Prof. Kitila Mkumbo: Ushauri wa Kishujaa umesababisha Tanzania ishtakiwe katika Mahakama za Kimataifa. Wasomi wetu waliwadanganya Viongozi

Mlimtukana Lissu leo mmeanza kushtakiwa na bado.
Hahaha hahaha. Mpaka leo Hpa kuna wapuuzi wanamuita lisu msaliti wa taifa. Lisu ninayemjua tangu kipindi cha GENERAL ON MONDAY akichambua mikataba ya hovyo ya madini hukoNYAMONGO awe msaliti kwa Tanzania hata kupigwa risasi ? Mungu atalipa kama hajalipa bado
 
..kuna kesi moja serikali haikutuma wawakilishi, mahakama ikatuteulia muwakilishi, hukumu ilipotoka tukapigwa.

..hayo ndio maamuzi ya kizalendo ya Magufuli na washauri wake.
Uliisikia lakini hotuba ya Magufuli akiwalalamikia Mawakili wetu? Kifupi kushtakiwa ICSID kila nchi ina mashtaka kule hata ile ya Biwater ipo. Hoja ni kutazama kwanza sheria zetu sisi kwa wawekezaji inasemaje. Kama kuna makosa hayo ndio ya kuzungumzia sio nani kafanya nini. Pitia hapa ujue kwanza sheria inayokulinda wewe International Arbitration 2022 - Tanzania | Global Practice Guides | Chambers and Partners
 
Hatutaki lawama, tunataka hatua!
Wakili havunji mkataba, mkataba unavunjwa na serikali kwa maagizo ya rais, waziri au baraza la mawaziri kwa ridhaa ya rais
 
Ni muhimu kwanza kutambua kesi hizo 7 ni za madai gani? Kama mtakumbuka ndege yetu ilizuiwa Canada na South kwa madai ya mwaka 1974. Je, hilo lilikuwa kosa la nani?
Hapa umeacha facts nyingi.
Mkulima Stein alishashitaki mahamani, akashinda kesi, akawa analipwa kwa utaratibu maalum katika serikali zilizofuata ikiwemo ya Kikwete.

Alipoingia Magufuli madarakani akajifanya mzalendo sana akaruka deni, hicho ndo chanzo cha Mkulima Stein kwenda mahakamani kukazia hukumu na kukamata ndege!
 
Hatutaki lawama, tunataka hatua!
Wakili havunji mkataba, mkataba unavunjwa na serikali kwa maagizo ya rais, waziri au baraza la mawaziri kwa ridhaa ya rais
Unalosema kweli lakini kumbuka ni Magufuli aliterudisha ofisi ya Wakili mkuu wa Serikali baada ya kutokuwepo kwa miaka. Hii ilitoka na sisi kushimdwa kupeleka mawakili katika baadhi ya kesi tukapigwa na kitu
kizito.. https://www.osg.go.tz/news/ofisi-ya...ia-kuendesha-mashauri-ya-serikali-kwa-ufanisi
 
Utaratibu upi? Hivi unaijua kesi hiyo au unazungumza tu kutaka kumpamba JK? Huyu alilishwa kitu ni katika mpango wa kumuondoa JPM. Rudi kaisome kesi yenyewe vizuri..
 

..huko ICSID hatuwakilishwi na mawakili toka hapa Tz.

..kuna taratibu zake za kumpata msuluhishi ambaye anaaminika na kukubalika na pande zote kusikiliza shauri.

..ofisi ya mwanasheria mkuu kazi yake ni kutoa ushirikiano na supporting evidence / documents kutetea upande wa Tanzania.

..tatizo huwa linaanza hapa nyumbani kwa viongozi wetu kujifanya wababe na kukiuka mikataba waliyosaini.

..Matokeo ya ubabe wa viongozi wetu ni kushindwa ktk mashauri mengi yanayopelekwa ICSID.

..Kama tunataka tusipigwe basi tuhakikishe tunatengeneza mikataba inayotulinda, na baada ya hapo tuiheshimu.

..Jambo lingine, ambalo ni gumu, na serikali inaogopa kulifanya, ni kujitoa ktk mikataba inayoelekeza kwamba migogoro na wawekezaji itakwenda ICSID, au uwekezaji hapa nchini italindwa kupitia MIGA. Hali hiyo itaondoa uwezekano wa Tanzania kushtakiwa huko nje.
 

Na niseme wazi, hata nikitofautiana na haya aliyoyasema hapa; ambayo ni sawa na uliyoyasema wewe, haina maana kwamba kuna sehemu tunaweza kubaliana katika jambo hili hili, tukielezana vizuri.

Sasa ngoja nikukumbushe pia, kwa vile nawe umenikumbusha.
Nilishasema humu JF, kwamba hali ya nchi yetu ilivyo sasa, hasa kwa hawa tunaowaita wanasiasa wetu, ni wachache sana kati yao walio na uwezo wa kusimama na kulitetea jambo lolote wakijua kwamba kutetea huko kutawanyiama chakula chao kinachopatikana kupitia kwa ufadhiri wa chama au kiongozi mkuu wa chama.

Naomba mtu yeyote anayeweza kunipa mfano, kwa mfano wa kundi lile la akina Njeru Kasaka kwa sasa hivi, ni nani ndani ya CCM, au hata ndani ya CHADEMA?. Ni nani? Ningemhesabu Lissu katika kundi hilo, lakini hali yake ninaielewa, siwezi kumlaumu.

