PSRS iendelee kuajiri au turudi kwa mashirika yaajiri tena kama ilivyokuwa awali?

PSRS iendelee kuajiri au turudi kwa mashirika yaajiri tena kama ilivyokuwa awali?

enzi zile za kuandika barua moja kwa moja kwenda kwenye taasisi husika kuna raia walikuwa wanaandika na hawakuwahi hata kuitwa, na hata waliopata kuajiriwa kujuana kulikuwa ni kwingi saba japokuwa utumishi wana mapungufu yao ila yanavumilika nimeshuhudia mtu ambae hana connection yoyote na fresh from school kapata nafasi ya ajira. Bora mara 100 ibaki utumishi kuliko kurejea katika taasisi husika

hata hii issue ya Dodoma japo tunaona ina changamoto zake ila ni bora maana ikianza kila kitu kumalizikia mikoani ndio mwanzo wa kupenyezana maana mtakuwa wote mnajuana mkoa husika, written zifanyike huko mikoani ila Oral zibaki tu Dodoma
 
Utumishi wapumzike, kwanza wana dharau, hawako considerate. Urasimu uko pale pale. Acha mashirika yaendelee kuajiri kama kawaida

Kuna mdogo wangu aliwahi kupangiwa interview branch ya mwanza tena wao ndo walikosea kwenye ku sort adress na tarehe ya interview inatangazwa alikua hospitalini Dar hoi, akapata nafuu siku moja kabla ya interview. kaenda pale DUCE na cannula mkononi alitoka hospitali kwa kujikaza anajaribu kuwaelezea situation anaomba afanyie interview pale walimkatalia. Nikasema kweli ni kazi yao. Ila ubinadamu sifuri
Wana mapungufu kweli ni kama haya lakini unaonaje kama wakirekebisha haya ili kuwe recruitment process nzuri na bora mana sasa wengi walokuwa hata shortlist hawaitwi sasa huitwa na wanapata ajira.

Mashirika yalipokua yanaajiri ni kimya kimya watu wachache hulinda maslahi yao na kupeana wao kwa wao unaona hii ni nzuri kuendelea?
 
Hujaelewa alichoongelewa aliongea miradi ambayo ni ya muda mfupi ajira zake sio lazima utumishi ili kuendana na muda wa miradi
Nimemuelewa vizuri sana.

Ajira hizo za mda mfupi itakua ni loophole ya kupitisha watu vile vile kuingia katika ajira za kudumu.

Ajira zote temporary na permanent zibaki PSRS.
Tabia ya Watanzania zinajulikana akiachiwa upenyo tu lazima atumie fursa hiyo kufanya madudu yake.
 
Utumishi wapumzike, kwanza wana dharau, hawako considerate. Urasimu uko pale pale. Acha mashirika yaendelee kuajiri kama kawaida

Kuna mdogo wangu aliwahi kupangiwa interview branch ya mwanza tena wao ndo walikosea kwenye ku sort adress na tarehe ya interview inatangazwa alikua hospitalini Dar hoi, akapata nafuu siku moja kabla ya interview. kaenda pale DUCE na cannula mkononi alitoka hospitali kwa kujikaza anajaribu kuwaelezea situation anaomba afanyie interview pale walimkatalia. Nikasema kweli ni kazi yao. Ila ubinadamu sifuri
Wapumzike Ili uingie jop kirahisi
 
Back
Top Bottom