Prof. Kabudi aieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania haijawahi kushindwa vita ya aina yoyote

Prof. Kabudi aieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania haijawahi kushindwa vita ya aina yoyote

Kabudi Tumeporwa kifaru na waasi wa ISS huko mpakani na msumbiji, askari wetu kwa mamia wanakufa na wengine wanamejeruhiwa,
Kuna Hatari ya kuipoteza mtwara na Lindi, acha porojo na vitisho

Sasa unaeleza mafanikio ya JWTz ili kuwatisha EU wakati ndo wanalivalisha kulilisha na kulipa siraha jeshi lenu
 
21 November 2020

WAZIRI WA MAMBO YA NJE TANZANIA PROFESA PALAMAGAMBA KABUDI AWAJIBU MABEBERU, HATUJAWAHI KUPIGISHWA MAGOTI, UCHAGUZI ULIKUWA HURU NA HAKI

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Palamagamba Kabudi aijibu EU - Umoja wa Ulaya kufuatia kikao cha bunge hilo la ulaya huko makao makuu ya EU kutishia uwezekano wa vikwazo kupitia Kamati yake Mambo ya Nje ya Bunge la Umoja wa Ulaya kujadili uwezekano wa kuibana Tanzania kwa vikwazo vya aina mbalimbali ikiwemo kusitisha msaada wa kuifadhili bajeti ya Maendeleo ya Tanzania.

Prof. Palamagamba Kabudi ameomba msaada wa vyombo vya habari nchini kuisaidia serikali ya Tanzania kwa kujitokeza na kuieleza Jumuiya ya Kimataifa ukweli wa mambo. Na kueleza Nyerere aliwahi kuwadindia Germany na United Kingdom na kukataa misaada na fedha zao. Prof. Palamagamba Kabudi anashangaa waTanzania kuanza kutetemeka ktk mitandao ya kijamaii kuhusu nchi yetu kuwekewa vikwazo.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haifuati sera za kidiplomasia za kujitenga kufanya kazi na Jumuiya za Kimataifa. Hivyo waziri Kabudi amesema Tanzania ipo tayari kukaa ktk meza moja na wadau wa kimataifa kuzungumzia mapungufu yaliyopo lakini si kwa kuburuzwa na mabeberu bila kuwa na facts mezani.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa watu wahuni wachache wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la Ulaya EU hawawezi kuitisha na kuidhalilisha Tanzania na watambue Tanzania ni nchi huru.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema maneno hayo mazito akiongea na Wafanyakazi wa Wizara hiyo muhimu ya Mambo ya Nje akatumia fursa hiyo kujibu uvumi kuwa Tanzania itanyimwa misaada na kuwakumbusha wafanyakazi hao kutembea vifua mbele kwani Tanzania siyo nchi ndogo kidiplomasia, kimsimamo, kiji-Geopolitiki na kiushawishi kimataifa.

.....................................................

EU Parliament Committee on Foreign Affairs discussion on Tanzania​

Tujikumbushe walioitwa "wahuni wachache" na Prof. Kabudi, tarehe 19 November 2020 jijini Brussels kwa dakika 45 mfululizo walisema nini kuhusu Tanzania ktk kikao cha Kamati ya Mambo ya Nje cha Bunge la Jumuiya ya EU
Tazama / sikiliza dakika 45 za mjadala ktk kamati hiyo:

Duh! Watu wengine ni hatari "kujimwabafy".
 
Wewe jamaa ni mjinga sana. Nadhani wewe ni kijana ila una akili ya babu kizee wa enzi za ukoloni.
Mkuu hii demokrasia mnayoihubiri ipo wapi sasa kama unanitukana kwa kuusema msimamo wangu.... [emoji3][emoji3] msimamo wangu unakuumizaje sasa mkuu unaye hubiri haki na amani?

Wewe ungekuwa kiongozi tayari ungeshanikamata kwa kesi ya utakatishaji.....
 
Prof. Palamagamba Kabudi ameianza safari hii ya kujaribu kuitetea Tanzania chini ya utawala wa CCM Mpya kwa mguu wa kushoto na kuteleza ki-diplomasia. Kuwaita wabunge wa bunge la Ulaya kuwa ni 'wahuni' na 'wachache' basi katika vita hii atashindwa vibaya.

