Prof. Kitila Mkumbo akanusha masharti ya Mkopo wa Korea Kusini. Asema utalipwa kwa miaka 40

Prof. Kitila Mkumbo akanusha masharti ya Mkopo wa Korea Kusini. Asema utalipwa kwa miaka 40

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo kupitia Ukurasa wakewa X (Twitter) amekanusha taarifa iliyotolewa na Sauti ya America inayoelezea Mkopo wa Tanzania na Masharti ya kuiachia kuchimba madini baharini.

Soma:
- Tanzania imepokea mkopo kutoka kwa Korea Kusini na kutoa sehemu ya bahari na madini

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Kitila Mkumbo ameandika:

1717442376481.png

URONGO. Hakuna masharti kama hayo. Mkopo huu ni sehemu ya makubaliano katika awamu ya pili ya ushirikiano wa miaka mitano ijayo. Ni mkopo nafuu utakaolipwa katika miaka 40 kuanzia mwaka wa 26 kwa riba ya 0.01%.
Kuhusu madini ya kimkakati (strategic mineral resources-SMR), mkakati wa Tanzania ni kutafuta wawekezaji watakaowekeza katika utafiti, uchimbaji na kuongeza thamani ndani ya nchi.
Tumeweka wazi duniani kote kuwa tunataka wawekezaji watakaosafirisha betri za magari na sio madini ya kimkakati kwa lengo la kutengeneza betri hizo nje ya nchi. Kuhusu uchumi wa buluu, tumesaini mkataba kwa lengo la kushirikiana katika kuboresha teknolojia ya uvuvi, kujenga bandari za uvuvi na viwanda vya kuchakata Samaki. Eneo lingine ni ushirikiano katika teknolojia ikiwemo kujenga chuo cha TEHAMA nchini.
PIA SOMA
- Ziara ya Rais Samia Korea Kusini atasaini Mkopo wa Tsh. Trilioni 6.51
 
Ila Watanganyika malofa sana.
Imagine mtu tena mwanamke anatoka nchi yake anakwenda kuwatawala Watanganyika nao wanakubali eti kisa katiba inasema hivyo.
Mbona katiba ya kwao huyo mama haimpi ruhusa Mtanganyika hata kumiliki mita 4 za mraba huko kwao?
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo kupitia Ukurasa wakewa X (Twitter) amekanusha taarifa iliyotolewa na Sauti ya America inayoelezea Mkopo wa Tanzania na Masharti ya kuiachia kuchimba madini baharini.

Soma:
- Tanzania imepokea mkopo kutoka kwa Korea Kusini na kutoa sehemu ya bahari na madini

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Kitila Mkumbo ameandika:


URONGO. Hakuna masharti kama hayo. Mkopo huu ni sehemu ya makubaliano katika awamu ya pili ya ushirikiano wa miaka mitano ijayo. Ni mkopo nafuu utakaolipwa katika miaka 40 kuanzia mwaka wa 26 kwa riba ya 0.01%.
Kuhusu madini ya kimkakati (strategic mineral resources-SMR), mkakati wa Tanzania ni kutafuta wawekezaji watakaowekeza katika utafiti, uchimbaji na kuongeza thamani ndani ya nchi.
Tumeweka wazi duniani kote kuwa tunataka wawekezaji watakaosafirisha betri za magari na sio madini ya kimkakati kwa lengo la kutengeneza betri hizo nje ya nchi. Kuhusu uchumi wa buluu, tumesaini mkataba kwa lengo la kushirikiana katika kuboresha teknolojia ya uvuvi, kujenga bandari za uvuvi na viwanda vya kuchakata Samaki. Eneo lingine ni ushirikiano katika teknolojia ikiwemo kujenga chuo cha TEHAMA nchini.
PIA SOMA
- Ziara ya Rais Samia Korea Kusini atasaini Mkopo wa Tsh. Trilioni 6.51


Jamaa naye ni chawa badala ya kuwa mtaalamu anaongelea mkakati sisi tunaongelea walicho sign

"Kuhusu madini ya kimkakati (strategic mineral resources-SMR), mkakati wa Tanzania ni kutafuta wawekezaji watakaowekeza katika utafiti, uchimbaji na kuongeza thamani ndani ya nchi. "

Hapa sasa anaongea nini Je Wakorea wanakuja kujenga hivyo viwanda ndiyo au hapana?
 
Back
Top Bottom