewa kabisa!

Unamaana Kwa Matamshi hayo "Results oriented" haijalishi MORAL VALUES katika process ya kufikia malengo yake? AU nikuulize moja kwa moja kama hutajali ... Hivi Unaunga mkono hayo matamshi yako? AU ulitaka ileweke kwa upande wa pili kuwa huungi mkono?

Ndio maana nauliza kwenye Kanuni inayo Define Development swala la Moral value, Nobility, Credibility and all human virtues ... LIPO? Au ni kulingana na Macho na mtizamo wa muhusika!

Kwa mfano Mtu anaposema Wachina wamepiga hatua! Wanamaendeleo mazuri na ya haraka ... Anatumia vigezo vipi? Bila kuvijali mimi nahoji kigezo cha Ustawi wa MAADILI na HAKI za BINADAMU ... Kinakuwepo kwenye mchakato wa Kusema maendeleo ni nini?

AU nichukue mfano mwingine Tuna taarifa kuwa Rwanda inafanya vizuri kimaendeelao nasikia inakwenda kasi kuliko hata Tanzania ... Nataka kujua kanuni gani zinatumika kufikia mtizamo huo na majibu hayo!

Na pia naongezea Kama hayo matokeo yaliyoitwa Maendeleo Mazuri na ya haraka yamefikiwa kwa kuangamiza Maadili, haki za binadamu na Ukandamizaji wa Kidikteta au vitu kama hivyo... bado yanakuwa kwenye range ya definition ya What is development and poverty eradication?
Hoja yangu ni kupinga mtazamo wa Zakumi na watu wengi wanaofikiria kwamba viongozi wetu hawakupanga ama kutegemea matokeo ya haya tunayoyaona.

Mimi najua fika kwamba Azimio la Zanzibar lilipangwa hususan kuhakikisha wao viongozi wanatajirika ama niseme wanakamata njia za uchumi kwa kujrithisha mali kupitia sheria ambazo zililegezwa kwao. Ukilisoma Azimio la Zanzibar vizuri utaona jinsi linavyopingana na Azimio la Arusha lakini bado hawa hawa viongozi wetu walkisema bado malengo yetu ni ujenzi wa Taifa la Kijamaa na Kujitegemea. Wameua TRA, ATC, na mashirika mengine mengi tu makusudi ili wao waendeshe biashara hizo (Kina Yona na Mramba).

Hao viongozi wetu ni wasomi wazuri tu iweje Waliyafilisi (liquidation) mashirika badala ya kubinafsisha? (Privatization).. Na bado mashirika kama Tanesco, Dawasco na TTCL yamedorora kikazi makusudi kutokana na kuendelea kutumia mitambo ile ile aloiacha mwalimu. Hivi kweli ni akili kujenga mabarabara kwa kutumia mabillioni wakati reli ya kati, kusini na kaslkazini zimekufa? hii pekee najua wanafanya makusudi ili wao waendelee kuwekeza ktk usafiri wa malori - Everything is results oriented ni sawa na kutembea na mwanamke bila kinga, ukasema sikutegemea mimba..

Kuhusu China mkuu wangu tuwaache hao jamaa kama walivyo maana tunalinganisha walipotoka na leo wamefika wapi, ndio maendeleo yanayozungumziwa na kwa kigezo cha kuutazama Ubepari at best.. Kwa kila kitu wamepiga hatua kubwa sana japokuwa sehemu nyingine za kijamii haiwezi kulinganishwa na nchi za magharibi lakini ikumbukwe ni miaka 15 tu toka wameanza ujenzi wa Taifa jipya. Leo hii mtu anatoka New York akienda China mwenyewe anabakia domo wazi kwa sababu ya miundombinu iliyojengwa na inayojengwa kwa maandalizi ya uwekezaji na uzalishaji..
 
................Mimi najua fika kwamba Azimio la Zanzibar lilipangwa hususan kuhakikisha wao viongozi wanatajirika ama niseme wanakamata njia za uchumi kwa kujrithisha mali kupitia sheria ambazo zililegezwa kwao. Ukilisoma Azimio la Zanzibar vizuri utaona jinsi linavyopingana na Azimio la Arusha lakini bado hawa hawa viongozi wetu walkisema bado malengo yetu ni ujenzi wa Taifa la Kijamaa na Kujitegemea. Wameua TRA, ATC, na mashirika mengine mengi tu makusudi ili wao waendeshe biashara hizo (Kina Yona na Mramba)........

You are quite right Bob Mkandara.............Azimio la Zanzibar halina tofauti na story ya Animal Farm......... we knew exactly what we want as a nation............ikafika pahala NIDHAMU ikatutoka....na ndio tunaona matokeo yake leo hii....na matokeo haya.....tulijua fika kuwa itakuwa hivi......

suala la "indigenous knowledge" ni muhimu sana.......na katika feasibility study za miradi mingi hili suala linaangaliwa lakini ni kwa ajili ya kurembesha ripoti tu......kwani bado tunaona rasilimali zetu za asili, ardhi ikiwemo zikiendelea kupoteza thamani yake na vingine kupotea kabisa siku hadi siku..........then the question is what do we do?...

huko nyuma tumezungumza mengi........nawakumbuka akina Rev Kishoka, Mdondoaji, Mkandara, Mzee Mwanakijiji, Nyani Ngabu, jmushi, Prof Mwl Kichuguu, Prof Mwl A. Moshi, Mwanasiasa, Steve D, Kuhani, Kyoma, Dr.WHO, Invisible na wengine wengi....kwa sasa ngoja niendelee kusoma michango yenu........


Wakuu EMT, Zakumi, Azimio Jipya, Mtazamaji na wengine heshima mbele kwa elimu.............
 
