Prophet Lovy Elias kukiwasha Kijitonyama

Prophet Lovy Elias kukiwasha Kijitonyama

Huyu Jamaa kapitia Mengi na sidhani kama ana fake kazi ya Mungu.
Kama ni mademu au Bata kala kuliko wengi,kama umemfuatilia tangu akiwa Longombaz na mwenzake ambaye ashatangulia mbele za Haki itoshe kusema tusikimbilie kuhukumu mtu Kwa mwonekano,Kama ni nywele hata Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu angeamua kusokota mngemwita muhuni?How dare you.
Mkuu umejuaje kuwa bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?
 
Kondoo hawezi kuvaa ngozi ya mbwa mwitu ila mbwa mwitu anaweza kuvaa ngozi ya kondoo ili awatafune wengi.
Biblia imetumia neno ngozi ikimaanisha kuwa mwonekano wa nje pia una nafasi kubwa.

Zama hizi malaika wa giza anajifanya malaika wa nuru ili apate kuwameza wengi.
Shikilia sana ulichonacho asije mwovu akakunyang'anya hata hicho.

Naona watu wa Mungu wanavyoachia hata kidogo walichomiliki awali!
 
We unatazama mwonekano Wa nje tu
basi nitafsirie hii mistari
{6AC98C7E-E7B7-47A2-BC93-4495C2D4C1A9}.png.jpg
 
Sio kweli ndo maana huwa mnaibiwa Kwa kudanganywa na outlook ya MTU mwonekano Wa nje ni Kama kava la simu tu kuna watu they dress decent Ila wanafanya mambo machafu Sana even in my family
Biblia imekwisha sema kimjaacho mtu ndicho kimtokacho. So kama unabisha na biblia sawa hatuna cha kukusaidia tena
 
kuna pastari mmoja kijana hapa dar alipenda sana kuvaa pensi huku anatembea mitaani watu wakahoji aliwajibu dar ni joto lazima avae vile. Akiwa anahubiri jumapili moja akamtetea mke wake mvaa vimini kuwa atavaaje magauni marefu, je yakimzongazonga na kuanguka, kero yote ya nini?. Kanisani kwake vijana walivaa na kunyoa mitindo yote kwa uhuru. Yupo mwingine naye ni kijana maarufu sana katika kazi yake ya sanaa ya uchekeshaji nadhani mnamjua huyu mwamba, yeye kaanzisha kanisa na linazidi kupata umaarufu, anaruhusu uende kuabudu kwake jinsi ulivyo. Ukitengwa na kufukuzwa kanisani kwako yeye anakupokea. Kanisani kwake wamejaa vijana na mabinti waliovaa ki ajabuajabu fresh tu. Yeye mwenyewe uvaaji wake ni utata mtupu japo ana suti za heshima ya uchungaji wake. Yule mwamba dhamiri haimchomi kupanda madhabahuni na nguo za kihuni, praise worship team yake sasa walivyovaa utashangaa unaweza kudhania upo amerika na ulaya, ni nguo za ajabu balaa
 
Ndo maana wenzetu waisilamu wanasema dini ya kweli na ya haki mbele ya M/Mungu ni Islan , kwa ajili ya wahuni kama Hawa, ukristu na wakristu tunadharaulika na kubezwa Kwa sababu ya wahuni kama hawa
 
Haihitaji hata kuwa na Roho Mtakatifu kujua kuwa LGBTQ iko nyuma yake
Nendeni miapandikiziwe ushoga bila kujijua maana ujinga na upumba hamutaki kuuacha
View attachment 2836284
unaenda kuwekewa mikono kumbe unapandikiziwa mapepo mabaya. Hii kuombewa kwa kuwekewa mikono na watumishi wa mungu ni kujihadhari sana, wengine si watumishi wa mungu ni maajenti wa shetani
 
Back
Top Bottom