Prof. Kabudi ataka Elimu ya Biblia itolewe shuleni kuanzia Chekechea hadi Sekondari na Biblia zigawiwe Bure ili kulinda Maadili

hongera, ile english kila nikikumbuka sajicheka. biblia ya kiingereza nikiisoma kwa sasa kidogo naelewa elewa nikijazia na tafsiri yake kwa kiswahili hahaha
 
Naunga mkono hoja.
Yeah. Uibuliwe mtaala utakao kuwa non-biased kisha waweke syllabus (levels) i.e. wanaoanza e.g. Chekechea, std 1, 2, 3............Chuo kikuu. Na hilo somo hilo lipewe jina sio la dini e.g. ulivyosema Falsafa (Philosophy).
Ahsante sana, ipo faida kubwa ya kuwaweka watu wadadisi tutajenga taifa moja la watu wasomi wanaojielewa sana aaani.
 
Maadili hayawezi kuletwa kwa kugawiwa au kusoma biblia .
Uko sahihi kwamba maadili hayagawiwi au kusoma biblia. Maadili ni Kipaji (TALENT) mtu anazaliwa nacho lakini kipaji hicho kinahitaji kikuzwe au kilelewe ili kikue.
Njia za kuibua na kukuza vipaji zipo nyingi; lakini mojawapo ni Kupata elimu i.e. kusoma shule. Kusoma Biblia inawafaa wale wanaoamini katika maandiko hayo.
Prof. ameshauri kuibua Mtaala wa somo la Maadili litakalokuwa linafundishwa kwenye Taasisi za Elimu hapa nchini kuanzia ngazi ya chini kabisa e.g. Chekechea hadi vyuo.
Kama itaonekana biblia inafaa kuwa ni mojawapo katika vitabu vya Rejea hilo watajua wenyewe wataalam.
 
Kwa asilimia kubwa maadili huwa yanaanzia kwenye familia.
Ndio maana kwenye darasa la wanafunzi kila mwanafunzi ana maadili ya tofauti na mwingine japo wote wanafundishiwa vitabu vya aina moja.
Na kuhusu biblia mbona hata walioisoma hiyo biblia ni walevi,matapeli(ref kiboko ya wachawi),wazinzi(michepuko,biblia hairuhusu waliooana kuachana lakini huwa wanatengana na kila mmoja anatafuta mpenzi mwingine wa kuishi naye na wanazalishana watoto wengine.
Au mnaongelea maadili gani?
 
Ni kweli watu wanatofautiana kwa mengi sio tu kwa Kimaadili. Na msingi wa Maadili huwa yanaanzia kwenye ngazi ya Familia - 100% correct.
Inapofikia umri mtoto anaenda shule; zoezi hilo la kuendeleza na kukuza Maadili lisisahaulike. Ndo Hoja mtambuka ktk Mada hii.
Kitabu cha Biblia kimetajwa kama mfano tuu lakini Vipo vitabu vya Kiada na Ziada ambavyo hutumika katika somo hilo.
Maadili yanayozungumziwa hapa, kwa mtizamo wangu; ni Ule Utashi sahihi binafsi wa kufanya lililojema na kuepuka lile lililo ovu katika Jamii mahalia.
(I stand to be corrected).
 
Kama ni utashi wa kufanya lililo jema/sahihi waanze kutoa elimu kwa wazazi wanaowalea hao watoto maana kwa asilimia 80% watoto huiga kile wanachokiona kwenye mazingira ya nyumbani kwao au kinachofanywa na wazazi.
Kwa mfano mtoto wa kizaramo ambaye tangu anazaliwa anawaona wazazi wake wanaenda ngomani kukata viuno kila wiki ukija kumwambia ni haramu kwenda ngomani hatokuelewa hata kidogo.
Au mtoto ambaye amezaliwa kwenye mazingira ambayo mama yake alikuwa akipika pombe na kumnywesha tangu akiwa mdogo hatokuelewa ukimwambia kuwa pombe ni mbaya.
Kwa vigezo hivi napinga hoja ya Profesa kabudi
 
Nukuu: "........utashi wa kufanya lililo jema/sahihi waanze kutoa elimu kwa wazazi wanaowalea hao watoto maana kwa asilimia 80% watoto huiga kile wanachokiona kwenye mazingira ya nyumbani kwao au kinachofanywa na wazazi."
Ni kweli na kama laiti hilo lingeliwezekana. Kwa bahati mbaya Wazazi imeshakuwa ni too late.
Kazi ianzie na hao Wazazi wa kesho i.e. Watoto.
Kwa mantiki hiyo sioni kama unampinga Prof. ila naona kama umechangia kuiboresha Hoja yake. Cjui lakini.....
 
Serikali haina dini, uyu mzee anazeeka vibaya
 
Mzazi ni mtu mzimq mwenye akili timamu ana uwezo wa kuchanganua baya na zuri ndio maana kuna baadhi ya wazazi huwa wanafanya maovu lakini
Wazazi ni watu wazima na wenye akili timamu wanajua kutofautisha jambo baya na zuri tofauti na watoto ambao hufanya kwa kuiga tu bila kujua madhara ya mbeleni.
Ndio maana utaona kuna baadi ya wazazi hufanya maovu kama kunywa pombe,kuvuta bangi,wizi lakini huwa hawataki watoto wao kujiingiza katika hayo maovu kwa sababu wanajua madhara yake ila wao huwa wanafanya tu kwa sababu tayari washakuwa waraibu
 

Ukitaka kuwafundisha watoto njia nzuri ni kuwafundisha kuhusu utu na kitu cha mhimu kabisa ni jamii kuishi kitu unachowafundisha watakuelewa mfano hata sasa watoto wengi mtu wanajua hiki kitu kizuri au kibaya , lakini tunawaambia watoto vitu vingi ambavyo sisi wenyewe hata kiasi flani hatuviishi .
 
Dini zote zinafundisha kuhusu waamini wake ni bora kuhusu wengine na ukitumia hiyo approach mtu ataanza kuona watu wengine hawafai ,sisi kama Jamii kwa ujumla inatakiwa tuwafundishe watoto wetu utu ,kuwathaminj wengine na siyo porojo hizi ni kwa maneno na vitendo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…