Prof. Kitila Mkumbo: Ushauri wa Kishujaa umesababisha Tanzania ishtakiwe katika Mahakama za Kimataifa. Wasomi wetu waliwadanganya Viongozi

..kipindi hicho Prof.Kitila alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji.

..suala hili wanaopaswa kubeba lawama ni Prof.Kabudi, na Prof.Kilangi.
Hapana, alikuwa Wizira ofisi ya rais wakati kitengo cha TIC kuhamishiwa Ofisi ya rais chini ya Mama Kariuki kama sikosei..
 
mfumo umewadekeza sana kwa kuonea wananchi bila kuwajibika au consequences zozote.
Haya mapungufu unayodai ni mapungufu, kiuhalisia siyo Mapungufu. Itoshe Kusema ni Mfumo uliojengwa na ni wa Kibeberu zaidi na ndio unaotumika na Wawekezaji zaidi kuliko Viongozi au Serikali za Kiafrika-its a zero sum game.
Supremacy at best.
kwa mfano kiongozi anaweza kutoa uamuzi nyumba za wananchi zivunjwe na kusitokee athari zozote kwake.
Tofauti ya mtoa maamuzi hapa hauondoi dhuluma ila huwa nazo zinatumika na Nchi tunazo taka kufanyia ulinganishi wa nani anayefanya kwa haki. Tofauti hapa ni nani aliyefanya hivi(Mweusi)Hayati Raisi Kiongozi aliyekuwa akihamasisha kuondokana na fikra na mawazo ya 'Unyonge' dhidi ya maamuzi yetu na yaliyo na tija Kwa mwananchi vs "Wawekezaji' au Mabeberu. Unatumia reverse psycology lakini kiuhalisia, maamuzi hayo yametokana na "Sheria" zillizoasisiwa na kurithishwa kutoka kwa "Wakoloni" na ambazo kwa wakati huo zilizokuwa na lengo za kuwaburuza wanyonge. Walakin akitumia Mwafrika sheria hiyo hiyo, yeye huambiwa amepitiliza madaraka yake na ni Dikteta-Hayati alitumia Sheria aliyorithishwa. Na mnapindisha hakutenda haki wakati Sheria na nguvu ya Dola inampatia uwezo huo kisheria. Hakika, kwa hoja mnazojenga kuwa haikuwa haki, ni uthibitisho kuwa sheria za Ukoloni na Ukoloni mamboleo unaegemea kutoa haki kwao tu. Na kwamba Mwafrika akitumia msumeno huo huo basi anayepata machungu hayo ni Mzungu.

Sheria zipitiwe na ziafiki mienendo na tamaduni na falsafa ya mwafrika.
Na wananchi hawana mahali pa kwenda kulalamika kwasababu viongozi wetu wana-control kila kitu ikiwemo mahakama.
Hawa "Wananchi" unaodai ndio Wanaolalamika na uhakika unasema/unamaanisha "Wawekezaji".....Ukweli ni kuwa Wananchi wanaolalalamika kila uchwao ni wale wanaobaki na kubaki na Umasikini hususan katika maeneo yanapo patikana Madini Wakati Wazungu/Mabeberu wakifaidika mara 1000+ Hayati alitaka kubadilisha mwenendo huo(status quo) ila kwasababu ya kukuta tayari Wawekezaji wanakuja na Uliyodhihirisha hapa kuwa
lakini hawa wawekezaji hawana tabia za kinyonge-nyonge kama Watanzania wa kawaida

☝️ Lugha hiyo hapo juu ni Lugha ya Kibeberu. It is Racist at its core.- Basi, pale anapotokea mtu kuanza kuwaondoa watu Fikra hizo za Kinyonge na kujitafutia haki(self advocacy) ndipo hapo manpokuja na kudai maushenzi.

