Prof. Anna Tibaijuka, ulikaa kimya wakati unahudumu katika Serikali kandamizi ya hiki unachokikemea sasa kulinda maslahi yako, na sasa kaa kimya!


Mtu akibaka mtoto. Keshokutwa akiona mwenzake anabaka hapaswi mzuia sababu yeye alishabaka? Prof hagombei nafasi yoyote. Alishutumiwa kubaka. Hakupelekwa mahakamani akashtakiwa. Amekaa mtaani ameona kuna mtu anataka kubaka mtoto au anabaka mtoto. Anyamaze? Lowassa alishtumiwa ufisadi akaja gombea urais kupitia chadema. Msiwe double standard
 
Kuna namna wanaccm wakielekea uzeeni wanakuwa wakweli!
Fuatulia... Nyerere... Mkapa... Mwinyi... Lowasa... Kinguge...
A very good observation and a true one! But kama hawakuleta /hakutetea haki wakati walikuwa na uwezo wa kutetea haki, they are as hopless as ever!
 
Lakini aliyoyasema yanaukweli hata JKNyerere aliandika kitabu cha tujisahihishe.
Yana ukweli sana, lakini at one time, akitetea maslahi yake alinyamaza kimya as if there was nothing wrong going on in the governmnt she was serving! "akayafagilia"!
 
Kwani wakati Tibaijuka anahudumu serikalini watu walishushwa kwenye magari wakaenda kuuawa?
Watu walitekwa na kuuwawa kwa kasi ya 5G?
Ili uelewe siku wanao na mwenzi wako atekwe au baba na mama yako watekwe na kuuawa kama mzee Ali wa Tanga
 
Ni sahihi kabisa, kama kweli Prof. Anna katoa kauli kukemea jambo ambalo kwa sasa anaona haliko sawa , ni haki yake Kikatiba kama Mtanzania mwingine. Tuheshimu mawazo yake na uhuru wake wa kujieleza kwa wakati na kwa jambo ambalo yeye anaona inafaa kulisemea ( kulikemea). Tunapaswa kuunga mkono yeyote anayekemea maovu bila kujali alikuwa upande gani au kwa sasa yuko na nafasi gani.
 
Reactions: RMC
Umewasahau wanasiasa walivyo! Huyo anatikisa kiberiti ili apate chochote kitu. Inawezekana amebanwa maslahi yake.

Na jinsi siasa zilivyo, unakuta anapewa teuzi fulani kwa masharti ya kusema mazuri, inabidi aanze kusema hivyo, halafu watu wanabaki kushangaa mbona haeleweki! Kumbe wanasiasa ndivyo walivyo wanaangalia maslahi yao!
 
You are VERY CORRECT!
 
HUU UKWELI, NA NI UKWELI MTUPU, ALIOUSEMA JANA ALIBIDI AUSEME AKIWA NDANI YA MFUMO AU ATOKE.KUONESHA KUWA HAKUBALIANI NA UKANDAMIZAJI DEMOKRASIA!!!!
 

Na hapa ndipo tutakapoendelea kufeli milele:

Tuwatambue wapigania ukombozi mamboleo wasiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili

Hivi huwa mnatafutaga u star kwenye ukombozi?

Itoshe kusema kwa mwendo huu, hakuna ukombozi hapa!

binti kiziwi, imhotep FYI.
 
Sisi tunaomini katika Toba ya Kweli, tunasamehe kweli mtu akisha Tubu na anakuwa amezaliwa upya.. So usimuhukumu Prof na usitabili kwamba akitokea akaitwa kuhudumu latika nafasi nyingine na utawala wa sasa kwamba ataitikia. Huyu mama alishasema anataka kustaafu na alifanya hivyo pasipo shinikizwa. Kumbuka angetaka kuendelea kuwa MP wa jimbo lake, mpaka sasa angekuwa amekalia hicho kiti, but she decided to voluntarily not to vie for the seat in the last election. She is a human of her own. Tuheshimu uhuru wake wa kutoa maoni.
 
HAPANA ! HAPANA ! HAPANA ! Na si kwamba hata huyu mama alinyamaza kipindi cha nyuma. Kile alichoweza kusemea na kukemea alifanya hivyo. Laiti kama kila Mtnzania angelitimiza wajibu wake, basi huenda tusingekuwa hapa tulipo, so tusimtwishe mzigo wa lawama mama huyu, sisi wengine tulikuwa wapi wakati mambo yanaharibika na tusipaze sauti zetu? Au tulisubilia kama yule mzee wa kule aliyesema kwamba Labda Mambo Yakija kuharibiska sana hapa Katikati ! na mpaka sasa hajaona kama yameharibika.
 
Uhuru wake nauheshimu sana tena sana. Ila niko diametrically opposed kwa yeye kujionesha kuwa ni mtu wa kujali demokrasia ambayo amekuwa sehemu ya uharibifu/ukandamizaji/kuitumikia mamlaka ya katili ya demokrasia. This is my argument.
Sina mamlaka na sitakuwa nayo milele kumkataza kusema au kufanya lolote! But we as people who can differentiate and integrate issues, tuseme , tuoneshe wapi huko alikotoka alikosea sana kuungana na watesi wa 60 milioni tanzanians!

Anaweza kweli akawa ametubu, lkn kwa mtu wa level yake sikutegemea akosee eti kesho ataomba kutubu. Apokee 1,6000,000 Tsh akijua fika kuwa ni za WIZI eti kesho atatubu na sisi tusahahu.......NEVER NEVER AND NEVER FORGET HISTORY1 Jitahidi usiandike historia mbaya , for such a prominent person as she was by those times kuwa tutasahau!
 
Ni kweli anaongea ukweli lakin hana sifa tena ya kuongea kwa kuwa alishapoteza hiyo sifa. Mfano ukipata kifungo gerezani na kuhukumiwa tayari huna sifa tena ya kugombea urais ingawa unaweza kuwa unaongea vizuri.The same to your prof.
Wewe usiwe rigid, hata hao Viongozi wako kwenye Chama walikuwa upande mwingine in one way or another lakini wakagundua kuwa huenda hawako mahali sahihi wakaondoka, na leo ndo makamanda wako kwenu. Sasa huyu mama anakosa sifa zipi za kumuziuia asiwe na haki na uhuru wa kutoa maoni kwenye masuala yanaoyogusa Taifa hata kama ni ndani ya chama chake? Myonge mnyongeni Haki yake mpe. Huyu mama bado ni hazina na anao upeo mkubwa, beyond your reach !
 
Nendeni mkalihubiri injili yangu mahali pote duniani. Na Chochote mtakachokuwa mmefunga duniani na mbinguni kitakuwa kimefungwa. So kama mama huyu alitubu na kusamehewa dhambi zake, wewe ni nani uendelee kumuhesabia dhambi? After all hata Liwali wa hapa kwetu duniani walishindwa kumleta mbele ya Pilato ili ashitakiwe na kuhukumiwa kwa kuwa no proof of allegations. She remains innocent until proven guilty !
 
Kosa moja halihalalishi losa lingine,
Mwache aseme, ametubu!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…