Prof. Assad: Niliondolewa kazini kinyume na taratibu kwasababu nilikuwa sifuati maelekezo ya Mtu

Prof. Assad: Niliondolewa kazini kinyume na taratibu kwasababu nilikuwa sifuati maelekezo ya Mtu

Hahaaaa
Huyu mzee ni baadhi ya wazee ambao walikua hawana time wala walikua hawaogopi simu za jiwe, ilikua kama anapiga jamaa anakata akimwambia sijui nyokonyoko mzee anamwambia acha upuuzi wewwe dunia siyo ya babaaako, kuna maviongozi sasahivi viazi kweli suala ukweli kwao ni kitendawili kisa V8 na matumbo yao, wakwanza Diblo Dibala
 
Analazimisha kuonekana ni mtu msomi anaejielewa ana misimamo.

Bahati mbaya alikutana na Chuma.

Nilichokuwa nampendea yule baba JPM ukijifanya wewe ni wa muhimu sana kwenye hii nchi yeye anakuonesha namna ulivyo takataka tu na nchi inaweza kwenda mbele bila wewe hahahah.

Profesa uliondolewa na kidume sasa unalialia nini!!?
Kama inavyoweza kwenda sasa bila ya yeye kuwepo, maisha mafupi hayaa. Tusijione tumemaliza kila kitu
 
Niliondolewa Ofisini kinyume na taratibu kwa sababu nilikuwa nasimamia na kufanya kazi kwa kufuata taratibu na miongozo ya kazi na sio maelekezo ya mtu,kuna mahali viongozi wetu wanashindwa kusimamia wanachokiamini kwa hofu ya kuporwa V8, wanahofu kukosa riziki.

Hili suala la kuniita CAG aliyemaliza muda wake binafsi linaniudhi, katiba ibara ya 144 inatamka wazi muda wa kumaliza na sababu za kukoma kuwa CAG, mimi nilipotolewa ofisini sikuwa nimemaliza muda wangu. Nadhani hatukuwa wazuri katika kusimamia katiba.

Mussa si jina langu, jina alilonipa baba yangu ni Jaffar. Wakati nasoma kulitokea matatizo fulani, ikabidi nitoke sehemu moja kwenda nyingine ili kumaliza masomo na hili jina la Mussa nikalipata huko ila watu wanaonifahamu wananijua kama Jaffar- Profesa Mussa Assad, CAG wa zamani.

Prof. Yuko sawa kulingana na misimamo na usimamiaji wa katiba kwa namna alivyoapa kuilinda na kuitumikia. Ila Magufuli alikuwa sawa kulinda kile alichoapa kukilinda na kukisimamia kama nyerere na sokoine tuu... Tujenge nchi tuache siasa tusaidieni sisi wanyonge kama mnavotuia
 
umesikiliza hukumu? kwamba CHIZI MAGUFULI alivunja KATIBA Waambie mazuzu wenzio mkalie pembeni kwenye KABURI LAKE
Katiba ipi kiongozi ambayo haivunjwa na viongozi wa sekta na taasisi zingine za kisiasa za ccm na serikali tuache ushabiki wa kisiasa tuangalie maisha yanaenda VP siasa za mzungu tuu
 
Assad ni mmojawapo wa wazalendo wachache wasio wachumia tumbo tu waliobaki.
Muda wake umeisha nadhani anapaswa kuwa mshauli wa wapinzani na huenda hawata nunuliwa tena kwa rupia.
 
Back
Top Bottom