Probability ya kuolewa ukishakuwa na mtoto ni 0.000001%

Probability ya kuolewa ukishakuwa na mtoto ni 0.000001%

Mtoa mada umenigusa mimi nimeachana na mchumba wangu, kwa sababu mimi niko masomoni Alianza kutoka na jamaa lingine, nimekuja kugundua baada ya mwaka mmoja kupita, najiandaa kwenda kwao kutoa mahari nakuta Binti ana mimba jamaa aliempa mimba nae kaishia mitini. Japo nilikuwa nampenda sana ila niliamua kumuacha ila alilia sana. Ila nilimuambia kwenye hii Dunia kupata Mme wa ndoto zako sio rahisi tena maana thamani yako ya kufanya choice umeiharibu mwenyewe.
Wewe sio Mungu hadi umuapie hivyo,na huenda M/Mungu aliyaruhusu hayo ili amuepushie matatizo ya kuishi na wewe!
 
Hivi kwani mtu asipoolewa atakufa? Wanaume wenyewe nyie wachache afu mnategemea kila mtu awe na mwanaume wake ndo azae.
Wew ukisema cha nini wenzako wanasema watakipata lini.
Na nyie endeleeni kuoa wanawake wabichi wasio na watoto ila wametoa mimba mpala mayai yameisha sisi single mothers we are happy the way we are ndo maana tulichagua kuzaa hali na kujua tutapata shida kupata wenza wa maisha yetu ila kwa sisi UHAI wa kiumbe ni bora kuliko NDOA.
Kula like 10000000
 
Ndoa ni muhimu ndo maana ikawepo na ikabarikiwa.

Mwanamke huwezi kuwa salama kama huna ndoa.

Na isitoshe kauli hizi huwa ni za wanawake walio kata tamaa baada ya kujichanganya wenyewe na kujikuta wana watoto na hawako kwenye ndoa, lakini thamini ya ndoa itabakia pale pale. HABARI NDO HIYO!
Usikariri
 
Single mothers nawapendaga sana, ukimugusia kumuoa tu siku hiyohiyo unakaribishwa kwake na unakula mzigo bila dhida.
 
Single mothers nawapendaga sana, ukimugusia kumuoa tu siku hiyohiyo unakaribishwa kwake na unakula mzigo bila dhida.
Kama uliwapitia wachache usiwajumlishe wote kuwa na tabia hiyo, kwa kidudu gani ulichonacho cha kuweza kuthibitisha hilo?wape heshma Dada zako ndugu,
 
Usikariri ndugu huo utafiti wako sijui wa wapi.?me nimeolewa nikiwa singo mama tena nime someshwa kuanzia A level mpaka chuo na kijana tumefunga ndoa akiwa na miaka 32 tunapendana tuna heshimiana
unaweza kua 1 kati milioni 20.
 
Yaani mtoa post hata wakuponde lakn ukweli utabaki pale pale mwanamke alie zalia nyumbani ni asilimia ndogo sana ya kuolewa na kijana ambae haja pata mtoto,yaan ataolewa na wanaume wenye watoto Wakubwa na wengne kuishia kuliwa tu nan aanze kulea litoto la mtu mwisho wa siku baba yake anakuja kuchukua umemkuzia, labda huyo mwanamke awe anajiweza kiuchumi lakn kama ndyo hana hata kaz yeyote kaz kutegemea kuletewa masimango yatamkimbiza tu maana mwanaume akitoka huko amevulugwa akija home litoto linapiga kelele wala sio lake na yy akifikilia hana mtoto,kifuatacho ni kofi tu nenda kwa mama yako
Duuuuh imenichekesha maana ndo ukweli huo....daaah
 
Hizo ni hisia zako, na huenda zimetokana na uzoefu wako binafsi, ila sio lazima iwe hivyo, kuna wanawake wengi wenye mtoto wameolewa bila shida, wanafurahia ndoa zao na pia kuna wadada kibao hawajaolewa na wala hakuna dalili ya kuolewa, pamoja na kwamba hawana watoto. Hiyo ni dhana potofu, tatizo sio kuwa na mtoto, tatizo ni kuwa na sifa za kuolewa, waoaji wanaangalia sifa bora za mke na haijalishi kama ana mtoto ama hana. Kama wewe mdada unahisi huolewi kwasababu una mtoto, huo si mtazamo sahihi, jiangalie upya, yawezekana huolewi kwasababu huna sifa za kuolewa na wala si kwasababu una mtoto. Kuna wadada wenye nafasi kubwa sana ya kuolewa pamoja na kwamba wana watoto, kwasababu ya ubora wao wa kuwa mke.
 
Hivi hawa single mothers wanajipaga mimba wenyewe????

Wengi tu humu nizao la hao single mothers, embu waacheni kama wewe huwezi kuoa wenzio wanawaoa.
tuwe wakweli tu,kwa jamii yetu ya kitanzania ndugu wakijua unaenda kuoa mwanamke mwenye mtoto kwanza linakuwa gumzo.Utasemwa mpaka basi,wengi huikimbia aibu hii.
 
Chonde! Chonde! Akina dada.

Usiombe ukazaa kabla ya kuolewa ukawa single mother.

Ndoto zote za kuwa na mume wa ndoto yako hukoma siku utakapo toka labour ukiwa na mtoto asiye na baba.

Machaguo yote hukimbia hata uwe mzuri vipi. Utajiweka vizuri, utavaa vizuri na njiani utasimamishwa na wakaka watanashati lakini Mwanaume wa karne hii na awamu hii ya 5 ukimwambia tu nina mtoto basi ata-pretend kwa muda ili ale mzigo na baadaye atasepa.

Mdada mwenye mtoto anaishia kuolewa na mibaba iliyokula maisha mpk imechoka. Labda jibaba limefiwa na mkewe, ama limetengana na mkewe na lina watoto wakubwa kama ww. Badala ya kula maisha kwenye 6 kwa 6 unabaki kulilea tu. Unapotaka ku-DO nalo weka soda karibu maana hayakawii kushusha pressure.

Ukiwa na mtoto wanaume wa ndoto yako ndo basi tena. Daaah! [HASHTAG]#Sorry4[/HASHTAG] Single Mothers.
Swali dogo la kizushi... wewe uliyeoa mwanamke asiye na mtoto.... una uhakika watoto unaolea ni wako??

Tuliokula chumvi nyingi tunasema... ni bora ulee mtoto unayejua si wako kuliko kulea mtoto unayedhani ni wako kumbe si wako. Ujinga wako ni mtaji wako.

Single mothers are the best wives... wameshajua machungu ya mahusiano and they are there to stay.

Moral: Toa kwanza boriti kwenye jicho lako, ndio utaona kibanzi kwenye jicho la mwenzako. Single mothers hawakujipa mimba wenyewe. Kuna single fathers kibao mtaani.

Aliyenisikia na kunielewa na aenende katika njia za haki.

Amen
 
Back
Top Bottom