Maana vitani hakuna kumdharau 'adui' yako lazima kwenda vitani kwa weledi mkubwa.
Boss, tambo lazima ziwepo unapoingia ulingoni😂😂
 
Kwa uelekeo huu lazima tutapata katiba tunayoitaka watanzania
 
Mkuu hii demokrasia mnayoihubiri ipo wapi sasa kama unanitukana kwa kuusema msimamo wangu.... [emoji3][emoji3] msimamo wangu unakuumizaje sasa mkuu unaye hubiri haki na amani?

Wewe ungekuwa kiongozi tayari ungeshanikamata kwa kesi ya utakatishaji.....
Bunge la ulaya limejadili udanganyifu uliofanyika kwenye uchaguzi. Kabudi badala ya kujibu hoja anaongea vitisho. Wewe unapiga makofi na kumpongeza. Huoni kama ni ujinga huo?
 
21 November 2020

WAZIRI WA MAMBO YA NJE TANZANIA PROFESA PALAMAGAMBA KABUDI AWAJIBU MABEBERU, HATUJAWAHI KUPIGISHWA MAGOTI, UCHAGUZI ULIKUWA HURU NA HAKI

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Palamagamba Kabudi aijibu EU - Umoja wa Ulaya kufuatia kikao cha bunge hilo la ulaya huko makao makuu ya EU kutishia uwezekano wa vikwazo kupitia Kamati yake Mambo ya Nje ya Bunge la Umoja wa Ulaya kujadili uwezekano wa kuibana Tanzania kwa vikwazo vya aina mbalimbali ikiwemo kusitisha msaada wa kuifadhili bajeti ya Maendeleo ya Tanzania.

Prof. Palamagamba Kabudi ameomba msaada wa vyombo vya habari nchini kuisaidia serikali ya Tanzania kwa kujitokeza na kuieleza Jumuiya ya Kimataifa ukweli wa mambo. Na kueleza Nyerere aliwahi kuwadindia Germany na United Kingdom na kukataa misaada na fedha zao. Prof. Palamagamba Kabudi anashangaa waTanzania kuanza kutetemeka ktk mitandao ya kijamaii kuhusu nchi yetu kuwekewa vikwazo.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haifuati sera za kidiplomasia za kujitenga kufanya kazi na Jumuiya za Kimataifa. Hivyo waziri Kabudi amesema Tanzania ipo tayari kukaa ktk meza moja na wadau wa kimataifa kuzungumzia mapungufu yaliyopo lakini si kwa kuburuzwa na mabeberu bila kuwa na facts mezani.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa watu wahuni wachache wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la Ulaya EU hawawezi kuitisha na kuidhalilisha Tanzania na watambue Tanzania ni nchi huru.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema maneno hayo mazito akiongea na Wafanyakazi wa Wizara hiyo muhimu ya Mambo ya Nje akatumia fursa hiyo kujibu uvumi kuwa Tanzania itanyimwa misaada na kuwakumbusha wafanyakazi hao kutembea vifua mbele kwani Tanzania siyo nchi ndogo kidiplomasia, kimsimamo, kiji-Geopolitiki na kiushawishi kimataifa.

.....................................................

EU Parliament Committee on Foreign Affairs discussion on Tanzania​

Tujikumbushe walioitwa "wahuni wachache" na Prof. Kabudi, tarehe 19 November 2020 jijini Brussels kwa dakika 45 mfululizo walisema nini kuhusu Tanzania ktk kikao cha Kamati ya Mambo ya Nje cha Bunge la Jumuiya ya EU
Tazama / sikiliza dakika 45 za mjadala ktk kamati hiyo:
Tuliambiwa na Balozi wetu wa Ubelgiji kuwa hakuna kitu kama Mjadala wa Kamati ya Mambo ya nje ya EU illiyotuongelea - eti ni uongo tu. Sasa waziri wetu naye amejibu kisichokuwepo au?

Nani mkweli hapa kati ya balozi na waziri?
 
