Preta njoo nikutongoze, wengine tulieni mjifunze

Preta njoo nikutongoze, wengine tulieni mjifunze

Preta nijibu pm yangu sim yako haipo hewani kwenye airtel money yako nimekutumia Million 7 kwaajili ya dinner ya kesho!! ooh sorry nimekumbuka ulinitumia email uliniambia kile ki Benz kipya kina slow pancha kipaki kuna ki Rolls Royce new model nimekiagiza Marekani moja kwa moja! Halafu weekend hii nadhani tutakuwa Dubai kwa ya matembezi!!
Hahaaaaa...... ama kweli wewe ndo Jambazi. lol...
 
Mapenzi ni kujituma, si uonewe huruma
Wewe hata si yatima, mali nyingi umechuma
Tochi yako naizima, gizani mpaka kiama
Huruma ni kwa walemavu na wasiojiweza, sio kwenye mahaba

Tengeru ni karibu, upweke katu hutaona
Njoo kwangu unitibu, maumivu nitapona
Tafanya taratibu, gusa kila kona
Preta achana na Vimpire_hunter, jina lake na avatar vinatisha.

Sooth maanaye mkweli, mi jina langu thabiti
Ninayo tamu asali, na kuna pipi kijiti
Achana nae wa mbali, ni kigumu kizingiti
Nitafute Tengeru Sokoni, siku ya mnada

Sina hata benzi, naamini sio kigezo
Pata na la dhati penzi, natilia sana mkazo
Hao sugu kwa uzinzi, kwao huo ndio mchezo
Preta, we will meet somewhere, someday in Arusha-I hope!
Kujituma kwa mke wa mtu, hilo wazolo wallah ni batili
Kamwe ndugu usithubutu, kama muungwana nia yako badili
Umuwache mke wa mtu, mimi moto ndiye mume halali,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.

Mpenzi Preta chunga sana, usijentupa kisa hawara,
Hao ni walaghai sana, katu haiwaishi mikwara,
Kwa hadaa hodari sana, angalia usije pata hasara,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi,

Preta wewe ndo wangu malkia, hata King'asti anajua hilo,
Watu8 mtani chonde shuhudia, pia mod Mexen Melo,
Hatukuanza kwa kuotea, kitambo tumelianza jambo,
Preta Wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.

Preta wewe ni kichuna wangu, wa milele na hata enzi,
Wewe ni mwandani wangu, chonde usigawe langu penzi,
Umekuwa mboni yangu, yadharau yao mabenzi,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.
 
Daaaahhhh....
We jamaa nimekukubali aseee....
Wewe hakyamama uko serious kabisa, nimegundua hutanii..
Labda nikuulize swali...Hambalulu ninini?....na Nswalu ninini?..Ni hayo tu, ukinijibu nahamia upande wako kumsaundisha Preta!!😀😀😀
PakaJimmy... I learned something new about you, brother!. Kukuchokonoa wewe huko unakojificha ni kuanzisha thread ya kumsema Preta!. Unaibuka mara moja... Happy new year bana!. Hivi huyu Preta ndo huyo kwenye hako ka picha?.
 
Achana nao my love,

Sasa Preta ujue mi nakuonaga sku nyingi tu humu,

Nakuzimia balaa, huwezi kushinda njaa, njoo nkupe chapaa, uwaringishie kitaa

Jina lako ni tam, mpaka napata ham, ya kukuomba utam, mpk nikutoe dam

(hapo kwenye dam natania tu)

Nikubali uwe wangu, uwe mwandani wangu, mtamu kama changu, njoo uchezee rungu

Nipe hambalulu, isiwe inaua kama ya lulu, nikujengee hekalu, ule ugali na nswalu

Pretaaaaa oooooh pretaaaaa nipe hambaluluuuu

Preta ooooh Pretaaa nihurumieeeee
hii ngoja nijaribu kwa beki tatu, baadae...
 
preta naitwa rugebalila ni mhaya kutoka kwetu kule kwa matajir kagera nina gar langu la v8 nzur sana natembelea full tank ikipungua lita tano naongez

kila nikionana na trafik njian na hajanisimamisha nageuza gar kumuhonga lak maana namuona labda alikuwa na mawazo nilipokuwa napita namiliki vitu ving sana na ninajuana na wabunge weng sana naomba unipe nafas kwenye moyo wako kwenda marekani itakuwa ni kama kichaa kwenda milembe
hii kweli sherehe imevamiwa na ngedere!!
 
