Prof. Ndalichako ni kweli Serikali inazifaulisha makusudi shule za Serikali dhidi ya shule Binafsi?

Prof. Ndalichako ni kweli Serikali inazifaulisha makusudi shule za Serikali dhidi ya shule Binafsi?

CCM inaharibu nchi, Rwanda inatengeneza simu Magari??
 
ex
Ni kwasababu rufaa inakatwa kwa huyo huyo aliyesahihisha mwanzo si kwa Mamlaka nyingine na kiuhalisia hata kuiita ile kuwa ni rufaa nao ni usanii mwingine tena.
exactly
 
Nimeongea na msahihishaji mmoja, ambaye namuamini, akaniambia nilichokiandika hapo.
Sio kweli mkuu kakuingiza Chaka.
Usahihishaji wa necta upo very systematic and fair hilo haliwezi kutokea.
Labda kama wanafanya baada ya kusahishisha lakini wakati wa kusahishisha hapana si kweli.
Kuhusu kukata rufaa usimshauri matokea ya necta huwa ni ya halali kabisa ndio maana wanaotoka kwenye rufaa ni asilimia ndogo Sana.
Kwanza mnafanya trial marking mpk tofauti ya wasahihishaji wa swali moja iwe ndogo Sana. Halafu ndio mnaanza tiki Sasa.
Sio kwamba ukipiga tiki imetoka no Kuna wanacheki na wanakera mzee.
Mnahesabu marks manually haalfu marks za Kila swali zinaingizwa kwenye system total itally na manual count.
Marks zikiingizwa kwenye system Kuna wanacheki kama zimeingizwa sahihi.
Baadae Mnacheki extreme cases.
Hapo unaonewaje?
Yaani Kila mahali Kuna cheker.
Kama taasisi zote zingekuwa systematic kama necta hii nchi ingekuwa mbali sana.
 
Kuna dogo fulani wa kike alijipendekeza nikamtongoza na akakubali kipindi anakaribia kumaliza mitihani. Ule ukaribu wa mimi na yeye nikagundua kichwani hamna kitu.
Cha kushangaza kabisa akapa div 2! yeye anashangaa amefaulu kwa mtindo gani! na anasema alitumia akili yale mwanzo mwisho!
Mwezi wa 6 mwishoni tumeonana nikamuuliza unaenda advance? akajibu sumu haijaribiwi kwa kuonja. Sikujua ana maana gani maana tulikutana kwenye kituo cha daladala.
 
Wakati huo huo hawasemi shule za private znazonunua mitihan ya Necta kuna mdogo wangu kasoma school moja kubwa sana kanda ya pwan huko alinambia mwenyew pepa walikuwa nalo wanafunzi wote wa fom 4....kwa advance gvt school kufaulu n halali kabisa
 
Private wengi huwa ni vilaza na hununua mitihani sasa mitihani ikidhibitiwa ndo paper hazivuji, pia government kwa advance wako vizuri maana wanaoenda kule tayari wamefaulu na wanaweza kujisomea with little supervision kutoka kwa walimu. Nilisoma government serikalini advance darasa zima lilifaulu na waliofeli zilikuwa four chache sana, na hata sasa nikiangalia Matokeo ya shule yangu mwaka huu wanafunzi wote 500 waliofanya mitihani ya kidato cha sita kuna division 1 na 3 tu.
Hafu sikuhizi wengi wanaoenda private advance ni waliofeli so kutokuwa na ufaulu mzuri ni expected kabisa.
Pia government shule zenye high school Zina walimu wazoefu na wa mda mrefu tofauti na private wanaajiri walimu less qualified na ukichangia mitihani kudhibitiwa wizi ndo kabisa
 
Wakati huo huo hawasemi shule za private znazonunua mitihan ya Necta kuna mdogo wangu kasoma school moja kubwa sana kanda ya pwan huko alinambia mwenyew pepa walikuwa nalo wanafunzi wote wa fom 4....kwa advance gvt school kufaulu n halali kabisa
Yani had shule za marian girl's zilikuwaga zinakuwa na paper mwaka wetu tulipata ma possible kutoka kwao ya mitihani kabisa
 
Pamoja na kuambiwa hayo je ulijaribu kufikiria mwaka huu Kuna nini cha tofauti kilifanyika........

1. Angalia management ya shule zilizofanya Vibaya ukigundua Kuna tofauti jua inaweza kuwa sababu... (Shule za feza)

2. Kama kulikua na mabadiliko katika usimamizi na uandaaji wa mitihani na muda wa ufanyaji wa mitihani hasa practicles hili linaweza kuwa sababu (shule zote za binafs)

3. Shule husika zilipewa usimamizi maalumu hasa baada ya kuhisiwa chochote??? Usimamizi unaweza kuwa kutoka baraza au idara Fulani nyeti.... kama ndio crosscheck.

4. Je kwa shule unayoiongelea lab tech wao (muandaaji wa maabara, chemical na vifaa vingine) anaumakini kiasi gani???

5. Je waliofaulu sana wametokea michepuo gani kwa kulinganisha na miaka mingine.... Kama arts wamekuja juu zaidi basi science Kuna sehemu ilibanwa so shule zilizokua zikibebwa na michepuo ya science lazima zingerudi nyuma.

Ukiyawaza haya na zaidi ya haya basi utapata majibu sahihi ya maswali yako with reference na matokeo ya kidato cha sita 2021.
 
Binafsi niliwahi hisi huenda shule za Serikali zinabebwa sana miaka hii.

