4 September 2020
Video source : millard ayo
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeihakikishia Uingereza pamoja na Jumuiya ya Kimataifa kuwa uchaguzi mkuu unaotegemewa kufanyika mwezi Oktoba mwaka 2020 utafanyika kwa amani, uhuru na haki.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi wakati akipokea nakala za hati za utambulisho za Balozi mteule wa Uingereza hapa nchini Mhe. David Concar
Prof Kabudi amesema kuwa paamoja na mambo mengine, amemhakikishia balozi mteule wa Uingereza nchini Mhe. Concar kuwa mchakato wa uchaguzi nchini unaendelea vizuri sana ambapo mikutano ya kampeni imeanza kwa ngazi zote (ngazi ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani) na mpaka sasa kampeni zinaendea vizuri.
"kama ilivyoada ya watanzania nimemhakikishia kuwa uchaguzi huu utafanyika kwa amani na utulivu na mwisho wa siku maamuzi yatakayotolewa na watanzania ya kuamua nani awe diwani, nani awe mbunge na nani awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yataheshimiwa na watanzania wote," Amesema Prof. Kabudi.
Kwa upande wake Balozi mteule Mhe.David Concar amesema kuwa katika maongezi yao mbali na kugusia suala la uchaguzi pia wameongelea namna ya kuimarisha mahusiano baina ya Tanzania na Uingereza na mazingira bora ya kuvutia zaidi wawekezaji kuja nchini,kukuza biashara hususani baada ya Uingereza kujitoa katika jumuiya ya Umoja wa Ulaya na pia kusaidia maendeleo katika maeneo ya afya,maji pamoja na elimu.
Source: TZ YAIHAKIKISHIA UINGEREZA NA JUMUIYA YA KIMATAIFA UCHAGUZI HURU, HAKI
Video source : millard ayo
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeihakikishia Uingereza pamoja na Jumuiya ya Kimataifa kuwa uchaguzi mkuu unaotegemewa kufanyika mwezi Oktoba mwaka 2020 utafanyika kwa amani, uhuru na haki.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi wakati akipokea nakala za hati za utambulisho za Balozi mteule wa Uingereza hapa nchini Mhe. David Concar
Prof Kabudi amesema kuwa paamoja na mambo mengine, amemhakikishia balozi mteule wa Uingereza nchini Mhe. Concar kuwa mchakato wa uchaguzi nchini unaendelea vizuri sana ambapo mikutano ya kampeni imeanza kwa ngazi zote (ngazi ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani) na mpaka sasa kampeni zinaendea vizuri.
"kama ilivyoada ya watanzania nimemhakikishia kuwa uchaguzi huu utafanyika kwa amani na utulivu na mwisho wa siku maamuzi yatakayotolewa na watanzania ya kuamua nani awe diwani, nani awe mbunge na nani awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yataheshimiwa na watanzania wote," Amesema Prof. Kabudi.
Kwa upande wake Balozi mteule Mhe.David Concar amesema kuwa katika maongezi yao mbali na kugusia suala la uchaguzi pia wameongelea namna ya kuimarisha mahusiano baina ya Tanzania na Uingereza na mazingira bora ya kuvutia zaidi wawekezaji kuja nchini,kukuza biashara hususani baada ya Uingereza kujitoa katika jumuiya ya Umoja wa Ulaya na pia kusaidia maendeleo katika maeneo ya afya,maji pamoja na elimu.
Source: TZ YAIHAKIKISHIA UINGEREZA NA JUMUIYA YA KIMATAIFA UCHAGUZI HURU, HAKI