Propaganda za kukuza uwezo wa Rwanda kijeshi zinahatarisha usalama wa nchi yetu hapo baadaye

Propaganda za kukuza uwezo wa Rwanda kijeshi zinahatarisha usalama wa nchi yetu hapo baadaye

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
PROPAGANDA ZA KUKUZA UWEZO WA RWANDA KIJESHI ZINAHATARISHA USALAMA WA NCHI YETU HAPO BAADAYE.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Kuna tabia ambayo imekomaa miongoni mwa watu ya kuisifia, kuitukuza, kuipamba, kuipa uwezo hata usiofaa nchi ya Rwanda katika sekta mbalimbali. Na Leo nitajikita kwenye sekta ya Ulinzi na usalama na hapa tunazungumzia Jeshi na Mbinu za kimedani.

Kwa Sisi Watibeli, Jeshi sio kuwa na watu wengi.
Jeshi sio kuwa na vifaa vya kisasa na vya kiteknolojia.
Jeshi sio ukubwa wa Miili au maumbile.
Jeshi sio kuwa na uchumi Mkubwa.

Jeshi ni zaidi ya hayo. Hayo ni Mambo madogo Sana Jeshini na yanatokea Nje ya Mwanajeshi.
Uanajeshi ni lazima uanzie ndani ya mwanajeshi mwenyewe.

Jeshi ni Mtazamo
Jeshi ni Imani
Jeshi ni Nidhamu
Jeshi ni Moyo wa Ujasiri
Hayo yote yapo ndani ya mwanajeshi. Mwanajeshi ili awe Mwanajeshi lazima awe na hayo Kwanza ndipo mafunzo, silaha, Mbinu n.k. ndio apewe.

Kwa namna hiyo Basi, utagundua lengo kubwa la Propaganda ni kuangusha ujasiri, Imani, mtazamo wa Mwanajeshi husika au jeshi husika katika upambanaji.

Kwa Sisi Wasomi wa Bibilia, Moja ya mambo makubwa ambayo yanajitokeza tokeza katika visa vya Biblia ni Propaganda ya kuwapa Waisrael Ujasiri, Imani, na mtazamo Chanya kuwa wao ni Bora kuliko watu wote Duniani.
Kisha ndipo Sheria za Torati zinawekwa ili kuwafanya wawe na Nidhamu.

Zipo Makumi ya aya zinazoeleza kuwa Muisrael Mmoja atakimbiza watu Mia WA mataifa mengine. Hiyo ni propaganda

Kuna kisa kingine ambacho Musa aliagiza Wapelelezi Kumi na mbili Kwenda kuipeleleza Nchi ya Kanaani. Wapelelezi wale Kumi na mbili waliporudisha ripoti. Wapelelezi Kumi wakatoa ripoti Yao kuelezea Jinsi nchi Ile ilivyo na watu wake walivyo Wakubwa na wenye nguvu na hodari. Kwa jinsi walivyokuwa wanaoelezea ni Kwa namna ya kuwakatisha tamaa na kuwatisha waisrael Jambo ambalo ni Kweli Waisrael waliingiwa na Hofu.

Lakini kwa Bahati, wapelelezi Wawili ambao ni Joshua na Kalebu wao wakatoa ripoti Yao inayokinzana na ripoti ya wale wapelelezi kumi. Wao wakasema in a positive ways.
Kusifia nchi wanayoiendea(Lengo Lao), kusifia Jeshi lao na Waisrael kwa ujumla, na mwisho kueleza sifa za maumbile ya adui Zao in a negative ways.
Wakasema, ni kweli wale watu ni Wakubwa Sana, wanamiili Mikubwa Mno na nguvu za Kimwili, lakini mioyoni mwao wanahofu juu yetu. Mambo makubwa tuliyoyafanya kuanzia kwa Farao, bahari ya shamu na kupiga mataifa yote tuliyokutana nayo imewanyong'onyesha Sana.
Hivyo waisrael na Jeshi la Israel Halina Sababu ya kuogopa watu hao kwani ni ukubwa wa Pua tuu ambao haulingani na wingi wa makamasi.

Ari, ujasiri, imani kwa Waisrael na Jeshi lao ikarejea lakini Musa kama kiongozi wa kijeshi na mwenye hiyo Movement akatoa maamuzi wale wapelelezi kumi wauawe ili wasije waletea Hofu na kuambukiza Hofu hiyo watu wengine.

