Habari wana JF
Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na msemakweli ni mpenzi wa Mungu, Dr. John Pombe Magufuli imekuwa ikijinasibu kuwa na pesa nyingi kutokana makusanyo makubwa ya kodi.
Ushahidi wa hili ni miradi mikubwa iliyoanzishwa na kuendeshwa na serikali, mfano ni ununuzi wa madege kwa pesa taslimu, ujenzi wa SGR, umeme wa Stiglers Gorge, flyovers, daraja Busisi nk.
Kama vyote hivi vinafanyika kwa uwezo wetu, nini kimetokea mpaka wanafunzi wa elimu ya juu wakose mikopo yao?
Waziri Prof. Ndalichako kunukuliwa ukijimwambafai kumiliki kiberiti kilichojaa na uko tayari kukitumia ili kuwadhibiti wanafunzi wasidai haki yao ni fedheha kwako wewe na serikali unayoitumikia!
Picha mnayotupa sisi wananchi huku ni kuwa Serikali yetu imejaa ulaghai, haina pesa imefilisika! Serikali tajiri haiwezi kutishia kiberiti wanafunzi!
Serikali wapeni wanafunzi mikopo yao ili mlinde heshima yenu mnayotuaminisha!