Profesa Shivji na wafanyabiashara kwenye siasa nadhani hajavuta kumbukumbu zake vizuri

Unaweza kuwapa nafuu ya gharama za biashara zao lakini angalia masuala kwa upana wake. Mfanyabiashara anaingiza uzoefu wake kibiashara kwa maoni mapana na uzoefu wake.
Tusitazame kutazama kwake maslahi yake tutazame uhusika wake wa masuala nyeti na mtazamo wake wa kiutendaji.

Nimetoa mfano wa Erick Hamisi wa TPA jinsi anavyowahusisha wafanyabiashara kama wadau wake wa karibu namna anavyopokea maoni yao ya kikazi badala ya kuwaona kama maadui wenye kutakiwa kumnyenyekea yeye kama bosi anayepita tu kama upepo upitao.

Upeo wa Mohamed Dewji huwezi kuulinganisha na ule wa mbunge fulani wa kawaida tu asiye na uzoefu wala ushawishi mkubwa wa kimataifa hata kama anayo maslahi yake ya kibiashara.a
 
Wewe inavyoonesha ni mtumwa wa fikra na ubwanyenye
 
hata mm sijamwelewa naona kahama mada kabisa yaani katuondoa kwenye mstari.
 
Jitahidi kurudia kusoma ulichoandika ndipo utume jumbe zako
 
Huyu Prof.anaishi Kwa fikra za kizamani Sana, NI wale wanaoamini kuwa mtumishi wa UMMA lazima awe maskini ,ndio kigezo cha uzalenfo!
 
Unyerere ndio urithi mbovu kuwahi kutokea. Siku urithi huu ukitoka kwa vichwa vya watanzanja itaja kuwa nchi bora sana
 
Kama zile nafasi za kuteua wabunge bado zipo, amteue Karamagi na kumpa nafasi kwenye cabinet.

Atamsaidia sana kwenye masuala ya nishati.
 
Wafanyabiashara watapoozesha kasi ya ujenzi wa bwawa la Nyerere ili waweze kuikodisha majenereta serikali na wao kulipwa capacity charges.
Si hilo tu, zimeanza kupigwa chapuo za kuibinafsisha TANESCO.
 
Si hilo tu, zimeanza kupigwa chapuo za kuibinafsisha TANESCO.

..binafsi napinga ubinafsishaji wa Tanesco.

..lakini kwa upande mwingine performance mbaya ya waliokabidhiwa kuendesha Tanesco ndio inayowapa kauli wanaotaka kuibinafsisha.

..Tumebadili Maraisi, mawaziri wa nishati, ma-dg wa shirika, lakini matatizo ya Tanesco yako palepale. Wote wameshindwa kui-fix Tanesco.

..Binafsi sina amani [ peace of mind ] na management na bodi iliyoletwa Tanesco.
 

..Nadhani tatizo ni rekodi za walioteuliwa huko Tanesco.

..Wangeteuliwa watu wapya, wenye sifa nzuri machoni mwa jamii, kusingekuwa na lawama unazozisikia.

..Nadhani wengi waliopinga hawataki kuona wateule wa awamu ya 4 wakirudishwa ktk utumishi kwani Magufuli aliwaondoa kwasababu ya ku-underperfom na maadili mabaya.

..Rais SSH alitakiwa kuibua watu wapya, wasafi, na mahiri, kutoka sekta binafsi na kuwaingiza kimkakati ktk mashirika ya umma.
 
Hao aliowaleta JPM na wao wakawa ni wapigaji kwa namna moja au nyingine. Tatizo hakuna msafi hata mmoja. Wanapoteuliwa kwa mara ya kwanza wananukia harufu ya usafi wakishakaa miezi sita au mwaka wanakuwa wamejifunza wizi na ufisadi.
 
Uelewa shida "Mgongano wa Kimaslahi"
 
Kongole kwa kutoa elimu fupi lakini yenye kueleweka
 
Mkuu ukikiweka kila kitu ndani ya uzi utatumia siku nzima na bado hutamaliza. Kumbuka kuchukuwa muhtasari tu kila unaposoma.

Prof Shivji ni mjamaa kama wajamaa wengine wote. Ni mtu mwenye kutilia shaka ile hulka ya kuwaamini wafanyabiashara.
Issue hapa ni neno dogo lakini linahitaji uelewaaaaaa

Sio paragraph baada ya paragraph za kutokuelewaaa unacho andika ni nini.
 
Issue hapa ni neno dogo lakini linahitaji uelewaaaaaa

Sio paragraph baada ya paragraph za kutokuelewaaa unacho andika ni nini.
Hizo paragraph zina maana kwa wenye uelewa mpana kuliko wewe. Mtihani ni ule ule na wote wanafundishwa na mwalimu mmoja, mmoja anapata alama tisini na mwingine arobaini.
 
Kama zile nafasi za kuteua wabunge bado zipo, amteue Karamagi na kumpa nafasi kwenye cabinet.

Atamsaidia sana kwenye masuala ya nishati.

Mh Karamagi nilimsahau naye atasaidia kutoa ushauri mzuri sana kama ule wa kubinafsishwa ticts. Nchi hii ina hazina kubwa ya viongozi wanao wajali wananchi wake. Waheshimiwa washindwe wenyewe kuwatumia kuwapa ushauri. Jaribu kufikiria mfanyabiashara Singasinga Habindra alivyotoa ushauri mzuri kuhusu fedha za Escrow. Uchumi usipopaa itakuwa ni kujitakia wenyewe.
 
Profresa Shivji ni mnafiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…