Prof. Palamagamba Kabudi: Vikwazo vipate baraka ya Umoja wa Maraifa

Umoja wa Mataifa ndiyo Marekani na Uingeleza sasa unataka wajipelekee mashitaka wenyewe?
 
Vikwazo mlivyowekea upinzani vilijadiliwa na nani? Kiburi hakina macho

Hapo mkuu umenena maneno mazito sijui serikali ya CCM inakumbuka hilo.

Mfano mmoja kati ya mingi ya vikwazo vya CCM kwa upinzani : Maalim Seif akienda Pemba wanamuwekea vikwazo visivyo vya kiungwana bila kuzingatia sheria ya vyama vingi, katiba au baraza la vyama vingi kuafiki. Serikali ya CCM hutoa matamko huku ikikiuka sheria, katiba na vikao halali vilivyoruhusu vyama vingi

 
Prof. kama unaongea Kiswahili basi iwe Kiswahili na sio kuchanganya. Kwani hujui stroke kwa Kiswahili kuwa ni mkwaju?
 
Huyu anashindwa kutofautisha kuwa siasa haina ukomo na uchaguzi ni sehemu ya siasa.
 
Hivi nikishakuwa na PHD itanichukua muda gani kuwa Profesa.

Nimeshaanza QT tayari, Nashukuru ushauri wa mdau mmoja wa JF pale nilipoamua kuisaka PHD na sasa itabidi nilifikilie hili la kuwa Profesa.
 
Hivi kweli kabisa USA akitaka kukuwekea vikwazo kuna mtu wakumzuia pale UN? Kama Urusi mwenyewe tu amewekewa vikwazo na USA pamoja na EU na hakuna aliyeweza kuzuia itakuwa Zimbabwe?.
 
Kuna haja ya kuunda tume kuifanyia uchunguzi mitaala inayotumika kwenye shule zetu, kama tunatumia ile ya mkoloni basi inawezekana kuna vitu wametuficha kuhusiana na elimu ili tuwe na kiwango fulani tu cha ufikiri na wao waendelee kututawala.
 
Marekani na wingereza ndio Umoja wa Mataifa yenyewe huyu mimacho yake sijui yukoje.

Hakuna anayepinga maamuzi ya marekani na wingereza. Hayupo especially dhidi ta nchi hizi maskini ambazo hazina effect yoyote kwenye mipango ya kidunia
 
Matatizo ya Zimbabwe wakulaumiwa ni Wazimbabwe wenyewe pale waliposhindwa kujua tofauti ya malaika na shetani na hata walipokuja kugundua muda ulikuwa ushapita.
 
Hahahaaa hao akina mama na watoto hata hiyo US hawaijui. Huku wanashindia viazi na maharage tu wanamshukuru Mungu. kukiwa hakuna vikwazo haya ndio maisha yao. Hata vikwazo vikiwekwa watu maskini hatuba cha kupoteza.
 
huyu jina lake ni Propesa Pumbavu Kaibuliwa Jalalani.

ndiyo maana!
 
USA aliipiga Iraq, Libya, akaingia Syria kufanya anayoyataka hao UN wameshindwa kumzuia, lakini matokeo yake wanaoteseka na kuumia ni raia wa hizo nchi.

ONYO: KAMA HUNA SABABU ZA MSINGI ZA KUBISHANA NA USA KAA KIMYA KWA MASLAHI YA WANANCHI WAKO
MASIKINI, UJUAJI MWINGI UTAINGIZA WATU WAKO KWENYE SHIDA ZISIZO NA MSINGI.
 
Kwanza baraka hutolewa katika mambo mazuri ya heri, mambo ya kuwekeana vikwazo yanahitaji kulaaniwa na si kubarikiwa.
Imefika wakati matatizo yetu tujaribu kuyatatua wenyewe, hao wazungu hawana urafiki wala huruma na sisi waafrika. Ukiona mzungu anakusaidia ujue anakulia timing ili uwe mwenye kumfanyia kazi kwa maslahi yake.
 
Na ni kinyume na UN charter,nchi moja kuamua kuweka vikwazo nchi nyingine kwa visingizio visivyo na mashiko.
Ikiwezekana nchi wanachama waamue kwa pamoja vikao vya baraza la usalama la UNO view vinahama kila Mwaka ili kukwepa ukiritimba wa nchi moja kuhodhi venue za vikao kunakoweza kupelekea injustices katika maamuzi.
 
Serikali ya CCM inachekesha sana, ikiwa kwenye uwanja wake ni ubabe, kujimwambafai na kunyanyasa kwa kebehi hakuna mfano.
Sasa uwaweke kwenye kona uone wanavyo lia na kulalamika, sijui wanawake na watoto! Sijui wagonjwa!
Wangekuwa na hisia hizo za wanawake na watoto wange wabambika waume za watu na baba za watoto kesi zisizo na kichwa wala miguu pia dhamana?
 
Umoja wa Mataifa ni mali ya Marekani hivyo ikiwa itagundua ukiukwaji wa sheria za kimataifa lazima ikushughulikie bila kupata ushauri kwa ye yote.
Kama ndivyo,Watangazie ulimwengu kuwa waliuadaa kwa nusu karne sasa la sivyo umoja huo hauna maana yeyote ya kuuita umoja wa mataifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…