Na baada ya kuyasema hayo kumhusu huyu Bwana anayeongelewa hapa nikasema kuwa nipo tayari kumsikiliza yeyote anayepaza sauti kwa sasa hivi, bila kujali alifanya nini huko nyuma wakati wa Magufuli, iwe ni kwa woga wakati huo, au iwe ni kwa kutafuta fursa ya uteuzi wakati huu, nipo tayari kumsikiliza mtu huyo kama sauti yake inatetea maslahi ya waTanzania.

Kwa hiyo, kwa sasa hivi, bila kujali anachokitafuta Luhaga Mpina, nitamsikiliza, kwa sababu sisikii sauti nyingine yoyote, na zaidi zaidi kwa masikitiko makubwa hata toka kule kwa CHADEMA, ambayo tulidhani ndio mbadala ttuliobaki nao. Lakini CHADEMA imetekwa, sasa tutafanyaje.

Natumaini nimejieleza vya kutosha.
Kama nimechanganya humo ndani, naomba msamaha, kwa sababu nilitiririka tu, sikurudi nyuma kuhariri chochote.

Cc Kalamu pita hapa, hoja hii hii nilisema juu ya Mpina.
 
Mimi naenda na FACTS sio habari za kuhadithiwa Government of the United Republic of Tanzania v Steyn and Others (28994/2019) [2019] ZAGPJHC 312 (4 September 2019)
 
Duh!

Mkuu 'Mkandara', hata nawe unaamini Magufuli aliondolewa?

Magufuli angekuwa anadunda hadi leo isingekuwa kiburi chake cha ujinga kuidharau COVID-19.

Ni tabia hizo hizo za dharau na kutotaka kufuata taratibu ndizo pia zilizovuruga mambo mazuri aliyonuia kuyafanyia nchi, kama haya ya madini.

Kwa mfano, angeachana na majivuno ya kujiona yeye hakuna wa kumpiga, akamwita Lissu na wengine na kuwasikiliza wanasema nini kuhusu swala hilo la mikataba, pasingekuwepo na tafrani zote zilizotokea na akina Lissu wasingefika huko walikofika.

Weaknesses za Magufuli zilikuwa katika tabia zake mbovu.
 
Bana wee kaondoka na covid au moyo? Tanzania walochanja ni mil. 3 kati ya mil.60 unataka kunambia hao wengine woote wasiochanja walikuwa wajinga? Mbona wapo wanadunda mtaani wazimaaa!

Kwanza walochanja kila siku wagonjwa! Tena nasikia wanawake ndio kabisa hata hedhi hazina mpango zinapotea. Mimba za kuhesabu..
 
Tusiende mbali sana na hili mkuu Mkandara, huo moyo uliomuondoa ulichagizwa na COVID-19.
Magufuli tayari alikuwa na tatizo ambalo COVID-19 ikimgusa tu, kama ilivyomgusa, anakwisha.

Kitaalam inaitwa alikuwa na 'a predisposing condition' ya kumalizwa.

Tusiende huko kwenye kuchanja na mambo mengineyo, huko ni ku-complicate' tu jambo lililokuwa wazi katika kuondoka kwa Magufuli na hata Mkapa.

Hili tuliachie hapa. Hakuna mchawi.
 
Taarifa hii imetoka kwa daktari gani au hospital gani? Hilo Tatizo la Moyo wangapi wana tatizo hilo Tanzania? hata Mzee Mwinyi analo miaka na Covid imepita, yule pale mzimaaa!

Ukweli ni kwamba jamaa alikuwa lazima aondolewe kwa sababu alikuwa na maadui wengi nje na ndani kutokana na Maslahi tu. Awamu hii wanajua na ndio maana kutwa ni kumkana JPM kama kwamba wamelazimishwa kusema wewe upo upande gani? Wote hawa ni Mtandao hawana msimamo ni WAOGA kupitiliza.
 
Mada za aina hii na hasa wanaozileta zinashangaza kwelikweli.

Huyu Kitila Mkumbo mwenyewe, si anajihesabu kuwa "msomi"? Kaingia serikalini na kawa hadi Waziri, na huko kwenye upinzani yote aliyohusika nayo yanajulikana.

Sasa yeye anayo tofauti ipi na hao wasomi wengine anaowazungumzia hapa.

Hapana, sikatai mada yake, ambayo ni kweli kabisa, ninachokataa ni unafiki wake.. Asijihesabu yeye kwamba anayo tofauti na hao wasomi wengine karibu katika maeneo yote wanakopatikana wasomi hao.

Kama anapokaa nje ya ulaji kidogo akili inamrudia, basi ningemshauri akae chini atazame ni kit/mambo gani hasa yanayovuruga wasomi wetu wasiweze kutimiza wajibu wao kama wasomi walio na uwezo sahihi.
Hapo atakuwa ametoa mchango muhimu kwenye taifa hili. Siyo kulalamikia mambo ambaye hata yeye ni mshiriki mkuu.
 
Kwenye search andika United republic of Tanzania
 
Sasa ulidhani Magufuli angeishi muda anaotaka yeye, au kifo cha lazima kimeandikiwa baadhi ila wengine wanakufa muda wanaotaka wao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…