Wanabodi,
Kitakacho Tokea
Kitakacho tokea ni ama baadhi ya vipengele vya sheria hii mpya vitapuuzwa, ama ili kuepuka aibu ya kupitisha sheria mbovu kwa mbwembwe, serikali itapeleka kimya kimya, marekebisho ya baadhi ya vipengele vya sheria hii, kikiwepo hicho kipengele cha arbitration, kitaondolewa ili kurejesha confidence kwa wawekezaji. Kwenye hili, time will tell, kama Nyerere na Sokoine walikuwa ni wakali ukweli ukweli, lakini walishindwa, hivyo kwenye hili la sheria kutekelezwa kwa retroactively, naowaomba mimi niwe mkweli bayana wa nafsi yangu, Mwalimu wangu Prof. Kabudi na wanasheria wake, waliotunga sheria hii kwa mtindo wa zimamoto, wamemdanganya rais Magufuli kwa kumtungia sheria yenye vipengele vya ajabu, halafu rais aka accent, then sheria hii itashindwa kutekelezwa, hivyo soon watapeleka marekebisho Bungeni na kumrudia rais a accent marekebisho hayo, na hili likitokea, naombeni hoja za bandiko hili zizingatiwe, Tanzania tutaonekana ni nchi ya ajabu, tunatunga sheria za ajabu kwa mbwembwe, tunazipitisha kwa mbwembwe, rais wetu ana zi accent kwa mbwembwe, lakini katika utekelezaji ndipo tunajikuta kumbe Bunge letu, na serikali yetu, iliyosheheni wanasheria manguli tena wengine ni waalimu wetu wa sheria wa chuo chetu kikuu cha Dar es Salaam ambao sisi tulipokuwa wanafunzi tukisomea sheria, waalimu hawa ndio waliotufundisha kuwa sheria yoyote inayotungwa kama ita act retroactively is a bad law, it's illegal, lakini leo, waalimu hawa hawa ndio wamegeuka wanasiasa na wao sasa ndio hawa wametunga illegal law, wakaipitisha, wakampelekea rais akaisaini ianze kutumika, huku wanajua fika retroactively law is illegal law kwenye jumuiya ya Madola, lakini bado wamepitisha, sasa siku ya kurejea Bungeni kuyarekebisha haya madudu yao ya kisheria, hizi sura zao wataziweka wapi?.
Paskali