You are quite right Bob Mkandara.............Azimio la Zanzibar halina tofauti na story ya Animal Farm......... we knew exactly what we want as a nation............ikafika pahala NIDHAMU ikatutoka....na ndio tunaona matokeo yake leo hii....na matokeo haya.....tulijua fika kuwa itakuwa hivi......

suala la "indigenous knowledge" ni muhimu sana.......na katika feasibility study za miradi mingi hili suala linaangaliwa lakini ni kwa ajili ya kurembesha ripoti tu......kwani bado tunaona rasilimali zetu za asili, ardhi ikiwemo zikiendelea kupoteza thamani yake na vingine kupotea kabisa siku hadi siku..........then the question is what do we do?...

huko nyuma tumezungumza mengi........nawakumbuka akina Rev Kishoka, Mdondoaji, Mkandara, Mzee Mwanakijiji, Nyani Ngabu, jmushi, Prof Mwl Kichuguu, Prof Mwl A. Moshi, Mwanasiasa, Steve D, Kuhani, Kyoma, Dr.WHO, Invisible na wengine wengi....kwa sasa ngoja niendelee kusoma michango yenu........


Wakuu EMT, Zakumi, Azimio Jipya, Mtazamaji na wengine heshima mbele kwa elimu.............


Ogah, Mkandara:

Kuna ukweli kuhusu maadili ya uongozi na viongozi kushindwa kufuata maadili hayo. Katika utangulizi wa thread hii nimeuliza je iwapo viongozi wa Tanzania watafuata maadili yote ya uongozi vizuri kabisa, kutakuwepo na maendeleo?

Ngoja nibadilishe lugha ya swali hili. Je kama viongozi wote watanzania watafuta maagizo ya Azimio la Arusha kutakuwepo na maendeleo?

Kwa maoni yangu viongozi wanaweza kufuata maadili ya azimio la Arusha kwa nguvu zote na bado maendeleo yasipatikane.

Kwenye utekelezaji wa kuleta mafanikio kuna mambo mengi. Kuna stakeholders ambao ni watalajiwa wa kutumia matokeo. Je wako tayari? Hakuna kipengere chochote cha Azimio la Arusha au Zanzibar kinachotaka kiongozi apate input kutoka kwa stakeholders.

Pili kwenye utekelezaji kuna environmental factors. Kutoa elimu ni noble idea. Lakini je kufundisha mtoto wa familia za wafugaji, wavuvi, na wakulima kutakuwa sawa? Azimio la Arusha au Zanzibar halisemi kitu chochote kile kuhusu environmental factors.

Tatu kwenye utekelezaji kuna umuhimu wa kutumia mbinu za utekelezaji zinazofaa (best practises). Azimio la Arusha au Zanzibar alisemi chochote kuhusu matumizi mazuri ya mbinu za utekelezaji.

Nne kwenye utekelezaji kuna umuhimu wa kutumia expertise. Azimio la Arusha au Zanzibar alisemi kuwa kiongozi anapotekeleza lazima atumie the best expertise available.

Vilevile haya maazimio ni product ya TANU, na CCM. CUF, CHADEMA na Vyama vingine vya kisiasa havina msimamo wa maazimio. Sasa kwanini tusio wanachama au wapenzi wa CCM tuhusike na mjadala wa maazimio haya?
 

Kwanza heri ya pasaka...

Nashukuru kwa mawazo mazuri yenye lengo la kuendeleza nchi yetu.

Mimi napenda kueleza pande zote tatu na jins gan kila pande imeshindwa kutekeleza jukumu lake il kuleta maendeleo kwa watanzania wenyewe na nchi nzima kwa ujumla. Pande ninazokwenda kuongelea ni VIONGOZI WA NCHI NA WATANZANIA WENYEWE, PAMOJA MITAALA YA ELIMU YETU.

Kwanza nianze na upande wa VIONGOZI:
Viongozi wa Tz hawana uzalendo si kwa nchi tu bal kwa wananchi kwa ujumla. Tuongelee umuhim wa kuwepo kwa financial institution in Tz.... tuache mabenk twende kwenye non banking financial institutions(NAFKR MMENPATA) sipend kuztaja majina... Hizi taasisi zinatoa mikopo mpaka asilimia 300% believe me or not. Hv tunakwenda wap? Tunawatakia nini watanzania? Haya achana na hiyo tuna TUNA SECURITY FUNDS, znafanya nn? Kaz yake ni kutumia pesa zetu kujiendeleza zenyewe...lakin unafk r tatzo ni nn? VIONGOZ WETU, HAKUNA SHERIA ZINAZOZBANA HZ TAASIS ZIWEZE KUWAFEVA WANACHAMA WAKE, wanakaa na pesa zetu zaid ya miaka 30 mwisho wa siku anakurudishia pesa ileile bila kuangalia thaman ya pesa kwa wakat huo,Tatzo n nn? UONGOZI...

NARUD KWA WATANZANIA WENYEWE, watanzania tuna tatzo la uvivu, hatuko tayar kufanya kaz kwa bidii, tunataka vtu kwa miujiza. Hatuko tayar kujitoa.

NAOMBA NIONGELEE MITAALA YA SHULE ZETU, SHULE za msing mpaka VYUO...
TUNAFUNDISHWA KUAJIRIWA, HATUFUNDSHWI KUJIAJIRI...

Napenda kumnukuu mmoja wa wshadhili wa chuo kimoja ni rafk yangu. Huyu bwana ana ADA,CPA NA MASTERS, ingawa sijui ana masters ya kitu gan... Nilmpigia simu na kumuuliza, how is life? Aliniambia NILITEGEMEA NIKISOMA SANA NDO NITAKUWA NA MAISHA BORA, LAKINI SIONI NILCHOKITARAJIA. Y? Elimu tuipatayo shuleni/haitupi elimu ya kujiajiri bali kuajiliwa.


