Project funding sources

Project funding sources

sijui hata nichangie nini , am speechless. ila hongora sana ndugu kwa ujasisri uliotukuka.
kila nikusoma naona umedhamiria haswa na speed ni 120. swali kidogo UTAKUWEPO KWENYE CHAI DAY?

Hakuna garantii ya mafanikio ikiwa utathubutu na kujaribu; ila kuna uhakika wa kukosa mafanikio endapo HAUTAJARIBU. -Clinton.
 
Mkuu MZUZU; utakuwepo kwenye CHAI DAY - 5 Feb 11 - Lunch Time Hotel, utakuwa ni wakati mzuri kwa wadau kubadilishana mawazo.
 
Asante kwa elimu... 😛opcorn:...I hope you have leagal protection of ur ideas..!
 
Du! inaoneka hii si sanda yakawaida inatengenezwa nakutiwa manukato yakila aina tokea Sept. 2009 mpaka leo. Atakaevishwa au kuivaa kwanza nikaburini baadae nipeponi au motoni .... aisee babangu
 
Mkuu mzuzu hivi tani moja ya mihogo mnanunua kwa bei gani? Maana nami nimehamasika sana kuingia kulima zao hili kwa imani ya kupata soko kutoka kwenu.
Gudtymes mkuu.
 
Kwa sasa bado hatujapanga bei ila tuna bei ya matazamio tu ila tutaweza kuwa firm Mara tu tutakapoanza kuzalisha. But tutakuwa na bei nzuri na tutalipa kwa dola ili kuhakikisha stability inakuwepo kwa wakulima watakaopata resources kwa mikopo ili waweze kupeoject matazamio yao

Thanx mkuu. Nadhani mpaka mwaka ujao mtakuwa tayari mmeanza rasmi.
Kwa taarifa nilizopata kilimo cha kitaalamu, hekta moja inazalisha hadi tani thelathini.
Nimepata shamba eneo fulani hapo pwani. Mkuu usichoke kutujuza maendeleo.
Thanx
 
Yah tunatazamia kuanza ujenzi soon doc za permits ndio zimechelewa sana. Kwenye maonyesho ya cassava week iliyopita walionyesha mbegu mpya ambayo inaweza kutoa hadi tani 40 kwa hekta na inakubali kwa ukanda wote wa Pwani. Nafikiri tutaitumia sana kwa hii project naona itasaidia watu wengi sana

Mzuzu. Mkuu nime Kupm hebu tuzungumze kidogo.
 
du!hongereni sana nimependa michango yenu. hivi kuna zile hele za mizengwe za serikali mamilioni ya fulani ziliamishiwa ofisi ya waziri mkuu inakuwaje?
japo serikali haipo hivyo nikisumbua mtu wangu tafuta mtu mshare naye kwa kumpa share kidogo not more than 25% mtaji mwingine atakaochangia utakuwa kama mkopo wenye riba nafuu na awe tayari kukubali kuwa wewe ndiye mwendeshaji wa mradi.
na nivizuri mkataba usiwe wa kudumu sana ikiwezekana kila baada ya miaka mitatu mnaangalia upya.ili msigombane waswahili partnership bado inatusumbua hivyo kwa kuanzia bora iwe hivyo
 
Tunaelekea hatua za mwisho kabisa mkuu, mazingira ya uwekezaji ya nchi yetu magumu sana sir, inabidi uwe na kichwa ngumu na mbishi ndio unaweza kusonga mbele hasa kwa watu maskini ambao hawajulikani kwenye cycles za waliopo madarakani but tunasonga mbele taratibu..Hopefully in few weeks tutaanza rasmi kuwekeza sasa baada ya kumaliza documentations muhimu zilizochukua muda mrefu sana, almost miaka 3 sasa

Kwa kuwa hukukata tamaa mwanzoni,naamini utamaliza kipande kilichobaki mbele yako.
 
Nimeisoma hii thread mwanzo hadi mwisho. Hongera sana Mkuu Mzuzu.
Umenishtua sana kwamba umetumia almost 3 yrs kupata documentation za ku-implent mradi, na bila shaka ni kwa sababu ya Ukiritimba tu uliopo na uliozoeleka humo Serikalini!!!, Damn.
Mkuu endelea kutujuza, ili nasi tujipange tulime muhogo
 
Heshima mbele wana JF,

Nimekuwa nahangaikia kupata habari au msaada wa mawazo kutoka sehemu mbalimbali nafikiri na hapa jamvini lazima kuna msaada mkubwa wa mchango naweza kupata kwani naamini hapa ni kitovu cha taaluma na ujuzi wa mambo.

Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikifikiria na kutafuta njia mablimbali za kuweza kufanya sisi kama vijana wa kitanzania katika mambo ya kiuchumi (nikimaanisha kuwa na biashara kubwa) tunazoweza kuanzisha vijana na kutufanya kuondokana na mawazo ya kuajiriwa hasa kwa vijana wenye elimu ya chuo kikuu. Lakini ninasikitika sana kuona watanzania wengi tunagombea nafasi za kuajiriwa tu na serikali yetu haina msaada wowote wa kuwezesha kuleta mafanikio. Serikali yetu inatafafsiri ujasiriamali ni kumwezesha mtu kupata rizki, mi naamini bila viwanda vidogo vya kati huo ujasiriamali hautakuwa na manufaa yoyote, wazalishaji wanatakiwa wajue soko na processing ikifanyika thamani ya mazao yao inaongezeka kwenye masoko ya kimataifa.

Kwa mtazamo wangu nimekuwa nikiamini watu wenye elimu ya chuo kikuu wanatakiwa kuwa na mtazamo wa kuanzisha ajira kwani wao wamepevuka upeo tofauti na waliokosa elimu hiyo.