PakaJimmy... I learned something new about you, brother!. Kukuchokonoa wewe huko unakojificha ni kuanzisha thread ya kumsema Preta!. Unaibuka mara moja... Happy new year bana!. Hivi huyu Preta ndo huyo kwenye hako ka picha?.
Mkuu Yegomasika
Salaam Mkuu wangu.
Hakika ni siku nyingi sasa zimepita kiongozi.
Naamini uko vizuri. Mambo ya maisha yanatupoteza kwenye ramani mkuu!.. Ila nimepata taarifa za uwepo wa thread inayomtaka Preta kwa udi na uvumba, nikaona hebu nije nitazamie, maana kabinti tumekalea wenyewe, sasa ni lazima tushuhudie uondokaji wake. Tunataka kaende kwa heshima japo kidogo Mkuu!
Hivi Mkuu ulinambia umeshaoa, au bado?...Haka kabinti kapo singo, na hiyo ndiyo picha yake halisi.
Mana sasa naona huyu, sijui Hunter, sijui Vampaya bado haeleweki!
Ukipita Arusha siku moja tafadhali sana nijuze nikuonyeshe dhahabu hiyo ilipo!...Utafurahi!
 
Kujituma kwa mke wa mtu, hilo wazolo wallah ni batili
Kamwe ndugu usithubutu, kama muungwana nia yako badili
Umuwache mke wa mtu, mimi moto ndiye mume halali,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.

Mpenzi Preta chunga sana, usijentupa kisa hawara,
Hao ni walaghai sana, katu haiwaishi mikwara,
Kwa hadaa hodari sana, angalia usije pata hasara,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi,

Preta wewe ndo wangu malkia, hata King'asti anajua hilo,
Watu8 mtani chonde shuhudia, pia mod Mexen Melo,
Hatukuanza kwa kuotea, kitambo tumelianza jambo,
Preta Wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.

Preta wewe ni kichuna wangu, wa milele na hata enzi,
Wewe ni mwandani wangu, chonde usigawe langu penzi,
Umekuwa mboni yangu, yadharau yao mabenzi,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.
Uwiii! Mbona wagombea mnaongezeka kwa kasi wakati Lubuva ameshatangaza majina rasmi ya wagombea?
 
Kujituma kwa mke wa mtu, hilo wazolo wallah ni batili
Kamwe ndugu usithubutu, kama muungwana nia yako badili
Umuwache mke wa mtu, mimi moto ndiye mume halali,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.

Mpenzi Preta chunga sana, usijentupa kisa hawara,
Hao ni walaghai sana, katu haiwaishi mikwara,
Kwa hadaa hodari sana, angalia usije pata hasara,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi,

Preta wewe ndo wangu malkia, hata King'asti anajua hilo,
Watu8 mtani chonde shuhudia, pia mod Mexen Melo,
Hatukuanza kwa kuotea, kitambo tumelianza jambo,
Preta Wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.

Preta wewe ni kichuna wangu, wa milele na hata enzi,
Wewe ni mwandani wangu, chonde usigawe langu penzi,
Umekuwa mboni yangu, yadharau yao mabenzi,
Preta wangu mahamumu, Achana na hawa walowezi.


Umevamia uwanja, una kasi na pupa
Utaja pakwa wanja, uishie kula mifupa
Nakukata kwa kwanja, nakuweka kwenye chupa
Dirisha la maombi limefungwa, jaribu kwa lara 1!

Wadai mefunga ndoa, hujawahi enda ibadani
Historiayo ina doa, hujulikani bomani
Hapa nakuchojoa, uchi mtupu sokoni
Hiyo ndoa umefungia wap?

Haupo kwake moyoni, acha turushe ndoana
Preta mekuja sokoni, rijali tunachuana
Hakujui hata usoni,wadai mumeoana
Hiyo ndoa ya ndotoni, imefutika baada ya kuamuka

Ni bora mie mlowezi, Tengeru mi mhamiaji
Wewe sifa yako wizi, mesomea ukabaji
Nzito hoja huziwezi, kwangu hoja ni kipaji
Mie mlowezi na mhamiaji, popote atakapoenda Preta, nitamfuata.

Nakupeleka India, uone mbili kwa moja
Waume huridhia,wao wawili mke mmoja
Japo spendi kuchangia, kwa Preta tajikongoja
Kama hutaki kula na wenzio, basi susa wengine tufaidi.
 
Back
Top Bottom