Mapendekezo:
1. Tuchague viongozi waadilifu na wenye uzalendo kwa nchi yetu.
2. Iundwe SECURITY FUND REGURATHORY AUTHORITY na FINANCIAL REGU ambayo ita regulate hz security funds.
3. Katba, katba,katba!! Jaman katba tuwe nayo karibu, tuifuatilie , tutoe michango yetu il tuweze kupata katba ambayo iyaweza kuwabana viongozi ambao si waadilifu.
4. Jaman mitaala yetu irekebishwe ili iweze kutoa elimu ya kujiajiri si kuajiriwa.
5. Nasi wananchi tubadlke tufanye kazi kwa bidii, tuachane na mambo ya miujiza, hata biblia inasema "ASIYEFANYA KAZI NA ASILE" hakuna kitu kizuri unachoweza kupata kirahisi, unapaswa kufanya kazi.

Watanzania tubadlike, viongozi peke yao hawawezi kuleta mabadliko kama sisi wenyewe hatuko tayari kufanya kazi, let's play our part and the government wl play its parts.
........let's take action.......
.....asanten watanzania....

Dr Mayunga:

Nashukuru kwa mchango wako. Nirudi kwenye sifa moja ya wananchi wenyewe.

Nimebahatika kukaa nje ya Tanzania. Katika nchi nilizokaa kuna spirit of nation au mentality. Wamarekani wanayo get it done, enterprenureship. Siku zote tunawataja Bill Gates au Steve Jobs. Lakini ni wamarekani wengi wenye kufanya hivyo. Kuna Mmarekani mweusi ambaye alikuwa anafanya kazi katika vipuri vya magari kama mlinzi au mesenja tu( nitatafuta story na kuileta). Kampuni ikawa inakufa kutoka na viwanda kukosa soko. Akahamua kuingia maktaba na kujifunza mambo ya management. Baaday akaandika proposal ya kuinunua kampuni na kuonyesha business plan yake. Sasa hivi kampuni inafanya kazi kwa faida. Huyu ni mtu ambaye hana elimu ya chuo kikuu lakini guts zake tu. Wajerumani wana mentality ya kutoku-compromise quality for quantity, precision, iron and blood (nguvu kazi).

Je watanzania tuna spirit gani? Mtu anakopa pesa benki anakwenda kucheza upatu au DECI, that explains a lot.

Nikiwa chuo hapo Tanzania kijana mmoja wa kisukuma alihamua kuacha shule na kwenda nyumbani kufanya biashara. Mambo yalipomshinda akarudi chuo na kutukuta wenzake tunamaliza. Tukamcheka sana lakini huyu jamaa angekuwepo Marekani, watu wangesema afadhari alijaribu.
 
Niiliwa Kuandika huko nyuma sisi watu wa mjini ( Ilala,kindndni,Mwanza mjiniarushamjin au NYC) sometime tuna kasumba Priority zetu za kmijini mjini ndio tunadahni zinatakuwa uwa za sehemu zote
Utaona watu wanapiga picha shule fulani kibondo.au kasulu au manyoni wakiwa wanafudishwa chini ya mwembe au wamekaa chini au shule ya kijijini ikiwa hina choo cha kmijini mjini ......Ofcorse ni tatizo shule kutokuwan a choo au madawati lakini je ni sahihi priority za shule ya msingi kibondo ziwe sawana bunge primary . Je Kuna faida kubwa kupeleka dawati kwa shule ambazo hata majumbani kwao hawana utamaduni wa viti ?

So Kwangu mara nyingi huwa nafikiria badala ya dawati kuwa 1st Priority Bora ile Pesa itumike kununua vitabu kwa kila mwanafuzi.Then Priority ya madawati na mengine yaje baadae



Zakumi bora hiyo elimu ya lazima kwa watu wazima ilisaidia kuondoa ujinga wa kusoma na kuandika . Hiyo ilikuwa hatua moja. Iikuwa na mapugufu lakini milestone ya kupunguza watu wasijuo kusoma na kuandika kwa TZ ilifanikiwa kidunia. Kotoka kwenye base hiyo ilitakiwa sasa itolewe elimu ya kumsaidia mwananchi katika Real life ya mazingira yake

Ila kwa sasa nachoshangaa kwa nn serikali haioni umuhimu wa kutoa elimu fulani kulingana na mazingira.

Enzi nasoma nakumbuka jiografia darasa la tatu tuliijifunza Mkoa , la nne Tanzania ,LaTano afrika........

Kwa mtiririko huo huo yangewekwa masomo amabayo hata kama mtu akiishia Prmary au sekondary Moa fulani basi awe na maarifa fulani ya jamii kulinganana eneo. Masomo kama haya mwazoni wanaweza kuyafundisha tu kama invyofundishwa (DS) A level

Mfano
  • mi naona si nafunzi wa tabora au singida wa darala sabaau hata Fourm IV wanamaliza bila kujua kitu kuhusu ufugaji wa nyuki na kurina asali
  • Si sawa wanafunzi wa mikoa inayozunguka ziwa victoria/Tanganyika/Nyasa kutofundishwa intro japo ya uvuvi na au Kuogelea

Ukiangalia taaluma ya hayo mambo mawilii inarithishwa na na sometime bado ni ya kazamani. sijui nani alaumiwe.

Kuna wanariadha wa ethiopia na kenya wameondoa umasikini wa famiia na vijiji vyao na zaidi kutangaza publicity nautaii wa nchi zao. Sasa sisi tatizo 99% tume focus kweny elimu ya kalamu. na mtu kufika mlimani,IFM mzumbe basi inaonekana huyo ndiyo anajua........

Mtazamji,

Kasumba ni kitu kibaya sana na kinatupotezea pesa nyingi. Hakuna ubaya mtu kusoma chini ya mwembe iwapo elimu inayopatikana chini ya mwembe inamfanyisha mwanafunzi kumudu mazingira yake.