Taifa letu limekosa viongoz waadilifu na wenye huruma kwa wenzao ,100% ya misaada inalenga kwa wananch wanaitwa wanyonge wanaimba wao ni viongoz wa wanyonge ila wanayoyafanya hawana ata chembe ya huruma n hao wanyonge ,binafs naumia kwa sababu najua madhara tutakayoyapata sio wao ,leo hii tunasaidiwa ila bado hali dhoofu je tukikosa kabisa ,viongoz wetu wawafikirie watu wa hali duni wasitake kuwapa mzigo wa makodi na mfumuko wa bei
Kwa jinsi unavyo tia huruma kukosa misaada sina shaka kabisa ukipewa uongozi wa nchi nadhani utaendesha nchi kwa misaada aisee

Africa mna kila kitu lakini kwa nini bado mnaendekeza misaada?
Hao Mabeberu wanaitegemea Africa kuendesha viwanda vyao na vyakula toka barani Africa, mbona msijiamini?
Ata wasipotoa misaada lazima waje tu hata kwa mfumo mwingine wa KIBIASHARA na bado Dola zao mnazipata tu,
Magufuli kaonesha kabisa kujiamini na inabidi hata wengine tujiamini na tulicho nacho bhna
Sisi tuna rasilimali kibao na wakisusia Western tutafanya biashara na Mchina wetu bhana asie kuwa na NONGWA kama wengine.
 
Bunge la ulaya limejadili udanganyifu uliofanyika kwenye uchaguzi. Kabudi badala ya kujibu hoja anaongea vitisho. Wewe unapiga makofi na kumpongeza. Huoni kama ni ujinga huo?
Tatizo lako ni moja....

Unataka niwasikilize wabunge wa EU na kuwaelewa kama unavyotaka wewe.

Nimsikilize Kabudi kisha nimwelewe kama unabyotaka wewe. Demokrasia ipi mnahubiri mkuu?

Bado naenda na msimamo wa waziri...utu wa taifa langu unakuja kwanza..
 
Kwamba ni bora kufa ukiwa umesimama,kuliko kuishi ukiwa umepiga magoti.Ila watakaoumia ni maskini. Mawaziri wataendelea kupata mishahara yao minene. Wale wenzangu na mie maisha yataendelea kukaza.
 
Hoja kubwa iliyopo ni kuwa kuna ukiukwaji wa haki katika chaguzi za Tanzania na hii si mara ya kwanza. Hakuna hoja ya vita ya kiuchumi.
Kuna tatizo ambalo Tanzania imelikuza si EU

Wabunge wa Tanzania wanaoongelea EU n.k wana haki kama Wabunge na ndiyo kazi yao.
Wana haki ya kumhoji Waziri wa Mambo ya nje, wana haki ya kusema lolote lile kama Wabunge

Wabunge wa EU wameongelea hoja ya uchaguzi na pesa za COVID-19 ambazo ni zao katika Bunge lao
EU wana haki ya kuongelea suala lao katika Bunge lao.
Hivyo, hilo lipo katika wigo wao halijuvuka na kuingia katika mkondo wa kidiplomasia.

Nimeshangaa Balozi ameomba kuzungumza na viongozi wa Bunge! kwa tatizo gani?
Hili suala halijaingia katika mzunguko wa diplomasia, na wala hakuna Diplomatic Row au statement ya EU.

Waziri anapoongea anali ingiza suala katika mkondo wa kidiplomasia na kauli yake ni ya kidiplomasia.
Hapa ndipo tatizo linapoanza, kwamba, waziri anachochea mgogoro ambao haupo kwa kuanzia

Wabunge wa EU wanaoongea kwanini kuna panic Tanzania?
Hatuwezi kuwapangia Wabunge wa EU nini cha kuongea

JokaKuu Mag3
 
Kama hayo yametamkwa na Kabudi, basi ana muda mfupi sana wa kukaa kwenye hiyo Wizara... Nina hakika atapumzishwa soon. Ngoja hizo kauli ziwafikie mabeberu..
 
Kuwa Nchi Huru sio kigezo Cha kukiuka haki za binadamu au kuvunja Katiba.

Aidha, kuwa Nchi Huru ni suala moja. Kuwa Nchi ya inayohejiheshimu na kuhfpeshimu utawala wa sheria ni suala jingine. Sisi ni Nchi Huru Ila tumeshindwa kujiheshimu.
 
Back
Top Bottom