Prof. Kabudi: Ndege ya Tanzania, Bombardier Q400 imekamatwa Canada na kesi ipo Mahakamani

Prof. Kabudi: Ndege ya Tanzania, Bombardier Q400 imekamatwa Canada na kesi ipo Mahakamani

Haohao ndio mnawaita wahisani wakitoamisaada aumikopo!!!
Mabeberu na michezo yao ya kishetani

Wamemshindwa kwenye karatasi sasa wanavizia mali zetu


Rais Magufuli funga Ubalozi wa Canada Ndani ya saa 72 ili watoe Maelezo
 
Nasisi wakulima wa korosho tunaungananae mkulima mwenzetu katika kesi hiyo ya madai
 
Haya mabeberu yanataka tutudhoofisha lakini tuko imara sana,niendelee kumpongeza Rais Dr Magifuli kwa utulivu huu
 
Ule mkakati uliofanyika pale ubalozi wa South Africa wakati ule labda utasaidia tena.
Yuleyule aliyefanya wakati ule na afanye tena sasa, ahamasishe watu waandamane hadi ubalozi wa Canada na mabango wakiimba "TUNATAAKA. NDEGE YEETU. TUNATAAKA. NDEGE YEETU"

Kitaeleweka tu
 
Tena deni linakaribia thamani ya ndege safari hii mkulima kashika penyewe
Tumuombeeni dua ili afanikiwe
Karma nyingine ya uchafuzi
 
Kama wanafuata sheria walifaa mbona hawajaheshimu maamuzi ya mahakama ya Afrika Kusini, kwani wao mahakama zao ndio zina nini zaidi ya zile za Afrika Kusini, ndio hii dharau dhidi ya sisi Waafrika, yaani mahakama zetu Afrika zinaonwa kama hovyoo.
Hii itakula kwao hao Canada maana hata mataifa mengine ya Afrika yanaona hii dhuluma na wataacha kuagiza chochote huko.
Thubutu yako, nani aache kuingia Canada ajili ya mshamba mmoja tu, limbukeni mawazo. ndege za kunua kwa watu siyo maendeleo, tengeneza za kwako.
LIPA DENI, NA BADO, RAIS HEWA.
 
Duh! Huyu mkulima amezidi sasa, Yani ndege mpya ambayo hata haijakabidhiwa ramsi kwa Tanzania inashikwa!!

Mamlaka nchini Canada zimekamata ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400.

Hii ni mara ya pili kwa ndege ya nchi hiyo kuzuiliwa nchini Canada.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi amethibitisha kukamatwa kwa ndege hiyo iliyokuwa iwasili nchini hivi karibuni.

Sababu ya kukamatwa kwa ndege hiyo, kwa mujibu wa Prof Kabudi ni kesi iliyofunguliwa na mkulima mstaafu raia wa Namibia Hermanus Steyn.

Steyn pia alifungua kesi nchini Afrika Kusini mwezi Agust iliyosababisha ndege aina ya Air Bus 220-300 izuiliwe na hatimaye serikali ya Tanzania kushinda kesi mahakamani

"Mhe. Rais ndege yetu aina ya Bombadier ambayo ilipaswa ifike Tanzania kutokea Canada imekamatwa na mtu yule yule ambaye aliikamata ndege yetu kule Afrika ya Kusini." - Prof. Palamagamba Kabudi, ailisema mjini Dodoma katika hafla ya kuapishwa kwa mabalozi.


...... Soma zaidi hapa Mkulima ‘akamata’ tena ndege ya Tanzania Canada
 
Huo mwaka 80 raisi alikuwa Nyerere?Huyu Mzee naye katuachia majanga!
 
Tanzania yaeleza hasira zake kwa Canada
Amesema Balozi wa Tanzania nchini Canada aliitwa nchini na kuelezwa jinsi nchi isivyofurahishwa na kukamatwa kwa ndege zake kila zinapokaribia kuja kuondoka nchini humo."Nimemwambia sio tu kwamba tunasikitika bali tunakasirishwa, na tunafikiri mheshimiwa rais kukushauri kama Canada inaendelea kuruhusu vitu kama hivyo sio wao peke yao wanaotengeneza ndege, hatukufanya makosa kununua ndege Canada, hata Brazil wanatengeneza ndege," amesema Profesa Kabudi.Amesema wameandaliwa wanasheria kwenda Canada kuipigania ndege hiyo.