Muhtasari huo tunajifunza mambo mengi lakini kubwa zaidi linaloendana na Mada hii ni nguvu ya propaganda na maneno katika Ulinzi na usalama na wanajeshi wetu.

Jeshi imara linatokana na wananchi imara.

Hawa watu wanaendesha propaganda za kuishusha nchi yetu na kuidunisha hasa kijeshi(kiulinzi na KIUSALAMA), sio tuu wanatukosea Bali wanahatarisha usalama wa nchi kwa wakati ujao.

Kama ikiendelea hivi itajengeka dhana kwenye jamii yetu kuwa Warwanda ni watu hodari kuliko Sisi. Sisi ni Duni mbele ya Warwanda Jambo ambalo ni Uongo lakini likiendelea litafanya mitazamo ya Watanzania kuligeuza Jambo hilo ni KWELI.

Hawahawa wananchi ndio baadaye watajiunga na Jeshi. Yaani watu wenye kujiona Duni na hofu dhidi ya Warwanda ndio watakuwa wanajeshi hata ikitokea vita watakuwa waoga na kushindwa mbele za adui Zao Warwanda.

Nini chakufanya?

1. Kitengo cha Propaganda hasa za kijeshi kisilale. Kijiimarishe na kuweka mipango na mikakati kufanya Watanzania waliamini Jeshi Lao.
Kwa sababu Jeshi likianza kutiliwa Mashaka hata ufanisi wake utapungua.
Kwa USA na mataifa mengine tunaona wo vitengo vya propaganda viko kila idea, huko Hollywood kwenye Filamu, kwenye Masuala ya kisayansi, na mambo ya Waandishi wa riwaya na tamthilia.
Kwamba ati Mwanajeshi Mmoja wa kimarekani anaweza kushughulikia maadui Mia moja wa mataifa mengine

2. Kutokana na baadhi ya watu kutokuwa na Akili au kuwa na chuki na nchi. Iundwe Sheria za kuzuia watu kuzungumzia mambo ya kijeshi na kiusalama kwa namna ya kudhalilisha, kumshusha heshima ya jeshi, kukejeli, kushusha morali au kudunisha.
Hii itaepusha na kuzuia wale wapiga propaganda zenye maudhui ya kudunisha Jeshi la nchi.

3. Watu wapewe uwezo wa kutoa maoni Yao lakini yawe maoni ya kujenga sio yenye lengo la kutukuza taifa jingine kuliko taifa kwa namna ya kukejeli taifa letu.

4. Mafunzo ya JKT yaendelee kutolewa kwa wanaomaliza kidato cha sita na kwa wale Wa kidato cha nne ambao wataendelea na vyuo vya Kati.

Ninawahakikishia, Maneno haya yakiendelea hivihivi watu na jamii itayaamini. Na matokeo ya kuyaamini Maneno ya aina hii hayatakuwa mazuri.

Lazima Sisi kama taifa tujitambulishe sio tuu kwa upendo wetu, umoja wetu Bali pia tujitambulishe kama watu wenye AKILI kubwa, na watu wenye kufanya mambo magumu.

Nawatakia maandalizi Mema ya Sabato

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
 
Uwezo wa nchi unapimwa kwa mambo ya msingi.

Nchi ambayo bado inapewa misaada ya matundu ya vyoo na ambayo inapoteza watoto wadogo wenye damu ya kisiasa inayochemka kama akina Soka nakuhakikishia, nchi hiyo ni failure ktk anga zote.

Akili isiyoweza kusolve matatizo ya msingi kama vile maji, matundu ya vyoo, madawati usitegemee inaweza kuwa nzuri kwenye mambo complex kama ya ulinzi ktk geopolitics.
 
Kushinda vita vya kijeshi kunahitaji mchanganyiko wa mambo mengi, na hakuna formula moja rahisi. Hapa kuna baadhi ya mambo muhimu ambayo yanaweza kuchangia ushindi:

## 1. Nguvu ya Kijeshi

  • Wanajeshi: Kuwa na jeshi kubwa lenye askari wengi wenye mafunzo mazuri na vifaa vya kisasa.
  • Vifaa vya Kijeshi: Kumiliki silaha za kisasa, kama vile ndege za kivita, meli za kivita, magari ya kivita, na mifumo ya ulinzi.
  • Teknolojia: Kuwa na teknolojia ya kijeshi ya hali ya juu, kama vile mifumo ya ujasusi, mawasiliano, na silaha za kisasa.

