Uchaguzi 2020 Prof. Rwekaza Sympho Mukandala: Hatma ya CCM 2020 bado haijulikani

Uchaguzi 2020 Prof. Rwekaza Sympho Mukandala: Hatma ya CCM 2020 bado haijulikani

August 9 2020
Zanzibar, Tanzania

Zitto - Mapokezi ya Maalim Seif, Membe huko Zanzibar, Ni ujumbe tosha kwa watawala wa CCM


WaZanzibari watuma salamu kuelekea October 28 2020 kuwa haki ya waZanzibari haipotei. Hivyo wanaenda tena kumchagua kiongozi wao Maalim Seif.
 
August 10 2020
Ikungi, Singida
Tanzania

WAZEE WA IKUNGI SINGIDA, WAONGEA MAZITO WAKATI WA KUMPOKEA TUNDU LISSU
Wazee wazungumzia walivyoporomosha maombi ili Mungu amponye Tundu Lissu akwepe mauti na pia apone majeraha yake ili arudie hali yake ya uzima wa afya na mwili.

Wazee wakaendelea kusema bado mioyoni mwao Tundu Lissu ni mbunge na huyo mbunge aliyepitishwa katika uchaguzi mdogo ni 'mbunge wa viti maalum'

Wazee tayari wamempa Tundu Lissu baraka za kuelekea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Source : CHADEMA MEDIA TV
 
11 August 2020
Kahama, Shinyanga
Tanzania

TUNDU LISSU, APEWA BARAKA ZA KUGOMBEA URAIS



Mgombea Urais Kupitia CHADEMA,Tundu Lissu amekutana na kuzungumza na Wanachama katika Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga.
 
Hali ya kisiasa ilivyokuwa mwezi Juni 2020 wakati wananchi wakimpokea mbunge wao akitokea Dodoma bungeni baada ya Bunge kuvunjwa

27 Juni 2020
Tunduma, Tanzania

Mapokezi ya Frank George Mwakajoka



Source : DSS Tunduma
 
13 August 2020
Musoma, Tanzania

TUNDU LISSU APOKEWA NA UMATI WA WATU



Tundu Lissu ameendelea kutembelea maeneo mbalimbali nchini Tanzania kusalimia na kusaka wadhamini kama sheria ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania inavyotamka mgombea adhaminiwe na waTanzanoa wa sehemu zote mbili za Tanzania yaani Tanganyika na Zanzibar.

Leo hii Tundu Lissu aliingia kwa kishindo mkoani Mara, kaskazini mwa Tanzania kutimiza takwa hilo la kisheria na kulakiwa na mamia ya waTanzania.
Source: CHADEMA MEDIA TV
 
17 Agosti 2020
Mikumi, Morogoro
Tanzania

MHE TUNDU LISSU AINGIA JIMBO LA MIKUMI NA KUPOKELEWA NA UMATI MKUBWA WA WANANCHI


Tundu Lissu akumbusha juu ya nasaha za kauli mbiu ya Mwalimu Nyerere iliyosisitiza utu ni UHURU katika kila kitu yaani Uhuru na Kazi pia Uhuru na Maendeleo na Uhuru na Umoja

Tundu Lissu anauliza kwanini Nyerere hakutanguliza Ma-barabara na Maendeleo au Miundo-mbinu na Maendeleo alijua kwanza utu wa mtu kupitia Uhuru kwanza ndiyo kitu muhimu ili kupata Maendeleo ya Kweli.

Tundu Lissu anasema binadamu siyo mifugo ukaamua kuondoa utu wao wa kuwa HURU kwa kisingizio kuwa kwa kuwanyima uhuru wa utu wao, kuwanyanyasa , kuwabeza ndiyo unataka kuwaletea Maendeleo.
source: CHADEMA MEDIA TV
 
17 Agosti 2020
Morogoro Mjini
Tanzania



Source: CHADEMA MEDIA TV
 
17 Agosti 2020
TUNAJENGA VITU KWA MAENDELEO YA WATU, WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA.



Waziri Mkuu aongea katika mkutano wa viongozi wa dini wa kupongeza juhudi

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amejibu hoja ya baadhi ya wanasiasa wanaobeza Maendeleo ya Vitu Tanzania katika ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa ndege akieleza kuwa serikali hiyo inajenga vitu kwa Maendeleo ya Watu.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awaonya viongozi kumsema Magufuli tu na kubeza, kutengeneza matukio ili kuonewa huruma. Serikali imesema kampeni na uchaguzi utaenda kwa amani na utulivu ili kuimarisha umoja.