Kushikiliwa kwa ndege hiyo kunarejesha kumbukumbu ya ndege nyingine ya Tanzania aina ya Bombardier Q400-8 iliyozuiwa nchini Canada mwaka 2017 kutokana na madai ya Sh87.3 bilioni zilizokuwa zikidaiwa na kampuni ya kikandarasi.
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi Kabudi amesema ndege ya Tanzania Bombardier Q400 iliyokuwa iwasili nchini hivi karibuni imekamatwa nchini Canada na kesi ipo Mahakamani

NDEGE NYINGINE YA TANZANIA YAKAMATWA CANADA

- Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi amesema ndege aina ya Bombardier Q400 imekamatwa

- Ndege hiyo iliyokuwa iwasili nchini hivi karibuni imekamatwa na kesi ipo Mahakamani

"Mhe. Rais ndege yetu aina ya Bombadier ambayo ilipaswa ifike Tanzania kutokea Canada imekamatwa na mtu yule yule ambaye aliikamata ndege yetu kule Afrika ya Kusini." - Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje.

======

Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amesema ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 imakamatwa nchini Canada.

Amesema aliyesababisha Bombardier kukamatwa ni Hermanus Steyn, raia wa Afrika Kusini ambaye alifungua kesi ya madai Mahakama Kuu nchini Afrika Kusini akidai fidia ya dola 33 milioni.

Kesi hiyo ilisababisha Mahakama hiyo kuizuia ndege ya Tanzania aina ya Airbus A220-300 kuondoka nchini humo Agosti, 2019.

Steyn, anadai fidia baada ya mali zake kutaifishwa na Serikali ya Tanzania mwaka 1980. Hata hivyo, Septemba 3, 2019 mahakama hiyo iliamuru ndege hiyo iliyokuwa imezuiwa katika uwanja wa ndege wa Oliver Tambo kuachiwa baada ya Serikali kushinda kesi bila kutoa fedha yoyote.

Akizungumza leo Jumamosi Novemba 23, 2019 mjini Dodoma katika hafla ya kuapishwa kwa mabalozi, Profesa Kabudi amesema, “ndege imekamatwa na kesi ipo mahakamani. Aliyesababisha ni yuleyule (Steyn) aliyesababisha ndege yetu kuzuiwa Afrika Kusini.”

Profesa Kabudi amesema kuendelea kwa vitendo hivyo ni hujuma za mabeberu wasiofurahishwa na maendeleo nchini.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli aliyewaapisha mabalozi hao, Profesa Kabudi amesema, “tulikwenda mahakamani tukamshinda (Afrika Kusini) akakata rufaa na wiki iliyopita tukamshinda tena, huyohuyo sasa amekimbilia Canada amekamata ndege ya Bombardier Q400 ambayo ilikuwa ifike nchini.”

“Jambo linalosikitisha ndege zilizokuwa zinatoka Marekani aina ya Dreamliner mbili hazikukamatwa zimefika lakini kila ndege inapotakiwa kuondoka Canada tunashangaa hao matapeli wanajuaje na ndege zinakamatwa.”
Amesema Balozi wa Tanzania nchini Canada aliitwa nchini na kuelezwa jinsi nchi isivyofurahishwa na kukamatwa kwa ndege zake kila zinapokaribia kuja kuondoka nchini humo.

“Nimemwambia sio tu kwamba tunasikitika bali tunakasirishwa, na tunafikiri mheshimiwa rais kukushauri kama Canada inaendelea kuruhusu vitu kama hivyo sio wao peke yao wanaotengeneza ndege, hatukufanya makosa kununua ndege Canada, hata Brazil wanatengeneza ndege,” amesema Profesa Kabudi.

Amesema wameandaliwa wanasheria kwenda Canada kuipigania ndege hiyo.

Kushikiliwa kwa ndege hiyo kunarejesha kumbukumbu ya ndege nyingine ya Tanzania aina ya Bombardier Q400-8 iliyozuiwa nchini Canada mwaka 2017 kutokana na madai ya Sh87.3 bilioni zilizokuwa zikidaiwa na kampuni ya kikandarasi.

Mabalozi walioapishwa katika hafla hiyo ni Meja Jenerali Anselm Shigongo Bahati (Misri), Mohamed Abdallah Mtonga (Abu Dhabi), Jestas Abouk Nyamanga (Ubelgiji), Ali Jabir Mwadini (Saudi Arabia) na Dk Jilly Elibariki (Burundi).



Chanzo: Mwananchi

Lile jopo la wanasheria waliotumwa S.Africa si litumwe tu? ndani ya siku mbili/tatu ngoma itakuwa imeisha.
 
Back
Top Bottom