Propaganda za kukuza uwezo wa Rwanda kijeshi zinahatarisha usalama wa nchi yetu hapo baadaye

Propaganda za kukuza uwezo wa Rwanda kijeshi zinahatarisha usalama wa nchi yetu hapo baadaye

Sasa Rwanda, Kagame kaweza kusolve vitu vidogovidogo hivyo hapa kwetu vinatushinda.

Hii maana yake Kagame ana upeo mkubwa kuliko viongozi wetu. Kama tukipigana nae, viongozi wetu hawana uwezo wa kiakili kumzidi ujanja.

Mmmh!
Unajua Warwanda wengi wanaokuja Tanzania hasa maeneo ya Geita, Kagera, kigoma na shinyanga wanafanya Kazi za shokoa?
 
JESHI husifiwa kwa uwezo wake wa Kimedani na nidhamu yake.
Kamwe Jeshi haliwezi kuwa inferior kwa sababu ya propaganda za Rwanda.
Tunasifu uimara wa Rwanda kwa sababu DRC imewashindwa?!
DRC ni kama hawana Jeshi,ni mkusanyiko wa vikundi vya waasi wa zamani!..hawana morali Wala hawana uzalendo wowote.
Kama Askari wa Congo anayepaswa kufia Vitani,kwa hiyari yake anakwenda kukabidhi Bunduki yake kwa waasi na anavuka mpaka!..huyo hafai kuwa Askari na Wala Hana Sifa za kuwa Askari.
Kingine,Wanajeshi wa Congo wanakosa Ari na moral ya kupigana kwa sababu zingine nyingi kama maslahi duni,huwezi ukawaita mercenaries ukawalipa $5000 wakati Askari wako unawalipa chini ya $100!
Pia hakuna kosa walilofanya M23 kujilinda kama jamii ya kitutsi iliyotengwa na inayonyanyaswa na Serikali kuu ya Kinshasa!
Kwa muktadha huu,huwezi kufananisha utendaji wa Jeshi dhaifu na Serikali dhaifu kama ya Congo na Nchi yetu ambayo ni Tajika katika medani za kijeshi!
Jeshi letu ni Jeshi lenye Nidhamu,Utii,Uzalendo,Ujuzi,uzoefu,utayari,VIFAA na Morali ya hali ya juu sana.
Rwanda inatajwa kwa sababu Iko Vitani tayari,hata sisi tulipoingia miguu yote Congo kuwafukuza M23 pia propaganda zilipigwa sana!
Kutajwa tajwa kama bingwa haimaniishi kuwa wewe ni bingwa kweli.
 
Watakuwa wapelelezi hao.

Hakuna kitu kama hicho Mkuu.
Ingawaje Wachache wanaweza kuwapo lakini sio katika level ya chini hivyo.

Mtu aajiriwe kuchunga Ng'ombe au kulima vibarua kwa Watu binafsi atafanya upelelezi kwa minajili ipo. Kwa taarifa zipi hapo MKUU.

Moja ya viashiria vinavyoonyesha Rwanda bado Sana unaweza kutazama uhamiaji. Huwezi kukita Mtanzania anaenda Kutafuta maisha Rwanda lakini ni Jambo la kawaida kwa Rwanda kuja Tanzania.
 
Unakosea!

Hili suala linahitaji utaifa. Unaweza ukaichukia serikali lakini si taifa.

Siasa za upinzani ziishie kwenye serikali na mambo ya siasa. Lakini taifa linapokuwa hatarini utaifa unapaswa kuwekwa mbele.
Upuuzi tu siwezi kupambana CCM ikiwa madarakani nitakuwa nimekufa kifo cha kipumbavu.

Na nakuhakikishia siku Tanzania ikiingia vitani itapigwa vibaya mno huwezi shinda vita ambayo serikali na wananchi sio kitu kimoja na ndicho kilichopo Tanzania.

