Prof. Janabi: Sijanywa juisi aina yoyote takriban miaka 20

Prof. Janabi: Sijanywa juisi aina yoyote takriban miaka 20

Wakuu!

Mmemsikia Prof. Mohamed Janabi, akiendelea kutupa madini ya kuzidi kulinda afya zetu? Ila hili limeniacha mdomo wazi kidogo kuhusu kunywa juice ambayo tuaamini ni sehemu ya kuboresha afya tena zile juice za kutengeneza mwenyewe.

==================

MKURUGENZI Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Mohamed Janabi, amesema ulaji wa chakula cha kila siku ndio unaotafsiri afya ya sasa na baadae, na kwamba walio na umri kuanzia miaka 35 ama 0 na kuendelea kuwa makini na aina ya mlo.

“Binafsi huwa sinywi juisi iliyotengenezwa au iliyotokea viwandani ni takribani miaka 20 tangu mwaka 2000. Sichanganyi matunda, nakula asubuhi tunda moja labda ndizi, mchana peazi na usiku kipande cha papai,” ameongeza.

“Jamii ibadili mtazamo kwamba uwekezaji wa maisha ya baadae, unaegemea kwenye uwekezaji wa mali, bali hatua hiyo inahitajika kwenye afya pia.”

Soma Pia: Tukifuata ushauri wa Professor Janabi tutaangamia kwa njaa

Prof. Janabi ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo, anayasema hayo kupitia ukurasa wake wa kijamii kuhusu maisha bora, ikiwa ni mwendelezo wa elimu kwa umma, kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza (NCDs) kama vile kisukari, presha na saratani.
Huyu mwamba sijui watoto wake wanamuonaje!
 
Wakuu!

Mmemsikia Prof. Mohamed Janabi, akiendelea kutupa madini ya kuzidi kulinda afya zetu? Ila hili limeniacha mdomo wazi kidogo kuhusu kunywa juice ambayo tuaamini ni sehemu ya kuboresha afya tena zile juice za kutengeneza mwenyewe.

==================

MKURUGENZI Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Mohamed Janabi, amesema ulaji wa chakula cha kila siku ndio unaotafsiri afya ya sasa na baadae, na kwamba walio na umri kuanzia miaka 35 ama 0 na kuendelea kuwa makini na aina ya mlo.

“Binafsi huwa sinywi juisi iliyotengenezwa au iliyotokea viwandani ni takribani miaka 20 tangu mwaka 2000. Sichanganyi matunda, nakula asubuhi tunda moja labda ndizi, mchana peazi na usiku kipande cha papai,” ameongeza.

“Jamii ibadili mtazamo kwamba uwekezaji wa maisha ya baadae, unaegemea kwenye uwekezaji wa mali, bali hatua hiyo inahitajika kwenye afya pia.”

Soma Pia: Tukifuata ushauri wa Professor Janabi tutaangamia kwa njaa

Prof. Janabi ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo, anayasema hayo kupitia ukurasa wake wa kijamii kuhusu maisha bora, ikiwa ni mwendelezo wa elimu kwa umma, kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza (NCDs) kama vile kisukari, presha na saratani.

Kwahiyo anataka kutuambia nini? Maana naona kama ngozi yake hata nuru inakosa. Unaachaje kula kwa staha sababu ya kuogopa utakufa?
Ngoja tuyaone
 
Juice za viwandani sio nzuri kwa afya, alitakiwa kuwaambie watu watumie juice walizotengeneza wenyewe.

Lakini viwanda vina sababu ya kuwepo. Sio kila sehemu kuna matunda mengi kama Tanzania. Prof anajichanganya. Dunia hii kila mtu aishi miaka zaidi ya 70 ili iweje?
Kuna watu toka wanazaliwa wagonjwa. Na kuna wengine mpaka wanazeeka hawajui ugonjwa. Tusichanganye mambo hapa. Kufa na kuzaliwa ni ahadi na anayetoa ni Mwenyezi Mungu tu. hata tukipenda vipi maisha, kufa lazima
 
19beca0af3a641638352700dadffde0a.jpg
 
Lakini viwanda vina sababu ya kuwepo. Sio kila sehemu kuna matunda mengi kama Tanzania. Prof anajichanganya. Dunia hii kila mtu aishi miaka zaidi ya 70 ili iweje?
Kuna watu toka wanazaliwa wagonjwa. Na kuna wengine mpaka wanazeeka hawajui ugonjwa. Tusichanganye mambo hapa. Kufa na kuzaliwa ni ahadi na anayetoa ni Mwenyezi Mungu tu. hata tukipenda vipi maisha, kufa lazima
uko sawa lakini kuchukua tahdhari ni muhimu, vinywaji vya viwandani vina madhara madhara kiasi gani ni jinsi unavyotumia.
 
uko sawa lakini kuchukua tahdhari ni muhimu, vinywaji vya viwandani vina madhara madhara kiasi gani ni jinsi unavyotumia.

