Kila mtu anataka atajirikie hapo rushwa kila konaMamlaka za kibongo zina ukiritimba sana!!??
so vifaranga vimekufa kwa njaa!!?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kila mtu anataka atajirikie hapo rushwa kila konaMamlaka za kibongo zina ukiritimba sana!!??
so vifaranga vimekufa kwa njaa!!?
Imetokea awami hii ya watakatifu .ingekuwa kipindi cha mwendazake ungekutwa inatrand mpaka kwa tweeter hukoHii serekali inawatu wa hovyo cjapata kuona
Makaratasi yanasababisha hasara kwa viumbe hai,Roho mbaya haijengi.View attachment 2466447
Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.
Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.
Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.
Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.
Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.
“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.
“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.
Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.
“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.
“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.
Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.
“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.
Umesema kweli Sana!Nchi hii ina wapuuzi wengi sana,ndio maana Proffesa Asad alisema watumishi wengi na viongozi serikalini wana uwezo mdogo sana
Ndio maana hatuendelei, maana wenye uwezo na akili wengi wakipata nafasi wanakimbilia nje,kuanzia wawekezaji, wanasiasa na wasomi,tunabaki na wapumbavu watupu
Wanaofaa kuwa maraisi wazuri na wabunge wamekimbia nchi,wafanyabiashara wakubwa wanawekeza nje,wasomi nao wakipata shavu nje hawarudi.
Ungekuwa mtu akifanya ujinga kama huo anafukuzwa kazi nadhani uwajibikaji ungekuwepovirikuwa vimekaa kiwanjani tu bila msosi.
jana kuamkia mwaka mpya naenda tanesco naawambia kuna tatizo la mita yenu inapiga shoti wananijibu subiri mpaka kesho wapo sikukuu
Wewe!Wavimwage baharini ili samaki nao washerehekee mwaka mpya! [emoji41]
Aliye bora kutoka familia bora yenye kipato.Nafasi moja inagombaniwa na watu 1000. Inatarajiwa atakayepata anawazidi wote Uwezo hivyo mtapata kilicho bora toka kwake. Masikini ya Mungu
Hii ndio cancer ya nchi yetu, inachukua within 7days kwa Botswana 🇧🇼 kupata permit ya uwekezaji, inachukua within 30days kwa Botswana kupata au kupewa majibu ya maombi ya permit ya ukaaji, hayo yote ni ndoto kwetu hapa, issue ya vifaranga hivi ilishakuwemo humu almost 7days ago sio issue ngeni, hapo kuna urasimu mkubwa, watu wana vibali vya kuingiza cheap chicken meat kutoka Brazil nchini, mwekezaji huyu wa ndani inaonekana ni tishio kwao, kama kawaida tutalalama humu na itaisha kama lile la moto kariakoo ,ajali ya ndege ziwaniKesi za namna hii huwa ngumu kwa kuzisikiliza upande mmoja tu. Je baada ya kuomba kibali Wizarani alipata majibu gani? Kama hakupata jibu lolote, hana wa kumlaumu.
Nchi hii uwajibikaji ni zezo!Ungekuwa mtu akifanya ujinga kama huo anafukuzwa kazi nadhani uwajibikaji ungekuwepo
Acha ujinga,hivi vitasisi vya Serikali kuna baadhi ya Watendaji ni wapumbavu sana TRADE BARRIERS hasa Wizara ya Kilimo.Kesi za namna hii huwa ngumu kwa kuzisikiliza upande mmoja tu. Je baada ya kuomba kibali Wizarani alipata majibu gani? Kama hakupata jibu lolote, hana wa kumlaumu.
Unakwenda ofisi yyt unakaa massa 2 hamna huduma, ukihoji wanakuambia usitufundishe kazi! Maccm haya!Ungekuwa mtu akifanya ujinga kama huo anafukuzwa kazi nadhani uwajibikaji ungekuwepo
Haya mambo yasikie kwa jirani tu, yakikukuta utaona kama dunia imekuelemea mkuu. Unapoomba kibali cha shughuli yako ni kama umewaambia una hela za kugawa. Swali, tutalia hivi mpaka lini????????Hii ndio cancer ya nchi yetu, inachukua within 7days kwa Botswana 🇧🇼 kupata permit ya uwekezaji, inachukua within 30days kwa Botswana kupata au kupewa majibu ya maombi ya permit ya ukaaji, hayo yote ni ndoto kwetu hapa, issue ya vifaranga hivi ilishakuwemo humu almost 7days ago sio issue ngeni, hapo kuna urasimu mkubwa, watu wana vibali vya kuingiza cheap chicken meat kutoka Brazil nchini, mwekezaji huyu wa ndani inaonekana ni tishio kwao, kama kawaida tutalalama humu na itaisha kama lile la moto kariakoo ,ajali ya ndege ziwani
Kabisa, hii nchi ina mazingira magumu Sana ya biashara na uwekezaji....tunakwama kila eneoHii nchi ina ujinga mwingi kweli kweli. kufanya biashara hapa lazima uwe master wa kona kona vinginevyo unafilisika.
Unachekesha. Kwa hiyo kwa kutokujibiwa ndio anakosa mtu wa kumlaumu? Au kinyume chake?Kesi za namna hii huwa ngumu kwa kuzisikiliza upande mmoja tu. Je baada ya kuomba kibali Wizarani alipata majibu gani? Kama hakupata jibu lolote, hana wa kumlaumu.