## 2. Mkakati na Uongozi

  • Mkakati: Kuwa na mkakati mzuri wa kijeshi ambao unaeleza jinsi ya kufikia malengo ya vita.
  • Uongozi: Kuwa na viongozi wenye uwezo na uzoefu ambao wanaweza kuongoza jeshi kwa ufanisi.

## 3. Uchumi

  • Rasilimali: Kuwa na rasilimali za kutosha kugharimia vita, kama vile fedha, chakula, mafuta, na vifaa vingine.
  • Uzalishaji: Kuwa na uwezo wa kuzalisha silaha na vifaa vingine vya kijeshi.

## 4. Morali

  • Morali ya Wanajeshi: Wanajeshi kuwa na morali ya juu na imani katika ushindi.
  • Umoja wa Kitaifa: Wananchi kuwa na umoja na kuunga mkono vita.

## 5. Diplomasia

  • Washirika: Kuwa na washirika wa kimataifa ambao wanaweza kusaidia katika vita.
  • Mazungumzo: Kuwa tayari kufanya mazungumzo ya amani ili kumaliza vita.

## 6. Mambo Mengine

  • Hali ya Hewa: Hali ya hewa inaweza kuwa na jukumu katika vita.
  • Jiografia: Jiografia ya eneo la vita inaweza kuwa na jukumu.
  • Bahati: Wakati mwingine, bahati inaweza kuwa na jukumu katika vita.

Ni muhimu kuzingatia kwamba vita ni jambo ngumu na lisilotabirika. Hata kama una mambo yote hapo juu, bado kunaweza kuwa na sababu ambazo zinaweza kusababisha kushindwa.

## Mwisho

Kushinda vita kunahitaji mchanganyiko wa mambo mengi, na hakuna uhakika wa ushindi. Ni muhimu kuzingatia kwamba vita vina madhara makubwa na vinapaswa kuepukwa kwa gharama zote.


Gemini AI
 
Njia rahisi ni modes wa hili jukwaa wafute nyuzi za namna hiyo na nyingine waziunganishe ili kuzima kick na kutrend kwa mambo ya namna hiyo, na wazalendo waandike nyuzi za kupaisha jeshi letu na kulitrendisha sasa wakikaa kimya raia wataamini halina maajabu
 
Njia rahisi ni modes wa hili jukwaa wafute nyuzi za namna hiyo na nyingine waziunganishe ili kuzima kick na kutrend kwa mambo ya namna hiyo, na wazalendo waandike nyuzi za kupaisha jeshi letu na kulitrendisha sasa wakikaa kimya raia wataamini halina maajabu

Acheni kulionea wivu jeshi la Rwanda.
 
Uwezo wa nchi unapimwa kwa mambo ya msingi.

Nchi ambayo bado inapewa misaada ya matundu ya vyoo na ambayo inapoteza watoto wadogo wenye damu ya kisiasa inayochemka kama akina Soka nakuhakikishia, nchi hiyo ni failure ktk anga zote.

Akili isiyoweza kusolve matatizo ya msingi kama vile maji, matundu ya vyoo, madawati usitegemee inaweza kuwa nzuri kwenye mambo complex kama ya ulinzi ktk geopolitics.
Moja ya kosa linalofanywa na wapinzani ni kufikiri wao wakipewa nchi wataongoza watu tofauti na Watanzania waliopo sasa. Ni muhimu kwenye mambo serious yanayogusa future ya nchi yetu hasa mambo ya ulinzi wa nchi, wote tuwe na sauti moja bila kujali wewe ni upinzani au chama tawala. Jeshi ndiyo chombo pekee cha ulinzi wa mipaka ya nchi yetu. Halistahili kubezwa hata kidogo. Kwa hapa East and Central Africa tuna jeshi Imara na bora sana.
 
PROPAGANDA ZA KUKUZA UWEZO WA RWANDA KIJESHI ZINAHATARISHA USALAMA WA NCHI YETU HAPO BAADAYE.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Kuna tabia ambayo imekomaa miongoni mwa watu ya kuisifia, kuitukuza, kuipamba, kuipa uwezo hata usiofaa nchi ya Rwanda katika sekta mbalimbali. Na Leo nitajikita kwenye sekta ya Ulinzi na usalama na hapa tunazungumzia Jeshi na Mbinu za kimedani.

Kwa Sisi Watibeli, Jeshi sio kuwa na watu wengi.
Jeshi sio kuwa na vifaa vya kisasa na vya kiteknolojia.
Jeshi sio ukubwa wa Miili au maumbile.
Jeshi sio kuwa na uchumi Mkubwa.