Wakati wa enzi ya mkoloni kuna watu walikwenda mashuleni wakivaa shuka. Viongozi wa Tanzania hawataki kutoa historia ya maisha yao. Lakini mzee Mandela anasema alivaa shuka.

Kwanini inakuwa ni lazima kwa mtoto wa kimasaai kwenda shule na uniform. Je kuna ubaya gani akienda darasani na shuka au msuli wake.

Kuhusiana na elimu ya watu wazima na elimu ya jadi. Mambo mengi kaeleza EMT. Kuna utafiti unaonyesha kuwa watu siojua kusoma na kuandika ni watu wa Oral Traditions. Wanahifadhi mambo yao mengi kichwani na wamejenga systems zao ambazo zinaendesha maisha yao bila wasiwasi wowote. Hivyo sio kweli wao ni wajinga. Ni welevu na wenye kumudu mazingira yao.

Babu yangu hakwenda shule. Huu ni mwaka zaidi ya 20 toka amefariki lakini ukienda kijijini utakuta nyumba aliyojenga kwa mikono yake bado imesimama na nyumba yenyewe ina zaidi ya miaka 60. Na alitumia kila kitu kipatikanacho kwenye mazingira yake.
 
Ogah, Mkandara:

Kuna ukweli kuhusu maadili ya uongozi na viongozi kushindwa kufuata maadili hayo. Katika utangulizi wa thread hii nimeuliza je iwapo viongozi wa Tanzania watafuata maadili yote ya uongozi vizuri kabisa, kutakuwepo na maendeleo?

Ngoja nibadilishe lugha ya swali hili. Je kama viongozi wote watanzania watafuta maagizo ya Azimio la Arusha kutakuwepo na maendeleo?

Kwa maoni yangu viongozi wanaweza kufuata maadili ya azimio la Arusha kwa nguvu zote na bado maendeleo yasipatikane.

Kwenye utekelezaji wa kuleta mafanikio kuna mambo mengi. Kuna stakeholders ambao ni watalajiwa wa kutumia matokeo. Je wako tayari? Hakuna kipengere chochote cha Azimio la Arusha au Zanzibar kinachotaka kiongozi apate input kutoka kwa stakeholders.

Pili kwenye utekelezaji kuna environmental factors. Kutoa elimu ni noble idea. Lakini je kufundisha mtoto wa familia za wafugaji, wavuvi, na wakulima kutakuwa sawa? Azimio la Arusha au Zanzibar halisemi kitu chochote kile kuhusu environmental factors.

Tatu kwenye utekelezaji kuna umuhimu wa kutumia mbinu za utekelezaji zinazofaa (best practises). Azimio la Arusha au Zanzibar alisemi chochote kuhusu matumizi mazuri ya mbinu za utekelezaji.

Nne kwenye utekelezaji kuna umuhimu wa kutumia expertise. Azimio la Arusha au Zanzibar alisemi kuwa kiongozi anapotekeleza lazima atumie the best expertise available.

Vilevile haya maazimio ni product ya TANU, na CCM. CUF, CHADEMA na Vyama vingine vya kisiasa havina msimamo wa maazimio. Sasa kwanini tusio wanachama au wapenzi wa CCM tuhusike na mjadala wa maazimio haya?

Zakumi, Ogah & Mkandara.

Ni Vema swala la MAADILI (ethics & all moral values) kama MSUKUMO wa kijamii, kwa mjadala huu limejitokeza waziwazi kwani binafsi nalichukulia kama Nguzo ya awali ya kusukuma chochote chenye maana ambacho kitastawisha na kukuza maendeleo na mwanadamu. Lakikini mara nyigi hii DRIVING FORCE imechukuliwa kama subsidiary component katika maswala ya maendeleo na kufuta umasikini, ujinga, maradhi nk.

Ninaamini kabisa kwenye Results oriented system hasa kwa sababu ni objective na tuseme inapimika na kutathmikina kiukweli. Lakini Lazima iwe driven na maadi ya kiwango cha juu.

Kama Maadili ni Mkono wa KULIA Basi Result Oriented system ni Mkono wa KUSHOTO vyote kwa pamoja tunapata MATOKEO lakini si kimoja peke yake.

Kama kuna azimio ambalo lingekuwa la msingi lingekuwa mfumo wowote ambao utakuwa objectively driven na Maadili unaokwenda na wakati husika na unaokubalika na jamii husika. Kama tukikubaliana kuwa huu ni wakati wa kuingiza kwa dhati kabisa mfumo wa Result oriented kwenye jamii ya Kitanzania basi, Hakika Nguvu ya kuusukuma iwe ni Maadili katika kina na upana wake. Kwani kama kuna mahali huo mfumo ulifanya kazi na kuleta mafanikio ya kishindo ni lazima ulikuwa driven na High ethical and moral values za jamii hiyo.

Swali ni kama jamii yetu ina kiwango cha dhati cha maadili, nidhamu, heshima na virutubisho vyote vya kibinaadamu vya kuubeba mfumo kama huo, kwani tumeyaona kwenye maazimio yaliyotajwa hapo juu. Kwani ni kuli tupu kuwa hakuna aliyeko tayari Kupata Maaumivi ili kukidhi Maadili ya kuedesaha hatakamradi kadogo ka saloon ya kusuka au kunyoa.

Kama ni hivyo swali linalalofuata ni kuwa ni vipi jamii ina reform na kuwa yenye maadili, ustahimilivu, nidhamu ya kazi, uadilifu, uzalendo, ubinadamu na MAUMIVU yanayoendana na dhana kama hizi ili iweze kuwa kamilifu kutumia mifumo kama hiyo ambayo imeshatumika sehemu nyingine mbalimbali na kuonyesha mafanikio ya kuridhisha?

