Premier League: Man United yaibamiza Liverpool 2-1, Agosti 22, 2022

Premier League: Man United yaibamiza Liverpool 2-1, Agosti 22, 2022

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Baada ya kuanza msimu vibaya kwa kupoteza mechi mbili mfululizo, Manchester United imeamka na kuipa Liverpool kipigo cha magoli 2-1 katika mtanange wa Premier League kwenye Uwanja wa Old Trafford.

United haikupewa nafasi kubwa ya kushinda katika mchezo huo, ilipata magoli yake kupitia kwa Jadon Sancho na Marcus Rashford dakika ya 16 na 53 huku goli la Liverpool likifungwa na Mohamed Salah dakika ya 81.

Kocha wa Man United, Erik ten Hag aliwaweka benchi Cristiano Ronaldo na Harry Maguire katika mchezo huo.

Kwa matokeo hayo yanaifanya Liverpool kucheza mechi tatu bila ushindi wowote msimu huu.
 
Yaan klopp kazi imemshinda yaani ata kama hao wagonjwa wakirudi sioni viungo wa kuunganisha hii timu yaan ni thiago pekee timu nzima
Mkuu wachezaji nao ni binadamu sio roboti wanachoka!!msimu huu mjiandae tu , tena mbona bado sana!!msimu ulioisha nadhani ndio timu iliyocheza michezo mingi zaidi ulaya!!
 
Tunaridhika mapema sana!
Liverpool wamechoka sana, hawana umakini tena! Ile kukabia kwenye box ya Man Utd, kisha unamuacha mtu free achague pa kupiga, ukutane na strikers makini, tungeokota sana mpira nyavuni.

Mechi mbili za kwanza, mpira umechezwa chezwa ila tukagongwa. Mechi ya leo, butua butua, tumepata pointi 3. Ngoja tuone.
 
Baada ya kuanza msimu vibaya kwa kupoteza mechi mbili mfululizo, Manchester United imeamka na kuipa Liverpool kipigo cha magoli 2-1 katika mtanange wa Premier League kwenye Uwanja wa Old Trafford...
Hiii ndo united Yangu ambayo haitabiriki. Kesho akikutana na Fulham anachezea Kumuacha, Ronaldo ilikuwa big move. Vibanda umiza tumevikimbia siku hiz.
 
Mzimu wa Sadio Mane unawatafuna! Yule jamaa alikuwa muhimu sana kikosini Liverpool!!

Hata Real Madrid walipomwacha Makelele walisuffer!

Man United bado sana!
 
Hongereni Kwa kufufuka, ila mnakomaaga na timu kubwa wakija wakina Brighton mnapumulia mashine
 
😂😂🤣🤣😅😅😆😆😁😁😄😄😃😃😀😀
 
Nimeamini man utd walihitaji saini ya casemiro kwa udi na uvumba. Mara tu fabinho alioingia asee kiungo ya liva iliimarika. Fabinho alifanya ukatili dimba la kati. Pamoja na man utd kuwaweka sjuna fred bado hawakujaa vizuri.
 
Back
Top Bottom