TANZIA Professor James Shaba afariki dunia. Alifanyia postmortem mwili wa Hayati Sokoine

Usisukumie uzalendo kwa wenzio, nawe unakula popcorn ukitazama show!

Tuonyeshe nawe uzalendo wako,
Umefanya nini so far ku advocate kile unachoongea humu!
Inaelekea wewe "mzalendo" wa JF tu!, zaidi ya hapo huna kitu cha kuonyesha kama mfano.
Nionyeshe ni wapi nilipodai uzalendo kama siyo kupungukiwa na akili.

Sihitaji kukuonyesha wewe nilichofanya kwa sababu sijadai kuwa nimefanya; hata kama kila siku ninafanya mchango wangu upande huo.
Kama ni kuwa "mzalendo" wa JF, hilo ni bora zaidi ya wewe unayedanganya watu humu kuwa umefanya kitu kumbe ni majigambo yasiyokuwa na msingi wowote.
 
Hopeless.
Haisaidii chochote, bali kuonyesha upumbavu tu unaokusumbua kila mara tunapokutana humu.
You have lost your privileges of engaging me directly.

Nakupeleka ignore list tusikutane tena.

Uniondolee shombo.

Kuanzia hapa sitaona post yako yoyote.

Itasaidia JF kuiondolea migongano ya kijinga.
 
 
Alipokuwa akilewa alitaka kutoa siri ya kifo cha sokoine, risasi kwenye paji la uso, wanakitengo wakahamishia maisha yake USA

..msipotoshe.

..Sokoine angekuwa kadungwa risasi mwili wake usingeguswa na Daktari yeyote.

..Na mwili wa Sokoine ulilazwa Karimjee Hall na wananchi walipewa fursa ya kumuona na kutoa heshima zao.

..ukiacha hilo, familia, watoto wa kiume wa Sokoine, walimfanyia Mzee wao Mila za Kimaasai kabla ya kumzika.

..Na mila hizo zinahusisha kumpaka marehemu mafuta yanayotoka ktk kidari cha ng'ombe dume.

..Madai kwamba Sokoine aliuwawa sio ya kweli, bali ni story za kijiweni za Watanzania.

..Prof.Shaba hakuhamishiwa Marekani na watu wa usalama. Alikwenda huko kuishi na wanawe baada ya kustaafu miaka ya mwisho ya 90.

..Watoto wote wa Prof walikuwa wakiishi Marekani.
 
African respect for the dead, speak only the good deeds of the dead!. Kumsema vibaya marehemu is equal to the consecration of the dead!.
P
Kumsema vibaya marehemu ni consecration of the dead ? Labda ulitaka kusema desecration of the dead.
"consecration is the act of dedicating something to God, sanctifying it and making it holy"

Anyhow, Waafrika hatuongelei marehemu vibaya ? Ukifa yamekwisha? Tunaanza kudanganyana kuhusu historia yako ? hahahahahaaaaaaa......

that explains why
1/ we have no recorded history
2/ we don't learn from mistakes
3/ we are stuck in the third world stench

Dr Shabba, to all who knew him, is remembered for wanton drunkness more than anything else
 
Nimepitia bandiko kuhusu Prof Shaba , nitajadili hoja chache

1. Kwamba Umri wa Prof.
Niwakumbushe Prof alioa mwaka 1963. Mtoto wake Hamish alifariki Marekani mwaka 2001 akiwa na umri wa miaka 36. Leo mtoto huyo angekuwa na miaka 58 takribani 60 ambao ni umri wa kustaafu. Wastaafu wa Tanzania tunawaita Wazee seuse Mzee Prof Shaba.

2. Kwamba alikata kinywaji kikali. Ni kweli lakini kinywaji kikali kinategemea lishe pia. Ukinywa gongo halafu ukaamkia mihogo na kushindia kauzu na karanga mustakabali wako si mwema.
Pombe kali si tatizo, bali unatumia vipi na unajitunza vipi.

3. Kwamba kwanini alikwenda Marekani, hakuacha alama katika utumishi wake.
Prof Shaba ni mmoja wa Wasomi wakubwa Barani Africa. Tukiangali kwa haraka, kundi lake ni la akina Prof Mathew Luhanga, Prof Msuya wa Bicohemistry, Prof Makene , akina Prof Mmari, Prof Sarungi n.k.

Prof Shaba ni mhadhairi 'pioneer' wa Faculty of Medicine (University of Dar es Salaam) miaka ya 70 hadi ilipokuwa college (MUCHS) na kuwa MUHAS ya sasa

Watu waliopitia Medicine katika mikono ya Prof Shaba ni maelfu na Universities za Medicine zinafundishwa na Wanafunzi na vijukuuWanafunzi waliopita mikono ya Prof Shaba.

Ndiyo maana leo Taifa linazizima. Prof Shaba ni moja ya Wahadhiri walioipaisha University of Dar es Salaam

Alama aliyoacha Prof Shaba hutaiona katika majengo, madaraja kama la Mfugale au viwanja vya Mpira.