Kwani ni hakika Uadilifu na Maadili yote ya kibinadamu yanaendana na MAUMIVU na KUJITOA kwa namna fulani kama sehemu ya Utekelezaji wake. Hivi ni kweli kuna Mtanzania aliyeko tayari kwa hilo? Kwa wanasiasa ndio kabisaaa, wote hili haliwezekani kwani hakuna mwanasiasa ambaye yuko tayari kuwaingiza wapiga kura wake kwenye maumivu ya uadilifu na kujitoa kwani hawatampigia kura kipindi kijacho na kiukweli hapa ndipo siasa za Tanzania zilipo, Kinachoendelea ni ujinga mtupu, ni kuwadanganya wananchi kuwaonyesha kuwa hawana haja ya kukabiliana na Maumivu ya nidhamu ya kazi, malezi, uongozi, kujieleimisha nk kama sehemu ya kujikubali katika kujitoa kujiletea maendeleo na kupata matokeo stahili yatakayo wawezesha Kijitegemea na kuheshimika kama binadamu huru na kamili! Na hatimaye kurejesha heshima na kujiamini kama Taifa!
 
Indigenous knowledge ni resource inayotumika at the local level na jamii husika kama basis ya kufanya maamuzi yanahusiana na mambo mbalimbali kama kilimo afya, elimu, natural resources management na shughuli nyingine muhimu za kijamii na kiuchumi. Indigenous knowledge ndiyo social capital ya watu maskini na pia ni asset kubwa ya ki-control maisha yao ya kila siku.

Kwa mfano, kwa Tanzania, indigenous knowledge kwenye kilimo iko kwenye form ya tacit knowledge (than explicit knowledge) gained through experience. Tacit knowledge inawasadia wakulima kufanya maamuzi bila kuhusisha principles. Kwa mfano, upandaji mazao, kukabidhiana wadudu wanaoharibu mazao, kutunza maji, vyakula, mgawanyo wa ardhi (soil and land classification, soil management, conservation and treatment of seeds).

Nakumbuka wakati nikiwa mdogo kijijini kwetu tulikuwa tunalima mahindi marefu. Ilikuwa inatuchukua zaidi ya miezi sita mpaka nane kuyavuna. Mara serikali ikaleta mbegu mpya za mahindi mafupi. Haya ulikuwa unavuna mapema sana. Lakini wazee kijijini walikuwa wananung'unika kimya kimya kuwa japokuwa waliweza kuyavuna mapema, hayo mahindi mapya yalikuwa yanamaliza rutuba ya ardhi kwa speed kali sana. Yalihitaji rutuba kubwa na maji.

Hali hii ililazimisha kutumia mbolea ya kukuzia ya chumvi chumvi badala ya mbolea za kawaida tulizokuwa tunatumia kwa sababu zilikuwa zinachukua muda mrefu kidogo kurutubisha ardhi. Zaidi, mbolea ya chumvi chumvi ilikuwa inaua kabisa ardhi in the long term. Matokeo yake walikuwa wanavuna mapema lakini kadri muda ilivyokuwa unaenda ardhi ilikuwa inakufa kwa kukosa rutuba.

Sasa hivi ukipanda tena mahindi pale hayastawi unless utumie mbolea ya chumvi chumvi. Lakini watu vijijini hawana uwezo wa kununua hiyo mbolea. Kama serikali ingetumia indigenous knowledge ya hawa wanavijiji wangejua kuwa kilimo cha yale mahindi yangeharibu ardhi in the long term.

Nikupe mfano mwingine huko Msumbiji. Baada ya miaka mingi ya civil wars, local community leaders waliweza ku-manage karibu 500,000 informal land transactions. Ndani ya miaka miwili tuu waliweza pia kusaidia wakimbizi zaidi ya milioni 5 ku-settle. Walifanikiwa haya yote bila kupata msaada toka nje (donors na serikali kuu).

Walifanikiwa kufanya hivyo kwa kujikita zaidi kwenye mila na desturi zao za kutatua migogoro iliyokuwa inajitokeza kati ya wakimbizi waliokuwa wanarudi na wale waliokuwa wanaishi kwenye hiyo ardhi wakati wa civil war. Matokeo yake, wamiliki wadogo wadogo wa ardhi waliweza ku-settle kwa haraka zaidi na kuanza tena kilimo kilichoweza kuchangia kukua kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo. Utakumbuka our traditional dispute settlement methods - win a little, loose a little. Lakini siku hizi, the winner takes all.

Mfano mwingine, huko Senegal, donors wakishirikiana na serikali kuu walikuwa walijitahidi kwa miaka mingi kupiga marufuku ukeketaji wa wanawake bila mafanikio. Eventually, indigenous knowledge ilisaidia kuleta mabadiliko kitaifa. Baada ya kuhudhuria an adult literacy course, makundi ya wanawake kutoka vijijini waliamua kulizungumzia tatizo hilo ndani ya jamii zao na kuweza ku-convince traditional spiritual leaders kuungana nao kupiga kampeni dhidi ya ukeketaji.

Ndani ya miaka miwili tuu, hao wanawake walifanikiwa kuwashauri jamii jirani 16 kupiga marufuku ukeketaji wa wanawake. Wanawake hao waliendelea kushawishi jamii nyingine kwa mafanikio makubwa na hatimaye serikali ikafanikiwa kupitisha sheria bila pingamizi yoyote to declare the practice illegal in Senegal. Kitu cha kushangaza ni kwamba kampeni ya hawa akina mama iliweza kusambaa pia kwa wanawake wa nchi jirani na kusaidia jamii zaidi ya 200 kupiga marufuku ukeketaji wa wanawake.