Ukweli, Wazungu na wawekezaji wengi hawana tabia za Kinyonge na wana tabia za Ukuu. Supremacy👇
Pia wawekezaji wana option ya kwenda kutafuta haki zao nje ya nchi ambako viongozi hawana control au mamlaka.
Hiyo option ndio inayowapa Kiburi. Hiyo option ndio inawapa kiburi "Wananchi" uliowataja huko juu na sio option walioipata "Wananchi" wanyonge wa Nchi yetu. Na pale inapotokea watetezi wa 'option' mna waua. It is Documented and it has been proved.
 
Tuliweka tahadhari gani wakati Magufuli alikuwa akibeza barakoa utadhani kitu gani. Alikuwa akiziita "matambara ya puani", siku nyingine akasema "zinafanana na titi la mwanamke". Mawaziri wake akawapiga marufuku kuvaa barakoa in his audience, akaenda church akamsifu paster ambaye hajavaa barakoa.

Magufuli alihandle vizuri wave ya kwanza ya Covid siyo ya pili. Ya pili alideny kabisa uwepo wake mpaka maaskofu wakatoliki walipotoka na kujilipua wazi kutangazia umma kuwa wanapoteza watawa wao wengi sana.
 
Naenda na fact kwa sababu kuna jamaa kamzungumia huyo mzungu kuhusiana na ndege yetu kukamatwa Canada. Tatizo lenu mnachanganya mada iwe kesi hizi 7 au kwa nini ndege zetu zilikamatwa. Kesi hizi zinasomwa mahakama tofauti sii lazima nchi moja

..zimekamatwa ndege tatu.

..bombadier iliyokamatwa Canada kwa kesi ya mkandarasi aliyevunjiwa mkataba na Magu wakati akiwa waziri wa ujenzi.

..airbus iliyokamatwa Afrika Kusini kutokana na kesi ya mzungu aliyenyang'anywa mali zake wakati wa utawala wa Nyerere.

..Boeing inayoshikiliwa Uholanzi. Madai ya kesi hii siyafahamu.
 

Rudi kasome tena kesi zenyewe halafu rudi ujadili, sio kubeba vitu wakati huujui ukweli..
 
Sasa Mkuu mtu akipinga kuvaa Barakoa ndio atakufa au? Watu wangapi hawakuvaa Barakoa na leo wapo hai. Watu wangapi waliugua Covid-19 Tanzania na bado wapo hai. Hakuna guarantee ya kupona ana kufa kwa sababu unapinga.

Hoha inabaki palepale, JPM alikuwa rais wa JMT, alipigiwa kelele aondike Chato alikojificha aje Dar. Kafika Dar umauti umemkuta tukaambiwa tatizo la moyo. Nyie mnasema ni covid-19 kwa report ya nani? Huo moyo pia kwa report ipi? Maana Lissu alitutangazia maoema JPM kisha kufa siku tatu kabla. Tunachojua sisi alipelekwa kwa Mzena sio Muhimbili wala Mloganzila.

Sii kosa kuhoji afya ya kiongozi wangu iwe JK, Mkapa au nani maana hata Nyerere wakati ule nilihoji humu nilipomsikia Warioba akisema alimkuta mwalimu kule nyumbani kwake Butiama anaumwa Mkanda wa jeshi akiuguzwa na Mkewe mama Maria! Nilijiuliza hivi kweli Mwalimu hata kama anaumwa Malaria ni mtu wa kuhudumiwa na mkewe?
 
Covid imeua mamilioni including watu wengi wazito, Magufuli yeye ni nani hata imuogope?.
Maalim Seif imemuondoa, Kwanini imshindwe Magufuli?
 
Really?

Mti shamba dawa ndiyo uende kunywa kikombe cha babu random dawa ya miujiza masharti kama ya mchawi.

Mkuu na wewe ni mmoja kati ya watu mlioamini ujinga wa kikombe cha babu?
Hakuna ujinga katika kuamini dawa hii ya miti shamba inaweza kuponya maradhi yasokuwa na dawa za Hospital kama kisukari.