Prof Shaba ameacha alama katika fikra za watu , alama itakaoishi milele kwasababu kila mwanafunzi ni zao lake.

Prof Shaba alikuwa mtu mzuri sana, alipenda sana Wanafunzi tena akisimama nao wanapoonewa.

4. Kwanini alikwenda Marekani! Ala! mtu ana watoto wake kwanini asiende kuishi mahali anapotaka

Yeyey alisomesha wakwakwe nao wakamlea Baba yao, tatizo lipo wapi.

Alikula pensheni ya kazi zake kupitia watoto wake. Prof Shaba hakutegemea hizi pensheni za ''Wenza' !

Ahsante ! ahsante , ahsante na Pumzikwa kwa Amani Prof J. Shaba.
 
Poor you!
Una tatizo linakusumbua, linaweza kuwa phsycological.
Hunifahamu wala sikufahamu, hivyo nijigambe ili iwe nini haswa!

Mambo niliyoweka hapa pengine wewe bado hujazaliwa na kama ulikuwa umezaliwa basi ni kinda usiyeweza ku comprehend matatizo ya wakati huo.
Nashukuru kwa member aliye post kuwa kuna kitu amejifunza kutokana na andiko langu, na kuwa limemsaidia kwenye research yake.
Asante mzee wangu , kuna kitu umenipa katika research yangu na ripoti yangu kuhusu jambo fulani huku Afya .

May God bless you

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app

Nikutonye tu kuwa, watu tunafahamu mengi mengi zaidi ambayo hatuthubutu kuyaweka hadharani kwa mustakabali wa nchi hii na vile vile usalama binafsi.
Tuna vifua!

Dr Shaba musimwone kuwa alikuwa mjinga kukaa kimya na kuongea only in parables.

Unapoanza kwenda personal on historical facts ambazo wengine wameziishi, tatizo liko kwako.
Ni sawa na kuanza ubishani na mtoto ambaye hata meno hayajaota.
 
Nakubaliana nawe kabisa, na ukweli ni kwamba mtu aliyeleta Cholera kutoka Asia alitokea Pakistan na alifia Rufiji.
Kuanzia hapo ugonjwa ukaanza kusambaa kwasababu hakukuwa na namna ya kudhibiti kuanzia alipolazwa , alipofariki, mazisihi, mikusanyiko n.k.

Ni kweli pia kwamba Madaktari na wataalam wa Afya hawakuwa na experience ukiacha kusoma kwahiyo ilichukua muda kidogo kuweza kuukabili hasa kutokana na hofu kwa watumishi wa afya ambao nao walikuwa waathirika.
Hakukuwa na Isolation centers kama tunazoona , wagonjwa walichanganywa.

Ninachosema hapa ni kuhusu masahihisho ya variants za cholera.
Pili, ile dhana kwamba kuosha maiti ndio tatizo pekee! hapana ni sehemu ya tatizo lakini si pekee

Juzi mwezi huu wa 12 kuna cholera Kagera, je, nako vipi ikiwa ni tatizo ni hilo ulilosema ?

Hoja yangu ni kwamba ikiwa tutaaminisha watu kuosha maiti ndio njia pekee tutawapotosha. Cholera ni virulent bacteria na fatality rate yake si nzuri hasa katika remote areas. . Ni communicable na waterborne disease.

Inaenezwa na hali ya uchafu, uhaba wa maji , matayarisho duni ya vyakula hasa mitaani na migahawani na yes kula kinyesi au matapishi. Nzi akihamisha wadudu ukaugua tayari umekula kinyesi au matapishi

Kuna ushahidi standard ya maisha na elimu vina matter. Tazama inatokea maeneo gani!

Habari njema, ni ugonjwa unaotibika.
 
He

Prof Shaba, alikuwa mtu muungwana mno. Hakuwahi kuwa na majivuno ya aina yoyote, a very simple man, mpenda utani na always kicheko kipo mdomoni mwake. Pia alikuwa Mwalimu mzuri sana katika fani yake. Alikuwa na marafiki wa cadre zote hasa wahudumu ambao alipenda kutaniana nao. Nakumbuka ofisi yake pale Central Pathology Laboratory (Histology) alikuwa hakosi wageni wa kwenda kumsalimia na kupata matibabu.

Tuliwahi kumuuliza kama haogopi cancer ya mapafu kutokana na uvutaji mwingi wa sigara akajibu kwani nikifa kwa malaria mapafu yangu yatakuwa na kazi gani?


Pumzika kwa amani Profesa James Shaba, Nguli wa Pathology.
 
Pombe haina madhara wewe kama inakutana na chakula cha maana tumboni haina madhara kabsa
 
Thats the Prof Shaba I know, kwa mara ya kwanza tulionana katika mazingira nimeeleza huko nyuma, tukawa na maongezi mazuri sana yaliyofanya nisimsahau, he left me a good impression.
 
Mwananzengo, mazee alikuwa sharp!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…