Uzuri wa indigenous knowledge haina gharama kubwa, inaongeza ufanisi kwenye programmes za maendeleo kwa sababu it is a locally owned and managed resource. Indigenous knowledge inasaidia kuongeza efforts za sustainable development kwa sababu process ya integration inatoa nafasi for mutual learning and adaptation, which in turn contributes to the empowerment of local communities, which is the core objective of most development efforts.

Kwa kuelewa za indigenous knowledge kuna mbongo mmoja ameandika article titled: "The relationship of indigenous knowledge and Technological innovation to poverty alleviation in Tanzania" (http://smartech.gatech.edu/xmlui/bi...efa_Mwantimwa_The_relationship.pdf?sequence=1) Huyu anaangalia zaidi jinsi uhusiani wa indigenous knowledge na teknologia katika kuondoa umaskini Tanzania.

EMT

Maelezo yamekidhi kwa kiasi kikubwa nilichokuwa nakitafuta!

Kwanza, Kuwa maana ya maendeleo ni uwezo wa kujitatulia MATATIZO yanayokuzunguka na kukukabili bila kupoteza au kuharibu UASILI wako kama mwanadamu ambao ni Uadifu na maadili yote kibinadamu, Period!! Kwa hiyo sidhani kuna jamii ambyo iko tayari kuendelea kuwepo bila sifa hizo na ushahidi ni hizi elimu ambazo tayari zipo na zilichipua katika jitihada ya kupamabana na matatizo ya jamii husika.

Pili, Kwa kuwa ni naamini ustawi wowote wa mwanadamu unahitaji kwa kiasi cha kutosha Maumivu ya nidhamu mbalimbali za kijamii hadi kufikia kuwepo na elimu na mbinu mbalimbali kama hizo lazima jamii husika zilipitia UZOEFU ambao bila shaka ulizigharimu Maumivi ya kijamii ya kuziwezesha kupata matokeo husika. Nategemea katika hatua za mabadiliko haya kilichokuwa na manufaa kwa jamii husika kilidumu na kuendelea na kile ambacho moja kwa moja hakikufaa kilitupiliwa mbali. Kimsingi sijui ni kiasi gani Taifa imetumia uzoefu kama huo? Uzoefu amabao sio wa kinadhari ni uzeofu ambao umejaribiwa na kufanyiwa kazi.

Tatu, Kwa kuwa Jamii ya Kitanzania ilipo sasa hivi inakabiliwa na tatizo kubwa la KIMAADILI kuliko la kiteknolojia kwenye Kufanya KAZI na kupata Matokeo yenye thamani KIBINADAMU na KITEKNOLOJIA, nafikiri ni lazima kufuatia au kufanyike tafiti kuweza kugundua MAADILI (Ethics and all human virtues) yalipatikanaje, yalijengwa vipi, yalilindwa vipi, yalidumishwa vipi hadi kufikia Matokeo ambayo yapo tayari. Matokeo yaliyopatikana kwenye mazingira yetu, ambayo siyo ya kutoka sehemu nyingine na hatimaye tujaribu kutumia mfumo wa maadili hayo kwanza.

Nne, Hivi elimu hizi si zilipelekea Matokeo na ufanisi wa namna fulani kwenye jamii husika? Kwa hii sio Result oriented? Kwa jibu lolote litakalopatikana hapo, Swali! Je Hatuwezi kufanya kama tu UPDATE!! hicho tunachoweza kukiita "Indigenous result oriented" badala ya kuja na ku install program mpya kabisa ya kitu hicho hicho kwa malengo hayo hayo?
 
Nne, Hivi elimu hizi si zilipelekea Matokeo na ufanisi wa namna fulani kwenye jamii husika? Kwa hii sio Result oriented? Kwa jibu lolote litakalopatikana hapo, Swali! Je Hatuwezi kufanya kama tu UPDATE!! hicho tunachoweza kukiita "Indigenous result oriented" badala ya kuja na ku install program mpya kabisa ya kitu hicho hicho kwa malengo hayo hayo?

Wengi wana-regard globalisation kama results-oriented ambayo ina-embrace consumerism, individualism, competition and efficiency. Globalisation inaweza kuua local cultures kwa kuwa ina-transform jamii kupitia sayansi na teknologia which may in turn lead to the demise of local knowledge.

Kwa sababu ya globalisation, unakuta jamii nyingi kutozingatia tena umuhimu wa local knowledge au inajaribu ku-invent concepts ambazo zina-comply na globalisation. Globalisation inatufanya tujikite zaidi kwenye results-oriented approaches ili kuwanufaisha consumers, ku-compete na wengine and kuwa more efficient bila hata kuangalia the impact of the results to the local community itself. Ndiyo yale aliyosema Mtazamaji kuwa unakuta mtu anajisifia mwaka jana tulijenga madarasa 1000 wakati hakuna hata kitabu kimoja kilichonunuliwa.

Hiyo "indigenous result-oriented" sidhani kama nimekuelewa. Nafikiri kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na community oriented development projects regardless of whether or not they are results oriented. Development projects ziwe zinaishirikisha jamii husika kwenye process zote (planning, monitoring, evaluation, etc). Kufanya hiyo kutakuwa na effective utilisation of indigenous knowledge.

Siyo unaamka asubuhi na kusoma/kusikia kwenye vyombo vya habari eti serikali imeamua kupeleka umeme kijiji kwako mwakani wakati wewe mwanakijiji hujashirikishwa kabisa kwenye hiyo project na kutokana na your local knowledge unajua wazi kuwa pale kijijini tatizo siyo umeme bali ni maji.

Unakumbuka enzi za sungusungu? Mara nyingi local communities zilikuwa zina-organise kila kitu kuanzia kupanga ratiba za walinzi, monitoring and evaluation. Nakumbuka kijijini kwangu, they way ilivyokuwa conducted increased the relations within the community maana hata wezi walijikuta nao wanalinda. Kwa hiyo hata kama community fulani inapingana na serikali lakini wakihusishwa kikamilifu kwenye development projects nao watapenda kushirikiana na serikali, in terms of sharing their knowledge, etc.
 