Waziri mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa asisitiza watanzania wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura baada ya kusikiliza sera za nani amesema nini katika ahadi zao za kuwaletea maendeleo.
 
16 August 2020
Mwanza, Tanzania

Katibu Mkuu John John Mnyika akizungumza katika Mkutano wa BAVICHA



Katibu Mkuu CHADEMA John Mnyika leo amekutana na Baraza la Vijana BAVICHA wakati wa uzinduzi wa sera mbadala ya vijana wa Tanzania bara na Zanzibar, uzinduzi umefanyikia Mwanza.
Source: Millard Ayo
 
Political scientist Dr. Aikande Kwayu, kuna uoga wa kuchambua siasa na maendeleo hapa Tanzania hivyo kuna ombwe kubwa la taarifa



Dr. Aikande Kwayu, mtanzania ambaye ni mchambuzi wa masuala ya kisiasa hasa katika maeneo mawili ya Sayansi ya Siasa na pia Mahusiano ya Kimataifa (Political Science na International Relations) , Dr. Aikande anasema Siasa inagusa maeneo mengi mfano Siasa katika Makampuni, Siasa za Kimataifa, Siasa ktk Jamii, Siasa ktkn Mgawanyo wa Rasilimali, Siasa za Chama (party politics) n.k hivi karibuni aliyeonekana akihojiwa na chombo cha habari kimataifa cha Al Jazeera.

Hapa nyumbani Tanzania kuna ombwe la uchambuzi hakuna uchambuzi au kusema vitu kuhusu vinavyotokea ndani ya nchi yetu, hivyo historia na mambo yaliyotokea Tanzania yanaandikwa na watu wa nje au kusimuliwa kwa undani na waandishi wa habari kutokea Nairobi, Johannesburg au ktk BBC , VoA, Aljazeera, DW n.k

Jamii ya Tanzania ina haiba tofauti kwa kulazimisha watu wafiche kusema wanachofikiri hasahasa katika kutoa mitazamo yao, inaonesha hakuna walio tayari kutoa mawazo yao kwa kuheshimu tofauti za mitizamo yao na mwisho kukubaliana kutofautiana baada ya kushindanisha hoja. Ukisoma maoni / comments za waTanzania ndani na nje ya nchi kunaonekana mbinyo wa jamii kulazimishwa kukubaliana kwa lazima lakini siyo kwa hoja anamalizia maoni yake Dr. Kwayu.
Source : Global TV online
Asante CHADEMA kwa kuongoza kutoa nafasi waTanzania kuongea kwa uhuru na kushangilia kile wanachokikubali.

Pia asante JamiiForums kwa kutoa uhuru wa hoja kinzani zinyukane hoja kwa hoja kwa afya ya kupanua uwezo wa kutazama mambo kwa mapana zaidi badala ya kushurutishwa kukubaliana na mtizamo finyu usiotoa nafasi kwa jamii kuhoji na kufikiri kwa kina kwa kuwa tu taarifa hiyo au hoja imetolewa na chanzo cha mwenye mamlaka serikalini
 
JAMAA AJITOSA KUMDAI HELA MAGUFULI "ACHIA FEDHA, MAISHA MAGUMU"


27 Nov 2019
Baada ya msafara wa rais Magufuli kusimama Igunga mkoani Tabora alipokuwa akizungumza na wananchi, mmoja amejitokeza na kumtaka rais Magufuli aachie pesa kwasababu maisha magumu... lakini pia rais magufuli amejibu hi
Source : MwanaHALISI TV
 
Magufuli, a bogus prophet who predicted the demise of the opposition parties towards the year 2020 but that has miserably failed to pass...!!!

Now, it's the time for the people to ignore him in the ballot box by choosing his main rival to take over as, throughout his five year tenure, he has been busy tormenting and persecuting his critics at the expense of implementing his party's development programme.
 
CCM muda wao wa kupumzika ushafika, hata ambao huwa hatupigagi kura mwaka huu saa 11 alfajiri kwa foleni..

CCM kwisha habari yao!! Wakikataa kukabidhi nchi inaingia katika ntiani nkubwa!!
 
Washington D.C
Tundu Lissu alivyoacha simulizi mjini Morogoro, watoa ushuhuda


Ujio wa Tundu Lissu ulikuwa na shamrashamra na wananchi wa mkoa na mji wa Morogoro hawajawahi kuwa na furaha na matumaini makubwa kama kuona Tundu Lissu akija kufufua matumaini yao.