Kwa wanaJF wanaojua jinsi ya kupata resources jamani ninaomba msaada wa mawazo.

Nimefanya feasibility study kwa miaka kadhaa sasa na hatimaye nimeaandaa business plan ya kufanya processing ya cassava (mihogo) kutengeneza starch. Mali ghafi hakuna asiyejua inapatikana nchi kwetu popote pale unahitaji kuwahakikishia wakulima soko tu na watakufanyia mambo ya kutosha. Hii itainua uchumi wa wakulima wadogo sana na hasa kwenye maeneo ambayo kilimo cha pamba kimeanguka na mikoa kame kama ya kati isiyo na zao la biashara kwani popote inastawi

Soko lipo juu sana na lengo ku export tayari kuna watu wanahitaji sana kuimport kutoka Tanzania nimejaribu kutangaza na kupata response nzuri sana. Kuna soko kubwa sana nchini (yote inaagizwa toka nje esp SA) kuna soko kubwa sana pale TBL na viwanda vingine vinavyotengeneza madawa, nguo, bia, tambi, biscuits, noodles, almost viwanda vyote vinavyotengeneza vyakula (canned na bottled) vinahitaji starch.

Tatizo kubwa nililonalo ni kwamba natafuta source ya funds kuanzisha kamradi haka ambacho profit margin yake ipo juu sana. Nipo tayari kwa mazungumzo specific ya jinsi ya kufanya ili mradi niweze kutimiza hii ndoto. Mradi huu unaweza kuwa expanded katika muda wa miaka 2 au 3 ukawa na plant nyingine ya kuzalisha ethanol kwa kutumia waste materials baada ya kuprocess cassava na tayari nimeanza kudraft plan yake. Nimejaribu kupita Tanzania investment bank na kuongea nao wakawa na interest ya kusaidia ila nikawa sina colateral wala mdhamini mwenye assets nzuri (mimi mtoto wa mkulima tu hata elimu yangu ni ya kuungaunga tu) ninaweza kuraise kidogo tu. Nimepita na NBC ikawa vilevile tu na mradi unakubalika na tatizo siaminiki tu kwa vile sina historia ya kushika pesa kubwa.

Ninaweza kusimamia hii kazi na ikawa juu kiasi cha kuridhisha na kushindana na biashara kubwa tu hata kuanzisha zingine safi zaidi.

Haya wadau naomba reference kwenye source au tujiunege na kuona nini cha kufanya. Nipo kwa wazi nasikiliza mawazo yenu na ushauri! unaweza kuchangia au kuniPM vyovyote utakavyoona

Ahsanteni sana

Project yako ni nzuri sana, nilipata sikia kuwa kuna wamarekani wanataka kujenga kiwanda cha aina hiyo kule Bungu, Rufiji. http://scheerfoundation.info/sites/default/files/The FJS African Starch Company.pdf hii pia itakua ukombozi kwa watu wa pwani ambao ni maskini wa kutupwa. Mimi pamoja na wenzangu tuna shamba ekari 100 kule rufifi tun aweza kiwa supplier wazuri wa mihogo kwako. kama hutajali hebu tuma business plan yako hapa, then tuwasiliane joemi.investment@gmail.com
 
Kila la kheri kaka, utafanikiwa tu naamin hapa jamvini kuna wengi wenye upeo na uthubutu. Binafsi nimefurahishwa sana na mtazamo wako
 
Tunaelekea hatua za mwisho kabisa mkuu, mazingira ya uwekezaji ya nchi yetu magumu sana sir, inabidi uwe na kichwa ngumu na mbishi ndio unaweza kusonga mbele hasa kwa watu maskini ambao hawajulikani kwenye cycles za waliopo madarakani but tunasonga mbele taratibu..Hopefully in few weeks tutaanza rasmi kuwekeza sasa baada ya kumaliza documentations muhimu zilizochukua muda mrefu sana, almost miaka 3 sasa


Ahsante sana Mkuu Mzuzu, nilianza kupata shaka kidogo juu ya huo mradi baada ya kuona ukimya, sasa nimefarijika, nitafanya kila linalowezekana kupata kipande cha ardhi mitaa hiyo ili niwe mdau muhimu kwako. Nakutakia kila la kheri.
 
Mkuu naomba uniweke kwenye ratiba yako nina resource za kutosha.
 
Naomba mapendekezo mkuu tufanyeje? Nataka kuoutsource sehemu kubwa ya kilimo nibaki na processing
Kwa kuwa una mashamba ya kutosha ingekuwa vizuri na wewe ubakie na sehemu ya mashamba ili kujipa uhakika wa production Kwa kuwa unaanza.Nina uzoefu wa kilimo cha muwa pale Bonde la Kilombero, Kuna mashamba ya Kampuni na ya watu binafsi, watu binafsi wanapata soft loans za kuweza kuwasupport kwenye mahitaji muhimu kama kupalilia na mbolea, lakini pia mashamba hayo tunakodi toka kwa wenyeji, ukibahatika kidogo kidogo unanunua toka kwa wenyeji, lakini sio haba inalipa.
 
Mawazo mazuri Mzuzu. Ngoja na mi nijipange, nitawajoin b'dae. Kila la heri.
 
Last edited by a moderator:
mkuu .... kwanza unatakiwa kutayarisha shamba darasa kwa ajili ya piloting .... andaa heka 50 zilimwe kitaalam halafu hapo ndipo gharama halisi za zao hilo la muhogo either in tons or else zitajulikana ... hapo itakuwa mwanzo wa ku-set buying price ex. works shambani

kama itaonekana gharama zitakuwa accommodated from your buying price with profit margin wadau wengi watakuwa interested

thanks
 
Back
Top Bottom