Poverty Elimination in Tanzania is a "Result Oriented Business"......Where are we?

Wakuu, mengi yenye weledi mmeyaandika.....ninachoona kwenye huu "mnakasha" ni kuwa wachangiaji wanajaribu kuainisha how efficient and/or effective hizo results zaweza kuwa katika jamii yetu hata tukafika pahala tunapopahitaji..............

Pamoja na kuwa kuna risks associated na modern technologies.......hatuhitaji ku-invent another wheel wakati technologies are readily available........due diligence inahitajika kwa vijana wetu wasomi kujua ni technologies zipi ni effective kwa mazingira yetu na ikibidi ziwe adjusted ku-suit (Chinese Government and other South East Asia Countries did a lot on these technologies).............but again/ofcourse not the detriment kwa rasilimali zetu........

Community participation kwenye miradi ya maendeleo ni jambo la msingi sana, mjumbe mmoja ameandika hilo katika post zilizopita....however, community bila elimu ya kuweza ku-marry the local/indigenous knowledge and modern knowledge.....itakuwa ni tatizo........

Zakumi anasema..........tunaweza tukawa na viongozi walio na maadili kama yalivyoainishwa ndani ya Azimio la Arusha na bado tusiweze kupata kile tunachotarajia...........

Maendeleo yeyote yana misingi yake, Uongozi wowote una misingi yake (hata wezi wana misingi yao...joke!), Professionals wana misingi yao.....kwa hiyo suala la maadili viongozi pekee haliwezi kuleta maendeleo kama halitakuwa complemented na nyanja nyingine za maendeleo...........

...kuhusu Azimio la Arusha....kama sikosei......Ni Azimio Jipya/Rev Kishoka alianzisha mjadala wa kulichambua......ulikuwa mjadala mzuri.......i.e. kuboresha pale tutapoona inafaa......my point here ni kwamba.....kujadili maazimio yaliyoletwa na vyama mbali mbali si dhambi...........hata kama sisi si wanasiasa au wanachama wa vyama husika..........i mean we must start somewhere!......atleast kulikuwepo na watu waliofikiri something.......au hata kuiga....ili mradi isiwe "copy and paste"......we must do our homework right........

Once again Wakuu.........heshima mbele kwa mjadala maridhawa........
 
AshaDii,

I suggest you should read: The Elusive Quest for Growth. Mwandishi William Easterly kafanya kazi katika nchi nyingi Afrika. Na vitu vingine anavyoeleza ni hivi tunavyovizungumza hapa.

Unauliza kama kuinua kiwango cha elimu kunaleta maendeleo, basi nchi nyingi za kiafrika zingekuwa zimeendelea. Kwa mfano 1972 Tanzania ilikuwa inapeleka shule 25% ya watoto. Na sasa hivi inapeleka zaidi 75% lakini umasikini bado hupo palepale.

Kama demokrasi ya nchi za magharibi (katiba) ni msingi wa maendeleo, kwanini South Korea, China au Asian Tigers zimeendelea zikiwa katika udikteta? Sera nzuri za maendeleo sio lazima zipangwe na katiba.

Inawezekana kikwazo chetu cha maendeleo kinatokana na kwamba we haven't found the missing link. Je hiyo missing link ni nini? Katiba? Good governance? Foreign Investments? Education?



Zakumi mimi belief yangu ni kua walau kuna hope for the future kuliko huko nyuma... Nimependa huo mtazamo wako wa "Missing Link" Na nikijaribu kufikiria hapa kweli kabisa jawabu sina ila ninazo assumptions nyingi sana; which does not solve the matter. Na hii inayofanya kue na quest ya kutaka kujua quest ya what/where/why we are stagnant na kurudi nyuma Ki mantik badala ya kusongas inasukumwa na the fact kua zile nchi (hasa Asian) ambazo tulikua nazo sambamba sio wenzetu tena na sasa wanadevelop kwa kasi ya ajabu!

BTW Tunarudi kule kule.... wapi naweza pata hicho kitabu kwa uraisi?
 
Zakumi, Ogah & Mkandara.

Ni Vema swala la MAADILI (ethics & all moral values) kama MSUKUMO wa kijamii, kwa mjadala huu limejitokeza waziwazi kwani binafsi nalichukulia kama Nguzo ya awali ya kusukuma chochote chenye maana ambacho kitastawisha na kukuza maendeleo na mwanadamu. Lakikini mara nyigi hii DRIVING FORCE imechukuliwa kama subsidiary component katika maswala ya maendeleo na kufuta umasikini, ujinga, maradhi nk.

Ninaamini kabisa kwenye Results oriented system hasa kwa sababu ni objective na tuseme inapimika na kutathmikina kiukweli. Lakini Lazima iwe driven na maadi ya kiwango cha juu.

Kama Maadili ni Mkono wa KULIA Basi Result Oriented system ni Mkono wa KUSHOTO vyote kwa pamoja tunapata MATOKEO lakini si kimoja peke yake.

Kama kuna azimio ambalo lingekuwa la msingi lingekuwa mfumo wowote ambao utakuwa objectively driven na Maadili unaokwenda na wakati husika na unaokubalika na jamii husika. Kama tukikubaliana kuwa huu ni wakati wa kuingiza kwa dhati kabisa mfumo wa Result oriented kwenye jamii ya Kitanzania basi, Hakika Nguvu ya kuusukuma iwe ni Maadili katika kina na upana wake. Kwani kama kuna mahali huo mfumo ulifanya kazi na kuleta mafanikio ya kishindo ni lazima ulikuwa driven na High ethical and moral values za jamii hiyo.