Binafsi sikuamini kwa sababu sikuwa mgonjwa wa kisukari lengine ningekuwa naumwa ningekunywa kikombe pahala popote. The fact is natumia sana miti shamba hapa nilipo kuliko dawa za Hospital. Nakunywa na Nafukiza kwa imani kama walivyojiponya wazee wetu.

Labda nisherehe kusema sikuchanja chanjo yoyote ya Covid -19 na namshukuru Mungu sijaugua hata Covid yenyewe!

Alhamdulillah
 
Covid imeua mamilioni including watu wengi wazito, Magufuli yeye ni nani hata imuogope?.
Maalim Seif imemuondoa, Kwanini imshindwe Magufuli?
Sijasema hakuna watu walokufa na Covid -19 lakini kwa Magu wewe umepewa taarifa hizo na nani? Peter yule wa Royal tour? Daktari gani umemsikia akitoa taarifa hiyo?

Anyway tuachane na haya tupo kwenye mikataba mibovu waloweka miaka ya 90. Hapa ndipo point yangu iliposimama.

Mimi namkubali kabisa Magufuli kujaribu kulikomboa Taifa letu kwenye mikataba hiyo na kama ndio sababu ya Kifo chake, basi yule ndiye Kiongozi nimtakae..
 
Hiyo dawa ya mitishamba unajua hata chemical formula yake?

You are an anti-vaxxer, I am not surprised by your dilapidated illogical views.
 
Mkuu JokaKuu , kwanza asante kwa bandiko hili, very insightful, pili kwa ruhusa yako nitalitumia bandiko hili kama mbegu ya kuoteshea bandiko langu fulani, ila hizi hoja za Prof. Kitila ni very valid.

Angalia tarehe ya bandiko hili, uangalie niliuliza nini na kulinganisha na alichoshauri Prof. Kitila Zita Act Retroactively? Tutavunja Mikataba Yote Iliyopo? Can we Stand? Do we have the Guts? humo nilisema
P
 
Hiyo dawa ya mitishamba unajua hata chemical formula yake?

You are an anti-vaxxer, I am not surprised by your dilapidated illogical views.
Nafanya sana utafiti hata wewe unaweza ku google inategemea unataka kufanya nini mwilini hata mazoezi ni dawa.

Kwa mfano kuzuia Flu na Maradhi ya SAR natumia vitunguu maji, limao, karafuu, kunywa na kujifukiza. Pia maziwa na Bizari kavu hunywa. Hutafuna mbegu za mronge kila mara.Toxic naondosha kwa kuchemsha maganda ya nanasi na matango.

Nadhani itakusaidia hata wewe, jifunze kutumia organic plants ni dawa asilia.
 
Utafiti wako ndo umekufanya uwe anti-vaxxer?

Umechapisha papers ngapi mpaka sasa? Ziko wapi?
 

Duuh
 
Hayo makampuni yalingoja mpaka mwamba aondoke ndio wafungue mashtaka ya kuvunja mikataba ya madini ??!! Wakati akiwa Hai aliyevunja mikataba walikuwa wanamuogopa kumshitaki ??!! Ukistaajabu ya Musa ……….. !! Michongo inakuja !!
Si wanapima upepo yule ameshtaki Amelipwa kwa nini mimi nisishtaki ili nilipwe wanaangalia na aina ya rais na utawala uliopo
 
Kuna ndugu yangu alidevelop matatizo ya tumbo baada ya kugonga sana malimau na matangawizi kipindi kile cha Covid. Sasa hivi tumeshamzika
 
Tazama records ya Uuzaji madini kwa Tanzania. Mwaka 2019 ndio tuliuza dhahabu nyingi tani 55 kwa mwaka, leo tumeshuka hadi tani 43 ni sababu gani ikiwa sheria ni zile zile mbovu..
Uongozi tu samia wala hajishughulish na hayo madin yeye anaangalia tozo ndo rahisi kwake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…