Tahadhari muhimu. Ila sio kudanganyana hapa kwamba lishe imekuwa kitu rahisi kwa kila mtu. Ukiwaona wanaoshindia mlo mmoja kwa siku sababu hawana option ya kula tofauti, utaelewa maana halisi ya ugumu wa maisha.
Akipata juice za box, atakunywa kwa raha zake. Kinachosikitisha ni kama vile assumption ni wote tuko level ile ile kwa kipato na maisha
 
Haya maisha tuyaacheni tu wakuu kila mtu kuna matatizo yake anateseka nayo.

Mimi binafsi sijanywa Juisi wala Soda yoyote ya kiwandani tangia mwaka 2005 mpaka leo,
Miaka yote hiyo sijawa mzinzi wala sikuwa mlevi wa vileo.
Lakini nimekuja kupata tatizo la kiafya ambalo halina tiba maisha yangu yote, na hili tatizo haliambukizwi limetokana na ajali.

Kwahiyo haya maisha ukiona pombe inakupa furaha wewe kunywa, mambo ya kusema kutunza afya unaweza kutunza afya yako na ukaja kupata matatizo mabaya kushinda watu ambao hawajali afya zao.
Pole sana mkuu
 
Kwamba Prof Janabi ni mbobevu kwenye masuala ya Lishe kuliko wataalam wa Lishe? Kwamba hajui mchanganyiko wa aina flani ya matunda yakichanganywa pamoja yanatengeneza alkali na kupunguza kiasi cha acid tumboni?
Ajikite kwenye mambo ya Moyo aachane na mambo ya Lishe...Kuna wakati ma2zo yake yanapotosha waziwazi alafu wataalam hawamwambii ukweli sijui wanamwogopa kisa ni boss wao?
 
Wakuu!

Mmemsikia Prof. Mohamed Janabi, akiendelea kutupa madini ya kuzidi kulinda afya zetu? Ila hili limeniacha mdomo wazi kidogo kuhusu kunywa juice ambayo tuaamini ni sehemu ya kuboresha afya tena zile juice za kutengeneza mwenyewe.

==================

MKURUGENZI Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Mohamed Janabi, amesema ulaji wa chakula cha kila siku ndio unaotafsiri afya ya sasa na baadae, na kwamba walio na umri kuanzia miaka 35 ama 0 na kuendelea kuwa makini na aina ya mlo.

“Binafsi huwa sinywi juisi iliyotengenezwa au iliyotokea viwandani ni takribani miaka 20 tangu mwaka 2000. Sichanganyi matunda, nakula asubuhi tunda moja labda ndizi, mchana peazi na usiku kipande cha papai,” ameongeza.

“Jamii ibadili mtazamo kwamba uwekezaji wa maisha ya baadae, unaegemea kwenye uwekezaji wa mali, bali hatua hiyo inahitajika kwenye afya pia.”

Soma Pia: Tukifuata ushauri wa Professor Janabi tutaangamia kwa njaa

Prof. Janabi ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo, anayasema hayo kupitia ukurasa wake wa kijamii kuhusu maisha bora, ikiwa ni mwendelezo wa elimu kwa umma, kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza (NCDs) kama vile kisukari, presha na saratani.
huyu siku hizi amekua mtu wa spinning kama makonda
 
Ukiondoa, Kula , kunywa na Ngono,....hii Dunia haina maaana kabisaaaa,....

muhudumu,..lete kitimoto kilo, na ndizi nne za kuponda,.....usisahau juice ya pasion jagi mbili,..

unafukiwa na kifusi ukiwa na Afya yako tele,..na msaada hupati...
janabi🚮
 
Ndiyo maana uso wake hauna nuru, mtu gani Kila kitu yeye hataki tule

Juice hataki tunywe

Nyama hataki tule

Samaki hataki tule

Biryani hataki tule

Beer hataki tunywe

Ugali hataki tule

Juzi nilikuwa mitaa ya Ofisi yake, nilikuwa nimeagiza wali Samaki na kachumbali, kuona anakaribia kwenye Meza yangu akafanya hadi nizuge chakula hakikua changu maana alishaanza kunipa risala zake 🙌

Sasa sijui anataka tufe na njaa kabisa ama nini 🙌
Basi afunge zile canteen zote zilizopo MNH, tujuwe moja kuwa hakuna kula
 
Yule Mzee sijui hata kama familia yake inakulaga hata nyama, hachelewi kuwalisha maharage Mwaka mzima 😜
Mungu amekupa mwili na appetite halafu unaanza kumkosoa MUNGU??

Mbona kufa kupo tu? Kwani mtu aishi miaka mingapi? Mungu katupa mamlaka kwenye wanyama watembeao na watambaao pia na mimea.

Kwanini uishi kwa shida na kujinyima bila sababu? Unataka uishi kama Methuselah wa kwenye biblia??
 
Back
Top Bottom