Hoja kubwa iliyopo ni kuwa kuna ukiukwaji wa haki katika chaguzi za Tanzania na hii si mara ya kwanza. Hakuna hoja ya vita ya kiuchumi.
Kuna tatizo ambalo Tanzania imelikuza si EU
Wabunge wa Tanzania wanaoongelea EU n.k wana haki kama Wabunge na ndiyo kazi yao.
Wana haki ya kumhoji Waziri wa Mambo ya nje, wana haki ya kusema lolote lile kama Wabunge
Wabunge wa EU wameongelea hoja ya uchaguzi na pesa za COVID-19 ambazo ni zao katika Bunge lao
EU wana haki ya kuongelea suala lao katika Bunge lao.
Hivyo, hilo lipo katika wigo wao halijuvuka na kuingia katika mkondo wa kidiplomasia.
Nimeshangaa Balozi ameomba kuzungumza na viongozi wa Bunge! kwa tatizo gani?
Hili suala halijaingia katika mzunguko wa diplomasia, na wala hakuna Diplomatic Row au statement ya EU.
Waziri anapoongea anali ingiza suala katika mkondo wa kidiplomasia na kauli yake ni ya kidiplomasia.
Hapa ndipo tatizo linapoanza, kwamba, waziri anachochea mgogoro ambao haupo kwa kuanzia
Wabunge wa EU wanaoongea kwanini kuna panic Tanzania?
Hatuwezi kuwapangia Wabunge wa EU nini cha kuongea
JokaKuu Mag3