Prof. Kabudi: Kwa sasa Wananchi hawatapewa dawa za kukabiliana na Corona kutoka Madagascar, inafanyiwa utafiti kwanza

Prof. Kabudi: Kwa sasa Wananchi hawatapewa dawa za kukabiliana na Corona kutoka Madagascar, inafanyiwa utafiti kwanza

Ndege ya Rais sio ya kijani pekee.
Ndio sio ya kijana si tumeambiwa ni ya research, kwani waziri wa nje kawa sample ? Ya majaribio tangu lini

Mbona wakisema wafanye chanjo watu wanalipwa pesa wanao fanyiwa majaribio.
 
Utetezi wa kijinga sana, unachoma pesa za walipa kodi, kwa kitu kisichokuwa na manufaa kwa wananchi.

Kulikuwa na haja kutuma ndege kufuata chupa mbili?!

Ni tafiti ngapi za dawa za asili za hapa nchini mnazofanya, maana hapa tumesikia watu wa tiba asili wakisema wanadawa za kutibu Corona, au nini kilifanya muwaamini Madagascar?!

Dawa zote zinazoingizwa nchini huwa mnazifanyia utafiti kabla ya wananchi kuzitumia?!

Mbona dawa za kujifukiza mliwataka wananchi wajifukize bila utafiti?!

Utafiti unatafiti nini, na kwa muda gani?!
 
Kwahiyo yeye kwa vile ni Waziri basi hakuna haja ya kupata verification ya experts wa afya wa nyumbani tu anywe sio? Ameamua tu kunywa je akidhulika nani alaumiwe?
Mwewe kweli anajazwa full tank na kubeba dignitaries kufata chupa mbili tu seriously?
 
"Tulizoleta ni kwa ajili ya matumizi ya Chattle tu. Wengine subirini"
 
Nimemsikiliza Mh Palamagamba Kabudi na wataalamu alio andamana nao kwenda kufata KIKOMBE cha MADAGASCA.

Hakika nimepatwa na mshangao mkubwa hasa pale nilipo sikia kuwa walipanda ndege ya Rais kwenda kufata chupa mbili kwa ajili ya kufanya uchunguzi kama kweli ni dawa au la?

Sasa najiuliza kama umefata Dawa ya majaribio kaa nini kuna picha zinaonesha ukiwa unakunywa kikombe hicho ambacho hakija dhibitishwa wataalam wa kutoka Tanzania?...
Hii ndiyo inaendana na kale kamsemo wetu "miluzi mingi humpoteza mbwa" juu yake weka " zakuambiwa changa............" Baada ya yote hayo naunga mkono utafiti wanaotaka kufanya. Nategemea utafuata Good Clinical Trials Practice pamoja na documentation zake.
 
Utetezi wa kijinga sana, unachoma pesa za walipa kodi, kwa kitu kisichokuwa na manufaa kwa wananchi.

Kulikuwa na haja kutuma ndege kufuata chupa mbili?!

Ni tafiti ngapi za dawa za asili za hapa nchini mnazofanya, maana hapa tumesikia watu wa tiba asili wakisema wanadawa za kutibu Corona, au nini kilifanya muwaamini Madagascar?!...
Box tisa zimekwenda kwa famila bora Chato
 
Naomba video au picha akiwa anakunywa.
IMG-20200508-WA0052.jpg
 
Hahaha....kama haijafanyiwa utafiti mbona yeye alionekana anagugumia mchupa, macho yamemtoka utafikiri nini yaani, acheni sanaa basi....dawa wagundue wengine wewe uje ufanye utafiti.

Kwa nini huo utafiti usifanyike kwenye hizi za kwetu, maana nimesikia watu kama watatu akiwemo na mbunge sijui wa jimbo gani wakidai wana dawa ya korona..
 
Sasa box 12 mtazigawanaje? Bora JPM agawe mwenyewe
 
Back
Top Bottom