TANZIA Prof. Mwesiga Baregu afariki dunia

TANZIA Prof. Mwesiga Baregu afariki dunia

Moja ya Vifo vilivyoniumiza sana ni pamoja na hiki cha Professor Baregu.Nilikuwa nafutahia sana michango yake ktk Malumbano ya Hoja,This week in perspective,na mahojiano ya redio na Television za nje...(Idhaa za Kiswahili).MUNGU AMLAZE MAHALI PANAPO MSTAHILI GWIJI HUYU.AMEN
 
Kwann covid 19 wasingekufa wao ,pimzika prof baregu,mwl,mzazi ,mlezi.pumzika kesho yangu
 
View attachment 1816939
Ni habari mbaya ambayo imetokea muda si mrefu.

Aliyekuwa Mhadhiri wa Vyuo Vikuu mbalimbali nchini, Prof. Mwesiga Baregu amefariki dunia mapema leo.

Prof. Baregu alikuwa pia Mjumbe wa Kamati kuu ya CHADEMA.

Pia Soma: Prof. Baregu alifukuzwa UDSM kwa sababu za kisiasa, huku Bashiru akiachwa kwakuwa ni CCM
View attachment 1817281

Dar es Salaam. Mwanachama wa Chadema na mwanazuoni, Profesa Mwesiga Baregu amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumapili Juni 13, 2021 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano ya umma Muhimbili, Aminiel Aligaesha amesema, “amefariki saa tano usiku wa kuamkia leo akiwa ICU (chumba cha uangalizi maalum) na alikuwa hapo kwa takribani siku 15.”

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Mkurugenzi wa Itikadi na Uhusiano wa kimataifa wa Chadema, John Mrema amesema chama kitatoa taarifa rasmi taarifa baada ya kikao na wanafamilia.

"Tunaelekea hospitali ya Muhimbili kukutana na wanafamilia halafu tutatoa taarifa rasmi," amesema Mrema.

Katika ukurasa wa mtandao wake wa kijamii wa Twitter Waziri wa Viwanda na Biashara, Profesa Kitila Mkumbo amesema, "pumzika kwa amani Profesa Baregu. Mmoja wa wasomi walioamini kuwa huwezi kutenganisha taaluma na siasa. Ulitufundisha baadhi yetu tunaokubali msimamo huo wasomi wanaweza kufanya siasa bila kupoteza sifa zao.’”

Mwingine aliyeandika ujumbe Twitter ni kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe akimtakia mapumziko mema Profesa Baregu.

Profesa Baregu aliyekuwa mhadhiri wa sayansi ya siasa na utawala wa umma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, baadaye alisitishiwa mkataba wake kwa kile kilichoelezwa kuchanganya utumishi na siasa.

Baadaye alihamia Chuo kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Alikuwa mjumbe wa kamati kuu ya Chadema hadi mwaka 2019.
Poleni sana wanachadema na familia nzima, jamaa, na marafiki wa Prof. Baregu. Mungu aipumzishe roho ya marehemu pema peponi. Aminah.
 
Impact yake katika siasa angalia humu wanavyomlilia kila thread. Hakuna atakayekamtwa kwa kushangilia kifo chake.
Sijui wewe unaongea nini kwani hata mimi namlilia lakini siyo kwa sababu ya alikuwa na political impact yoyote kwangu.

Labda hujui maana ya political impacts
 
Mungu anasamehe watu wanaotubu wakiwa wazima (kabla ya kifo). Mungu hatumii middlemen. Kwamba watu wengine watakuombea toba baada ya kufa na Mungu akakusamehe ni ubatili. Mend your ways before you die.


Wewe unadhani Mungu ni kama wewe usiweza kusamehe kwa kuombwa Msamaha kupitia watu wengine???!!.

Wapo watu wanaoweza kumuombea mtu Msamaha kwa Mungu na Mungu akawakubalia, sisemi kwamba ni lazima apokee maombi ya msamaha bali anayo hiyari ya kupokea au kutopokea tunachofanya sisi ni kumuombea tu kama binadamu mwenzetu kwani sisi sote kifo ni unavoidable isitoshe pia watu tujifunze kuombeana katika jambo la aina hii licha ya kwamba kujitahidi katika mema ndiyo the most Paramount thing.
 
That does not make sense. Kwa nini utende mema duniani sasa? Fanya ukatili kama Magufuli halafu omba ndugu wakuombee ukishakufa. Ingekuwa ni kweli unachokisema, then kusingekuwa na motivation ya kutenda mema ukiwa hai.

Angalau imani yangu inasema ukishakufa, hauwezi kubadilisha kitabu ulichokiandika wakati ukiwa hai. Najitahidi kukiandika kitabu changu sasa wakati nikiwa hai. Hakuna mtu atakaibadilisha baada ya mimi kutoweka. Kama ni maombi, najiombea sasa hivi.
Wewe unadhani Mungu ni kama wewe usiweza kusamehe kwa kuombwa Msamaha kupitia watu wengine???!!.

Wapo watu wanaoweza kumuombea mtu Msamaha kwa Mungu na Mungu akawakubalia, sisemi kwamba ni lazima apokee maombi ya msamaha bali anayo hiyari ya kupokea au kutopokea tunachofanya sisi ni kumuombea tu kama binadamu mwenzetu kwani sisi sote kifo ni unavoidable isitoshe pia watu tujifunze kuombeana katika jambo la aina hii licha ya kwamba kujitahidi katika mema ndiyo the most Paramount thing.
 
Kwa heri Mwamba

Huyu Gwiji ndie alikuwa Mmoja wa Supervisor wa PhD ya Dr Kondilize Rice (1982) baadae alikuja kuwa Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani
Hiyo si kweli. Baregu alikuwa Stanford akiwa mwanafunzi.
 
Back
Top Bottom