Serikali iache kutengeneza classes hizo za kipuuzi, watakapo anzisha vita watapigana wao na wajomba zao hii ni 2025 sio 1978
 
Ukweli usemwe tu
Hatuwezi kuwa taifa lenye nguvu kama Professor mmoja anajitokeza bila aibu na kulalamika kuhusu US kukata misaada ya madawa utafikiri tunawadai
Leo tumekuwa ombaomba mpaka Vyoo tunapokea misaada yake
Hii ni aibu kubwa sana
Tuambiane ukweli sio kuficha ficha mambo na kujisifia uongo
Tulikuwa wababe sana enzi zetu na naomba tujipange kwa kuongeza bajeti kubwa kwenye Wizara ya Ulinzi
 
Jeshini wapo wanaulinda Taasisi, wapo wanaolinda rais na wapo wanaolinda nchi na nafikiri umenielewa.

Huyo mama yupo kukamilisha taratibu za kisiasa kulingana na kanuni na mwongozo wa kisheria unavyotaka.

Ila mengineyo wapo ambao wanaoyasimamia.

Hakuna ambaye anayemuonea wivu Kagame. Suala ni usalama wa nchi, kama mambo huyafahamu omba ufahamishwe.
Hakuna jeshi Tanzania ni kundi la wanachama wa CCM wanao valishwa combat na kwa ujinga wao wanalinda watu wapumbavu wanao hatarisha huo usalama wa taifa.
 
Hamna taifa kama jeshi linasaliti wananchi kisa watu wachache huo ujinga hatuna na hii sio miaka ya 1950s mzee hii miaka humdanganyi mtu
Upo sahihi ukweli lazima usemwe siku hizi hatuna jeshi la wananchi tena limebaki la CCM.
 
Jeshi limesaliti wapi wananchi?

Twende kwa mifano hai tusiende kwa mihemuko!
Moja ushiriki wao katika siasa chafu za uchaguzi za kuwasimika CCM Tanganyika na Zanzibar.
 
Upuuzi tu siwezi kupambana CCM ikiwa madarakani nitakuwa nimekufa kifo cha kipumbavu.

Na nakuhakikishia siku Tanzania ikiingia vitani itapigwa vibaya mno huwezi shinda vita ambayo serikali na wananchi sio kitu kimoja na ndicho kilichopo Tanzania.

Serikali iache kutengeneza classes hizo za kipuuzi watakazo anzisha watapigana wao na wajomba zao hii ni 2025 sio 1978
Sawa!
 
PROPAGANDA ZA KUKUZA UWEZO WA RWANDA KIJESHI ZINAHATARISHA USALAMA WA NCHI YETU HAPO BAADAYE.

.

Ari, ujasiri, imani kwa Waisrael na Jeshi lao ikarejea lakini Musa kama kiongozi wa kijeshi na mwenye hiyo Movement akatoa maamuzi wale wapelelezi kumi wauawe ili wasije waletea Hofu na kuambukiza Hofu hiyo watu wengine..

Ninawahakikishia, Maneno haya yakiendelea hivihivi watu na jamii itayaamini. Na matokeo ya kuyaamini Maneno ya aina hii hayatakuwa mazuri.

Lazima Sisi kama taifa tujitambulishe sio tuu kwa upendo wetu, umoja wetu Bali pia tujitambulishe kama watu wenye AKILI kubwa, na watu wenye kufanya mambo magumu.

Nawatakia maandalizi Mema ya Sabato

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
Nyie Wanyarwanda tupumzisheni!! Ukubwa wa jeshi la Rwanda hadi kutishia Tanzania uko wapi? Mbona katika majeshi 20 bora ya Afrika la Rwanda halipo!!
Screenshot_20250131_105207_Chrome.jpg
 
Kushinda vita vya kijeshi kunahitaji mchanganyiko wa mambo mengi, na hakuna formula moja rahisi. Hapa kuna baadhi ya mambo muhimu ambayo yanaweza kuchangia ushindi:

## 1. Nguvu ya Kijeshi

  • Wanajeshi: Kuwa na jeshi kubwa lenye askari wengi wenye mafunzo mazuri na vifaa vya kisasa.
  • Vifaa vya Kijeshi: Kumiliki silaha za kisasa, kama vile ndege za kivita, meli za kivita, magari ya kivita, na mifumo ya ulinzi.
  • Teknolojia: Kuwa na teknolojia ya kijeshi ya hali ya juu, kama vile mifumo ya ujasusi, mawasiliano, na silaha za kisasa.