2020 mdogo wangu alihitimu kidato cha nne shule ya Serikali na alikuwa ni zero brain kabisa ila cha kushangaza eti kapata division two, ukweli niliumia sana na kujiuliza ni wapi kuna tatizo.
Jamaa una roho ya kwanini!!
Unaumia mdogo wako kufanya vizuri mitihani yake?
 
Nimeongea na msahihishaji mmoj akaniambia nilichokiandika hapo.
Alisema waliwapunguzia alama za ufaulu wa shule binafsi?
Au
Waliwaongezea ufaulu wa shule za serikali?
Au
Walifanya yote yaani kupunguza kwa wengine na kuongeza kwa wengine?
 
Mifumo ya propaganda na ukandamizaji iliyobuniwa na awamu ya 5 bado ipo inafanya kazi,na pia kuna maelekezo (directives) yaliyo tolewa na mwendazake bado yapo live yanafanya kazi,itachukua mda hiyo hali kubadilika.
 
Sidhani shule za serikali zinaxofanya vizuri ziko vizuri hasa hivi unategemea shule kama Tabora boys na Girls na kibaha na Mzumbe wadhindwe kutoa ufaulu mkubwa kitaifa? Kuna shule za serikali hata private wanaziogopa na Sasa hivi wamebuni mbinu ya kutoa scholarship kusomesha vipanga wanaofaulu shule za serikali na kwenda kwao
wengine wanaesomesha bure wakiwa na uhakika watazipaisha shule zao

Pili tatizo la walimu shule nyingi za serikali kimetatuliwa asilimia kubwa Sasa ya walimu wa secondary O level Ni degree holders sio wale wa Diploma ufundishaji vizuri umeongezeka
Wakati private wengine walimu wanaofundisha Ni kidato Cha sita!!
Mwalimu wa kiwango cha diploma kwa sekondari ndio mwalimu. Degree kiuhalisia ni mbwembwe tu hana ualimu kihivyo labda awe alipitia diploma course....!
 
Wakati huo huo hawasemi shule za private znazonunua mitihan ya Necta kuna mdogo wangu kasoma school moja kubwa sana kanda ya pwan huko alinambia mwenyew pepa walikuwa nalo wanafunzi wote wa fom 4....kwa advance gvt school kufaulu n halali kabisa
Wananunua toka wapi? Necta ndio watunzi, publisher na distributors wa hiyo mitihani. Je inatokaje ? Unataka kusema baraza linauza paper????
 
Hicho kitu hakuna,kwa kidato Cha sita hakuna tofauti Kati ya private and government schools. Pia kumbuka shule za serikali ndio huchukua cream. Hivyo usitegemee kuzidiwa ovyo na shule binafsi.
 
Mh. Prof Ndalichako,

1. Kuna taarifa kuwa Serikali imekuwa kwa makusudi ikijitahidi kuziinua shule za Serikali/kata katika mitihani at the detrimwent of shule za binafsi hasa zinazofanya vizuri.

2. Kwa makusudi kabisa inasemekana shule za binafsi zinazofanya vizuri/zenye historia ya kufanya vizuri watahiniwa wanapunguziwa marks ili shule za serikali/Kata zionekane zinafanya vizuri.

3. Najua si rahisi kulikubali kuwa hilo linatendeka, lakini habari za ndani kabisa zinasema ni hivyo. Kumbuka kuwa wasahihishaji wanatoka kwenye jamii tunayokaa hivyo kunawez kukawa na kaukweli ka aina fulani.

4. Vijana kutoka shule binafsi wanalalamika kuwa haiwezekani wakafeli hivyo kama ilivyoonekana kwenye mitihani ya juzi kidato cha sita na wanachelea kuomba remarking/rufani maana hawana imani tena na usahihishaji.

5. Mh. Prof, unalisemeaje hili?

6. Naamini hili kama linafanyika lazima liwe na Baraka za wakubwa na LABDA wewe ukiwa mmoja wapo? (inawezekana pia hujui), lakini common sense inaniongoza kufikiri kuwa haliwezi kufanyika bila wewe kujua.

KWA NIA NJEMA NALILETA KWAKO
Walishurutishwa na marehemu kufanya hayo mageuzi ili wazazi mkimbilie kupeleka watoto shule za kata
 
Mh. Prof Ndalichako,

1. Kuna taarifa kuwa Serikali imekuwa kwa makusudi ikijitahidi kuziinua shule za Serikali/kata katika mitihani at the detrimwent of shule za binafsi hasa zinazofanya vizuri.

2. Kwa makusudi kabisa inasemekana shule za binafsi zinazofanya vizuri/zenye historia ya kufanya vizuri watahiniwa wanapunguziwa marks ili shule za serikali/Kata zionekane zinafanya vizuri.

3. Najua si rahisi kulikubali kuwa hilo linatendeka, lakini habari za ndani kabisa zinasema ni hivyo. Kumbuka kuwa wasahihishaji wanatoka kwenye jamii tunayokaa hivyo kunawez kukawa na kaukweli ka aina fulani.

4. Vijana kutoka shule binafsi wanalalamika kuwa haiwezekani wakafeli hivyo kama ilivyoonekana kwenye mitihani ya juzi kidato cha sita na wanachelea kuomba remarking/rufani maana hawana imani tena na usahihishaji.

5. Mh. Prof, unalisemeaje hili?

6. Naamini hili kama linafanyika lazima liwe na Baraka za wakubwa na LABDA wewe ukiwa mmoja wapo? (inawezekana pia hujui), lakini common sense inaniongoza kufikiri kuwa haliwezi kufanyika bila wewe kujua.

KWA NIA NJEMA NALILETA KWAKO
Halafu baada ya rufaa wataenda kusahishia nje ya nchi?
 
Back
Top Bottom