Jeshi ni zaidi ya hayo. Hayo ni Mambo madogo Sana Jeshini na yanatokea Nje ya Mwanajeshi.
Uanajeshi ni lazima uanzie ndani ya mwanajeshi mwenyewe.

Jeshi ni Mtazamo
Jeshi ni Imani
Jeshi ni Nidhamu
Jeshi ni Moyo wa Ujasiri
Hayo yote yapo ndani ya mwanajeshi. Mwanajeshi ili awe Mwanajeshi lazima awe na hayo Kwanza ndipo mafunzo, silaha, Mbinu n.k. ndio apewe.

Kwa namna hiyo Basi, utagundua lengo kubwa la Propaganda ni kuangusha ujasiri, Imani, mtazamo wa Mwanajeshi husika au jeshi husika katika upambanaji.

Kwa Sisi Wasomi wa Bibilia, Moja ya mambo makubwa ambayo yanajitokeza tokeza katika visa vya Biblia ni Propaganda ya kuwapa Waisrael Ujasiri, Imani, na mtazamo Chanya kuwa wao ni Bora kuliko watu wote Duniani.
Kisha ndipo Sheria za Torati zinawekwa ili kuwafanya wawe na Nidhamu.

Zipo Makumi ya aya zinazoeleza kuwa Muisrael Mmoja atakimbiza watu Mia WA mataifa mengine. Hiyo ni propaganda

Kuna kisa kingine ambacho Musa aliagiza Wapelelezi Kumi na mbili Kwenda kuipeleleza Nchi ya Kanaani. Wapelelezi wale Kumi na mbili waliporudisha ripoti. Wapelelezi Kumi wakatoa ripoti Yao kuelezea Jinsi nchi Ile ilivyo na watu wake walivyo Wakubwa na wenye nguvu na hodari. Kwa jinsi walivyokuwa wanaoelezea ni Kwa namna ya kuwakatisha tamaa na kuwatisha waisrael Jambo ambalo ni Kweli Waisrael waliingiwa na Hofu.

Lakini kwa Bahati, wapelelezi Wawili ambao ni Joshua na Kalebu wao wakatoa ripoti Yao inayokinzana na ripoti ya wale wapelelezi kumi. Wao wakasema in a positive ways.
Kusifia nchi wanayoiendea(Lengo Lao), kusifia Jeshi lao na Waisrael kwa ujumla, na mwisho kueleza sifa za maumbile ya adui Zao in a negative ways.
Wakasema, ni kweli wale watu ni Wakubwa Sana, wanamiili Mikubwa Mno na nguvu za Kimwili, lakini mioyoni mwao wanahofu juu yetu. Mambo makubwa tuliyoyafanya kuanzia kwa Farao, bahari ya shamu na kupiga mataifa yote tuliyokutana nayo imewanyong'onyesha Sana.
Hivyo waisrael na Jeshi la Israel Halina Sababu ya kuogopa watu hao kwani ni ukubwa wa Pua tuu ambao haulingani na wingi wa makamasi.

Ari, ujasiri, imani kwa Waisrael na Jeshi lao ikarejea lakini Musa kama kiongozi wa kijeshi na mwenye hiyo Movement akatoa maamuzi wale wapelelezi kumi wauawe ili wasije waletea Hofu na kuambukiza Hofu hiyo watu wengine.

Muhtasari huo tunajifunza mambo mengi lakini kubwa zaidi linaloendana na Mada hii ni nguvu ya propaganda na maneno katika Ulinzi na usalama na wanajeshi wetu.

Jeshi imara linatokana na wananchi imara.

Hawa watu wanaendesha propaganda za kuishusha nchi yetu na kuidunisha hasa kijeshi(kiulinzi na KIUSALAMA), sio tuu wanatukosea Bali wanahatarisha usalama wa nchi kwa wakati ujao.

Kama ikiendelea hivi itajengeka dhana kwenye jamii yetu kuwa Warwanda ni watu hodari kuliko Sisi. Sisi ni Duni mbele ya Warwanda Jambo ambalo ni Uongo lakini likiendelea litafanya mitazamo ya Watanzania kuligeuza Jambo hilo ni KWELI.

Hawahawa wananchi ndio baadaye watajiunga na Jeshi. Yaani watu wenye kujiona Duni na hofu dhidi ya Warwanda ndio watakuwa wanajeshi hata ikitokea vita watakuwa waoga na kushindwa mbele za adui Zao Warwanda.

