Prof. Mbarawa: Treni hii ya Tanzania siyo high speed train kama zile za vichwa vilivyochongoka, Wananchi eleweni hilo

Prof. Mbarawa: Treni hii ya Tanzania siyo high speed train kama zile za vichwa vilivyochongoka, Wananchi eleweni hilo

Kibonde chameleon kilisibitishwaje bila kupima ubongo kama alivyo fanyiwa baba wa taifa.
 
Kama hizo za wenzetu zinaenda 200km/hr na zetu zinaenda 160km/hr sasa speed 40 tu ndo ifanye tuletewe majitu yasio eleweka yamerepewa mpka basi dah tunapigwa alaf tunapewa maelezo ya kupigwa na bado watatupa hela kipindi cha uchaguzi tutawarudisha kutupiga tena
 
Hapa Prof Mbarawa, kule Dkt Mwigulu, Màra Paap Mzee Makamba Sr, ukigeuka tu eeee Wastaafu, Wauniiiiiiiiiiiiiiiiiii......Makamba Jr na Awesu kazi iendelee.
 
Waziri wa Uchukuzi Prof Mbarawa amewataka Wananchi kutochanganya Treni hii ya Tanzania na zile za high speed zenye vichwa vilivyochongoka.

Prof Mbarawa amesema picha zinazorushwa mitandaoni na watu wasio na nia njema ni zile za high speed zinazotembea zaidi ya km 200 kwa saa.

Za kwetu ni hizi mnazoona tunazipokea na haya ni Mabehewa 14 ya Daraja la tatu(economy) na mwezi February mwakani tutapokea Ya Business class na First class

Mabehewa haya ni kwa ajili ya masafa marefu na yatavutwa na Vichwa vya Umeme lakini yale ya high speed Vichwa vyake vinaunganishwa direct na mabehewa, amesisitiza Mbarawa

Source ITV Habari
Washatuchosha aiseh, Mtu unachoka hadi ukiona kweny TV watu wamekaa kijani unatoka ndani nduki kuogopa usije pata mshtuko wa moyo.
 
Kwema hizo train ni ghali sana kuliko ghrama ya uwekezaji kwenye hiyo rail. Unakuta watanzania wanasema kitu flani ni ghali kuliko kila lakini ukichugulia unakuta ufisadi wa bilioni 50 zaidi. Marekani sio kwamba nimeshindwa ni priority tu .kama tumenunua drimliner. Bullet ya train zinatushindaje jamani
Narudia,

Reli yetu ni ELECTRIFIED...

Kuwa electrified haimaanishi inaweza kutumika na hizo Bullet Train....

RELI za high speed trains ni tofauti na hii ya kwetu (sio in terms of physical structure).

Hii ya kwetu ina uwezo wa ku-handle trains zinazotembea hadi 160km/hours wakati Bullet Trains/High Speed Trains zinatembea from 250km/hours na kuendelea!

So, ili SGR yetu iweze ku-handle Bullet Trains basi inatakiwa iwe completely modified, na hata reli zake zinaitwa high speed rails.

Na hilo likifanyika, ina maana itabaki fahari tu kwamba tuna high speed rail na high speed trains lakini 99.9% HAWATAWEZA ku-afford coz ukweli ni kwamba, nauli zake zinakuwa kubwa sana kuzidi hata nauli za ndege!

Pili, sijasema Marekani wameshindwa bali ni kama hazipo tu kwa sababu wanaona not commecially viable.

Suala la priority ni la serikali lakini private sector wakiona very profitable, watajenga tu lakini ndo kwanza kuna eneo dogo sana ndo wamewekeza na ma-research kila siku!!

The problem watu mnaongea kishabiki, kwa staili ile ile kwamba "nchi kama Tanzania inakosaje kuwa na ndege zake yenyewe wakati ki nchi kama Rwanda wanazo"

With that Pride, zikanunuliwa ndege ambazo leo hii zinaingiza kutia hasara tu!
 
Back
Top Bottom