Prof. Lipumba: Bajeti iliyosomwa ni mbovu haijawahi kutokea tangu tupate uhuru. Takwimu nyingi haziko sahihi

Kwa hiyo hicho kilichoandikwa hapo ndio uchambuzi wa Professor Mbobezi na nguli wa uchumi!? Au mmepunguza alichosema? Maana sioni Hizo takwimu (facts and figures) alizotoa hapo!
 
Ni ukweli mtupu.
Mwigulu ni msomi wa uchumi ila ana uwezo wa kwenye vitabu tu syo ktk nyanja za kuweza kuvitendea kazi
 
Lipumba kalinganisha may na June hayo yako ya Ukraine vita ya Ukraine iliyoanza February baki nayo mwenyewe
Wapi kwenye uzi kumeandikwa May na June.!? Hapo imeandikwa May 2021 na May 2022. Kwani hata hizo takwimu zimechukuliwa kabla ya bajeti kusomwa. Kwa hiyo Lipumba kaeleza facts kulingana na time frame hiyo. Wewe unakuja kuleta vioja vya time frame ya May na June ya mwaka huu...Ujinga huu kawaeleze wajinga wenzako mnaolipwa posho kutoka ikulu..
 
Mwigulu anaandaa bajeti ili kumfurahisha bosi wake bila kuihusianisha na mipango, matokeo yake ndio haya ametengeneza bomu asilojua alitegue vipi.

Matokeo yake kila akitolea ufafanuzi wa jambo anazidi kuongeza maswali badala ya kutamaliza.
Wampe mbunge wa vunjo hiyo chance, dr Chaaz Kimei
 
Lakini hata mimi naunga mkono kuwa hii bajeti nadhani ni ya ovyo kwa maana serikali yetu kutenga trilioni moja na kichele kwa ajili ya maendeleo AF trilioni 13 kwa matumizi ya kawaida hilo jambo linatia wasiwasi sana
 
Mwingilu Nchemba kila kitu kwake ni Siasa tu.

Mwaka Jana alikuja na Tozo zisizo kuwa na kichwa Wala miguu hadi sipik n Wabunge na Rais na Mawaziri wakashangaa wakati bajeti ishapita.

Hata sasa tutegemee maumivu.
 
Mwingilu Nchemba kila kitu kwake ni Siasa tu.

Mwaka Jana alikuja na Tozo zisizo kuwa na kichwa Wala miguu hadi sipik n Wabunge na Rais na Mawaziri wakashangaa wakati bajeti ishapita.

Hata sasa tutegemee maumivu.
Nilijua nyie sisiemu wenzety mna mfumo mwingine wa kifedha? kumbe ndio huu huu wa watanzania wote?
 
Hapo Mwigulu Nchemba kabugi.
Kuunganisha vitambulisho vya taifa na kodi ni upuuzišŸ¤”
 
Umenena vyema Professor Lipumba, waziri aliyepo kiti kimempwaya, anawaza kuchora Jina lake tena juu ya mawe Nchi nzima.

Dr Charles KIMEI atatufaa Kwa nafasi hiyo. Amen
 
Aisee...

Ajabu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…