Profesa Mkenda, tunaomba utupatie ufafanuzi

Profesa Mkenda, tunaomba utupatie ufafanuzi

Makupa

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
6,822
Reaction score
4,034
Waziri wa Elimu hakika umekuwa unajitahidi sana kutendea haki Wizara unayosimamia na kwa hakika hapa mheshimiwa Rais anastahili kupongezwa kwa kukuona kuwa unafaa kuongoza Wizara hii jeti sana kwa taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Waziri tunaomba dawati la wizara linalosimamia ubora wa elimu kutupia jicho swala la shule binafsi za msingi na haswa za bweni kwenye mambo yafuatayo:

1. Darasa la saba kuanza masomo saa kumi na mbili asubuhi hadi saa tatu usiku.

2. Hawa wanafunzi masomo bado ni watoto wadogo mno na miaka yao ni kati ya miaka 11-13
Tunatambua swala la shule husika kutaka kuhakikisha kuwa wanafunzi husika wanapata alama A kwenye mitihani ya taifa. Hata hivyo, suala la Afya za hawa watoto ni muhimu kuliko kukaririshwa mwaka mzima kwa siku saba za wiki.

Prof toeni mwongozo ili kulinda afya za hawa watoto.Prof je wizara haina mwongozo wa ufundishaji kwa shule za msingi? Ni sahihi mtoto wa miaka kumi na moja kuamka saa kumi usiku ili aweza kuanza masomo saa kumi na mbili hadi saa tatu usiku?
 
Unajua kila mtu anapeleka mtoto Private ili apate matokeo mazuri katika mitihani. Walimu wakitumia mbinu za kiwafanya vihiyo wawe vipanga, tunaanza kulalamika. Si umtoe umpeleke shule ya serikali? Hatujui tunataka nini! No sweet without sweat bwashee
Hivi mkuu,uane mtoto ambae anamshwa saa kumi usiku ili aanze masomo saa kumi na mbili asubui hadi saa tatu usiku kwa siku saba za wiki?

Unadhani hata akipata alama A kwenye mitahani ya darasa la saba wakati tayari hakuwepewa muda mzuri wa kupumzika na kukua wakati sahihi si ni lazima ataathirika kiafya
 
Waziri wa Elimu hakika umekuwa unajitahidi sana kutendea haki Wizara unayosimamia na kwa hakika hapa mheshimiwa Rais anastahili kupongezwa kwa kukuona kuwa unafaa kuongoza Wizara hii jeti sana kwa taifa kwa ujumla...
Hii ya saa kumi nambili kuanza masomo sio shule binafsi tu hata za serikali baadhi ziko hivyo hususani za Dar es salaam. Mwanangu kuna shule anasoma basi kila siku anatoka nyumbani saa kumi na moja kuwa vipindi vya asubuhi.

Kuna lingine ambalo huyu waziri anatakiwa kulijuwa sikuizi fedha za mnazowaingizia mashuleni walimu wameamua kujigawawia na badala yake wazaxi wanachangishwa kila kukicha.

Mfano wilaya ya Temeke kuna mtihani wa darasa la saba wa kata wazazi tumeambiwa tuchangie. Kuna mtiahani wa mock wilaya wazazi tumeambiwa tuchangia hapo sija taja mitihani ambayo kila wiki tunachangia.

Sasa sijui hizi pesa zinazoingizwa mashuleni zinafanya kazi gani?
 
Hii haikubaliki, ni mateso kwa watoto. Elimu haipaswi kuwa mateso.
Wathibiti uboro pale wizarani wamelala tu ,ndio maana hizi shule binafsi zimeamua kuwatumia watoto kwa gharama yoyote ile ili tu shule ziweze kupata daraja la A.
 
Me nafkr ingekua vzr ungetuainishia hapa madhara ambayo wanaweza kuyapata kwa kuamka saa 10 kuanz kusom saa 12 mpk saa3 ili tuelewe athar zake
Mtoto mdogo anatakiwa kupata muda wa kutosha wa kupumzika na kucheza pia ili aweze kukukua vyema. Hivi kweli mtoto ananza masomo saa kumi na mbili hadi saa tatu usiku anapata wapi muda wa kupumzika na kucheza? Je wewe binafsi ulipokuwa shule ya msingi ulisoma kwa pressure kubwa kiasi hiki?
 
Afazali hao wanafunzi wa bweni wanakula then wanaendelea na masomo, shule za kata watoto wanashindishwa njaa kuanzia saa 12 asbh hadi saa 12:30jioni, bila kuonja chochote hasa Geita
 
Back
Top Bottom