Mji wa Morogoro ulikuwa na viwanda vingi vikubwa vilivyotoa ajira rasmi mfano kiwanda kikubwa cha Tumbaku kimekufa na ajira 6,000 rasmi yaani wafanyakazi kupoteza ajira mwaka jana mwishoni.

Viwanda vingine vikubwa vya ngozi, canvas, ceramics, kusindika matunda kwa kutaja kwa uchache vyote vimekufa.
Source: Swahili Villa
 
18 JULAI 2020
Viwanja vya MwembeTogwa
Iringa, Tanzania

AITAKA SERIKALI KUACHA VITISHO UCHAGUZI HUU WA 2020


Tundu Lissu awapa nasaha serikali na wasimamizi wa uchaguzi kuwa hali imebadilika, dunia nzima inaitazama Tanzania hivyo hakuna nafasi watu wasiojulikana wasijulikane.
Source : CHADEMA MEDIA TV
 
Siasa na Utawala
Profesa Rwekaza Sympho Mukandala anazungumzia kigezo muhimu na kikubwa cha siasa na uongozi na kubaki madarakani kwa muda muafaka, Ni je wananchi wanafuraha?

Prof. Mukandala anasema haitoshi baba wa nyumba kuleta nyama, samaki na chakula kila siku nyumbani lakini familia yake inaishi bila furaha. Prof. Mukandala anataka utoe tathmini katika maeneo yao chini baada ya muhadhara wake na kutoa alama/ maksi juu ya utawala wa CCM


  • Kiongozi kuongoza kwa hiyari, kushawishi na siyo kushurutisha
  • Wakati wa janga kubwa kwa nchi, kiongozi kuwa mbele pamoja na wananchi kukabiliana na changamoto hiyo
  • Kukithiri kwa Umasikini wa watu
  • Maendeleo ya Vitu kuleta Umasikini ktk Maendeleo ya Watu
  • Ajira na Viwanda
  • Kilimo Kwanza na Masoko ya Kilimo , Mifugo, Uvuvi
  • Wananchi kukosa kushirikishwa ktk kipi ni kipau-mbele kwao maana serikali haitoi nafasi wananchi kusema
  • Sera za kiuchumi za serikali kukazania Maendeleo ya Vitu na kusahau kabisa Maendeleo ya Watu.
  • Utawala wa sheria
  • Uhuru wa Kujumuika na Kufanya Siasa
  • Kupiga vita rushwa
  • Kushindwa siasa za Ushawishi kubaki Siasa za Kushurutisha
  • Tanzania kuelewa diplomasia ya kujinafasi ki Geopolitics ktk majukumu kikanda / Kimataifa : SADC , EAC , Africa Union , United Nations, WHO, Benki ya Dunia World Bank, Fuko la Fedha IMF
  • Uwezo wa Mwenyekiti wa CCM kuzuia chama kisiwe na mpasuko si tu CCM Tanganyika na hata CCM Zanzibar kuelekea 2020

Kipimo cha kufanya vizuri CCM hakiwezi kupimwa kwa vile serikali yake imeweza kutengeneza miundombinu lukuki na kulazimisha watu waridhike wakati wananchi hawana furaha kutokana na ukata mifukoni mwao. Kipimo halisi ni hayo madokezo hapo juu.


Source :

Kudo's and big up!
Natumaini Jiwe ataperuzi kwene Ukrasa huu na atatafakari kwa kina....!!!!🤣🤣
 
19 August 2020
Mbeya, Tanzania

WaTanzania wapo tayari kufanya maajabu



Source : CHADEMA MEDIA TV
 
19 Agosti 2020
Moshi, Tanzania

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AMTAKA DC SABAYA KUMPA TAARIFA MSAFARA WA LISSU KUSHAMBULIWA



Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, ametoa kauli rasmi ya serikali kuhusiana na vurugu zilizotokea katika mji wa Bomang'ombe wilaya ya Hai wakati mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Tundu Lissu alipofika wilayani humo kutafuta wadhamini.

Katika taarifa hiyo rasmi aliyoitoa leo Agosti 19, 2020, mkuu huyo wa mkoa ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo, amemtaka mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, kumpatia taarifa ya maandishi ya namna alivyoshughulikia suala hilo.
Source : Mwananchi digital
 
Back
Top Bottom