Nini chakufanya?

1. Kitengo cha Propaganda hasa za kijeshi kisilale. Kijiimarishe na kuweka mipango na mikakati kufanya Watanzania waliamini Jeshi Lao.
Kwa sababu Jeshi likianza kutiliwa Mashaka hata ufanisi wake utapungua.
Kwa USA na mataifa mengine tunaona wo vitengo vya propaganda viko kila idea, huko Hollywood kwenye Filamu, kwenye Masuala ya kisayansi, na mambo ya Waandishi wa riwaya na tamthilia.
Kwamba ati Mwanajeshi Mmoja wa kimarekani anaweza kushughulikia maadui Mia moja wa mataifa mengine

2. Kutokana na baadhi ya watu kutokuwa na Akili au kuwa na chuki na nchi. Iundwe Sheria za kuzuia watu kuzungumzia mambo ya kijeshi na kiusalama kwa namna ya kudhalilisha, kumshusha heshima ya jeshi, kukejeli, kushusha morali au kudunisha.
Hii itaepusha na kuzuia wale wapiga propaganda zenye maudhui ya kudunisha Jeshi la nchi.

3. Watu wapewe uwezo wa kutoa maoni Yao lakini yawe maoni ya kujenga sio yenye lengo la kutukuza taifa jingine kuliko taifa kwa namna ya kukejeli taifa letu.

4. Mafunzo ya JKT yaendelee kutolewa kwa wanaomaliza kidato cha sita na kwa wale Wa kidato cha nne ambao wataendelea na vyuo vya Kati.

Ninawahakikishia, Maneno haya yakiendelea hivihivi watu na jamii itayaamini. Na matokeo ya kuyaamini Maneno ya aina hii hayatakuwa mazuri.

Lazima Sisi kama taifa tujitambulishe sio tuu kwa upendo wetu, umoja wetu Bali pia tujitambulishe kama watu wenye AKILI kubwa, na watu wenye kufanya mambo magumu.

Nawatakia maandalizi Mema ya Sabato

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
A very poor hypothesis, as the matter of fact it's rubbish.
Theories zako ni za kitoto mno, jeshi imara linajengwa kuanzia kwenye recruiting(si hawa wetu wanaoingia kwa vimemo, siku hizi hata TISS mpaka uwe UVCCM) na training.
Back in the day things were different.
As long as things on the ground zinatuonyesha kuwa jeshi la PK liko vizuri haiwezekani watu wasiseme, kukwepa kusema yale yanayooneka ni hypocrisy na haiwezi kusaidia kulijenga jeshi letu. Jeshi halijengwi kwa kupigiwa upatu mitandaoni au wanajeshi hawawezi kujengea kwa sababu tu wanasifiwa mitandaoni, wapate mafunzo na wajengwe nidhamu ambayo pia iwaimarishe mental strength ila recruitment iwe ya maana.
Ni kihoja kusema comments za mitandaoni zitaathiri uwezo wa jeshi hata kama lipo vizuri kiuhalisia on the ground.
 
A very poor hypothesis, as the matter of fact it's rubbish.
Theories zako ni za kitoto mno, jeshi imara linajengwa kuanzia kwenye recruiting(si hawa wetu wanaoingia kwa vimemo, siku hizi hata TISS mpaka uwe UVCCM) na training.
Back in the day things were different.
As long as things on the ground zinatuonyesha kuwa jeshi la PK liko vizuri haiwezekani watu wasiseme, kukwepa kusema yale yanayooneka ni hypocrisy na haiwezi kusaidia kulijenga jeshi letu. Jeshi halijengwi kwa kupigiwa upatu mitandaoni au wanajeshi hawawezi kujengea kwa sababu tu wanasifiwa mitandaoni, wapate mafunzo na wajengwe nidhamu ambayo pia iwaimarishe mental strength ila recruitment iwe ya maana.
Ni kihoja kusema comments za mitandaoni zitaathiri uwezo wa jeshi hata kama lipo vizuri kiuhalisia on the ground.
Inasikitisha sana. Eti mtu uwe UVCCM ndo umachukuliwa TISS.

Na kweli watu wengi wasio raia tulivyokuwa chuoni ndo walikuwa wanajifanya UVCCM kindakindaki.

Maajabu wengi wao leo wako TISS na wengine kwenye nafasi nyeti Serikalini.

This country is already tucked up na inabidi CCM iondolewe madarakani ili haya mambo yashughulikiwe vizuri
 
Uwezo wa nchi unapimwa kwa mambo ya msingi.