## 2. Mkakati na Uongozi

  • Mkakati: Kuwa na mkakati mzuri wa kijeshi ambao unaeleza jinsi ya kufikia malengo ya vita.
  • Uongozi: Kuwa na viongozi wenye uwezo na uzoefu ambao wanaweza kuongoza jeshi kwa ufanisi.

## 3. Uchumi

  • Rasilimali: Kuwa na rasilimali za kutosha kugharimia vita, kama vile fedha, chakula, mafuta, na vifaa vingine.
  • Uzalishaji: Kuwa na uwezo wa kuzalisha silaha na vifaa vingine vya kijeshi.

## 4. Morali

  • Morali ya Wanajeshi: Wanajeshi kuwa na morali ya juu na imani katika ushindi.
  • Umoja wa Kitaifa: Wananchi kuwa na umoja na kuunga mkono vita.

## 5. Diplomasia

  • Washirika: Kuwa na washirika wa kimataifa ambao wanaweza kusaidia katika vita.
  • Mazungumzo: Kuwa tayari kufanya mazungumzo ya amani ili kumaliza vita.

## 6. Mambo Mengine

  • Hali ya Hewa: Hali ya hewa inaweza kuwa na jukumu katika vita.
  • Jiografia: Jiografia ya eneo la vita inaweza kuwa na jukumu.
  • Bahati: Wakati mwingine, bahati inaweza kuwa na jukumu katika vita.

Ni muhimu kuzingatia kwamba vita ni jambo ngumu na lisilotabirika. Hata kama una mambo yote hapo juu, bado kunaweza kuwa na sababu ambazo zinaweza kusababisha kushindwa.

## Mwisho

Kushinda vita kunahitaji mchanganyiko wa mambo mengi, na hakuna uhakika wa ushindi. Ni muhimu kuzingatia kwamba vita vina madhara makubwa na vinapaswa kuepukwa kwa gharama zote.


Gemini AI
Bahati au sio
 
Njia rahisi ni modes wa hili jukwaa wafute nyuzi za namna hiyo na nyingine waziunganishe ili kuzima kick na kutrend kwa mambo ya namna hiyo, na wazalendo waandike nyuzi za kupaisha jeshi letu na kulitrendisha sasa wakikaa kimya raia wataamini halina maajabu
Kwahiyo kufanya hivyo inaweza kuleta msaada wowote? Maana mwisho wa siku kama uimara haupo hiyo haiwezei kuongeza uimara na kama upo hata watu wakiwa negative hakuna kitakacho badilika.

Katika mambo ya vita kujinasibu kwamba una nguvu ni ishara ya udhaifu kwa maana watu wenye nguvu huwa hawazizungumzii nguvu zao.

Kuna msemo unasema jifanye mnyonge wakati unanguvu na ujifanye unanguvu wakati mnyonge.

So positive na negative zote zinajenga ila kitakacho bomoa ni details nyeti ikitokea ndio zikaanza kuwekwa hadharani hapo ndio hatua ichukuliwe.

Ila hizi nyuzi na details ambazo hazina ukweli wowote sidhani kama zinaweza kuleta athari chanya au hasi kwa namna yoyote ile zaidi ya kufurahisha genge tu hapa.
 
Kinacho fanywa na rwanda ni military politics which is ata sisi tunabidi tumjibu kwa kupasha ndege zetu za kivita zipite pite angani kamera za tbc zi record kama habar wapost over, au tufanye kama kiduku anavyo fanya ana jaribu mabom yake kweny bahari na sisi twende ziwani mwanza tufanye majaribio ya mabomu yetu.
 
Sasa kama jeshi linachukua magari yake na kuipa CCM ili ibebe wajumbe wa mkutano mkuu na kuwapeleka DODOMA kwenda kumpitisha mtu kinyume cha taratibu hata za CCM yenyewe, hapo kuna kitu hapo?
 
Maswala ya jeshi ni complex kidogo, Wenyewe wanajua wanachofanya hata hivyo suala la jeshi la rwanda kukuzwa kwa propaganda ni la kuangalia sasa si la kupuuzwa.
Nauhakika wazee wa MI wanalifanyia kazi
VIVA TANZANIA.
 
Back
Top Bottom