Hana kosa, kajibu aliyoulizwa lakini "unprofessionally" kabisa na kazubaa sana kama zezeta. Ni kama mtu ambae hajaenda shule. Sikutegemea kabisa Profesa awe vile, hafai kabisa, huyo abaki kwenye ukiritimba wa wizarani tu. Asipelekwe hata kufundisha kabisa. Ni bogus kabisa.
Ikiwa maprofesa ndiyo kama huyo, wanafunzi wake watakuwa ni utumbo tu.
Mbona mhasibu wa wizara kajieleza na kajibu vizuri sana, mpaka akawa anawapa somo wazungu.
Wanasheria wetu, karibia wote na profesa mruma ni bogus kabisa. Kwenye English ndiyo wabovu kabisa, kuna huyo lead wao ndiyo alikuwa anasoma kama mtoto wa chekechea, neno moja moja. Ni bogus kabisa, ni aibu hata kusema kuwa ni mwanasheria. Pambaf kabisa.
Kuna wakati team leader kaniushi sana, Madame President wa kikao kaomba watu waende break ya dakika tano, yeye akakataa, ni mpumbavu sana, yeye haelewi kuwa wanapewa break wakajambe, waende haja zao ndogo Kistaarabu, yeye alitaka aambiwe nendeni mkajambe/ Sijuwi jitu la wapi lile lisilokuwa na manners? Yaani mama mtu mzima tena ndiyo rais wa kikao anawaomba mwende break ya dakika tano, unamkatalia! Pambaf kabisa.