Nchi ambayo bado inapewa misaada ya matundu ya vyoo na ambayo inapoteza watoto wadogo wenye damu ya kisiasa inayochemka kama akina Soka nakuhakikishia, nchi hiyo ni failure ktk anga zote.

Akili isiyoweza kusolve matatizo ya msingi kama vile maji, matundu ya vyoo, madawati usitegemee inaweza kuwa nzuri kwenye mambo complex kama ya ulinzi ktk geopolitics.
Unakosea!

Hili suala linahitaji utaifa. Unaweza ukaichukia serikali lakini si taifa.

Siasa za upinzani ziishie kwenye serikali na mambo ya siasa. Lakini taifa linapokuwa hatarini utaifa unapaswa kuwekwa mbele.
 
Moja ya kosa linalofanywa na wapinzani ni kufikiri wao wakipewa nchi wataongoza watu tofauti na Watanzania waliopo sasa. Ni muhimu kwenye mambo serious yanayogusa future ya nchi yetu hasa mambo ya ulinzi wa nchi, wote tuwe na sauti moja bila kujali wewe ni upinzani au chama tawala. Jeshi ndiyo chombo pekee cha ulinzi wa mipaka ya nchi yetu. Halistahili kubezwa hata kidogo. Kwa hapa East and Central Africa tuna jeshi Imara na bora sana.
Acha ujinga Hilo ni jeshi la ccm sio wananchi
 
Unakosea!

Hili suala linahitaji utaifa. Unaweza ukaichukia serikali lakini si taifa.

Siasa za upinzani ziishie kwenye serikali na mambo ya siasa. Lakini taifa linapokuwa hatarini utaifa unapaswa kuwekwa mbele.
Hamna taifa kama jeshi linasaliti wananchi kisa watu wachache huo ujinga hatuna na hii sio miaka ya 1950s mzee hii miaka humdanganyi mtu
 
Inasikitisha sana. Eti mtu uwe UVCCM ndo umachukuliwa TISS.

Na kweli watu wengi wasio raia tulivyokuwa chuoni ndo walikuwa wanajifanya UVCCM kindakindaki.

Maajabu wengi wao leo wako TISS na wengine kwenye nafasi nyeti Serikalini.

This country is already tucked up na inabidi CCM iondolewe madarakani ili haya mambo yashughulikiwe vizuri
Unachokisema ni sahihi!

Wanayarwanda wengi wapo CCM na wengi walipewa nafasi. Ila amini kuwa hao watu wapo nafasi za chini hata huko Tiss. Hawapo nafasi za juu za kimamlaka. Hata makao makuu huwezi kuwaona.
 
Hamna taifa kama jeshi linasaliti wananchi kisa watu wachache huo ujinga hatuna na hii sio miaka ya 1950s mzee hii miaka humdanganyi mtu
Jeshi limesaliti wapi wananchi?

Twende kwa mifano hai tusiende kwa mihemuko!
 
Jeshi limesaliti wapi wananchi?

Twende kwa mifano hai tusiende kwa mihemuko!
Jeshi limesaliti wananchi wake wanaopotezwa na halitoi tamko lolote jeshi limesaliti wananchi wake kuendelea kulinda chama tawala kushinda chaguzi hivyo Hilo sio jeshi la nchi ni la chama tawala hizi sio zama za mazuzu kudanganyana
 
Unakosea!

Hili suala linahitaji utaifa. Unaweza ukaichukia serikali lakini si taifa.

Siasa za upinzani ziishie kwenye serikali na mambo ya siasa. Lakini taifa linapokuwa hatarini utaifa unapaswa kuwekwa mbele.
Vita ni pamoja na kuwa na viongozi wenye ufahamu . Kama una watu wanaogeuza binoculars kuangalia mazoezi ya Kijeshi halafu ndo mawaziri wenye dhamana ya majeshi, unadhani hao wanaweza kufanya jeshi liwe bora?

Lakini je unataka nimuonee wivu Kagame na jeshi lake zuri?.

Ubora wa jeshi letu hautakuja kwa kuionea wivu Rwanda.
 
Unachokisema ni sahihi!

Wanayarwanda wengi wapo CCM na wengi walipewa nafasi. Ila amini kuwa hao watu wapo nafasi za chini hata huko Tiss. Hawapo nafasi za juu za kimamlaka. Hata makao makuu huwezi kuwaona.
Acha ukabila na uwongo
 
Back
Top Bottom