Swali ni kama jamii yetu ina kiwango cha dhati cha maadili, nidhamu, heshima na virutubisho vyote vya kibinaadamu vya kuubeba mfumo kama huo, kwani tumeyaona kwenye maazimio yaliyotajwa hapo juu. Kwani ni kuli tupu kuwa hakuna aliyeko tayari Kupata Maaumivi ili kukidhi Maadili ya kuedesaha hatakamradi kadogo ka saloon ya kusuka au kunyoa.

Kama ni hivyo swali linalalofuata ni kuwa ni vipi jamii ina reform na kuwa yenye maadili, ustahimilivu, nidhamu ya kazi, uadilifu, uzalendo, ubinadamu na MAUMIVU yanayoendana na dhana kama hizi ili iweze kuwa kamilifu kutumia mifumo kama hiyo ambayo imeshatumika sehemu nyingine mbalimbali na kuonyesha mafanikio ya kuridhisha?

Kwani ni hakika Uadilifu na Maadili yote ya kibinadamu yanaendana na MAUMIVU na KUJITOA kwa namna fulani kama sehemu ya Utekelezaji wake. Hivi ni kweli kuna Mtanzania aliyeko tayari kwa hilo? Kwa wanasiasa ndio kabisaaa, wote hili haliwezekani kwani hakuna mwanasiasa ambaye yuko tayari kuwaingiza wapiga kura wake kwenye maumivu ya uadilifu na kujitoa kwani hawatampigia kura kipindi kijacho na kiukweli hapa ndipo siasa za Tanzania zilipo, Kinachoendelea ni ujinga mtupu, ni kuwadanganya wananchi kuwaonyesha kuwa hawana haja ya kukabiliana na Maumivu ya nidhamu ya kazi, malezi, uongozi, kujieleimisha nk kama sehemu ya kujikubali katika kujitoa kujiletea maendeleo na kupata matokeo stahili yatakayo wawezesha Kijitegemea na kuheshimika kama binadamu huru na kamili! Na hatimaye kurejesha heshima na kujiamini kama Taifa!
Mkuu wangu umenipa shibe.. yaani nimeshiba na darsa hili vizuri sana kiasi kwamba nakubaliana na wewe 100%..lakini umesahau kitu kimoja tu ambacho kipo juu ya yote haya - DIRA

Unajua binafsi yangu naamini sababu ya umaskini wetu ni kukosa DIRA..na ndilo lililosukuma sisi kupoteza hata Principals, ethic na moral values kwa sababu hatujui tunakwenda wapi.. Nothing bound us together to begin with, hata tufikie kuweka maazimio. Tatizo la umaskini wetu sii tu sisi wananchi kwa ujumla wetu ama leadership bali vyote hivi vimefikwa na mapungufu kwa sababu hatuna DIRA ya Taifa gani tunalotaka kulijenga isipokuwa taifa la kufikirika kama hadithi za vitabuni zinazosubiri kutengenezwa sinema. Tusijidanganye ya kwamba tunataka kujenga Taifa la Ujamaa na Demokrasi hii ni hadithi maana haiwezekani na wala hakuna chumi yoyote duniani unaolenga Demokrasia na Ujamaa kama malengo ya Utaifa ktk kutafuta maendeleo. HAKUNA kitu kama hicho ktk mwongozo wa Kitaifa maana huu ni UTU ambao maskini na hata tajiri wote kwa ujumla wao wanzipenda zifa hizi.

Hivyo hata maendeleo yetu yanayopatikana ni sinema tu hayana ukweli ndani yake maana hayalengi kutafuta yaliyo juu ya Umaskini, Ujinga na Maradhi maana haya ni Maazimio yetu tu ambayo kama tutafanikiwa kuyapata tutatafuta maazimio mengineyo wakati dira yetu haibadiliki. Lakini kama Taifa tunataka tuwe nini?. Sasa baada ya hapo ndipo vitu kama ethic na moral values zinapokuja in play ili tupate objective resultrs..
Kwa mfano, kwa kijana anayetaka kuwa daktari, huyu anakuwa na malengo yake toka shule na ndiyo yatamsukuma ktk dira ya kufikia kuwa Daktari japokuwa nyumbani ni maskini lakini umaskini ule hauwezi kuwa sababu yakle kuutaka Udaktari ama ili apate kufuta umaskini ni lazima awe Daktari..Hivyo atakwenda shule ku pursue Udaktari na sii umaskini na ndio itakuwa dira yake. Na maadam focus yake kubwa itakuwa kuwa daktari, basi umaskini utamwondokea siku atakapo kuwa daktari kwa sababu lengo lake halikuwa kufuta umaskini wa familia yake bali awe daktari na mengine yatajijaza yenyewe. Kama Azimio lake ni kuondokana na umaskini basi hata shule hatamaliza atajikuta anauza Nyanya au Umachinga barabarani kwa sababu hakuwa na Dira ya who he wonna be isipokuwa azimio la kuondokana na umaskini..

Hivyo basi sisi wananchi wote kwa sababu tunaweka sana matumaini ktk kuondoa Umaskini, tunafikiria Umachinga kama ndio njia rahisi na nyepesi kutokana na shida kubwa tulizonazo, tunauza madini yetu kwa bei na karanga, hatujali tunaibiwa kiasi gani ili mradi tunapeleka chakula mezani kila kukicha lakini hatufahamu 20 years from now who we wonna be..wala hatuna malengo zaidi ya kutazama umachinga huu utachukua muda gani kutuondoa ktk umaskini tofatui kabisa na nchi za Asia wao walilenga kuwa taifa la ushindani na wakawekeza ktk kujiwezesha kufikia hapa walipo na bado hawajafika wakutakako.
 
Back
Top Bottom