Project funding sources

sijui hata nichangie nini , am speechless. ila hongora sana ndugu kwa ujasisri uliotukuka.
kila nikusoma naona umedhamiria haswa na speed ni 120. swali kidogo UTAKUWEPO KWENYE CHAI DAY?

Hakuna garantii ya mafanikio ikiwa utathubutu na kujaribu; ila kuna uhakika wa kukosa mafanikio endapo HAUTAJARIBU. -Clinton.
 
Mkuu MZUZU; utakuwepo kwenye CHAI DAY - 5 Feb 11 - Lunch Time Hotel, utakuwa ni wakati mzuri kwa wadau kubadilishana mawazo.
 
Asante kwa elimu... 😛opcorn:...I hope you have leagal protection of ur ideas..!
 
Du! inaoneka hii si sanda yakawaida inatengenezwa nakutiwa manukato yakila aina tokea Sept. 2009 mpaka leo. Atakaevishwa au kuivaa kwanza nikaburini baadae nipeponi au motoni .... aisee babangu
 
Mkuu mzuzu hivi tani moja ya mihogo mnanunua kwa bei gani? Maana nami nimehamasika sana kuingia kulima zao hili kwa imani ya kupata soko kutoka kwenu.
Gudtymes mkuu.
 

Thanx mkuu. Nadhani mpaka mwaka ujao mtakuwa tayari mmeanza rasmi.
Kwa taarifa nilizopata kilimo cha kitaalamu, hekta moja inazalisha hadi tani thelathini.
Nimepata shamba eneo fulani hapo pwani. Mkuu usichoke kutujuza maendeleo.
Thanx
 
Jamani nimependa hii kitu
Japo nina mawazo tofauti ya kimradi
Napenda kilimo lakini najiandaa na kilimo cha mbogamboga
 

Mzuzu. Mkuu nime Kupm hebu tuzungumze kidogo.
 
du!hongereni sana nimependa michango yenu. hivi kuna zile hele za mizengwe za serikali mamilioni ya fulani ziliamishiwa ofisi ya waziri mkuu inakuwaje?
japo serikali haipo hivyo nikisumbua mtu wangu tafuta mtu mshare naye kwa kumpa share kidogo not more than 25% mtaji mwingine atakaochangia utakuwa kama mkopo wenye riba nafuu na awe tayari kukubali kuwa wewe ndiye mwendeshaji wa mradi.
na nivizuri mkataba usiwe wa kudumu sana ikiwezekana kila baada ya miaka mitatu mnaangalia upya.ili msigombane waswahili partnership bado inatusumbua hivyo kwa kuanzia bora iwe hivyo
 

Kwa kuwa hukukata tamaa mwanzoni,naamini utamaliza kipande kilichobaki mbele yako.
 
Nimeisoma hii thread mwanzo hadi mwisho. Hongera sana Mkuu Mzuzu.
Umenishtua sana kwamba umetumia almost 3 yrs kupata documentation za ku-implent mradi, na bila shaka ni kwa sababu ya Ukiritimba tu uliopo na uliozoeleka humo Serikalini!!!, Damn.
Mkuu endelea kutujuza, ili nasi tujipange tulime muhogo
 

Project yako ni nzuri sana, nilipata sikia kuwa kuna wamarekani wanataka kujenga kiwanda cha aina hiyo kule Bungu, Rufiji. http://scheerfoundation.info/sites/default/files/The FJS African Starch Company.pdf hii pia itakua ukombozi kwa watu wa pwani ambao ni maskini wa kutupwa. Mimi pamoja na wenzangu tuna shamba ekari 100 kule rufifi tun aweza kiwa supplier wazuri wa mihogo kwako. kama hutajali hebu tuma business plan yako hapa, then tuwasiliane joemi.investment@gmail.com
 
Kila la kheri kaka, utafanikiwa tu naamin hapa jamvini kuna wengi wenye upeo na uthubutu. Binafsi nimefurahishwa sana na mtazamo wako
 


Ahsante sana Mkuu Mzuzu, nilianza kupata shaka kidogo juu ya huo mradi baada ya kuona ukimya, sasa nimefarijika, nitafanya kila linalowezekana kupata kipande cha ardhi mitaa hiyo ili niwe mdau muhimu kwako. Nakutakia kila la kheri.
 
Mkuu naomba uniweke kwenye ratiba yako nina resource za kutosha.
 
Naomba mapendekezo mkuu tufanyeje? Nataka kuoutsource sehemu kubwa ya kilimo nibaki na processing
Kwa kuwa una mashamba ya kutosha ingekuwa vizuri na wewe ubakie na sehemu ya mashamba ili kujipa uhakika wa production Kwa kuwa unaanza.Nina uzoefu wa kilimo cha muwa pale Bonde la Kilombero, Kuna mashamba ya Kampuni na ya watu binafsi, watu binafsi wanapata soft loans za kuweza kuwasupport kwenye mahitaji muhimu kama kupalilia na mbolea, lakini pia mashamba hayo tunakodi toka kwa wenyeji, ukibahatika kidogo kidogo unanunua toka kwa wenyeji, lakini sio haba inalipa.
 
Mawazo mazuri Mzuzu. Ngoja na mi nijipange, nitawajoin b'dae. Kila la heri.
 
Last edited by a moderator:
mkuu .... kwanza unatakiwa kutayarisha shamba darasa kwa ajili ya piloting .... andaa heka 50 zilimwe kitaalam halafu hapo ndipo gharama halisi za zao hilo la muhogo either in tons or else zitajulikana ... hapo itakuwa mwanzo wa ku-set buying price ex. works shambani

kama itaonekana gharama zitakuwa accommodated from your buying price with profit margin wadau wengi watakuwa interested

thanks
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…